The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

Kwa kauli yake aliyowahi kutoa wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani kuwa mtu yoyote atakaye toka ccm kwenda upinzani ni mwenda wazimu, basi yeye ni mwenda wazimu tu bado kuvua nguo na kula majalalani.

Hapana....hakutoka kwa hiyo si mwenda wazimu...kwa mujibu wa kauli yake mwenyewe
 
Sasa ninasema hivi, kama mtakuwa mnaendelea kunisema na hamtaunga mkono yale yanayofanywa na Rais, nitajiondoa upinzani.
Kwani kuna mpinzani gani bado anakutaka rudi tu hata leo naona umechelewa, itakuwa nafuu kwa wapinzani kuvuja kwa pakacha nafuu kwa mchukuzi
 
huyu nae maisha yalishamchosha..sina hakika kama kadi ya CCM aliwahi kuirudisha :sick:
 
Anaota uwaziri wa mambo ya ndani? Huko Vunjo watamchagua kweli?
 
huyu nae maisha yalishamchosha..sina hakika kama kadi ya CCM aliwahi kuirudisha :sick:

kama huna hakika kama aliwahi kurudisha kadi ya CCM kwa nini unasema maisha yalishamchosha? kwa taarifa yako huyu jamaa bado yuko kwenye payroll yao. Kama unabisha kamuulize makamba.
 
Itakuwa ni vema na haki kuendelea na CCM kwa wazi, kuchangiwa pesa ni kudhihirisha kuwa ni mwana CCM. Hivi naibu waziri mkuu mastaafu haiendelei kutunzwa na serikali? Hata kazi ya upinzani haijui huyo, nionavyo mimi ni 1. kuikosoa serikali, 2. kuielekeza serikali, 3. kutoa uhuru kwa wananchi katika kuwakilishwa, 4. mbadala wa chama tawala katika kuongoza nchi na hii ni fimbo kwa chama tawala, 5. kuleta ushindani, 6. kufanya mazuri zaidi kuliko chama tawala.

Kama JK amefanya mazuri, basi wapinzani wanatakiwa kupewa nchi na kufanya vizuri zaidi; wakishindwa wanapewa wengine! Watanzania tutajuaje wengine ni wazuri bila kuwapa ajira?
 
Mimi sioni tabu kwa mwana mpotevu kurudi kwa baba yake. MREMA alipotea njia alidhani angeweza kustahimili peke yake upinzani. Arudi tu nyumbani!!!
 
Kwani kuna mpinzani gani bado anakutaka rudi tu hata leo naona umechelewa, itakuwa nafuu kwa wapinzani kuvuja kwa pakacha nafuu kwa mchukuzi


Luteni mbona unatekwa kirahisi hivyo? kwa jinsi ninavyomjua Mrema na trend ya maneno anayoweweseka hivi sasa naweza sema yuko mbioni kurudi CCM ila bado kidogo tu angali anafanya timing ya muda muafaka, Anajijua kuwa wapinzani wameshamjua na anajijua kuwa jina lake lilikuwa kubwa upande wa wapinzani basi anataka kuonyesha wanainchi kuwa anarudi CCM huku akitegemea watu watamfuata na hii ikiwa mbinu mmojawapo ya kuokoa jahazi la CCM toka kwa watanzania wale fuata upepo 70% waliokata tamaa na utawala wa mkulu ambao kwa vyovyote wanaelekea kupunguza idadi ya ushindi wa kishindo uliopatikana 2005.. in short Luteni "changanya na za kwako"
 
Mnahangaika bure, Mrema sasa hivi ni lumpeni tu...hafai upinzani wala CCM. Ungeona wajumbe wa CCM walivyokuwa wanamzomea huko Kizota usingesema CCM wanamhitaji kwa lolote.....Mrema hakutumwa na mtu upinzani ila aliingia kwa tamaa ya kuwa rais, baada ya kujizolea umaarufu kwenye serikali dhaifu ya Mwinyi. sifa kwa JK ni kwa sababu amehurumiwa akalipiwa matibabu, yy kadhani JK anamhitaji kwenye serikali yake ijayo! Anatamaa kaa nini mfilisi huyu! Kule Vunjo hatapata kitu, na CCM watamtosa kinoma, maana hana lolote kwa sasa.

Pole Mrema, ulicheza karata vibaya (japo hiyo ni bahati ya nchi yetu, maana ww Hitler angeonaneka cha mtoto kwako) na sasa utasugua benchi mpaka kiama.
 
Hata hivyo Mrema mimi bado nakudai kifuta jasho kwa kusukuma gari lako toka UDSM admin block mpaka Ubungo na kuishia kupigwa mabomu na FFU....kumbuka ulituhadaa enzi hizo, wakati serikali ya mzee ruksa ikiongozwa na mama Sitti.
 
Hivi huyu mgombea wa TLP anapigiwa kampeni na nani? wakati mwenyekiti wake (Lyatonga) anampigia kampeni Kikwete? a lot of mad ...
 
Luteni mbona unatekwa kirahisi hivyo? kwa jinsi ninavyomjua Mrema na trend ya maneno anayoweweseka hivi sasa naweza sema yuko mbioni kurudi CCM ila bado kidogo tu angali anafanya timing ya muda muafaka, Anajijua kuwa wapinzani wameshamjua na anajijua kuwa jina lake lilikuwa kubwa upande wa wapinzani basi anataka kuonyesha wanainchi kuwa anarudi CCM huku akitegemea watu watamfuata na hii ikiwa mbinu mmojawapo ya kuokoa jahazi la CCM toka kwa watanzania wale fuata upepo 70% waliokata tamaa na utawala wa mkulu ambao kwa vyovyote wanaelekea kupunguza idadi ya ushindi wa kishindo uliopatikana 2005.. in short Luteni "changanya na za kwako"
Ngisibara

Nafikiri hukunielewa mbona unasema kitu kile kile nilichomaanisha? mimi huwa si wa kutekwa mawazo kirahisi namna hiyo huwa niko makini sana na maneno yangu.
 
Hivi huyu mgombea wa TLP anapigiwa kampeni na nani? wakati mwenyekiti wake (Lyatonga) anampigia kampeni Kikwete? a lot of mad ...
Ni ajabu na kweli, mpiga debe wake Mrema anasema sera za CCM ni nzuri na Kikwete amezitekeleza zote, sasa kama zimetekelezwa zote mgombea wao atakuwa anataka nini zaidi.
 
Back
Top Bottom