Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,150
Ukizoea harufu ya rushwa hata mke utatami kumpata kwa rushwa tu.
Airport kisanga kimoja kikiongozwa na jamaa mmoja aitwae 'Chacha wa TRA'; Kwa kweli kila mmoja ameshindwa kumuelewa.... Egypt Air wanaletaga maji ya sadani.
Wanaitisha kwenye mizigo then wanaanza kugawa kila box bure kwa kila department za airport. Meneja huyu amefanya hivi zaidi ya miezi kadhaa tangu ianzishwe...na watu wamekuwa wakishukuru kwa kuminimaizi baadhi ya cost za maji.
Leo maji yakapita kama kawaida box tano ziko wazi wakaja madada wa TRA wakaangalia wakaziachia tena kwa kuomba box moja... gafla baada ya muda akatoka kijana mmoja aitwae Chacha alipoona maji yanagawiwa akakasirika akaanza kukoroma ooh peleka yaliyobaki pale TRA... akambiwa mbona yamepita huko na dada mmoja akatoa 'go ahead'?
Kama kawaida akang'ang'ana yaende... kufika anawaambia porte bila kujua hakuwa mhusika wa EgyptAir anataka apewe dollar 20 ayaachie akafika mpaka 15usd... hii ni njaa za aibu... wewe mtu hauzi anawagawia na nyie mnachukua maji kweli hii ni haki...? Inatia aibu sana yule mmisri akaamuru zipelekwe ofisini zote na hana hata senti ama ampigie fedha kamili sh ngapi zinatakiwa anaomba aandikiwe na risiti. Hapo kimbembe kikaanza akaona aibu akawaachia...
Jamani hizi njaa zenu TRA MTAZIACHA LINI? KWA NINI MNATAKA KUISHI KAMA MIUNGU WATU!? WAKUU WA TRA TUNAOMBA MSAADA WENU HUYU KIJANA ANAPITISHA MIZIGO MINGI TU KWA DILI WAKATI MAJI AMBAYO NA YEYE KACHUKUA ANATAKA ALIPWE TUTAFIKA HIVI?
Airport kisanga kimoja kikiongozwa na jamaa mmoja aitwae 'Chacha wa TRA'; Kwa kweli kila mmoja ameshindwa kumuelewa.... Egypt Air wanaletaga maji ya sadani.
Wanaitisha kwenye mizigo then wanaanza kugawa kila box bure kwa kila department za airport. Meneja huyu amefanya hivi zaidi ya miezi kadhaa tangu ianzishwe...na watu wamekuwa wakishukuru kwa kuminimaizi baadhi ya cost za maji.
Leo maji yakapita kama kawaida box tano ziko wazi wakaja madada wa TRA wakaangalia wakaziachia tena kwa kuomba box moja... gafla baada ya muda akatoka kijana mmoja aitwae Chacha alipoona maji yanagawiwa akakasirika akaanza kukoroma ooh peleka yaliyobaki pale TRA... akambiwa mbona yamepita huko na dada mmoja akatoa 'go ahead'?
Kama kawaida akang'ang'ana yaende... kufika anawaambia porte bila kujua hakuwa mhusika wa EgyptAir anataka apewe dollar 20 ayaachie akafika mpaka 15usd... hii ni njaa za aibu... wewe mtu hauzi anawagawia na nyie mnachukua maji kweli hii ni haki...? Inatia aibu sana yule mmisri akaamuru zipelekwe ofisini zote na hana hata senti ama ampigie fedha kamili sh ngapi zinatakiwa anaomba aandikiwe na risiti. Hapo kimbembe kikaanza akaona aibu akawaachia...
Jamani hizi njaa zenu TRA MTAZIACHA LINI? KWA NINI MNATAKA KUISHI KAMA MIUNGU WATU!? WAKUU WA TRA TUNAOMBA MSAADA WENU HUYU KIJANA ANAPITISHA MIZIGO MINGI TU KWA DILI WAKATI MAJI AMBAYO NA YEYE KACHUKUA ANATAKA ALIPWE TUTAFIKA HIVI?