The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

If you cannot beat them join them! Ni dhana ya kipumbavu lakini. But what do you expect from the man from Kiraracha whose sell by date political-wise is long passed? Mrema is a shadow of his fomer self as time has countinued to catch up with him. No wonder he looks a bit senile. Poor Mrema and his zealot admirers!
 
If you cannot beat them join them! Ni dhana ya kipumbavu lakini. But what do you expect from the man from Kiraracha whose sell by date political-wise is long passed? Mrema is a shadow of his fomer self as time has countinued to catch up with him. No wonder he looks a bit senile. Poor Mrema and his zealot admirers!


some comments jus tend to suprise me.katika awamu zote nne ipi ndio ina pambana na ufisadi. nadhan tukubaliane kwamba ya kikwete ndio inayoongoza. every tanzanian anajau kikwete hafai na maamuzi hawezi lakini yeye ndio kama kaanzisha vita dhidi ya mafisadi. katika awamu zote ni stories tu ambazo tulikuwa tunazipata. kikwete kuwapeleka mahakami mawaziri ni maamuzu au sacrifice kubwa amefanya. kikwete hawezi kufanya kila kitu watu wanataka. lakiniameanzisha wengine waje kumalizia.

na hao wana CCM wanaomsema hadharani ni cowards and stupid. inabidi wayaseme hayo kwenye vikao vya NEC ya CCM ni kuwashaur other member wasimpe nafasi ya kugombea tena. sisi wananchi na wapinzani there is nothing we can do about it bali ni kumsema tu. but ikifika election next year nani huku ndani ya JF hajui kama CCM na Kikwete watashinda.
 
mrema hana lolote...anaona uchaguzi umekaribia...

Kukaribia kwa uchaguzi tutashuhudia chui wengi watakao vaa ngozi za kondoo kwa sababu katika hali ambapo kura zinaweza kuibiwa na chama Tawala CCM bila aibu kwa baadhi ya viongozi wa Upizani CHAKUSIKITISHA!Wananunuliwa kwa ahadi za kusaidiwa na CCM kuwagawia kura wakati wa uchaguzi.MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Mag3;Naaminia uchambuzi wako,lakini hapa naona umetumia jazba kidogo,sijamwita member yeyote humu stupid thinker,na niliposema "tusiwe" sikujisingle out,you can think and reason better than that.

Pia nimezipima kauli za Mrema rather than just "kumpima kwenye mizani" ni two different issues hapo,kuwa makini....Ku conclude kwamba nimesema ama ninadhani kuwa Lyatonga hakosei ni assumptions zako ambazo ni baseless.

Na issue hapa si kuhusu huo unaouita usanii wa JK, kabla hatujaconclude kuhusu hatua ambazo keshachukua(pitia posting yangu iliyopita nilipogusia kuhusu msimamo wa wengi hapa JF kuhusu hatua alizozichukua,wengi tukisema ni hatua nzuri kama hakuna usanii)Ni tofauti na issue basic ya mjadala huu ambapo ni kuwa "JK"Hajafanya kitu" hence uoenevu....Kama tuki conclude kwamba ni full usanii,then we will be in a different page...Again ni issue mbili tofauti na hivyo kuwa makini.

Kuhusu list of shame hilo linaeleweka,lakini tumeshajua kuwa CCM ndiyo walichota pesa hizo hili warudi madarakani,hivyo basi kumkataa JK na kutegemea mwingine kutoka CCM kuwa ataendeleza sera za tofauti ni uonevu....Na hayo ni mawazo ya wengine ambayo pia uyarespect.

Mrema amesema "wale wanaosema "hajafanya kitu" na wewe umeiweka issue kwenye perception kwamba anafagilia mbaya...Nayarespect maamuzi yako lakini nikisisitiza kwamba sidhani kama ni uchambuzi sahihi.

Mkuu jmushi1, ninajua Lyatonga anao mashabiki na hata siku moja sitegemei kuwa na ubavu wa kuwabadilisha fikra zao. Nimeshuhudia wanawake walivyoweza kulala barabarani uchi kumtetea mpiganaji wao Agostino. Nilishuhudia alivyoweza kubadilisha vyama kama shati huku anasindikizwa na mashabiki wake watiifu. Nimeshuhudia akivurugana na viongozi wake kila alipokwenda lakini wapenzi wa mzee wa kiraracha wakimganda kama smaku. Pamoja na yeye kuwa shushushu mkubwa lakini ni ushushushu wa wengine ndio unalaumiwa kuwa ulichangia sana katika kuiua NCCR-mageuzi. Pamoja na yeye kuwa kamanda wa vikosi viliyopiga vita uanzishwaji wa vyama vingi, watiifu wake hawakusita kumelevate kama mwana mageuzi namba one. Hapana Mkuu, hilo wazo la kudhani hao watu wanaweza wakakubaliana na mawazo yangu, sina.
Binafsi ninafarijika na jinsi utawala wa Rais Kikwete unavyopambana na vitendo vya ufisadi kwa kuwa sasa ni ajenda ya serikali na ya wananchi na haya ni muendelezo wa mapambano niliyokuwa nimeyaanzisha nilipokuwa serikalini
Mkuu jmushi1, yanayonipa taabu ni hayo matamushi hapo juu na timing yake. Hivi sasa kuna zoezi kubwa linaendelea la kumsafisha JK lakini huko CCM kumezidi kuchafuka na hakuna wa kumsafisha mwingine - sana sana wanazidi kuchafuana. Wajuaji ndani ya CCM sasa wanatafuta wapiga debe nje ya CCM na kauli kama hii ya Mrema hata kama ingetolewa kwa nia nzuri si wakati wake. Mrema kwa tamko lake hili anaungana na wale wote tunaowaita mafisadi - wote wanaridhika na jinsi JK anavyoendesha kwa mafanikio makubwa vita dhidi ya ufisadi.
nadhani baadhi ya wadau kuna kitu wanashindwa kumuelewa mrema....
mrema is a proffessional SPY...and qualified propaganda artist...lakini pamoja na yote mara zote mrema anatofauti kubwa na wanasiasa wengi..ana nidhamu anayotakiwa kuwa nayo spy yeyote [acha hawa wa siku hizi]...kwanza kwake TAIFA ni jambo la kwanza,pili pamoja na uropokaji wa mrema huwa anachagua ya kuongea...,ndio maana hata siku moja mahakama haijaweza kumtia hatiani hata mara moja kwa uchochezi....!!
Wow, kweli mtu akipenda chongo huita kengeza - Mkuu Phillemon Mikael, hizi sifa unazompa Lyatonga zatosha kabisa kutupa wengine picha halisi ya fikra za watiifu wa Mrema. Ni mara ya kwanza nasikia kuwa mropokaji huchagua cha kuongea na the mere fact kwamba mahakama haijawahi kumtia hatiani katika huu mfumo wetu probably explains it all. Kwa alipofikia hivi sasa, Mrema is a liability kwa wanaotaka mabadiliko lakini kwa kuwa umeendelea kudai kuwa yawezekana wengine hatumfahamu Mrema, basi nitaachia hapa.
 
..tatizo tumejikita zaidi ktk masuala ya ufisadi wakati kuna mambo chungu nzima yanaharibika nchini.

..tukianza kuchunguza masuala kama huduma za afya, elimu, maji, masuala ya ardhi, ajira, uwekezaji,etc kote huku utakuta hakuna hata sehemu moja ambapo mwananchi/mpigakura ana haki ya kufurahia/kuridhika jinsi serikali yake ilivyoyashughulikia.

..haya masuala ya ufisadi naona yana muelekeo wa usanii-sanii. naona kama tunatumia muda mwingi kumuandama Mkapa and Co., wakati wanaotuumiza sasa hivi ni JK na wazembe wenzake.

..kelele za ufisadi has not worked so far ktk kuongeza kura kwa vyama vya upinzani. matokeo ya chaguzi ndogo za ubunge na serikali za mitaa yanaelekeza hivyo.

..Wapinzani wanapaswa kujisahihisha na kujipanga upya ktk jinsi wanavyowa-approach wapiga kura. jambo moja ambalo wanaweza kufanya ni kuwahamasisha wapiga kura wa Tanzania wawe more demanding kwa serikali yao na wao wenyewe.

NB:

..huyo Mrema naye he is washed out na alikuwa fisadi alipokuwa CCM. he had a chance kuwalipua mafisadi wakati wa uchaguzi wa 1995 lakini akaishia kujiuma-uma tu.
 
Kila chama alichoingia amesababisha migogoro mikubwa dhidi ya wale ambao walionesha upinzani wa kweli dhidi ya ccm hivyo baadhi alifanikiwa kuwatimua uanachama n.k.

Amekuwa na hulka (aliyotumwa) kung'ang'ania top post katika kila chama pinzani aendacho na hajawahi kufikiria kuachia madaraka yake. na yeyote atakayempinga ktk uchaguzi mkuu wa chama atamwita all names na zaidi atasema "huyu ni SHUSHUSHU, ametumwa kuniangamiza" ili aonewe huruma na kubakia ktk mamlaka.

Ila kikubwa kilichompeleka upinzani ni hiki anachokifanya sasa.... Baada ya makada (nasema wooote) wa CCM kushindwa kumsafishia njia muungwana kurejea 2010 basi mshkaji ameamua bila soni kuokoa jahazi kwa kutoa fagizi (za kijinga) kwa muungwana. Hasa pale anaposema kwamba kuna hatihati ya ccm kutolewa madarakani (hii inathibitisha kwamba yeye ni mmoja wao) hivyo ni budi mazuri ya muungwana yakaangaliwa ili kumpa nafasi ya muhula wa pili, amekiri kwamba endapo muungwana angekuwa leader miaka ya tisaini asingehama ccm. Ni sawa na muumini ambaye anaamua kumrudia SHETANI anapoona mambo yake hayaendi kinjia mkato! MPINZANI (uchwara) huyu badala ya kufikiria kukiimarisha chama apate kura nyingi mwakani kumbe anaogopa kupewa majukumu ya kuongoza nchi. Sijapata kuona mtu akijibidiisha masomoni ili amwachie mwenzie nafasi ya kwanza darasani.

Je inawezekana kwamba huu ndo muda muafaka wa gladiator (mchovu) kurudi kundini???? Inaonesha Muungwana anamuhitaji na yeye anamuhitaji muungwana. Amechoka na amepoteza haiba
 
Kila chama alichoingia amesababisha migogoro mikubwa dhidi ya wale ambao walionesha upinzani wa kweli dhidi ya ccm hivyo baadhi alifanikiwa kuwatimua uanachama n.k.

Amekuwa na hulka (aliyotumwa) kung'ang'ania top post katika kila chama pinzani aendacho na hajawahi kufikiria kuachia madaraka yake. na yeyote atakayempinga ktk uchaguzi mkuu wa chama atamwita all names na zaidi atasema "huyu ni SHUSHUSHU, ametumwa kuniangamiza" ili aonewe huruma na kubakia ktk mamlaka.

Ila kikubwa kilichompeleka upinzani ni hiki anachokifanya sasa.... Baada ya makada (nasema wooote) wa CCM kushindwa kumsafishia njia muungwana kurejea 2010 basi mshkaji ameamua bila soni kuokoa jahazi kwa kutoa fagizi (za kijinga) kwa muungwana. Hasa pale anaposema kwamba kuna hatihati ya ccm kutolewa madarakani (hii inathibitisha kwamba yeye ni mmoja wao) hivyo ni budi mazuri ya muungwana yakaangaliwa ili kumpa nafasi ya muhula wa pili, amekiri kwamba endapo muungwana angekuwa leader miaka ya tisaini asingehama ccm. Ni sawa na muumini ambaye anaamua kumrudia SHETANI anapoona mambo yake hayaendi kinjia mkato! MPINZANI (uchwara) huyu badala ya kufikiria kukiimarisha chama apate kura nyingi mwakani kumbe anaogopa kupewa majukumu ya kuongoza nchi. Sijapata kuona mtu akijibidiisha masomoni ili amwachie mwenzie nafasi ya kwanza darasani.

Je inawezekana kwamba huu ndo muda muafaka wa gladiator (mchovu) kurudi kundini???? Inaonesha Muungwana anamuhitaji na yeye anamuhitaji muungwana. Amechoka na amepoteza haiba
LOL!ulinitisha kweli mpwa!😀
kumbe ni wito maalum!

NASHUKURU KAMA UMEJUA KUWA YUPO KAZINI
 
viongozi wa kitanzania ni bendera kufuata upepo...wako wako tuu hawana msimamo kabisa wako kama wacheza sinema vile bana ona sasa...hawako kutetea maslahi ya wananchi bali wanaangalia wapi kuna msosi kama mafisi vile
 
Huyu ni Mchaga!Lamwai yuko wapi?Ni mchaga!Pesa Tanzania imeua utu na heshima!
Wachaga mnatuaibisha!Afadhali Mhaya ana msimamo!
 
viongozi wa kitanzania ni bendera kufuata upepo...wako wako tuu hawana msimamo kabisa wako kama wacheza sinema vile bana ona sasa...hawako kutetea maslahi ya wananchi bali wanaangalia wapi kuna msosi kama mafisi vile
Ina maana ile asilimia 70 wote ni viongozi...???
 
Huyu ni Mchaga!Lamwai yuko wapi?Ni mchaga!Pesa Tanzania imeua utu na heshima!
Wachaga mnatuaibisha!Afadhali Mhaya ana msimamo!
toa mfano wa MHAYA mwenye msimamo!.............
 
anaganga njaaa................huyu ni ndumila kuwili anaeleweka kwa siasa zake za kupandikizwa na ccm huyu ni mtu wa usalama wa taifa wala hawezi kuasi vinginevyo angechukluliwa hatua kali sana kwa hiyo yanayotokea ni matokeo ya mfumo wetu.........tunayo kazi sisiemu wameshindikana
 
toa mfano wa MHAYA mwenye msimamo!.............

hili nalo linahitajio kubishana kwamba mchaga kwake maslahi kwanza utu na maslahi ya wengine baadae?
acha hizo sio lazima upate mfano kila mtu anajua hivo na iko huvo....
 
Mkuu Geof niwie radhi kama nilikupandisha BP ila ukweli ndo huo kwamba jamaa arudi home (uza nyumba ujenge heshima bar).

unakumbuka ile story ya Makari Hodari? kuna kawimbo katamu ktk hadithi ile, ila napenda kuimprovise beti ya mwisho isomeke
"baba yake Kimamba (muungwana),
Madonda Kalamba,
Mwanangu (kiraracha) nitie kipamba yoho! yoho!"

kuthibitisha kauli yangu soma quote hii
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Part (TLP) Augustino Mrema, amesema watu wanaosema Rais Jakaya Kikwete amezungukwa na wezi ni wachochezi na wanahatarisha usalama wa taifa.
Mrema aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akichambua kauli za baadhi ya wanasiasa wakongwe ambao pia ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walizozitoa mwezi uliopita kwenye kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF).
Wanasiasa hao wakiongozwa na Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Joseph Butiku, walidai kuwa Rais Kikwete amezungukwa na wezi katika serikali yake na hivyo kumwia vigumu kuchukua maamuzi yoyote magumu kwa mustakabali wa nchi.
Alisema watu wa aina hiyo ni wachochezi na kwamba kauli zao zinatakiwa kukemewa na wananchi wote kwa madai kuwa Rais Kikwete amechaguliwa kwa mujibu wa katiba ya nchi. Wakati Mrema akiwakemea wanasiasa hao, yeye pia aliwahi kutoa kauli kama hizo walizotoa wenzake katika vipindi mbalimbali katika harakati zake za kisiasa hapa nchini mpaka akafikishwa mahakamani ili kuthibitisha kauli yake.
Kati ya madai aliyowahi kuyatoa, kwa mfano, ni pamoja na kusema Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, na mawaziri waandamizi katika serikali yake walihongwa Sh. milioni 900.
Mkutano huo wa Mrema na waandishi wa habari ulisimamiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Clement Mshana.
Aidha, Mrema aliongozana na viongozi wa chama chake akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa TLP, Hamad Tao. Katika kongamano la Mwalimu Nyerere, makada wa CCM na viongozi wa vyama vya upinzani walipata fursa ya kutoa maoni yao ambapo kikubwa walimtaka kujitenga na baadhi ya mafisadi ambao wanatumia nafasi zao kujinufaisha.
Miongoni mwa makada wa CCM walioshiriki katika mkutano huo ni pamoja na Mawaziri Wakuu wastaafu, Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, Joseph Butiku na yeye Mrema alialikwa na alishiriki.
Alipoulizwa ni kwa nini hakutumia nafasi aliyoalikwa katika kongamano hilo kuwaambia makada hao waache kutoa lugha za uchochezi kwa Rais Kikwete, Mrema alikataa kujibu swali hilo na badala yake akamwachia Naibu Katibu Mkuu wake, Tao, ili ajibu.
Tao aliwajibu waandishi wa habari kuwa, Mrema aliomba nafasi ya kuwajibu kwa kunyoosha kidole juu mara tatu lakini mwenyekiti aliyekuwa akiongoza mjadala huo akakataa kumpa nafasi.
Alipoulizwa kuhusu kusema Mkapa alipokea rushwa ya jiwe la dhahabu na kama hiyo haikuwa lugha ya uchochezi inayohatarisha usalama wa nchi, Mrema pia alikataa kujibu swali hilo na kumpa tena Tao alijibu.
Hata hivyo, Tao hakutoa majibu kama swali lilivyotaka isipokuwa alizunguka na kusema kuwa mtu akipewa zawadi inayopitiliza, hiyo inahesabiwa kama rushwa.
Mrema alipobanwa maswali na waandishi wa habari aeleze kama kuna kitu amepewa ili azungumze hayo aliyoyasema alisema yeye hatarajii chochote kutoka kwa Kikwete wala hana mpango wa kutaka kurudi CCM.
"Mimi mwakani naenda kugombea ubunge katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro na najua nitapata tena bila nguvu ya mtu yoyote, hivyo sijikombi kwa Kikwete," alisema.

CHANZO: NIPASHE
 
Wahaya nao hawana msimano. Karamagi katukong'oli na TICTS yake nk.

Mh, Karamagi alituibia akiwa na msimamo aisee ndio maana hakuacha hadi alipoundiwa zengwe... Huu mfano kidogo upo kimtindo, mimi ningesema Lwakatare hana msimamo na Kamara maana nae kabadili maneno kidogo
 
Wala kauli yeyote ile ya Ndugu Mrema yule wa TLP na matendo yake havitakiwi kutushangaza au kutupiga bumbuazi lolote na kwa namna yeyote ile. Huyu jamaa anafahamika kuwa CCM tangu zamani tu na ndiye hasa anayevuruga hata umoja wa wapinzani kutaka kuwa kitu kimoja. Nashauri tusijadili sana suala hili maana litatupotezea muda bure na tunayemjadili yuko tu kama bendera!
 
Kila chama alichoingia amesababisha migogoro mikubwa dhidi ya wale ambao walionesha upinzani wa kweli dhidi ya ccm hivyo baadhi alifanikiwa kuwatimua uanachama n.k.

Amekuwa na hulka (aliyotumwa) kung'ang'ania top post katika kila chama pinzani aendacho na hajawahi kufikiria kuachia madaraka yake. na yeyote atakayempinga ktk uchaguzi mkuu wa chama atamwita all names na zaidi atasema "huyu ni SHUSHUSHU, ametumwa kuniangamiza" ili aonewe huruma na kubakia ktk mamlaka.

Ila kikubwa kilichompeleka upinzani ni hiki anachokifanya sasa.... Baada ya makada (nasema wooote) wa CCM kushindwa kumsafishia njia muungwana kurejea 2010 basi mshkaji ameamua bila soni kuokoa jahazi kwa kutoa fagizi (za kijinga) kwa muungwana. Hasa pale anaposema kwamba kuna hatihati ya ccm kutolewa madarakani (hii inathibitisha kwamba yeye ni mmoja wao) hivyo ni budi mazuri ya muungwana yakaangaliwa ili kumpa nafasi ya muhula wa pili, amekiri kwamba endapo muungwana angekuwa leader miaka ya tisaini asingehama ccm. Ni sawa na muumini ambaye anaamua kumrudia SHETANI anapoona mambo yake hayaendi kinjia mkato! MPINZANI (uchwara) huyu badala ya kufikiria kukiimarisha chama apate kura nyingi mwakani kumbe anaogopa kupewa majukumu ya kuongoza nchi. Sijapata kuona mtu akijibidiisha masomoni ili amwachie mwenzie nafasi ya kwanza darasani.

Je inawezekana kwamba huu ndo muda muafaka wa gladiator (mchovu) kurudi kundini???? Inaonesha Muungwana anamuhitaji na yeye anamuhitaji muungwana. Amechoka na amepoteza haiba

Mkuu, nimeona kwenye news jinsi Mrema anavyojaribu kumtumia JK... kinachonisikitisha ni kwamba ameacha hata kunadi chama chake na sera zake na kwa sasa yuko bize kupigania ubunge wa vunjo, in one of his statement amesema anaweza kugombea ule ubunge bila nguvu ya kuwa CCM... sasa hapo ndipo ninaposikitisha tena!! Yaani sasa hivi amehamishia mawazo kwenye ubunge kabisaaa

Na ile afya yake kwa kweli ni mgogoro...
 
ukweli ni kwamba kwasasa Mrema ni sumu kali sana kufisha au kudhoofisha mageuzi ya kisiasa nchini.
 
Back
Top Bottom