Tofauti kati ya Uasherati na Uzinzi?

Tofauti kati ya Uasherati na Uzinzi?

Ph-25

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2012
Posts
1,159
Reaction score
540
Habari wakuu,tukumbushane kidogo kuhusu maandiko juu ya kichwa cha mada hapo juu..

Je ipi ni dhambi kutokana na maandiko na amri za mungu..?!

Karibu kujifunza..
 
Hivi wadau wa jukwaa hili si wajitokeze?
Hata nami natamani majibu mrua!

mkuu hii mada nilitupia mmu najua memba wengi wange toa yao ya moyoni huku watu wavivu kuja bna,mods na bifu zao wameileta huku hapa sasa ndo nashndwa kuelewa kabisaa.
 
Habari wakuu,tukumbushane kidogo kuhusu maandiko juu ya kichwa cha mada hapo juu..

Je ipi ni dhambi kutokana na maandiko na amri za mungu..?!

Karibu kujifunza..

Zote ni dhambi kwa mujibu wa maandiko!
 
watu wanasema zote ni dhambi lakini sioni wakionyesha ni maandko yapi yanaharamisha yote. Nijuavyo mimi (kwa wakristo) amri ziko kumi na amri ya 6 inasema "usizini" tafsiri ya kuzini japo sina halisi lakini sidhani kama itajumuisha uasherati. Maandko ya Biblia kwa kiwango kikubwa yako centered katika amri hizo kumi. Sasa najiuliza wapi uasherati umeharamishwa kwa mujibu wa AMRI?
 
watu wanasema zote ni dhambi lakini sioni wakionyesha ni maandko yapi yanaharamisha yote. Nijuavyo mimi (kwa wakristo) amri ziko kumi na amri ya 6 inasema "usizini" tafsiri ya kuzini japo sina halisi lakini sidhani kama itajumuisha uasherati. Maandko ya Biblia kwa kiwango kikubwa yako centered katika amri hizo kumi. Sasa najiuliza wapi uasherati umeharamishwa kwa mujibu wa AMRI?

mkuu uasherati sio dhambi,hawa wanazingua tu.
 
UASHERATI.. kufanya ngono kabla hujaoa/kuolewa.
UZINZI..kufanya ngono nje ya ndoa.. ZOTE NI DHAMBI NA ZINA HUKUMU.
ACHA!

tupatie andiko mkuu,linalo sema izo zote ni dhambi.
 
mkuu lakini amri za mungu zinasema usizini.? Uasherati unakuaje dhambi.? Ufafanuzi kidogo.
Kitu au jambo lolote lile ambalo mungu amekataza mja, kwenda kinyume chake ni dhambi.
Kuzini lile tendo la kujamiiana na mwanamke ambaye si mkeo. Uashirati kwa ufupi ni sifa za mja ambaye hupenda kuzini.
Dini karibu zote ambazo zinaamini uwepo wa mungu na kuwa yeye ni muumba wa kila kitu[tunavyovijua na tusiyoyajua] zinaamini hivyo
 
Kitu au jambo lolote lile ambalo mungu amekataza mja, kwenda kinyume chake ni dhambi.
Kuzini lile tendo la kujamiiana na mwanamke ambaye si mkeo. Uashirati kwa ufupi ni sifa za mja ambaye hupenda kuzini.
Dini karibu zote ambazo zinaamini uwepo wa mungu na kuwa yeye ni muumba wa kila kitu[tunavyovijua na tusiyoyajua] zinaamini hivyo

mkuu unajua amri za mungu sivyema kuzichakachua.? Ktk amri zake kumi amesema ktk amri ya saba kua "usizini." neno limesimama lenyewe bila utegemezi wa neno uasherati... Sasa iweje leo uasherati iwe dhambi.?
 
Uasherati ni tendo la hiari la kujamiiana kati ya watu ambao wote wawili si wanandoa kwa kila mmoja!
Uzinzi ni tendo la hiari la kujamiiana kati ya mtu ndoa na mpenzi zaidi ya mke/mume halali nje ya ndoa!
Yote ni machukizo mbele za Mungu!
 
Kitu au jambo lolote lile ambalo mungu amekataza mja, kwenda kinyume chake ni dhambi.
Kuzini lile tendo la kujamiiana na mwanamke ambaye si mkeo. Uashirati kwa ufupi ni sifa za mja ambaye hupenda kuzini.
Dini karibu zote ambazo zinaamini uwepo wa mungu na kuwa yeye ni muumba wa kila kitu[tunavyovijua na tusiyoyajua] zinaamini hivyo
Kweli mkuu hata kuogopa tu ni dhambi (maana amesema usiogope)
 
Back
Top Bottom