Tido Mhando aula Al Jazeeera

Tido Mhando aula Al Jazeeera

- People, please suala la Tido na TBC lilikuwa ni la ajira na sio siasa, ni mambo madogo madogo kama haya ndio yanaturudisha nyuma sana hili taifa na huenda ni kwa sababu ya umasikini zaidi kwa sababu kazi yoyote unayoipata kwa ajira ya mkataba, maana yake ni kwamba mkataba ukiiisha umeisha ni uamuzi wa muajiri wako kuamua kama atakuongeza muda au hapana na wewe muajiriwa unatakiwa kuwa umejitayarisha kubaki au kuondoka!

- Tanzania tumezoea hisia za kuhamia kabisa kwenye kazi tulizoajiriwa kwa mkataba na kuamini kwamba ni zetu na ni lazima waongeze tu mkataba ukiiisha, hapana people waajiri wako wana haki kisheria kwenda njia tofauti kama wanaona hauko sawa na line yao ya sababu za kuwepo kwao kwenye biashara, inatakiwa kuwa kawaida sana hiyo na nothing to do na anything, Tido who is my very good friend, aliajiriwa na TBC kwa mkataba ambao uliiishia kwenye ku-renew, waajiri wake wakasema hawamuhitaji tena kwa sababu wanataka kwenda njia tofauti, sasa what is the problem hapo?

- I mean kwa mwendo huu Tanzania, itatuchukua muda mrefu sana kuendelea, umeona juzi Oprah, mkataba umeisha na ABC, ameamua kwenda njia yake mwenyewe badala ya kulilia kupewa mpya, ndio maana ya mkataba Lebron, mkataba ulipoisha na Cleveland, akaamua kwenda The Heat, ndio maana ya mkataba wa ajira, TBC hawakumkosea Tido na wala Tido mwenyewe hajawahi kulalalmika kwamba amekosewa!


- So what is the fuss for?

Willie @ NYC, USA.

Kwa ajira za mkataba wa muda maalum kama wa Tido, inapokaribia kuisha ni lazima mwajiri kumtaarifu mwajiriwa endapo hatamuhitaji tena (hata renew) walau mwezi mmoja kabla, na kwa mikataba ya serikali, angalau miezi sita kabla. Kunyamaza kimya kuna maanisha kwamba mkataba utakua renewed. Hata Serikali yenyewe haikua imejiandaa maana iliwachukua muda kumpata mrithi wake. Nakumbuka hata watangazaji siku hiyo walikua na huzuni sana na asubuhi yake ktk kipindi cha magezeti, habari ya Tido hawakuisoma pamoja na kwamba ilipewa uzito mkubwa kwenye magazeti yote.

Tido ni mtu mzima, proffessional, mstaarabu na alikuja kusaidia na kwa kweli amefanya kazi nzuri, asingeweza kulalamika. Alichokifanya ni kuangalia mbele. Kutokulalamika haina maana kwamba alitendewa haki eti kwa sababu mkataba uliisha.
 
WanaJF nimewahi kusikia kwamba yule Mtangazaji wa AJE idhaa ya Kiingereza (kabla alikuwa CNN) Bwana Riz Khan ni Mtanzania Mwenye Asili ya Kiasia, kuna ukweli wowote?
 
Team ya Manchester City inamilikiwa na Mwarabu Mwislam; Kocha wake ni Mwarabu Mwislam, Dr. wa team ni Mwarabu Mwislam na wachezaji wote wa team ni Waarabu Waislam!! Nani anabisha?
Tehe! Tehe !! Hapo umemuweza huyo kichwa maji!!
 
Tido mashine ya ukweli na kama CDM ingelikuwa tayari na Tv huyu jamaa angetufaa sana...ng'ombe hazeeki maini kaka Tido we kaza uzi
 
TIDO hongera sana, Mungu hamtupi mja wake, hata hao magamba wangekufitini vipi wewe ni KICHWA siyo MKIA. Ila uwe makini na imani zako haba, na huko watakutoa tena wakikuahidi kititia cha nguvu usikubali. sikiliza roho yako inakokupeleka.

Ki ukweli nimefurahi, siasa hizi unaleta kwenye maisha ya mtu siyo kitu kizuri sana. Unamto amtu kwenye neema yake halafu unamfitini.

Tuko pamoja kaka.
 
-...Tido who is my very good friend, aliajiriwa na TBC kwa mkataba ambao uliiishia kwenye ku-renew, waajiri wake wakasema hawamuhitaji tena kwa sababu wanataka kwenda njia tofauti, sasa what is the problem hapo? Willie @ NYC, USA.
Penye njia tofauti hapo ndo nimepapenda.Najiuliza ni njia ya TvT au ya kuipendelea sana serikali na chama tawala? Hili ni shirika la umma, kila mtanzania ana-interest nalo, na watz wengi wanakubali kwamba Tirdo aliliendesha kwa weledi na ufanisi mkubwa, kutoka TvT isiyo na mvuto na iliyokuwa nyuma kiteknolojia hadi kuwa TBC inayowavutia hata waandishi(watangazaji) kutoka vituo vingine kujiunga nayo.

TBC ya Mhando iliwabana kwa kiasi fulani wapinzani(the playing field was not level), TBC ya leo inawakandamiza wapinzani. Kwa kasi waliyoanza nayo TBC ya kuona kama wapinzani ni maadui wa watz, they are heading the way of a Dodo, just like ATCL!
 
Mungu Mkubwa safi sana nadhani atahamasisha utawala bora na kupinga sera za kinafiki kwa viongozi wa tanzania na afrika, pia atasaidia kutoa ajira kwa watz walionda shule wakaelimika sio kina kobonde na umbumbu wao.safi sana iseeeee.
 
Back
Top Bottom