PreGE2025 THRDC: Tumesikitishwa na kukamatwa kwa Lissu na kufunguliwa kesi ya uhaini, DPP aondoe shtaka hilo Mahakamani

PreGE2025 THRDC: Tumesikitishwa na kukamatwa kwa Lissu na kufunguliwa kesi ya uhaini, DPP aondoe shtaka hilo Mahakamani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umesikitishwa na kukamatwa na kufunguliwa kesi ya uhaini, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Tundu Lissu, ambapo wametoa wito kwa mwendesha mashtaka kuondoa kesi hiyo au kubadili hati ya mashtaka ili kumuwezesha kuachiliwa kwa dhamana.

Akizungumzia suala hilo leo April 11, 2025 Mratibu THRDC Kitaifa, Wakili Onesmo Olengurumwa amesema kwamba mazingira na utaratibu uliotumika kumkamata Tundu Lissu haukuzingatia usalama wake, usalama wa raia waliokuwa kwenye Mkutano pamoja na usalama wa Polisi.

Olengurumwa amesema nguvu iliyotumika ni kubwa na yenye kuleta hofu kubwa kwa Wananchi kushiriki michakato ya uchaguzi. Ameeleza kuwa Jeshi la Polisi kama walijua kuna tuhuma dhidi ya Lissu wangemwita kwa wito au kumchukua kwa utaratibu rafiki wa kisheria nje ya eneo la Mkutano halali.

Aidha Mtandao umesema kuwa, hata maneno anayotuhumiwa kuyatamka hayana uzito mkubwa wa kufikia kuandikiwa kosa la uhaini.

"Uhaini ni kosa kubwa hapa nchini lisilokuwa dhamana na lenye adhabu ya kifo au maisha. Ni kosa ambalo kwa miaka mingi sasa hapa nchini halijawahi kutumika pengine kutokana na uzito wake."amesema Olengurumwa

Amesisitiza kwamba katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi ni dhahiri kuwa lazima kutakuwa na kauli mbalimbali kutoka kwa wanasiasa na wananchi, ambazo zinaweza zisiwapendezeshe makundi mengine au Serikali.

Amehasa kuwa katika mazingira hayo inahitaji watu kuwa na uvumilivu wa hali ya juu ili kuepuka kuvunja amani ya Nchi.
 
DPP ataliondoa ili baada ya msoto mkali na mateso mengi
 
Hatimaye wameibuka chama cha kupigania haki za mchongo wangapi wapo magerezani hatujasikia mkasikitika!
 
Huo ni mwanzo wa mwisho wa mateso kwa watanzania. Huyo ni mkombozi hawata mfanya lolote na wakimfanya chochote wategemee matokeo mabaya sana. Hawawezi ushindani
 
Hivi hawa kazi yao maalum ni ipi haswa?

Kutoa matamshi au?
 
Halafu usikute huko mliko huwa mnajifanya kutaka jeshi la polisi na mahakama viwe huru huku nyie hapa mnavishinikiza vifuate matakwa yenu na sio sheria.

Hamtaki jeshi na mahakama vifanye kazi zao kwa uhuru.

Lisu ni mwanasheria na pia ana mwanasheria wake.jeshi limefanya kazi yake kumkamata mtu anatangaza kufanya uasi na kumfikisha mahakamani kwa mujibu wa sheria.
mahakama ndio itaamua kulingana na utetezi wake kama ana hatia au la na sio kelele za zako au za watu wengine.
 
Ningekuwa na uwezo wanafiki hawa ningejitega ile wanatamka neno la kwanza tu 'BOOOOOOOM'! Wanafiki kweli kweli
 
Watanzania nani tena atuambie kuwa haya yanaoyoendelea ni uonevu kwa raia, kwa jamii na vyama vya kisiasa.

THRDC, TEC, Shura ya Maimanu, Msajili wa Vyama vya Siasa , Tundu Lissu, CHADEMA, ACT Wazalendo, CHAUMMA ya mzee Rungwe n.k wote hawa wanasema kuna uonevu lakini tumekaa bila kuchukua njia ya kisiasa kuingia barabarani kuandamana tunabusiri njia ya mfumo wa,haki jinai (criminal justice system) utupatie haki ! kweli ?
 
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umesikitishwa na kukamatwa na kufunguliwa kesi ya uhaini, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Tundu Lissu, ambapo wametoa wito kwa mwendesha mashtaka kuondoa kesi hiyo au kubadili hati ya mashtaka ili kumuwezesha kuachiliwa kwa dhamana.

Akizungumzia suala hilo leo April 11, 2025 Mratibu THRDC Kitaifa, Wakili Onesmo Olengurumwa amesema kwamba mazingira na utaratibu uliotumika kumkamata Tundu Lissu haukuzingatia usalama wake, usalama wa raia waliokuwa kwenye Mkutano pamoja na usalama wa Polisi.

Olengurumwa amesema nguvu iliyotumika ni kubwa na yenye kuleta hofu kubwa kwa Wananchi kushiriki michakato ya uchaguzi. Ameeleza kuwa Jeshi la Polisi kama walijua kuna tuhuma dhidi ya Lissu wangemwita kwa wito au kumchukua kwa utaratibu rafiki wa kisheria nje ya eneo la Mkutano halali.

Aidha Mtandao umesema kuwa, hata maneno anayotuhumiwa kuyatamka hayana uzito mkubwa wa kufikia kuandikiwa kosa la uhaini.

"Uhaini ni kosa kubwa hapa nchini lisilokuwa dhamana na lenye adhabu ya kifo au maisha. Ni kosa ambalo kwa miaka mingi sasa hapa nchini halijawahi kutumika pengine kutokana na uzito wake."amesema Olengurumwa

Amesisitiza kwamba katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi ni dhahiri kuwa lazima kutakuwa na kauli mbalimbali kutoka kwa wanasiasa na wananchi, ambazo zinaweza zisiwapendezeshe makundi mengine au Serikali.

Amehasa kuwa katika mazingira hayo inahitaji watu kuwa na uvumilivu wa hali ya juu ili kuepuka kuvunja amani ya Nchi.
Soon tutasikia Embassies
 
lakini tumekaa bila kuchukua njia ya kisiasa kuingia barabarani kuandamana tunabusiri njia ya mfumo wa,haki jinai (criminal justice system) utupatie haki ! kweli ?
Anza wewe na familia yako Mkuu, tutafuatia.
 
Back
Top Bottom