BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 422
- 1,049
Hakuna taarifa yoyote inayoendelea, Jeshi la Polisi mbona mnafanya maamuzi ambayo ni ya kidikteta, juzi hapa si Mkuu wa Mkoa kasema wanashughulikia tatizo hilo na hadi kufikia Januari 15, 2024 kila kitu kitakaa sawa
Sasa mbona mnakamata Wakulima na kuwaacha wafugaji ambao wanaendelea kupelekea mifuo yao kwenye mashamba hayo wakati Mamlaka nyingine zinasema maeneo hayo ni ya hifadhi, inakuwaje hifadhi kisha kunakuwa na mifugo tena ikiwemo mifugo ya Wanasiasa?
Majibu ya Jeshi la Polisi haya hapa - Wakulima 27 Wilayani Kiteto washikiliwa na Polisi kutokana na mgogoro wa Ardhi
Pia soma = Manyara: Wakulima Kiteto warejea kwenye mashamba waliyoondolewa, watuma ujumbe kwa Rais Samia wakidai wameporwa Ardhi yenye mashamba yao