The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Watu wanavyoukwaa Urais:

. kwa uroho na uchu wa cheo
. kwa ajali ya mkuu wake
. kwa kusukumwa na wezi na mafisadi
. kwa kukubalika na watu wakiamini anaweza
. kwa kujititimua mtu mwenyewe akijua ataweza,
. kwa kukosa kazi nyingine ya kufanya maana zote kubwa kamaliza,
. kwa kujiona ana elimu na maarifa tosha kuongoza,
. kwa kuchaguliwa na viongozi wa dini,
. kwa kuchaguliwa na vijana,
. kwa kuchaguliwa na wazee,
. kwa kuchaguliwa na wanawakae,
. kwa kuchaguliwa na wajinga,
. kwa kuchaguliwa na shetani,
. kwa kuchaguliwa na Mungu.

Mwenye kazi ngumu sana ni huyu wa mwisho. Atataka kweli kuongoza watu kwenye njia iliyonyooka lakini siku zote atakuwa akishindana na mashetani wa kweli na mashetani watu. Hawa wengine kazi yao ni rahiiisi, kwani kazi yake inakuwa ni kulipa fadhila au kutoa ahadi tu!

Wa mwisho ni rahisi kukataa kuendelea kuwa Rais. Lakini anayechaguliwa kwa njia hizo zingine ataamini yeye tu ndiye anayefaa Urais.

Wa mwisho anajua Mungu kampa watu kuwatumia. Atawatumia kuongoza vyema nchi. Lakini aliyeupata kwa njia hizo zingine sikuzote atajifanya yeye Mungu na walio chini yake watu. Hushindwa kuongoza vizruri na akaishia kufanya madudu mwanzo mpaka mwisho.

Wa mwisho huamini anayeiongoza nchi ni Mungu naye kapewa kufanya kazi ya Mungu. Yule anayekuja kwa njia nyingine huamini yeye ndiye anayeiongoza nchi.

Wa mwisho hufahamu yeye ni binadamu wa kawaida na hana ubora wowote kwa wacha Mungu. Wa aina nyingine huamini yeye ni bora zaidi na mtakatifu na wengine ni watu wa kawaida. Hujenga pepo ya duniani huku akibomoa pepo ya akhera!
Wa mwisho hadanganyi. Na hasemi uongo. Wa njia nyingine hudhani kazi yake ni kudanganya na uongo. Hatimaye hujidanganya hata yeye mwenyewe.
 
Shibuda tena. Basi kazi ipo hapo mwakani.

Dr Barubaru
 
Nawasalimu wana JF,baada ya kuwa mtazamaji na msomaji kwa muda mrefu sasa nadhani ni wakati muafaka kwangu kuwa mchangiaji ili kuijenga nchi yangu. Kwa kuanza ni hili la wana Ccm kuanza kuongelea nani atakuwa mgombea ndani ya chama chao, kila mmoja anapaswa kujua kipindi hiki ni cha kuijenga nchi yetu na kujiletea maendeleo, wakati ukifika kiongozi atajulikana.
 
Dokezo. Lile kundi la tatu nililosema ni la Wenyeviti Wastaafu wa Mikoa wa CCM likimjumlisha mzee Pancras Ndejembi, Hemed Mkali na wengineo!

Wazee hao wamesema kuwa wanataka utamaduni wa Chama chao wa kumpa raisi aliye madarakani miaka 10 ya utawala udumishwe na hawaoni alichokosa mheshimiwa JMK hadi wanachama watake kumpa miaka mitano tu!
 
I was too astonished,apparently we have a lot of stuffs to do in this wicked country but all what we can do is just gather ourselves na kuongelea uchaguzi wa miezi zaidi ya kumi na nane mbele?

I dont see the point of all of these,kwa wanasiasa ni mtaji tosha but je faida ya kwa hawa vijana wa DODOMA, wakina mama wa Moshi na wazee wa Pwani, Dodoma na Dar kuna tija gani hapa?

Let us unite so that we can overcome our prevailling challenges,UCHAGUZI BAADAE. GOD BLESS BLACK SKIN.
 
Tatizo la Tanzania ni njaa kali na watu mbalimbali kujipendekeza kwa watawala kama njia ya kujipatia/kujihakikishia mlo. Watu hao hao leo wanaandama kwa ajili ya mtu fulani, akija kiongozi mwingine utawakuta wamo tu.

Haya maandamano ya namna hii ni kupoteza muda na bora waende kufanya kazi za kuwasaidia wao na familia zao.

Kama watu wanampenda kiongozi, si wasubiri siku ikifika wakampigie kura? Mtu unaacha kazi zako za uzalishaji na kwenda kusukuma mikokoteni ya wanasiasa? tena sio mara moja, bali mara kadhaa kwa hiyo miaka mitano.

Wanasiasa nao walivyo wajinga, wanafikiri kufanyiwa hivyo ndio kupendwa.

Kwasababu Watanzania walio wengi bado wanaishi kwa kubangaiza, hii kugeuka vibaraka vya wanasiasa itaendelea tu. Ukiwa na njaa huwezi kuwa huru.

JK inajulikana atakuwa mgombea wa CCM, sasa hizi kelele zingine zote za nini?
 
Wa Tz tumezoea kuwa na Rais kwa vipindi viwili sasa kelele za nini kuhusu Mh. Kikwete?? Kuna nini hasa kinachofanya watu waanze kampeni sasa??
 

Wanaotaka kumpinga Kikwete hawajaharibu chochote maana katiba ya CCM inawaruhusu kugombea pamoja na Kikwete kuwa madarakani kwa awamu moja tu.

Hamuwezi kuwa na katiba halafu mkaidharau kila wakati ili kukidhi matakwa ya 'utamaduni wa kuachiana' Kikwete hafai Urais ni muoga na akiachiwa tena kurudi madarakani anaweza kuipeleka nchi pabaya.

Tumchague kiongozi jasiri asiyemuogopa yoyote yule ndani ya Tanzania na siku zote ataweka mbele maslahi ya Tanzania na Watanzania. Kikwete kashindwa kufanya hivyo.
 
I am sick and tired of this type of politics!!!! It says a lot about our politics!!! sucks!!!
 
I am sick and tired of this type of politics!!!! It says a lot about our politics!!! sucks!!!

You should have known by this time that; "politicians are like diapers, they are alike and they have same uses. Change 'em and keep changing them but the end is always the same, none ends clean"
 
Gembe,
Mkuu kweli kabisa mimi ni mmoja kati ya watu wanaoamini hakuna mgombea zaidi ya Kikwete.. Ndio ukweli ndani ya chama hicho na kama wewe unaye mtu mwingine - mtaje, simple as that... Madudu yote ya CCM wahusika ni viongozi wote akiwemo huyo unayemfikiria na hakuna hata mmoja aliyesimama na kufanya tofauti hadi sasa hivi.

Nchi nzima imedumaa, Kikwete anapingwa na wengi kwa kutofanya yale aliyoahidi sasa nambie nani kati ya viongozi wa CCM ametimiza yale aliyoahidi kwa wananchi wake..Kila mmoja wao ana mapungufu tena makubwa zaidi kwa kila ahadi, wote wamejikita ktk siasa kuliko vitendo..

Licha ya yote haya, Mwinyi hakuwa na mshindani, Mkapa hakuwa na mshindani, hawa wote wameoza..iweje Kikwete aliyesinyaa ndiye mfikirie anatakiwa kuwa na mshindani..Ama hizi ndio kampeni za Lowassa/Rostam!..
Kama huyo mgombea wako anashindwa kufanya mabadiliko leo hii CCM wakiwa madarakani ataweza vipi akiwa pekee maanake waoandamana ni wana CCM wenyewe wapiga kura..
 

Mimi naamini ndani ya CCM tunaweza kabisa kupata kiongozi jasiri atakayeweka mbele maslahi ya Tanzania na Watanzania badala ya mafisadi na chama cha mafisadi. Haiwezekani nchi ya watu 40 millioni kushindwa kumpata kiongozi bora kuliko Kikwete. Kikwete siyo kiongozi hata kidogo alitaka kuwa Rais bila kujua uzito wa kuwa Rais sasa kila kitu kinamshinda ahadi zote alizotoa wakati wa kampeni hadi sasa hakuna hata moja aliyoitekeleza, halafu mnataka tena aendelee kuwa madarakani hadi 2015!!!!!?. WE CAN DO BETTER THAN THAT!!!! 🙁
 

Yakifanyika Maandamano kwa hilo nitashiriki kuunga mkono. Kwa ninayoyaona na kusikia kutoka CCM ni bora huyo Kikwete mara mia.
 


Upo dunia ya leo? Karume ni Doctor kama kina Nchimbi tena doctorate yake inatoka mitaa ya aliko Mkuu Obama.
 
NOno

Kweli kabisa hana lolote huyo Karume eti ni rasi anakaa hata miezi 6 bila ya kusikia chochote asemacho wala hata kutetea kwa labda anafaa kuwa mwenyekiti wa street
 


Hili la kutegemea makeke ndiyo yanayotuponza. Mwinyi kwani alikuwa na makeke alipoongoza? Halafu sisi Watanzania hata achaguliwe nani tabia zetu zitamfutaza kwani huwa tunapogoza shuka kutaka Rais afanye kila kitu na sisi tucheze Bongo fleva, taarabu na moja baridi moja moto.
Kama wenyew hatujabadilika kila atakaekuja hana atakalofanya. Kwani hizo Wizara alizoziongoza Magufuli hazina au kuwa na rushwa wakati wake?
Tumepita Marais watatu kabla ya Kikwete hebu tujiulize kipi cha msingi kilichowekwa na mmojawapo wa waliopita ambacho Kikwete amekirudisha nyuma?
 



MKUU Gembe, Kwa heshima zote naomba kuuliza namba ya kadi yako ya CCM. Aidha naomba kujua kama ni mwanachama katiba yenu inasemaje? Si kuna vikao vya kuamuwa mambo yenu?

Hizi kelele za kuwa kikwete asiruhusiwe kugombea tene Urais wa Tanzania tunazitowa wapi? Kwa misingi ipi? Iwapo CCM wataamuwa kumweka Kikwete ni uamuzi wao usiotuhusu sisi unless tukubaliane kuwa Watanzania hatuna akili ya kujua kipi kinatufaa.
Hili la kusema CCM isimuweke Kikwete ni sawa na kule Zanzibar ambako CCM wanawambia CUF wasimsimamishe Sheif Sharifu.
Yeyote atakaependekezwa na chama chake hawezi kuwa Rais kwa matakwa ya chama chake bali ni Watanzania wote watakaompigia kura.Iwapo Kikwete ameprove failure ni wajibu wetu sisi Watanzania kumkataa katika Uchaguzi. Ni juzi tu tulimsikia Chiligati akisema kuwa CCM ina wanachamamilioni 4 tu kati ya milioni nyingi zilizomchagua Kikwete. Jambo dogo tu ni kuzishinda hizo kura milioni 4 ili kumpa ushindi mgombea mwengine.
CCM tumekuwa tukiipigia kelele kwa sera zake mbaya leo tunajali nani wa kumuweka katika uchaguzi? Ninavyofikiri mimi kama kweli tumechoka na Kikwete na CCM kwa ujumla wao basi ni BORA wakimuweka huyo ambae Watanzania weshamchoka ili ashindwe kwa urahisi.
Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM na anachofanya ndicho wanachotaka wana CCM wenyewe na ndio maana wanampigia debe kwa hivyo kama tunataka mabadiliko ni kuiondowa CCM yenyewe kwani hata akitoka mwengine badala ya Kikwete atakuwa kwenye urais kuendeleza sera za CCM kitu ambacho Kikwete anakifanya vizuri sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…