nguruka wa kig0ma
JF-Expert Member
- Jan 16, 2020
- 2,946
- 2,929
Serikali imewajengea uwezo hao wakulima unaosema wanatakiwa kuijenga nchi yao?Ndo maana tunasema tanzania upinzani ulishakufa ,hivu hii nguvu mnayoitumia kuonesha wakulima wazalendo watanzania kuwa wanaonewa na serikali yao, kwanini msingeitumia kuwaelimisha umuhimu wa kuchangia au kulipa kodi kwa moyo mkunjufu maana wao ni jukumu lao kujenga nchi sababu ni watanzania na nchi haiwezi jengwa na na watu wa nchi jirani?
Kwahiyo aliyeandikiwa hiyo barua ni mnyonge ausio!? Acheni ushabiki wa kijinga; tembelea Mang'ola uwaone mabwanyenye. Utaratibu wa wenye mashamba makubwa kulipia kodi ya mapato upo siku zote na ukifuatilia barua hiyo anapewa maelekezo ambayo alitakiwa kuwa ameyatekeleza kabla ya hiyo notice.Baada ya matajiri kuisha sasa ni zamu ya wanyonge kulipa kodi na kufilisiwa. Kwani nasema uongo ndugu zangu?
Kwahiyo aliyeandikiwa hiyo barua ni mnyonge ausio!? Acheni ushabiki wa kijinga; tembelea Mang'ola uwaone mabwanyenye. Utaratibu wa wenye mashamba makubwa kulipia kodi ya mapato upo siku zote, na ukifuatilia barua hiyo anapewa maelekezo ambayo alitakiwa kuwa ameyatekeleza kabla ya hiyo notice.
Anyway, lazima tulipe kodi ili tuweze kujitegemea; endeleeni kutegemea ubeligiji.
Hata hivyo hao si walishalipa ushuru wakati wananunua?.Mkuu hivi unawafahamu wakulima kweli?Wakulima huuza mazao yao wakati mwingine yakiwa bado shambani.Hao wanaotunza stock ya mazao ni wafanya biashara au wachuuzi wa mazao.Mfano kule Kahama kuna wafanyabiashara wakubwa wanama godown ya kuhifadhi mpunga hata miaka mitatu wakisubiri bei ipande.
Wakulima wengi hawawezi kuwa na uwezo huo wa kuvumilia bei ipande
Haitowezekana.Dr Mpango kaitaka TRA kubuni namna ya kukusanya Tril 2 kila mwezi... tupo kwenye utekelezaji.
Target ni 2 trillion per annum, tutakoma mwaka huu. Bado kodi za birthday, ushereheshaji, kashata na kahawa, machinga, gengeni, usukaji nywele, upakaji ina, upakaji wanja kukata nyusi na rangi kwa kina mama! Ndio, hiyo ndiyo TRA yetu, wavivu wa kufikiri, kupenda kuumiza watu wa vipato vya chini na kupenda vya kunyonga...
Nilitaka kutafutia hati shamba langu, ngoja niache tu. Nimekuwa na vibarua kati 10-40 wakati wote, japo sijawahi kupata chochote. Nimetumia zaidi ya shilingi milioni 800. Kwa hali inavyoenda, ni aheri kusimama kwanza. Umepoteza hela, halafu hawa maharamia TRA wanaweza kuja kubambikia kodi ya ajabu.Umenena vyema japo wapo wakulima wa aina nyingi. Huwezi kusema sumry Ncha Kali aliyelazimika kuachana na biashara ya mabasi akaingia ktk kilimo hana uwezo wa kusubiri bei!!!!! Vivyohivyo kwa mtoto wa mkulima mr kayanza.
Huyo unaye ona kalimwa barua ujue TRA wamesha fuatilia mwenendo na wanajua anaendeshaje kilimo chake. Tusicho kijua ni kwamba huwenda pia wamesha nusa mamilioni kwenye account yake.
Kumbuka hao jamaa hawajihangaishi bila kunusa kuwa mahala fulani wanaweza kupata chochote. Ukisha sikia kaambiwa miaka mitatu ujue mamilioni yanamhusu.
Kumbuka ya st. Jude school.
Maashaallah kwake kila goti litapinda
Warudishe kodi ya kichwa, waanzishe kodi ya kichwa kwa wanyama - ng'ombe, mbuzi, nguruwe, kondoo, mbwa, paka, kuku, sungura, kanga, na njiwa. Pia waanzishe kodi ya gurudumu itakayohusu baiskeli na mikokoteni yote.Na kodi ya baiskeli wasisahau pia.
Ndio sera za ufipaWarudishe kodi ya kichwa, waanzishe kodi ya kichwa kwa wanyama - ng'ombe, mbuzi, nguruwe, kondoo, mbwa, paka, kuku, sungura, kanga, na njiwa. Pia waanzishe kodi ya kurudumu itakayohusu baiskeli na mikokoteni yote.
Lazima miradi wa reli, bwawa la Nyerere ba ununuzi wa ndege, ikamilike.
Sent using Jamii Forums mobile app
Basi watoze kodi kuvuta oxygen kwa siku sh.50Dr Mpango kaitaka TRA kubuni namna ya kukusanya Tril 2 kila mwezi... tupo kwenye utekelezaji.
Bado kodi ya kichwa irudi, Mpango ameagiza TRA wakusanye Trillion 2 kwa mwezi
Mkuu hapa haongelewi mkulima mdogo mdogo, huyo anayeongelewa ni mwekezaji tena ameajiri wafanyakazi kwenye shamba lake, ndio aachwe asilipe kodi???Huku no sawa na kukama ng'ombe maziwa bila huduma yakinifu . ( Utatoa damu mwisho was siku)
Mkulima huyu amejengewa mazingira Bora ya kilimo?
Anapatiwa masoko?
Mpunga mpka Sasa upo maghalani Bei no sawa na kipindi Cha mavuno, serikari haishughuriki na chochote.
Wakulima wengi ni wadogo wadogo hawana hata uwezo wa pump ndogo za maji ili kumwagilia, Sasa ivi wanaangalia mawingu.
Alafu unataka kumtoza ushuru kwa kipato gani, kwa huduma gani anazopata toka serikalini?
Hahahaha...Mbona ulishindwa alipowaletea magwanda?
Uliza sumbawanga walituma Moto ukalamba kofia babu yupo fiti tu mpk leo
Baada ya hapo kifuatacho eti sijui umebeba Vigunia vyako vya mchele kutoka Igunga unakuja kuzunguusha Tandale Sokoni, angalau ili watoto waende chooni mara paap unashusha tu Vigunia vyako TRA hao wanataka risiti ya efd huna faini milioni tatu wakati mtaji wa hiyo biashara hata milioni haufiki