Prof Phraoh AI
JF-Expert Member
- Mar 25, 2024
- 1,268
- 2,310
Atheists wengi wanaposikia hoja ya Mungu kama Muumba wa ulimwengu wanajibu haraka kwamba "Ulimwengu ulikuwepo milele hauhitaji muumba."
Jibu hilo linaonekana rahisi. Linaonekana la akili. Linaonekana kama njia nzuri ya kukimbia swali zito.
Lakini ni sayansi sio mimi P h a r a o h sayansi yenyewe inakataa jibu hilo kwa nguvu kubwa.
ni sheria ya sayansi kua nishati haiwezi kuundwa wala kuharibiwa inabadilika tu kutoka hali moja kwenda nyingine.
Hii inamaanisha nini?
Nishati yote iliyopo sasa ilikuwepo tangu mwanzo. inachofanya ni ku badilika tu.
Swali linakuja moja kwa moja
Nishati hiyo yote ilianza wapi?
Kama ulimwengu ni wa milele nishati hiyo ilikuwepo milele. Lakini sheria ya pili inakuja na kulipiga jibu hilo chini kabisa na kuivunja vunja hoja ya atheist kwa ushahidi wa kisayansi
Sheria hiyo ya pili inasema ulimwengu unaelekea entropy disorder inayoongezeka siku zote kwenda mbele tu. Kila mchakato wa asili unapoteza nishati inayoweza kutumika.
Maana yake kwa lugha rahisi:
Kila kitu kinachofanya kazi jua, nyota, nishati yoyote polepole polepole inaisha. Inakwenda. Haiwezi kurudishwa
( hata jua letu siku moja litaisha )
Fikiria mshumaa unaowaka. Unaungua unapotea hauwezi kurudi kuwa mshumaa tena.
Vivyo hivyo nyota zinaungua na kutoweka. Nishati inapotea polepole. Ulimwengu unakwenda kuelekea heat death hali ya giza kamili ambapo hakuna nishati, hakuna mwendo, hakuna kitu.
Kama ulimwengu ungekuwa wa milele kwa wakati uliopita ungekuwa tayari umefika heat death.
Giza kamili. Hakuna nyota. Hakuna nishati. Hakuna chochote.
Lakini tuko hapa. Jua linawaka. Nyota zinaungua. Nishati ipo.
Hii inamaana moja tu mchakato huu haukuanza milele iliyopita. Ulianza mahali fulani.
Mwaka 1927 mwanasayansi Georges Lemaître aligundua kwamba ulimwengu unaendelea kupanuka.
Kama unapanuka sasa maana yake awali ulikuwa mdogo. Mdogo zaidi. Mdogo zaidi hadi mahali fulani palipokuwa na mwanzo.
Mwaka 1964 Arno Penzias na Robert Wilson wakigundua cosmic microwave background radiation mwangwi wa mlipuko wa mwanzo Big Bang.
Ushahidi haukuwa wa dini ulikuwa wa kisayansi kabisa. na walishinda Nobel prize
Stephen Hawking atheist na mwanasayansi mkubwa alikubali kwa kusema
"Almost everyone now believes that the universe, and time itself, had a beginning at the Big Bang."
Kama vitu vinaweza kuanza kuwepo bila chanzo basi kwa nini vitu vyote visianze kuwepo bila chanzo kila wakati bila mpangilio wowote?
Kwa nini tembo wasianze kutokea jikoni kwako sasa hivi bila chanzo?
Kama jibu lako ni haiwezekani umekubali vitu haviwezi kuanza from no where
Wengine husema basi na Mungu Lazima awe na chanzo hilo swali la ''Mungu alitoka wapi'' lina imagine kwamba Mungu ni kitu cha ndani ya ulimwengu kinachohitaji chanzo kama vitu vingine.
Lakini Mungu kwa definition ni Necessary Being kitu ambacho kipo kwa asili yake yenyewe kisichohitaji chanzo kingine.
Swali la kweli sio "Mungu alitoka wapi" bali "kwa nini Necessary Being lazima iwe Akili badala ya ulimwengu wa kimaada?"
Na jibu ni hili ulimwengu wa kimaada unaonyesha mwanzo Akili Kubwa hainyeshi mwanzo wowote.
Arno Penzias aliyegundua mwangwi wa Big Bang ambayo Big bang atheist wengi huitumiankama reference yao bila kujua inawakaba wenyewe
Aliyegundua alisema hivi:
"The best data we have are exactly what I would have predicted had I nothing to go on but the five books of Moses"
( alisema hana jibu zaidi ya hapo labda atumie Vitabu vitano vya musa (torati) )
Jibu hilo linaonekana rahisi. Linaonekana la akili. Linaonekana kama njia nzuri ya kukimbia swali zito.
Lakini ni sayansi sio mimi P h a r a o h sayansi yenyewe inakataa jibu hilo kwa nguvu kubwa.
ni sheria ya sayansi kua nishati haiwezi kuundwa wala kuharibiwa inabadilika tu kutoka hali moja kwenda nyingine.
Hii inamaanisha nini?
Nishati yote iliyopo sasa ilikuwepo tangu mwanzo. inachofanya ni ku badilika tu.
Swali linakuja moja kwa moja
Nishati hiyo yote ilianza wapi?
Kama ulimwengu ni wa milele nishati hiyo ilikuwepo milele. Lakini sheria ya pili inakuja na kulipiga jibu hilo chini kabisa na kuivunja vunja hoja ya atheist kwa ushahidi wa kisayansi
Sheria hiyo ya pili inasema ulimwengu unaelekea entropy disorder inayoongezeka siku zote kwenda mbele tu. Kila mchakato wa asili unapoteza nishati inayoweza kutumika.
Maana yake kwa lugha rahisi:
Kila kitu kinachofanya kazi jua, nyota, nishati yoyote polepole polepole inaisha. Inakwenda. Haiwezi kurudishwa
( hata jua letu siku moja litaisha )
Fikiria mshumaa unaowaka. Unaungua unapotea hauwezi kurudi kuwa mshumaa tena.
Vivyo hivyo nyota zinaungua na kutoweka. Nishati inapotea polepole. Ulimwengu unakwenda kuelekea heat death hali ya giza kamili ambapo hakuna nishati, hakuna mwendo, hakuna kitu.
Kama ulimwengu ungekuwa wa milele kwa wakati uliopita ungekuwa tayari umefika heat death.
Giza kamili. Hakuna nyota. Hakuna nishati. Hakuna chochote.
Lakini tuko hapa. Jua linawaka. Nyota zinaungua. Nishati ipo.
Hii inamaana moja tu mchakato huu haukuanza milele iliyopita. Ulianza mahali fulani.
Mwaka 1927 mwanasayansi Georges Lemaître aligundua kwamba ulimwengu unaendelea kupanuka.
Kama unapanuka sasa maana yake awali ulikuwa mdogo. Mdogo zaidi. Mdogo zaidi hadi mahali fulani palipokuwa na mwanzo.
Mwaka 1964 Arno Penzias na Robert Wilson wakigundua cosmic microwave background radiation mwangwi wa mlipuko wa mwanzo Big Bang.
Ushahidi haukuwa wa dini ulikuwa wa kisayansi kabisa. na walishinda Nobel prize
Stephen Hawking atheist na mwanasayansi mkubwa alikubali kwa kusema
"Almost everyone now believes that the universe, and time itself, had a beginning at the Big Bang."
Kama vitu vinaweza kuanza kuwepo bila chanzo basi kwa nini vitu vyote visianze kuwepo bila chanzo kila wakati bila mpangilio wowote?
Kwa nini tembo wasianze kutokea jikoni kwako sasa hivi bila chanzo?
Kama jibu lako ni haiwezekani umekubali vitu haviwezi kuanza from no where
Wengine husema basi na Mungu Lazima awe na chanzo hilo swali la ''Mungu alitoka wapi'' lina imagine kwamba Mungu ni kitu cha ndani ya ulimwengu kinachohitaji chanzo kama vitu vingine.
Lakini Mungu kwa definition ni Necessary Being kitu ambacho kipo kwa asili yake yenyewe kisichohitaji chanzo kingine.
Swali la kweli sio "Mungu alitoka wapi" bali "kwa nini Necessary Being lazima iwe Akili badala ya ulimwengu wa kimaada?"
Na jibu ni hili ulimwengu wa kimaada unaonyesha mwanzo Akili Kubwa hainyeshi mwanzo wowote.
Arno Penzias aliyegundua mwangwi wa Big Bang ambayo Big bang atheist wengi huitumiankama reference yao bila kujua inawakaba wenyewe
Aliyegundua alisema hivi:
"The best data we have are exactly what I would have predicted had I nothing to go on but the five books of Moses"
( alisema hana jibu zaidi ya hapo labda atumie Vitabu vitano vya musa (torati) )