Ukisimama kuurekebisha mfumo wa ukusanyaji Kodi Tanzania.
Utakuta unatekebisha Mfumo Bepari, Unyonyaji, Ukabaila.
Kodi lazima tulipe lakini lazima kuwepo na Ubinaadamu. Kodi lazima iendane na huduma ya jamii inayotolewa na Serikali.
Kuna nchi nyingi, usipolipa kodi, unaona hata aibu kutokana na kiwango kikubwa cha huduma Serikali inayotoa na jinsi Serikali na wadau wake wanavyowaangalia na kuwajali wananchi wake.
Waafrika hawakimbilii Ulaya bure kwenda kuosha viombo na kipiga deki. Haki za Binaadamu zipo Canada.
TB Joshua, tafadhali tunakuomba badilisha Ushauri wako. Wananchi wetu wanateseka.
Nyie ndio mnawaongoza na kuwashawishi baadhi ya viongozi wetu. Wanawatii ushauri wenu. Pilipili imezidi mdomoni. TB Joshua na Wanaijeria wenzako, hali ni mbaya.
George Bush aliyedharau amri ya Umoja wa Mataifa na kwenda kuivamia Iraq pasipo halali, anasema "Mwenyezi Mungu alimtuma".
Muinjilisti Mmoja Mashuhuri huko Marekani ndio aliyekuwa mshauri wake mkuu. Aibu tupu.
Ewe Mola Tuhifadhi na kuwa Wajinga, na Kutoiona Haki. Utulinde na Viongozi Matapeli wa Kidini. Hakika Waumini Matapeli ndio wameyaangusha na kuyapoteza mataifa yaliyopita.
Afrika Kusini, Wazungu wachache Makaburu enzi ya Ubaguzi wa rangi, walibarikiwa na Viongozi wao wa kidini.
Ewe Mola Muumba, tukomboe kwenye Ujinga, tuwezeshe tuwe na Taifa linalotenda haki.