This is too much, Morogoro to Mwanza 17 hours

This is too much, Morogoro to Mwanza 17 hours

Hebu soma vizuri nilichoandika hapo nyuma sababu kuu ya sheria hiyo na vile vile niliwaomba mfanye utafiti ili tujue hasa tatizo nini? na vile vile ninaweka utafiti wa wataalam kuhusu ajali hizo. Hivi bado hujapata picha???? Soma tafakari halafu tujadili
Umewahi kutumia basi kwenye hizo nchi za wenzetu? Kwa barabara kama za hapa mwendo ni kama anaotaka magu. 15. 30. 50 na 80 max.
 
Binafsi napenda mwendo pole na Niko makini sana ikiwa dreva atakiuka, kama unataka kuwahi nunua gari lako binafsi
 
tatizo la ajali sio mwendo kasi peke yake gari nyingi ni mbovu kuanzia matairi hadi engine, pia kuna malori yamebadirishwa kuwa mabsi kiukweli safari ya mwanza dar inakera
Wenye akili tu ndo watakuelewa.... Kuna maskini uchwara wanafuahia sana hii. They don't care about time management
 
ETI !!!!!!! TRUNK ROADS ZETU ZOTE NCHINI ZINAKIDHI VIWANGO VYA KIMATAIFA!!! ACHENI SIASA FANYENI UTAFITI HALAFU MUANDIKE
Kweli wewe ni Abunwasi... Barabara zetu kwa akiri yako kabisa ziko salaama, au unaongea tu....?? Chalinze Segera tu unaona hiyo barabara ni salaama?? Hata Kimara Posta tu barabara hiyo iko salaama?? Watembea kwa baiskeli, miguu, nk wanapita wapi. Tumia akiri brother usiropokeropoke tu. Unaudhi sana
 
Ni kitu kizuri kwa kweli....

Kama uliyoyaeleza ni ya kweli!!!
Maana ajali nazo zimepungua kwa kiasi chake
 
Kweli wewe ni Abunwasi... Barabara zetu kwa akiri yako kabisa ziko salaama, au unaongea tu....?? Chalinze Segera tu unaona hiyo barabara ni salaama?? Hata Kimara Posta tu barabara hiyo iko salaama?? Watembea kwa baiskeli, miguu, nk wanapita wapi. Tumia akiri brother usiropokeropoke tu. Unaudhi sana
Mimi ni Abunwasi wewe ni nani? Take chalinze- segerea in the context of all trunk roads in the country and tell me.
You guys are emotionally charge to the extent that you can not think rationally[i am sorry for this statement]. If you will read carefully my contribution to the thread together with a portion of research on TZ accident. Someni thread vizuri,tafakari halafu andika. Kwa bahati mbya mmgeuza JF kuwa kama FB na mmelifanya jamvi hili kuwa la kawaida kiasi kwamba hata wale nguli ambao tafakuri zao[hata kama tulikuwa hatukubaliani nazo] zilikuwa zinatufanya kuchemsha bongo, kufanya utafiti na kutoa mchango. siku hizi mtu akikosa usingizi and hana kitu cha kufanya anakimbilia humu WHAT A SHAME
 
Me nadhani Kuna umuhimu wa kupitia sharia zetu.. wangeruhusu basi zitembee usiku kucha unatoka zako ubungo saa 1 usiku unaingiaa mwanza asubuhi tu.
Mkuu umewafikiria na wanaopandia njiani?
 
Jombaaa ungeisubiri kisbo,kiboko ya njia ya mwanza,kulala njianlabda gar liharibike,lakin ukitoka dar mwanza,,au mwanza dar kumbuka lakin ulale kwako ukitumia kisbo au kibo
 
973fce6e5b6cbf6da823d42cc52f0886.jpg


Serikali jengeni Barabara kama hizi. Tunataka kuwai muda ni muhimu
 
Duuuh kweli utawala wa Magufuli umekuja kutukazia sheria zilizokua zinavunjwa miaka nenda rudi

Safari za kutoka DSM/Morogoro kwenda mikoa ya kanda ya ziwa kama Mwanza zimekua ndefu mno siku za hivi karibuni

Nimetumia takribani masaa 17 kutoka Moro kwenda Mwanza

Safari inachosha sana na ukifika kwenye Zebra hata kama hakuna mtu anavuka simama atleast Dk 1 au sekunde kadhaa then endelea kukanyaga mafuta

Madereva wa mabasi wamepewa masharti watembee speed 50 mpaka 80 ukizidisha fine au uwe umetoa rushwa.

Yani MTU anatoka DSM kwenda Washington kwa ndege kama Boeing au Airbus anawahi kufika lakini wewe wa kutoka Daslam au Moro kwenda Mwanza bado tu unahangaika na siti yako

Bora kupanda pangaboi walahi nasema.
Kweli aise. Nilitoka Mwanza-Arusha ila nilishuka Makuyuni ulikuwa Kama saa 12 jioni.
 
Mkifa mnalalamika
Kama kuna mtu ambaye ajawai au Ndugu yake kupata ajali lazima atatetea ujinga Sana huu
Nachukua nafasi j
Hii Sana kuipongeza serekali Sana
Jeshi la police pongezi zenu Sana Ndugu zangu kwa kazi zuri
 
Kuna haja ya kujiamini kuwa Watanzania wanayaweza Yale tunayoyaona mwingine. Haileti maana kujenga barabara nzuri halafu ukazijaza matuta. Waadhibu wanaokiuka sheria za barabarani, madereva na watumiaji wengine hata waenda kwa miguu. Kuna faida gani ya kuwa na highway halafu ukaendesha kama uko barabara ya kokoto? Weka vizuizi pale ambapo barabara inakatizwa na treni. Zamani ilikuwa hivyo. Sasa kuna ugumu gani? Tuache njia za mkato badala yake tukazie utii wa sheria kwa kila MTU.
 
Kweli nimeamini sisi watanzania ni washenzi tu. Maana enzi tunakufa kama nzige tulikuwa tunatoa lawama kwa serikali, haya wamedhibiti speed mnaanza kulaum tena. Wakiruhusu msafiri na usiku gari likitekwa, ama ajali itokee usiku msaada hautapatikana on the go mtalaumu tu. Nawaona full matatizo
 
Back
Top Bottom