Third terminal at Dar es Salaam airport

Third terminal at Dar es Salaam airport

Mimi sijui wakubwa wa nchi hii mipango yao wanaiiga kutoka taifa gani dhaifu. Huwezi kuwa na uwanja wa kuhudumia watu milioni sita wakati kasi ya uwekezaji inatisha. Miaka miwili baadaye watabomoa! Kuna mahali tumemkosea Mungu.

Umenena mkuu.
Na huu ni ugonjwa upo in all sectors of our economy and government.
Wataalam ndio hao hao waliobuni miundombinu ya ajabu ya afya, elimu, ardhi etc etc.... Kila sehemu ni majanga matupu.

Kiwanja cha ndege sio majengo tu. Kuna runway/s ambazo ndio muhimu zaidi. Kwa nafasi iliyopo JKNIA hakuna nafasi ya kuongeza urefu wa runway iliyopo au kujenga mpya kabisa. Kuna reli ya Tazara imeizingira airport kwa upande upande Jet club na Kitunda.
Runway iliyopo ni fupi mno. Ndege kubwa za masafa marefu haziwezi kuruka na maximum load bila kupitia mji mwingine kuongeza mafuta.
Kuna mapungufu mengi mno ya waziwazi kabisa. Wataalam mburura wa UPE ndio wenye maamuzi haya ya ajabu ajabu.

Wakoloni waliona haja ya kujenga Dar Airport kwenye miaka ya 50s. Walihamisha kutoka eneo la mwanzo...
KUNA ANAEJUA AIRPORT YA KWANZA DAR ILIKUWA WAPI???
Jibu kesho!
 
Heathrow ya TZ mkuu,,,kwani Arusha si ni Geneva ya Afrika,,,hutaki jinyonge mkuu.
mkada, kwanini unataka nijinyonge?
Au hupendi niione Tz yenye neema ikija?
wana CCM bwana, baada ya kuona mambo magumu @)!% sasa mnatamani dunia ijifukie kila mtu afe mmbaki nyie tu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Bukyanagandi.Ni kweli unachosema lakini hata hiyo Heathrow, ilianza na third terminal mwaka 2008 wakaongeza Terminal 5, hata London ukituwa unaona kama Gowdown kwa juu hebu angalia hapa chini uwanja wa Heathrow.
Yes, hata mimi nilikuja gundua kosa langu baadae kabisa - kumbe nilikuwa na angalia bird's eye view na sio jengo kwa uhalisia wake - thanks 4 the photo - naona ulipiga terminal 5. Je, ukupata tatizo na watu wa usalama!! Tukirudi kuhusu design ya third terminal ya uwanja wetu wa ndege, Mkuu bado nasisitiza kwamba design ya jengo la mwanzo yaani ndege zinapo park ukiangalia nyuma ya jengo hilo linaonekana limejengwa ki-godown/workshop regardless ya kama unaliangalia ukiwa angani au ukiwa aridhini unless kama sehemu ya chini ya jengo hilo imekuwa designed spefically kuhifadhi CARGO kubwa kubwa na sio baggages, kama ni hivyo hapo naweza kuhafikiana nao. Jengo la pili yake hilo kidogo limekuwa designed vizuri lakini not 2 my liking, nisijue wenzangu wanalionaje? Mkuu juzi juzi hapa Waziri Mkuu alikuwa Uchina na akakutana na Viongozi wa Kampuni kubwa ya kusafirisha abiria kwa ndege, kampuni hiyo hiyo inadesign na kujenga Terminals za Airport nchini mwao mpaka nchi za nje - mfano Merikani, sasa hawa jamaa wa Civil Aviation kwa nini awalinganishi design za hawa wa Holanzi/ma Brit na design za kampuni hii ya Kichina inayo sifika Duniani kote. Kama Waingereza wameona umuhimu wa kuomba Wachina waje kwao ku-redesign na Kujenga yard ya London Dock sisi tunashindwa nini kuwa-emulate i.e tujenge majengo yanayo vutia. Mimi ndio maoni yangu mkuu, ila naipa pongezi Serikali kwa dhamila yake nzuri ya kutaka kulifanya Taifa letu linonekana la ki-leo.
 
Haya ndio mfano typical wa namna viongozi wetu wanavyofikiria. Si mipango ya muda mrefu bali mazingira yanayowazunguka.
 
Ritz...
Airport ya mkoloni ni pale Leaders Club....
Jengo la bar ndio lilikuwa terminal..

Tukirudi kwenye mada.
Eneo liliopo kwa upande wa barabara ya Nyerere (Pugu road) labda bado ipo nafasi ya terminals na support structures.
Tatizo kubwa ni katika kufanya runway length extension au kujenga parallel runway. Dar airport runway haizidi futi 10,000 ambazo ni chache mno kisheria kwa ndege kubwa kuweza kuruka na uzito wa juu.... (High Take Off Gross Weight). Kama maendeleo yatakwenda vilivyo, ikifikia kuingiza abiria 3mill na kutoa 3mill, inamaanisha runway utilisation itakuwa overstretched.
Kama wataalam wangekuwa wabunifu wazuri, pale ni pa kuhama, wawaachie jeshi/domestic na VIPs kutumia.
 
Mbona sehemu ipo kubwa tu, Airport ya mkoloni ilikuwa Ferry pale karibu na Kanisa la St Joseph mwaka 1954 ndiyo wakaamia Ukonga.

Watanzania kweli tumelogwa! Yaan hiyo station ya train mnaita international airport""!! Kwa mipango hii, kwa chama hiki na mbulula wao wanaotetea ugoro huu humu tusali tu na kuomba maana hakuna kitu hapo! Ndo yaleyale kujenga uwanja wa taifa pembeni ya uwanja wa shamba la bibi matokeo yake huwezi ni kama shamba la bb hauna kazi! Lakin kama uwanja mpya ungejengwa Kibaha au mlandizi na shamba la bibi ungeboreshwa matokeo yangekuwa Chanya Kabisa,,,,
 
Hata mi ndio nashindwa kushangaa hapa...wamesahau mwanzo wa hesabu ni moja....sasa tunaongelea viwanja vya dunia ya kwanza na kutokujua kwa nini chetu ni simple...pesa...pesaaa....


Usiige kunya kwa tembo.
Huo unatutosha kutokana na uwezo wetu, tukitaka tujenge kama cha Cape town international airport, tutakula majani humu kama ilivyokua kwenye ununuzi wa ndege ya Rais
 
Hakuna kitu hapo, yaana runing ziko mbili! Kweli hiki ni kituko.
 
Huu uwanja wa Jomo Kenyatta ndiyo wakuutolea mifano wakati mweingine tuwe makini wanaukumbi hebu angalieni huu uwanja hapa chini amabao Mwita Maranya anautolea mifano kila kikicha.


Usilinganganishe Jomo Kenyatta airport na Mwl Nyerere airport , Jomo Kenyata kila baada ya dakika 20 ndege inaruka ,Mwl Nyerere airport ni kama airstrip tu
 
Kila kitu na wakati wake, sasa ndio mkataba umeshakamilishwa.

Yaani FaizaFoxy kukamilika kwa mkataba kumechukua miaka zaidi ya mitano!!!!

Ujenzi utachukua muda gani???

Kwa serikali yetu!!!..Afadhali tungeshughulika na Matatizo ya Umeme ...Ambao unagusa jamii kubwa zaidi...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ritz unapenda siasa!!! hata hii umeitupia huku!!

Mimi naamini hata wewe huridhiki na huo mchoro ..Ila ndio hakuna la kufanya..

Tanzania nchi ya maajabu sana...

Raia anaweza kumiliki Ndege lakini serikali haiwezi..

Pengine unge-binafsishwa tungepata bora kuliko huo tunao utarajia...
 
Last edited by a moderator:
Yaani FaizaFoxy kukamilika kwa mkataba kumechukua miaka zaidi ya mitano!!!!

Ujenzi utachukua muda gani???

Kwa serikali yetu!!!..Afadhali tungeshughulika na Matatizo ya Umeme ...Ambao unagusa jamii kubwa zaidi...

Umeme tayari umeshashughulikiwa na implementation za miradi mbali mbali ya umeme zimeshaanza, tembelea tovuti ya TANESCO ujionee.

Hii inayoongezwa ni terminal tu, kulikuwa kuna mambo mengi ya msingi, Airport zinazokuja Tanzania ni nyingi kuliko unavyofikiria. Hii ni solution ya muda wakati Airport tatu mpya za Kimataifa zikiwa kwenye pipeline.
 
  • Thanks
Reactions: prs
Go Tanzania Go,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,Love you Tanzania.Kitu kama Heathrow Airport

Kaka hii haifikii hata departure lounge moja ya Cairo airport! Naimanisha ukienda Cairo airport section a..ina A1 mpaka A30 that means means A ina departures lounge 30 na inaweza kuhandle ndege 30 kwa wakati mmoja. Na hapo wana a.b.c.d.f........... Hii terminal 3 haifikii hata nusu ya part A ya cairo airport.

Ninaloshangaa mimi viongozi wetu ni watembezi sana na wanajua jinsi international airports zinavyofanana! Till wanakubali kuwa hii itakuwa wonders!!!!!! Ni ajabu.. tunafikiria 5 years ahead not even 20 years!
 
Umeme tayari umeshashughulikiwa na implementation za miradi mbali mbali ya umeme zimeshaanza, tembelea tovuti ya TANESCO ujionee.

Hii inayoongezwa ni terminal tu, kulikuwa kuna mambo mengi ya msingi, Airport zinazokuja Tanzania ni nyingi kuliko unavyofikiria. Hii ni solution ya muda wakati Airport tatu mpya za Kimataifa zikiwa kwenye pipeline.
Mh!kama solution ya muda planning yake inachukua miaka 7 na utekelezaji bila shaka utachukua miaka si chini ya saba...basi hizo solutions za muda mrefu tutasubiri mpaka Yesu atakaporudi.
Haya twambie hizo airports mpya ni zipi?
Serikali yetu ina matatizo mengi...likiwemo kutopenda kusikia ushauri wa wataalam na kuweka siasa mbele..ona mbeya(songwe) airport..hadi fastjet ilkuwa imeshindwa kutua pale mpaka walifanya marekebisho ya ziada.unafikiri hiyo itaweza kupewa hadhi ya kimataifa.wakati tuliambiwa inajengwa international aiport!
 
Mbona sehemu ipo kubwa tu, Airport ya mkoloni ilikuwa Ferry pale karibu na Kanisa la St Joseph mwaka 1954 ndiyo wakaamia Ukonga.

No!sidhani km nafasi inatosha kihivyo!badala ya serikali kutumia nguvu kuhamisha watu na kulipa fidia!wangefikiria kuwa na uwanja nje ya jiji..na kweka miundombinu ya kuunganisha airport na jiji...km fast trains! For sure haya mawazo kuna kiongozi mwenye upeo atakuja na kufanya haya..na hawa viongozi wa sasa watajiona kama walichezea kodi za wananchi na kuwasumbua wananchi.

Sisi badala ya kuhamisha uwanja ukapelekwa nje ya mji tunahamisha wananchi na kuwapeleka nje ya mji! Si mawazo endelevu!!!!!
 
Mh!kama solution ya muda planning yake inachukua miaka 7 na utekelezaji bila shaka utachukua miaka si chini ya saba...basi hizo solutions za muda mrefu tutasubiri mpaka Yesu atakaporudi.
Haya twambie hizo airports mpya ni zipi?
Serikali yetu ina matatizo mengi...likiwemo kutopenda kusikia ushauri wa wataalam na kuweka siasa mbele..ona mbeya(songwe) airport..hadi fastjet ilkuwa imeshindwa kutua pale mpaka walifanya marekebisho ya ziada.unafikiri hiyo itaweza kupewa hadhi ya kimataifa.wakati tuliambiwa inajengwa international aiport!

Hivi unafikiri Rome ilijengwa siku moja?
 
Hivi unafikiri Rome ilijengwa siku moja?

Ndo tunavyopeana hopes kwa kutumia misemo kama hiyo!rome haikujengwa siku moja lakini bila shaka hiyo miaka 1000 ilipangwa! Sisi tunaangalia miaka 5 mbele..hatujamaliza planning tiyari mahitaji yameishaongezeka.hili linajidhihilisha hata katika maelezo yako katika post ya mwanzo!
 
Ndo tunavyopeana hopes kwa kutumia misemo kama hiyo!rome haikujengwa siku moja lakini bila shaka hiyo miaka 1000 ilipangwa! Sisi tunaangalia miaka 5 mbele..hatujamaliza planning tiyari mahitaji yameishaongezeka.hili linajidhihilisha hata katika maelezo yako katika post ya mwanzo!

Sasa fikiria 1,000 na Katanzania ketu, ndio kwanza kana miaka 49.

Halafu tuoneshe maendeleo ya Roma ya miaka 50 ya mwanzo tulinganishe.
 
Sasa fikiria 1,000 na Katanzania ketu, ndio kwanza kana miaka 49.

Halafu tuoneshe maendeleo ya Roma ya miaka 50 ya mwanzo tulinganishe.

kwa Tz hata tulizopata uhuru sawa hatulingani kiuchumi..Ingawa tumebarikiwa Rasilimali za kutosha..

Tumekuwa tukikaribiana kiuchumi na nchi kama Malaysia miaka ya 2000 mwanzoni..Lakini hivi sasa wametuacha mbali mnooo..Huku wakitegemea zao la....Mpira na Mafuta kidogo..

Tunahitaji kubadilisha mfumo..

Tatizo ni Leadership na sio Muda. FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom