Tofauti kati ya Uasherati na Uzinzi?

Tofauti kati ya Uasherati na Uzinzi?

asante mwanalemi kwa ufumbuzi wako mzuri, embu sasa nielekeze nikasome huo mstari wa biblia unaokataza uasherati na ukatanguliwa na neno amri.
Mapi japo sijakuelewa vizuri, mistari iko mingi na humu imetajwa mingi "ukatanguliwa na neno amri" ndipo tatizo langu sijaelewa. Hata hivyo Mapi kama mtu anasoma Biblia na anaiamini basi kila akisomacho humo ni amri ya Mungu akitenda kinyume na jinsi linavyosema lile neno basi anastahili adhabu, kama imeandikwa usizini wewe ukazini unastahili hukumu.
 
Uasherati ni tabia ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na watu wengi wengi (promiscuity)

Uzinzi ni neno pana linalojumuisha maana kadhaa hivi ila mbili za muhimu zaidi
1. Kufanya mapenzi (kwa mtu aliye ktk ndoa) na mtu ambaye si mkeo/mmeo (adultery)
2. Watu ambao hawajaoana kufanya mapenzi (fornication)

Kwahiyo unaweza kuwa mzinzi bila kuwa muasherati ila muasherati ni mzinzi
Kikubwa ni kwamba vyote vinatumia reproductive organs. Na hapo ndo dhambi inaanzia.
 
Habari wakuu,tukumbushane kidogo kuhusu maandiko juu ya kichwa cha mada hapo juu..

Je ipi ni dhambi kutokana na maandiko na amri za mungu..?!

Karibu kujifunza..

Kwako Ph-25:
Awali ya yote niweke wazi kuwa dhambi hazitokani tu na "Amri Kumi za Mungu" bali kila lisilo la haki ni DHAMBI, 1Yoh 5:17.
Tofauti ipo kati ya Uasherati na Uzinzi ingawa tendo lenyewe linafanana. Uasherati ni kufanya tendo la ndoa kwa mwanaume asiye na ndoa na anafanya tendo hilo na mwanamke asiye na ndoa (au mwanamke asiye na ndoa kufanya tendo la ndoa na mwanaume asiye na ndoa). Kufanya uzinzi ni pale mtu mwenye ndoa anapofanya tendo la ndoa na mtu aliye na ndoa au asiye na ndoa. NDOA ni mkataba. Kwenda nje ya ndoa ni sawa na kuvunja mkataba. Mtu asiye na ndoa kwenda kufanya tendo la ndoa na mtu mwenye ndoa huo ni uzinzi pia kwani, kuna mmoja wao anavunja mkataba na yule aliye na ndoa naye.

Wengine wanaeleza kuwa uasherati ni kufanya tendo la ndoa na wapenzi wengi. Lakini msingi mkuu wa "uasherati" ni kufanyika kwa tendo la ndoa kwa watu wasio katika ndoa. Kufanya tendo la ndoa na wapenzi wengi huo ni umalaya au ukahaba (kwa Kiingereza ni "promiscuity"). Uasherati kwa Kiingereza ni "fornication" na Uzinzi kwa Kiingereza ni "adultery". Moja ya ushahidi wa kuwa uasherati na uzinzi ni tofauti ni neno hili 1Korintho 6:9-10. Hapa waasherati na wazinzi wametajwa kila moja peke yake katika mstari moja , wa 9.

Katika Biblia Takatifu, neno UZINZI limetajwa sehemu nyingine likimaanisha kuvunja maagano na Mungu. Kwa leo muda haunitoshi, ninaweza kurejea siku nyingine. Ninakuachia "HOMEWORK (KAZI YA KWENDA KUJISOMEA)": "Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo ..., Mithali 6:32. Halafu soma kisa cha "...kijana moja asiyekuwa na akili..." Mithali Sura yote ya 7. Jemak.
 
Back
Top Bottom