Thibitisha kwamba HAKUNA MUNGU

Thibitisha kwamba HAKUNA MUNGU

Lazima mwizi ahukumiwe kwa mujibu wa sheria.

Mkimalizana hapohapo, utakuwa hutumii sheria, unatumia maamuzi yako binafsi. Kinyume na sheria.

Sasa nyie mlihakikisha vipi na mna uthibitisho upi wa kwamba Mungu yupo?

Maana mpaka kufikia kusema Mungu yupo, ina maana kuna aliyewahi kumshuhudia.

Sasa ni nani aliwahi kumshuhudia huyo Mungu?

Ni nani alimshuhudia huyo Mungu yupo, akahitimisha kweli yupo?

Mungu angekuwepo wala kusingekuwa na haja ya kuhoji uwepo wake, Kila mtu angejua kwa uhakika kabisa Mungu yupo bila utata na imani.

Kila mtu angejua Mungu yupo kwa uhakika kabisa bila imani.

Kisicho kuwepo ndio hakijulikani.

Kilichopo kinajulikana.

Sasa ninyi mnadai Mungu yupo, ina maana mnaju yupo.

Sasa mlijuaje yupo?

Mnathibitishaje yupo?

Tutajuaje kwamba kitu hakipo kwasababu ni kweli hakipo au kipo ila umekosekana tu uthibitisho wa ku prove kipo?"
Mimi ninao ushahidi kuwa Mungu yupo.Itatosha kumaliza hili au mpaka uone huo ushahidi?
 
It’s not about faith—logic doesn’t depend on belief. Contingent beings need a cause; an infinite regress is impossible. Therefore, there must be a Necessary Being—uncreated, without beginning. This is reasoning, not mere faith
How did you know there is necessary being?

Don't force your Allah to be a necessary being.

Prove how did you know there's necessary being?

And why only Allah is a cause not Jesus, not Zeus, not Krishna?
 
Ukitumia akili yako vizuri, kuna NGUVU KUBWA YA ASILI INAYOONGOZA HUU ULIMWENGU. Jina la hili nguvu silifahamu.Wewe unalifahamu??
Probably uko sahihi

Probably hiyo ni nguvu ambayo iko generated na ulimwengu wenyewe.

And probably hiyo nguvu sio Mungu ni kitu kingine tu ambacho watu bado hatujakijua.

Lakini kuipa sifa ya kusema iliiumba watu, ulimwengu, ina upendo wote, nguvu zote, ujuzi wote, iko kila mahali at the same time makazi yake rasmi ni juu sehemu inaitwa Mbinguni.

Kusema nguvu hii inahitaji kuabudiwa, kusifiwa tena kwa kuitolea na hela (hela iliyopewa jina la sadaka) na kwamba usipofanya hivyo nguvu hii itakuchoma moto wa milele.

Nadhani kwa decriptions hizi unakuwa beyond limit na hapo unakuwa huepuki swali langu la thibitisha Mungu yupo.
 
Tunajua kwa sababu ni mantiki, Logic, kila kiumbe contingent kina chanzo, msururu hauwezi kuwa usio na mwisho.

Hivyo lazima kuwe na Kiumbe wa Lazima—asiyeumbwa, asiye na mwanzo. Quran inathibitisha hili kwa maneno:
1.Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
2.Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
3.Hakuzaa wala hakuzaliwa.
4.Wala hana anaye fanana naye hata mmoja..
(Surah Al-Ikhlas 112).

Mantiki inathibitisha, na revelation inathibitisha
Mantiki haiambatani na contradiction

Mantiki inakataa kitu kuwepo bila chanzo.

Ngoja nikufikirishe.

Kwamba Mungu alikuwepo yeye kabla ya chochote si ndio?

Alikuwepo wapi?

Hapo alipokuwa paliumbwa na nani? Unaweza kunichorea picha kupitia maelezo nipate concept?

Kama alipaumba yeye maana yake hapo sio kabla ya chochote.

Au unaweza kunipa mfano wa kabla ya chochote ni upi?
 
Mzigo wa uthibitisho unamwangukia mdai wa hoja .
atheism inakataa dai lisilo thibitishwa , likithibishwa hakuna atakae kataa dai lako .
Jee kanuni ya uthibitisho kwamba Mungu yupo ni kanuni ile ile ya mkatale kwamba Mungu yupo?

Wanaosema Mungu yupo wanatumia kanuni sawa na wale wanaosema Mungu hayupo?
 
Sasa thibitisha Mungu yupo. Maana unakiri una ushahidi.
Hapa sitaji vifungu kiongozi.Ushahidi nilionao unaoneka.Hapa zitabaki porojo tu.Kama huko interested utanitafuta napatikana otherwise hapa hamtafika hitimisho.Binadamu pekee nayeweza kuprove kuwa Mungu yupo ni mimi lakini mpaka unione sio ushahidi wa maandishi au vifungu vya maneno ya watu wa kale hapana.Ni kitu kinachoonekana
 
Sijasema revelations zinatoa proof kwamba Mungu yupo.Haya sio maneno yangu.Nimesema revelations zote zinabaki kama Miongozo tu ya kusema Mungu yupo lakini haziwezi kuprove chochote.

Mungu kwangu ni muumbaji,na mamlaka iliyo juu ya mamlaka zote(nimechukua maneno kutoka kwenye vitabu vya dini sio maneno yangu)
Na mimi sijasema umedai revelations zinatoa proof, rudia tena kusoma nilichoandika utanielewa.

Umesema umechukua maneno hayo kutoka kwenye vitabu vya dini.

Kwa hiyo ni maneno ya kuaminika kwasababu yametoka kwenye vitabu vya dini?
 
Mantiki haiambatani na contradiction

Mantiki inakataa kitu kuwepo bila chanzo.

Ngoja nikufikirishe.

Kwamba Mungu alikuwepo yeye kabla ya chochote si ndio?

Alikuwepo wapi?

Hapo alipokuwa paliumbwa na nani? Unaweza kunichorea picha kupitia maelezo nipate concept?

Kama alipaumba yeye maana yake hapo sio kabla ya chochote.

Au unaweza kunipa mfano wa kabla ya chochote ni upi?

Swali lako lina kosa la msingi: ‘wapi’ na ‘kabla’ ni dhana za nafasi na muda.

Allah hakuwepo ndani ya muda wala nafasi—yeye ndiye aliyeumba muda na nafasi. Kuuliza ‘alikuwa wapi kabla’ ni kama kuuliza kaskazini ya kaskazini—ni contradiction ya mantiki
 
Yaani hapo tayari umeshaonyesha uelewa finyu wa mambo.

Kwa kuanzia tu, ambacho hakipo utathibitishaje kwamba hakipo?

Hapo tayari ushaonyesha uwezo mdogo wa kufikiri na kuchanganua mambo kwa mantiki.
Ufinyu wako wa kusoma na kuelewa mada ndiyo umekupotosha.

Unaposema kitu hakipo si lazima uoneshe ni kwa nini hakipo. Lazima kuwe na kanuni ya kuonesha kitu kipo ama hakipo.

Kwa mfano oxygen haionekani kwa macho lakini ipo. Huwezi kusema hakuna oksijeni bila ya kutumia vifaa vya kupimia oksijeni.

Hapa mjadala ni kanuni gani mnaosema hakuna Mungu mnatumia?

Kinachotakiwa ni kuelezea kimchakato na kikanuni mmefikiaje kusema hakuna Mungu.
 
Swali lako lina kosa la msingi: ‘wapi’ na ‘kabla’ ni dhana za nafasi na muda.

Allah hakuwepo ndani ya muda wala nafasi—yeye ndiye aliyeumba muda na nafasi. Kuuliza ‘alikuwa wapi kabla’ ni kama kuuliza kaskazini ya kaskazini—ni contradiction ya mantiki
That's the same description of something that does not exist

Hata kisichokuwepo kina sifa hizo hizo

Hakifungamani na nafasi wala muda zaidi ya dhana tu.
 
Na mimi sijasema umedai revelations zinatoa proof, rudia tena kusoma nilichoandika utanielewa.

Umesema umechukua maneno hayo kutoka kwenye vitabu vya dini.

Kwa hiyo ni maneno ya kuaminika kwasababu yametoka kwenye vitabu vya dini?
Ok,Mungu yupo.Mwenye kutaka proof anitafute.Anayetaka porojo anaweza kuendelea.Kiufupi huwezi kupata hitimisho hapa.Mbaya zaidi na wale watakao anza kuleta vifungu vya biblia au quran kujaribu kuprove uwepo wa Mungu hapo ndio hamtamaliza.Lakini kwa ambaye yuko interested ninao ushahidi tangible sema sio wa maandishi na hata nikikueleza hapa huwezi kuamini zitabaki porojo ukioniona unaweza kuelewa hili.
 
How did you know there is necessary being?

Don't force your Allah to be a necessary being.

Prove how did you know there's necessary being?

And why only Allah is a cause not Jesus, not Zeus, not Krishna?
A Necessary Being isn’t assumed—it’s concluded.

Contingent things exist, an infinite regress is impossible, so reason demands a self-existent cause.

Allah fits this by definition; Jesus, Zeus, and Krishna are contingent, dependent, and limited—so they cannot be the Necessary Being.
 
Yuko wapi sasa huyo mungu...?
Weka hata picha yake tumuone...
Kwa ivo wewe kwako mungu ni picha?

hanumaan-768x999.webp

Hii ni picha ya Mungu wa kihindu.
 
Back
Top Bottom