This is Rostam I know... The Story Behind the Man

This is Rostam I know... The Story Behind the Man



HII NDIO TAARIFA YA GAZETI LA KULIKONI TOLEO LA LEO KUHUSU UTAJIRI TATA WA ROSTAM AZIZ:

MJADALA kuhusu utajiri tata alionao mbunge wa Igunga, Rostam Aziz sasa umevuka mipaka kufuatia jarida la kimataifa liitwalo 'Africa Intelligence' kuhoji biashara lilizoziita kuwa ni za kizani zinazoendeshwa na mbunge huyo, huku likisema kuwa biashara za mwanasiasa huyo ambaye pia ni mfanyabiashara zinaacha maswali mengi kuliko majibu.

Katika toleo lake la hivi karibuni, jarida hilo ambalo pia linapatikana kwenye mtandao wa 'internet' linabainisha kuwa utata kuhusu biashara za Rostam unachagizwa na jina lake kutoonekana katika kampuni hata zile anazozimiliki.

"Mfanyabiashara Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni chama tawala ambaye pia aliwahi kudhaniwa na Bunge kuhusika katika tuhuma kadhaa za ufisadi, pia ni mwanzishaji wa kampuni mahiri," inasomeka sehemu ya makala kuhusu Rostam katika jarida hilo na kumwelezea kuwa ni "mfanyabiashara asiyeeleweka".

"Wakati anapoanzisha (Rostam) kampuni mpya mara nyingi hucheza na majina. Licha ya kuwa mmiliki wa kampuni kadhaa, ambazo baadhi yake zina anwani na/au namba za simu zinazofanana, jina lake hutokea katika kampuni moja tu iitwayo 'African Trade Development (T) Ltd (ATDL)."

Kwa mujibu wa nyaraka zilizopo katika ofisi za Wakala wa Usajili wa Leseni za Makampuni (Brela) kuhusu kampuni hiyo, yeye ameorodheshwa kama mmoja wa wakurugenzi wa ATDL lakini kwa jina la Rostam Sakarri, linaelezea jarida la Africa Intelligence.

"Katika kampuni nyingine zote wakurugenzi wake pia wana majina yanayoshabihiana na jina la Rostam kwa namna moja au nyingine ambayo ni kama; Rostom A. Sakarr, Rustom Aziz Sakarr, Rustam Sakarri and Rustam Sakaari," inafafanua makala hiyo.

Jarida hilo limeendelea kubainisha kwamba katika orodha ya wanahisa wa kampuni nyingine Rostam huonekana kujificha katika kivuli cha majina yenye asili ya Iran kama vile Chakaar na Mehrab.

Jina la Rostam Aziz halijitokezi kabisa katika nyaraka za Brela hata walau kwa nusu ya kampuni ambazo zinapaswa kuwa chini ya umiliki wake kama vile Africa Tanneries Limited, Tanzania Leather Industries Limited, Wembere Hunting Safari Limited, Tanzania Packages Manufacturer Limited na hata ile inayofahamika sana inamilikiwa na yeye ya Caspian Construction Limited.

"Rostam Aziz alitangaza hadharani kwamba ameinunua kampuni ya Habari Corporation ambayo inachapisha magazeti kadhaa na inayoendesha chuo cha mafunzo ya uandishi wa habari cha MAMET," lilisema Africa Intelligence, na kuongeza ; "Hata hivyo jina lake halionekani katika orodha ya wanahisa wa kampuni ya Isenegeja ambayo kimsingi ndiyo ilinunua kampuni hiyo ambayo baadaye ilibatizwa jina la New Habari (2006) Limited kwa ajili ya kuendelea na uchapishaji wa magazeti ambayo anaimiliki hadi sasa. Mambo ya kustaajabisha kweli!"

Jarida hilo linalochapishwa Paris nchini Ufaransa linasema mbunge huyo ambaye alikuwa mtunza hazina wa CCM Taifa "Sasa anawachanganya vichwa vigogo wa Chama cha Mapinduzi".

"Baadhi ya vigogo serikalini wanahisi kwamba Rostam alikuwa na mpango wa kuuza hisa zake katika kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom ili kupata fedha zitakazotumika katika mapambano ya uchaguzi mkuu wa 2010," linasema jarida hilo.

Utafiti uliofanywa na KULIKONI siku chache zilizopita, tuhuma zinazomwandama mfanyabiashara huyo hivi sasa zinaonekana kuharibu sifa ya chama tawala hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Mbali na kuwa mbunge wa jimbo la Igunga mkoani Tabora, Rostam pia ni mjumbe katika Kamati Kuu ya CCM.

Hivi sasa ni dhahiri kwamba umaarufu wa mwanasiasa huyo umekuwa ukipungua mbele ya vigogo wa chama chake cha CCM ambao kimsingi wanaamini kuwa atakuwa mzigo katika chama hicho.

Baadhi ya makada waandamizi ndani ya CCM wanabainisha kuwa wakati vigogo watatu wa kisiasa waliangushwa kufuatia kutajwa kuhusika katika kashfa ya ununuzi wa mitambo tata ya Richmond, Rostam pia alipaswa kuchukuliwa hatua kwani naye ni mmoja wa wahusika wakuu wa kashfa hiyo.

Taarifa ya Richmond ilisababisha kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wengine wawili ambao ni Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha.

Hata hivyo pamoja na kwamba alitajwa katika taarifa hiyo, Rostam bado anaendelea kushikilia nafasi nyeti katika chama chake licha ya maazimio yaliyopitishwa na Bunge kwamba wahusika wote waliotajwa waondolewe katika nafasi zao za chama na serikalini.

 
Nilishawahi kusema before kuwa Rostam anajua anachokifanya, kwa vile ni rais wa Chama Cha Mapinduzi hakuna lolote analoweza kufanywa na msaidizi wake ambaye ni mwenyekiti ndugu JK. Hakika wanangu mtatoza Kodi mpaka mchanganyikiwe hadi siku ya kiama
 
Habari yenyewe kutoka mtandaoni Africa Inteligence ni hii hapa

TANZANIA
A truly mysterious businessman

The former treasurer of the government party, Rostam Aziz, cultivates an air of mystery. His name often does not even appear in the companies he owns.

The businessman Rostam Aziz, an MP for the Chama cha Mapinduzi (CCM, governing party), under suspicion by Parliament of being involved in several recent scandals, is also a fervent company creator. When he forms new companies, he gives the impression of juggling with the names. Although he owns around a dozen companies, some of which have the same address and/or phone number, his name only appears clearly on one of them, African Trade Development (T) Ltd (ATDL). Even then, in the Business Registration and Licensing Agency (Brela) document concerning this company, he is listed as a director of ATDL but under the name Rostam Sakarri. All of the company's other directors have fairly similar sounding names that are more or less derived from his: Rostom A. Sakarr, Rustom Aziz Sakarr, Rustam Sakarri and Rustam Sakaari. On the shareholder lists of other companies, the Tanzanian businessman appears to hide behind Iranian sounding names like Chakaar and Mehrab.

Nor is the name Rostam Aziz listed on Brela documents of at least half a dozen other companies which are supposed to belong to him, such as Africa Tanneries Ltd, Tanzania Leather Industries Ltd, Wembere Hunting Safari Ltd, Tanzania Packages Manufacturer Ltd and even the most well-known of them, Caspian Construction Ltd. Rostam Aziz has publicly stated that he has acquired Habari Corporation Ltd (HCL), a company publishing several newspapers and the proprietor of the media training institute Mamet. However, his name does not appear on the list of shareholders of Isenegeja Ltd which effected this purchase, nor on that of New Habari (2006) Ltd which was created to run this press company and which he nevertheless claims to own. A mystery indeed!
 
Inaweza ikasaidia sana kudodosa ukweli wa mambo, kama ilivyokuwa kwa tuhuma za ununuzi wa Radar...... keep it up "Magazeti ya Kimatatifa"
 
Kweli urafiki washinda undugu! wahenga walisema. Yaani Kikwete bado kang'ang'ania gunia la miiba!
 
Duuu ni balaa kama hata ..............walio nje wameshajuaa ni balaaa
 
Duuu ni balaa kama hata ..............walio nje wameshajuaa ni balaaa

Inaweza ikathibitisha usemi wa zamani wa mwalimu wangu kuwa, mbio za panya sakafuni, huwa zinaishia ukingoni.Yes, kuna mwisho katika kila kitu, ingawa sijui mwisho wa maisha ya ujanja ujanja kama wa huyu bwana unakuwaje.
Nahisi as time goes on, he becomes more exposed. He will have to fight galantly to survive. Hatakuwa muwekezaji kama anavyotaka aonekane. Atakuwa anaangaliwa kwa mashaka mashaka.Sidhani kama bado Chama kitaendelea kumbeba mana utakuwa mzigo mzito ambao mtu yoyote mwenye akili timamu hatataka kuushiriki.Dawa ni kubadilika. Times change.
 
tunaompiga vita tunaambiwa sie wabaguzi....na hao wa nje ni wabaguzi? RA alaaniwe wana JF sasa nashauri tufunge siku 7 kumuomba mwenyezi Mungu ampe adhabu kali Rostam Aziz
 
tunaompiga vita tunaambiwa sie wabaguzi....na hao wa nje ni wabaguzi? RA alaaniwe wana JF sasa nashauri tufunge siku 7 kumuomba mwenyezi Mungu ampe adhabu kali Rostam Aziz
Hili nalo neno mkuu. Huyu bwana anafanya mind zetu ziwe obsessed naye tu. Tunasahau kufikiria maendeleo ambayo tunayahitaji sana
 
tunaompiga vita tunaambiwa sie wabaguzi....na hao wa nje ni wabaguzi? RA alaaniwe wana JF sasa nashauri tufunge siku 7 kumuomba mwenyezi Mungu ampe adhabu kali Rostam Aziz

Huyu bwana bingwa wa kushtaki, let us hope that atawashitaki hata hawa "African Intelligence"
 
Last edited:
RA alaaniwe wana JF sasa nashauri tufunge siku 7 kumuomba mwenyezi Mungu ampe adhabu kali Rostam Aziz

Maneno mazuri but kumbuka mara nyingi dua la kuku halimpati mwewe.......so the best thing we can do kuondoa hii mambo yote, ni kuhakikisha the current regime inakuwa thrown out....hapa nguvu ya raia waliofunguka macho wanaweza kufanya hivyo.....!

Vinginevyo tutabakia tukilialia huku hawa mwewe wakiendelea kudonoa vifaranga vyetu the way they like na hawataishia kizazi hiki tu, hao mwewe wanazaliana so haya manyanyaso tutawarithisha na wajukuu, vitukuu, vilembwe........vyetu!
 
Hapa anazungumziwa ROSTAM AZIZ mwanasiasa na mfanyabiashara 'hatari' aliyejipatia fedha nyingi Tanzania kwa kutumia udhaifu wa viongozi na wananchi wake waliolala fofofo huku nchi yao ikitafunwa. Huyu hawezi kutumia jina lake kwenye makampuni yake kwa vile ana machale sana. Anajua kuna siku waTZ wataamka toka usingizini na kuanza kumshughulikia kutokana na kuwaibia.
Amevuna sana Tz na sasa taarifa zinasema anamiliki benki kadhaa nchi za nje ikiwemo Dubai. Pia ana vitega uchumi vingi vya kutisha katika nchi mbalimbali. Anawekeza nje kwa sababu anaajijua sio raia wa nchi hii na wakati wowote anaweza kutimkia kwao Iran au sehemu nyingine duniani ambako amenunua uraia.
Nashangazwa sana na baadhi ya waTz wenzetu kumtetea mtu huyu hatari, ambaye sasa anaanza kushtukiwa hata kimataifa.

Mkuu,
Hakuna anayemtetea RA.Tunachoongea hapa na uoga wetu wenyewe.Kama mtu anavielelezo na hayo mambo, basi nikwenda mahakamani.
 
RA analindwa kwa kuwa anakula na Viongozi wetu lakini ushahidi wa kimazingira uko wazi kuwa anaihujumu Nchi hii,ila kuna siku mirija yake ya unyonyaji itakatwa.Wana JF tumpelekee Rais Obama habari zake ili atusaidie kumkamata gaidi huyu wa uchumi wa TZ.
 
Kweli kabisa huyu ROSTAM AZIZ ni GAIDI wa uchumi wa Tz. Kama serikali ya JK inamlinda tutaomba msaada wa kimataifa ili akamatwe na kushtakiwa.
 
sasa kwanini BRELA hawafunuwi pazia (lifting the veil), wanangoja nn?
 
Takururu mpo!!!!Hii dunia ndogo sana...ukweli na uwazi utajidhihirisha wenyewe siku za karibuni. kilio cha watanzania si kilio cha wendawazimu eti!!!!
 
Mkuu,
Hakuna anayemtetea RA.Tunachoongea hapa na uoga wetu wenyewe.Kama mtu anavielelezo na hayo mambo, basi nikwenda mahakamani.

Tuna serikali tuliyoichagua ndio inatakiwa ifanye kazi hii....
 
Mzee yusuf makamaba siku zote alikuwa akihutubia watanzania na kusema ukitaka biashara zako ziende vizuri ni lazima ujiunge na chama cha mapinduzi .
 
Back
Top Bottom