The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

Wana Jf naomba niwashukuru wote ambao wamekuwa wakitoa changamoto zao mbalimbali kuhusu uchaguzi wa 2010 kwa sababu wamesaidia kwa namna moja au nyingine kuelimisha kwa kiasi kikubwa sana umma wa wawatanzania kuhusu uchaguzi wa mwaka huu. Najua siyo wote wanaosoma JF lakini ninafurahi na kujivuna kuwa kuwa kuna baadhi ya ndugu zetu wa agazeti wanaowakilsha yale yanayotolewa ndani hapa kwa wananchi kwa kupita magazeti yao. Jambo hili linanipa imani kuwa asilimia kubwa ya yanayoandikwa hapa ndani yanawafilia watanzania wengi kupitia magazeti mbali mbali. Nawashukuru sana ndugu zetu waandishi wa magazeti kwa juhudi zao na naomba waongezi juhudi ili kuhakikisha kuwa yale yote muhimu yanayoandikwa na JF yanawfikia watanzania wasioweza kuifikia au kuipata kona ya JF. Baada ya kusema hayo naomba nirudi kwa mzee wangu wa kiraracha bwana AUGUST LYATONGA MREMA A.K.A MZEE WA SIKU SABA. Naamini wengi wanakumbuka enzi zake za siku saba hata kwa waume za watu alipokuwa ndata mkuu pale mambo ya ndani hadi kuoewa unaibu waziri mkuu kwa mikiki yake mpaka waziri wa kazi hadi alipoanjia ngazi kwa manufaa ya wadanganyika . Kwa ukweli alifanya maamuzi ya kijasiri ambapo kila mtanzania alimwopna shujaa wa wanyonge hata asilimia kubwa walikuwa tayari kumpa urais wa nchi 1995 kama siyo CCM kuwa na mbinu kubwa. Nilichokiweka akilini mpaka leo ni pale wakati wa kutangaza nia ulipotimia siku moja Mrema akatamka hadharani kuwa '"Nyerere huyu ndiye alityeniambia nihamie upinzani ili niimarishe upinzani na Nyerere huyu huyu ndiye anayeniambia nisigombee urais nikagombee ubunge''. Hapa nilijiuliza maswali mengi ambayo ndo napata jibu sasa hivi.

Awali baada ya kauli hii nilijiuliza kwamba Mrema ni kivuli cha CCM kilichopandikizwa na Nyerere ili kuonekane kuna upinzani? Kabla sijapata jibu Mrema kaivuruga NCCR Mageuzi akishikiana na Mabere Marando akahamia TLP. Tangu aingie TLP hajafanya jambo lolote la maana zaidi ya kupiga domo kama mchungaji yule anayeongea anapokuwa amechacha ijapokuwa na mheshimu kwa kuweza kuitetea katiba ya Jamhuri kuliko mtanzania yeyote ili isipokuwa hayati Nyerere. Tangu JK aingie madarakani Mrema amekuwa akijikomba sana kwa kwake kwa kumsifia na kusifia CCM. Wote mnaona yote yaliyotokea Dodoma na kwenye mkutano mkuu wa TLP juzi. Mrema huku akijua chama chake kimeshamteua mgombea urais alisimama na kudiriki kusema mbele ya wanachama wenzake kuwa '"CHINI YA UONGOZI WA JK NA GHALIB BILAL SERIKALI ITAKUWA NZURI SANA'' Hivi mtu mwenye akili anamwelewaje huyu mtu? Hii ndiyo sababu kubwa ya kumwita mrema kuwa ni fisadi wa siasa na kuwadi mkuu wa CCM. Anathubutu kupiga kifua mbele ya wanachama wa TLP kuwa CCM imemchangia 200,000/= za kwenda kuchukua form za ubunge Vunjo kupitia TLP. Hii inakuja akilini kweili? NAOMBA NIHITIMISHE KWA KUWAOMBA WANAVUNJO WASIJE WAKALOGWA KUMCHAGUA NDUMILA KUWILI HUYU. SIWAAMBII MUMCHAGUE NANI ILA NAASHAURI MSIMCHAGUE HUYU KIGEUGEU anayeweza keshokutwa akamtukana ahata rais huku akijidai anashinda kesi zote za kubambikiwa. PIGIENI kura hata koti lililotundikwa kwenye mti kuliko Mrema. Nawatakieni kila la heri na uchaguzi wa amani na wa kidemokrsia.
 
msamehe bure huyu ndugu hajui atendalo, anatafuta fadhila
 
Nilimtazama Mrema akiongea kwenye mkutano mkuu wa CCM nikamuangalia tena juzi kwenye mkutano wake wa TLP nikaona jinsi sura (na afya) yake ilivyoharibika, nikapata wazo moja tu: huyu ni mtu aliyekwisha! Anatia huruma kweli. Hivyo ndugu zangu hamna haja ya kumtolea ukali; badala yake muoneeni huruma. Hata huko CCM hahitajiki; walishamfix. Kweli ni aibu kwa mtu aliyeinuka kwa nguvu kubwa miaka ile ya 90 leo hii anaonkena kama kinyago (literally) na anaongea maneno ambayo ni aibu kwa mwanasiasa mwenye heshima zake.
 
nijuavyo kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu. kama mrema atarudi ccm, atathibitisha tuhuma zimhusuzo kuhusu kutumwa kudhoofisha upinzani.
 
Mzee wa kirarachaaaaa..........

Its like "....kazi mliyonituma nimeimalizaaa....., akakata roho...." huyo ndo Mrema bana!😛ound:
 
sasa mbona TLP imesimamisha mgombea kwa nafasi ya Urais, ¬? yule ni kichaa sasa msameheni.
 
..makala inamhusu Augustino Mrema ambaye aligombea Uraisi mwaka 1995.

..sikuwahi kuvutiwa na Mrema hata siku moja. kwangu mimi Mrema came across as a very myopic and crude political opportunist. kitu cha ajabu ni kwamba alikuwa na wafuasi wengi kwelikweli, na wengi wao ni watu niliowaheshimu.


..makala nzima inapatikana hapa:Kama vile tumemsahau Mrema, tumeisahau CCM!


Raia Mwema said:
Vyovyote vile; wasomaji wangu wengi walinishangaza kwa kunitumia e-mails na sms nyingizenye kuonyesha kushtushwa na kukerwa na ‘usanii’ ulioonyeshwa na Mwenyekiti wa TLP, AugustineMrema wakati wa mkutano huo.

Nasema wamenishangaza kwa kumshangaa Mrema na si kuishangaa CCM kwa namna ilivyouendesha mkutano huo; maana waliuendesha kama vile ni replica ya mkutano wa 1995 au 2000 au wa 2005; licha ya kwamba changamoto na mazingira ya sasa nchini vinahitaji mjadala wenye utofauti.

Yawezekana kwamba labda wasomaji wangu wanaichukulia CCM kuwa ni ile ile ya jana na leo, na ndiyo maana hawakushangaa na mambo yalivyokwenda? Kama hivyo ndivyo, kwa nini hawakuamini pia kwamba Mrema naye ni yule yule wa jana na leo?

Labda wanaikumbuka CCM lakini wamemsahau Augustine |Lyatonga Mrema. Labda niwakumbushe kidogo kuhusu mwanasiasa huyu ambaye sasa ni dhahiri umaarufu wake nchini unakwenda kuzimu kwa kasi ya kutisha (inashangaza CCM bado inamwona ni ‘mtaji wa kisiasa’).

Watanzania wachache mno walimfahamu Mrema kabla hajateuliwa na Mzee Ali Hassan Mwinyi kuwa waziri miaka ile ya tisini. Ingawa alikuwa mbunge, Mrema hakuwa na kawaida ya kujadili hoja zozote bungeni zenye maslahi mapana ya Taifa; labda hoja ihusu suala la kilimo cha kahawa jimboni kwake.
Lakini alipoteuliwa na Mwinyi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Watanzania ndipo hasa walipoanza kuiona sura ya kweli ya Mrema na uwezo wake wa uongozi. Mifano ya vituko vyake vya staili yake ya uongozi ni mingi, lakini niwakumbushe wasomaji wangu vichache tu.

Mrema aliibuka na dhana ya ulinzi wa sungusungu kama jibu la kisayansi la kukabiliana na wimbi la uhalifu nchini. Akaagiza kila mtu alinde sungusungu la sivyo ashitakiwe. Watu wakashangaa kwa sababu kwanza, ulinzi wa sungusungu ni suala la hiari lakini pili, hapakuwepo na sheria ya kumshitaki asiyelinda sungusungu.

Lakini yeye aliendelea kutoa amri hiyo isiyotekelezeka kisheria, na matokeo yake ni kwamba yalikuwepo matukio chungu nzima ya udhalilishaji watu waliokataa kulinda sungusungu, ambayo ilikuwa haki yao kukataa jambo hilo la hiari.

Kituko chake kingine ni ile amri aliyoitoa kwa ma- DC na ma-RC kwamba ofisa yeyote wa Serikali atakayechelewa kuingia ofisini saa moja na nusu asubuhi, kiti chake kichukuliwe na kipelekwe kwake!


Agizo hilo nalo lilipuuzwa kama lilivyostahili kupuuzwa, na watu wakaanza kuhoji uwezo wake wa kufikiri na kuongoza. Alipoona utekelezaji wa agizo hilo unashindikana na unakejeliwa, Mrema akaachana nalo na kurukia mambo mengine mapya.


Na ni wakati huo alipowageukia Wahindi. Kwanza alianza kuwashambulia kuwa ni wakwepaji wakubwa wa kodi; kisha wakawa marafiki zake wakubwa, lakini alipohamia NCCR Mageuzi na kuwania urais, mwaka 1995, akawageuka tena na kuwaita ma********* bila hata kupepesa kope!

Alipoanza kuwaandama Wahindi wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mrema alikuwa akiwapa siku saba waripoti nyumbani kwake Moshi ili wajieleze kuhusu tuhuma za ukwepaji kodi. Vikao hivyo vya nyumbani kwake viliendeshwa bila hata maofisa wa ushuru kuwepo.

Baadaye Mrema alikuwa akiibuka Dar es Salaam na kusema kuwa Wahindi hao wamekubali kulipa kodi walizokwepa baada ya kuzungumza nao. Watu wakazidi kumshangaa Mrema na kujiuliza maswali kibao: Vipi Wahindi hao awaite nyumbani kwake Moshi na si ofisini kwake Dar es Salaam? Vipi mazungumzo hayo ayafanye peke yake? Vipi mhalifu aliyekosa apewe fursa ya kulipa badala ya kuchukuliwa sheria?

Lakini waliotatizwa na maswali hayo walipata majibu haraka; maana haikuchukua muda Mrema akaanza kuonekana anatembea na Wahindi katika safari zake kadhaa.

Ipo simulizi ya mama mmoja mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana mjini Moshi ambaye alimwalika Mrema kusimamia harambee ya shule yake. Siku ya siku mwalimu huyo, pamoja na wenzake, wakafika kwenye uwanja wa michezo kumpokea Mrema ambaye angetua kwa helkopta ya polisi.

Helkopta ilipofika, mtu wa kwanza kushuka alikuwa ni Mhindi, wa pili ni Mhindi, wa tatu ni Mhindi, wa nne ni Mhindi, na ndipo mwalimu mkuu alipoanza kuwaambia wenzake kwamba ile sio helkopta ya serikali bali ya wafanyabiashara wa Kihindi; hivyo waendelee kusubiri helkopta inayomleta waziri. Lakini ghafla Mrema akashuka kutoka kwenye helkopta ile ile akiwa wa mwisho.

Kwenye harambee yenyewe ya shule akawaambia wananchi kwamba Wahindi wale alioandamana nao ni “ndugu zake”, na walimchangia mamilioni si haba!

Wakati fulani akiwa Zanzibar aliwahi kuchangiwa zawadi kemkem na wafanyabiashara wa Kihindi; naye akawashukuru mno na kusema kwamba anawashangaa wale wanaomshangaa kuandamana na Wahindi na kuhoji kuwa hao wanaotaka aandamane na masikini; hao masikini watamsaidia nini?

Katika hili la kuwaita Wahindi ni “ndugu zake”, aliwahi kusema hiyo pia siku alipoandaliwa tafrija ya pongezi (‘kwa kuchapa kazi’?) na wakazi wa jimbo lake waishio Dar es Salaam. Wakati wa kufungua dansi, Mrema akachagua kufungua dansi na mke wa mfanyabiashara wa Kihindi anayeitwa Abdallah Bora; huku akirudia kusema kwamba mfanyabiashara huyo ni “ndugu yake”.

Lakini kama nilivyoeleza mwanzo, baadaye alipohamia NCCR Mageuzi na kuwania urais mwaka 1995, akawatosa hao Wahindi aliowaita “ndugu zangu”. Badala ya kuwaita “ndugu zangu” akawa anawaita ma*********!

Huyo ndiye Mrema
(lest we forget).

Kwa hiyo, vituko vyake vya mjini Dodoma wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM, mwishoni mwa wiki iliyopita, ni mwendelezo tu wa vituko vya maisha yake ya kisiasa ambayo ni dhahiri sasa yanaelekea ukingoni. Nitashangaa kama Vunjo watamchagua kuwa mbunge wao mpya!

Alipopewa nafasi kwenye mkutano huo ya kutoa salamu za TLP kwa kuzungumza “machache”, Mrema akaamua kuitumia fursa hiyo kumsifu mno Rais Kikwete na CCM; kiasi cha watu kujiuliza: Kama anaiona CCM ni nzuri kiasi hicho, anangoja nini TLP? Kwa nini harejei CCM? Lakini jibu ni kwamba anaifaa CCM akiwa TLP (upinzani) na si akiwa CCM kwenyewe!

Lakini wakati akiisifu CCM kwamba haishikiki na kwamba Kikwete ni kiongozi asiye na mfanowe, mjini Dar es Salaam viongozi wenzake wa TLP walikuwa wakiandaa mkutano mkuu wa kuteua mgombea urais kwa tiketi ya chama chao!

Nilipoeleza wiki iliyopita kwamba Watanzania tumeugeuza urais na ubunge kuwa jambo jepesi na la mzaha; nilimaanisha mambo kama hayo.

Hebu fikiria: Mwenyekiti wa TLP (Mrema) anasema Kikwete na CCM yake ni kiboko na hawakamatiki; tena anasema hayo kwenye Mkutano Mkuu wa CCM ambako anafikia hata hatua ya kucheza jukwaani anaposhangiliwa na wajumbe, halafu baada ya hapo anarudi Dar na kuongoza kikao cha TLP cha kuchagua mgombea urais wa kuchuana na Kikwete! Kama huu si uendawazimu wa kisiasa ni nini?

Kwa nini Mrema na TLP yake wapoteze bure muda na pesa zao kumchagua Muttamwega Mgaywa kuchuana na Kikwete ilhali “Kikwete hakamatiki na sera za CCM ni nzuri mno”? Kwa nini wasimthibitishe tu Kikwete kama wenyewe CCM walivyofanya katika mkutano wao huo wa Dodoma? Kwa nini Mrema mwenyewe apoteze muda wake na pesa zake kugombea ubunge wa Vunjo kwa tiketi ya PLT ilhali ameshaifagilia CCM kuwa ina sera nzuri na haikamatiki!

Ndugu zangu, huyo ndiye Mrema, na hiyo ndiyo CCM. Nawashangaa wale walionitumia e-mails na sms
za kumshangaa Mrema kwa aliyoyafanya Dodoma. Tusishangae kama vile hatumjui Mrema au hatuijui CCM na jinsi inavyoendesha siasa zake nchini!

Kwa hakika, hata ule uamuzi wa Dk. Bilal kunyimwa fursa ya kuwania urais wa Zanzibar na badala yake kupozwa kwa kupewa ugombea mwenza wa Bara (makamu wa rais mtarajiwa), ni ushahidi mwingine wa jinsi siasa za Tanzania zilivyozama katika kukidhi maslahi binafsi na ya makundi, na si maslahi ya Taifa.

Ingekuwa wanasiasa wa CCM hawaongozwi na ubinafsi, Dk. Bilal angeikataa nafasi hiyo ya ugombea mwenza, kwa sababu umakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano sio alioutaka au alioona ana uwezo nao.

Angeikataa nafasi hiyo, kwa sababu alichotaka ni urais wa mahali pake pa asili pa kuzaliwa (Zanzibar) ili ‘awakomboe’ watu wake kutoka katika umasikini, na si kupachikwa umakamu wa urais mtarajiwa wa Jamhuri ambao si matamanio yake.

Lakini aliukubali uteuzi huo. Kwa nini aliukubali ugombea mwenza wa Bara? Jibu ni rahisi: Ni kwa sababu ndani ya moyo wake alichotaka ni ukubwa tu, na haijalishi ni ukubwa katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano au ni ukubwa katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa hiyo, kwake aliona ni heri nusu shari kuliko shari kamili!


Suala la
vision yake ya kuwakomboa Wazanzibari katika tope la maendeleo duni, alilisahau kabisa baada ya kupozwa na ugombea mwenza wa urais wa Jamhuri (ugombea mwenza wa Bara).

Hizo ndizo siasa za CCM katika Tanzania. Ni siasa za makundi na ubinafsi ambazo, mwisho wa yote, kila mmoja anaangalia anapata nini yeye binafsi na si nchi yake au jimbo lake linapata nini.


Vyovyote vile; kwa kuzingatia mfumo wa uchaguzi ulivyo Tanzania na muundo wa tume yenyewe ya uchaguzi ulivyo, Kikwete na CCM yake watashinda kwa kishindo Oktoba 2010, lakini amini usiamini itakuwa miaka mingine mitano ya kutangatanga nyikani
(lost in the wilderness) bila visheni yoyote ya kueleweka ya kuiondoa nchi yetu kwenye umasikini mkubwa katikati ya utajiri wa maliasili nyingi.

Na kwa mfumo huu na kwa CCM hii, wachache matajiri watazidi kuwa matajiri na masikini walio wengi watazidi kuwa masikini.


Nihitimishe kwa nukuu ile ile ya Clarence Darrow: When I was a boy, I was told that anybody could become a politician… anybody could become a president, Iam beginning to believe it.”


Tafakari!
 
Mrema ni sawa na POPO, ambaye huwezi kujua kwamba ni mnyama ama ni ndege.
 
..makala inamhusu Augustino Mrema ambaye aligombea Uraisi mwaka 1995.

..sikuwahi kuvutiwa na Mrema hata siku moja. kwangu mimi Mrema came across as a very myopic and crude political opportunist. kitu cha ajabu ni kwamba alikuwa na wafuasi wengi kwelikweli, na wengi wao ni watu niliowaheshimu.


..makala nzima inapatikana hapa:Kama vile tumemsahau Mrema, tumeisahau CCM!
Mkuu JokaKuu, hukuwa peke yako. Tuliomfahamu Mrema kwa undani tulijua na tulionya tangu mapema kabisa kuwa NCCR Mageuzi imelamba dume kwa kulipokea hilo pandikizi la CCM lakini wapi. Niliwahi kuanzisha mjadala humu ndani kuhusu Mrema, angalia nilivyoshambuliwa na wapenzi wa huyo mwendawazimu:


Nasikia kichefuchefu sana watu wanapomsifia Augustino Lyatonga Mrema wakati ukweli ni kuwa aliyapiga vita mageuzi kwa nguvu zake zote hadi pale alipotumwa na mabwana zake wa CCM awavuruge wapinzani. Kwangu mimi huyu mwenda wazimu atabaki kwenye historia kama aliyeua mwamko wa mageuzi uliokuwa unaenea lakini kwa utaratibu usio na mikwaruzo. Bila Mrema upinzani hivi leo ungekuwa mbali na ingawa najua wapenzi wake watajitokeza kumtetea, matumaini yangu ni kuwa atakapoamua kurudi CCM watamfuata huko huko.
 
Acheni ageuke Vuvuzela la chama twawala kwani hivi usalama wa taifa anajiuzulu kazi ? akijiuzulu ni kifo. Mzee maisha yamekuwa magumu CCM wamemtupa kalipiwa kutibiwa na kumbe kucheza sindimba pale Dodoma ni kwa sababu alilipwa 2000000/= za ile show yake hahahahaha kweli pesa mh

Pesaa peesaa kweli pesaa......................
 
Sio lazima mtu mpaka aokote makopo na kula jalalani ndio watu wamtambue kuwa yeye ni mwehu.
 
Ni vyema na haki akapumzikie huko...
Hiyo timing haitamsaidia zaidi ya kuonekana kwenye gazeti keshoake afu watu wanampotezea kimoja..
 
Nafikiri mtu anayemfahamu vizuri mrema ni mchungaji Mtikila alikuwa mtu wa kwanza kuwaambia watanzania mrema si mpinzani watu hawakuani wakajazana NCCR, wakabeba wakaenda naye TLP sasa wameshikwa na butwa.......
 
Mrema ni mgonjwa na all he needs is to seek medical advice
 
Mie sikuamini macho yangu, nilipomwona mrema akisakata rumba la kumpamba jk katika mkutano mkuu wa ccm. Ama kweli ukistajabia ya Musa utayapata ya firauni.
 
Binafsi nilianza kuwa na wasiwasi na Mrema baada ya ule mdahalo pale Kilimanjaro
 
Kwani ina maana mpaka sasa hivi wana JF hamfahamu kuwa Mrema ni mtu wa system na kazi yake kubwa ni kodhohofisha upinzani?
 
Back
Top Bottom