THE OTHER HALF
EPISODE 4
"…katika maisha si lazima kufanya jambo sahihi muda wote. Muhimu zaidi ni kujitahidi kadiri uwezavyo kutimiza unaloliamini… Japokuwa ulimwengu mzima kila upande, kila bara, kila nchi imekuwa na imani yake na kujitahidi kufanya ya kwake wanayoona sahihi na hatimaye kutengeneza utengano, lakini pale ulimwengu mzima unapopambana na adui mmoja, tishio moja, na tunapolia kilio kimoja… huu ndio muda ambao ulimwengu mzima uinuka na kuwa na imani moja, huu ndio muda ambao nguvu iliyopo katika roho ya binadamu udhihirika… tunapopambana wote kwa pamoja, mwishoni mwa vita si sahihi kujiuliza kama tumeshinda au tumeshindwa, jambo la msingi zaidi ni kuhakikisha tunaacha alama juu ya uso wa dunia, ili karne kadhaa zijazo, wataokuwepo wajue sisi tulikuwa ni akina nani, na kwa ushujaa gani tulipambana kutetea Dunia..!"
WASHINGTON, D.C: WHITEHOUSE
Watu wote waliokuwepo Whitehouse ndani ya Situation Room walikuwa wamebaki na mshangao baada ya kuyasikia maelezo ya mzee Caleb.
Wate walikuwa wamepigwa na butwaa wasiamini kile ambacho walikuwa wamekisikia. Walichoelezwa kilikuwa kama kisa cha hadithi ya kusadikika ambayo haiwezekani katika maisha halisi.
Lakini kwa kuzingatia jinsi matukio yaliyokuwa yanatokea duniani haikuwa ngumu sana kwao kuamini hiki walichoelezwa.
Mzee Caleb alikuwa amewasimulia kisa cha zaidi ya miaka elfu kumi iliyopita. Kisa kilihusu uwepo wa kisanduku kinachoitwa Pithos ambacho kilitengenezwa na Mungu wa Kigiriki aliyeitwa Zeus.
Hadithi hii karibu kila mtu duniani alikuwa amewahi kuisikia lakini hakuna mtu ambaye aliwahi kuiamini. Watu wote waliichukulia kama simulizi tu za kale za kusadikika. Ni mpaka dakika hii baada ya mzee Caleb kuwapa maelezo ya kutisha kuhusu simulizi hii walau kulikuwa na watu kadhaa ndani ya situation room ambao walianza kuamini uhalisia wa hadithi hiyo.
Mzee Caleb aliwaeleza kwamba, Mungu Huyo wa Kigiriki, Zeus alikuwa amechukizwa sana na wanadamu ambao kwa kipindi hicho wote walikuwa ni wanaume. Ndipo hapa akamtengeneza mwanmke wa kwanza duniani na kumpa jina la Pandora (likimaanisha "aliyejaliwa kila kitu"). Mwanamke huyu alipewa uzuri usio kifani na ushawishi na mvuto wa kipekee kwa wanaume. Pia Mungu Zeus alimpa mwanamke huyu zawadi ya sanduku ambacho alimuamuri kamwe asikifungue. Ssanduku hiki kilikuwa kimejaa chupa ambazo Mungu Zeus alizijaza kila aina ya udhalimu na ufedhuli uliopo duniani. Na kadiri ambavyo sanduku hili litabakia limefungwa basi dunia itabakia kuwa salama pasipo kushuhudia kiwango kikubwa cha tishio, ukatili au ufedhuli.
Akamsisitiza sharti moja muhimu, kamwe asifungie sanduku hili.
Mzee Caleb akawaeleza kuwa baada ya kufariki kwa mwanamke Pandora, sanduku hili limekuwa likirithishwa kwa siri kubwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Kwa zaidi ya miaka elfu mbili sanduku hili lilikaa sehemu ya siri nchini Ugiriki.
Baadae katika kipindi cha utawala wa mfalme Alexander, akalipeleka sanduku hili nchini Misri ambapo lilikaa hapo kwa Karne kadhaa. Baadae yakatolea matukio na sanduku hili likaenda kuhifadhiwa nchini Israel katika hekalu la mfalme Suleiman.
Baada ya hekalu la mfalme Suleiman kubomelewa baada ya kutamalaki kwa dola ya Rumi, sanduku hili likaenda kuhifadhiwa Vatican katika makazi ya Papa wa Kanisa Katoliki ambapo lilikaa hapo kwa karne nyingi mpaka kufikia karne ya 16 miaka ya 1550 mji wa Vatican ulipovamiwa na kubomolewa kwa kuchomwa moto Sanduku hili lilipotea na halikuwa kuonekana tena.
Mzee Caleb akawaeleza kuwa inasemekana kwamba sanduku hili lilikuja kugunduliwa na maharamia wa kimarekani katika bahari ya Atlantiki mahali fulani baharini miaka ya 1780 na waliloligundua baada ya kulijua ni sanduku la Pandora wakaenda kumkabidhi Rais wa kwanza wa Marekani, George Washington.
George Washington akalificha sanduku hili mahali ambapo ni yeye pekee anajua lilipo na akamtumiachoraji kuchora Picha yake na kuiwekea alama kadhaa za mafumbo ambayo yanamuwezesha mtu kung'amua Sanduku lilipo.
Mafumbo haya ya kwenye mchoro, Rais George Washington alimrithisha siri hii Rais aliyekuja kumrithi John Adams, ambaye naye alipoondoka madarakani akamrithisha siri hii Rais aliyemfuatia Thomas Jefferson, na yeye Jafferson alipoondoka madarakani siri hii akamrithisha Rais James Madison na desturi hii ya kurithishana siri hii imeendelea hivi kwa kila Rais wa Marekani vizazi na vizazi mpaka Rais wa sasa Bi. Laura Keith.
Chumba kizima cha Situation Room kilikuwa kimegubikwa na ukimya wa mshagao na hofu kwa takribani dakika kumi nzima hakuna aliyekohoa wala kujisogeza kwenye kiti. Kila mtu alikuwa kwenye ombwe la mawazo na tafakari kuhusu hiki walichokisikia kutoka kwa mzee Caleb.
"Kwahiyo hayo matukio yanayotokea duniani kote yanahusiana nini na Sanduku hili la Pandora au sijui Pithos… sijaelewa utofauti wake.!" Hatimaye Makamu wa Rais David Logan akavunja ukimya.
"Majina yote mawili ni sawa tu, Jina la 'Sanduku la Pandora' ndilo limezoeleka katika historia, lakini Zeus mwenyewe alivyomtengeneza mwanamke Pandora na kumpa zawadi ya lile sanduku aliliita jina 'Pithos'.! Na nikijibu swali lako sanduku hili linahusiana nini na kinachotokea sasa duniani…. Ni kwamba naamini wale wavuvi nchini Maldives waliookota ile chupa na kuifungua, ile chupa imetoka kwenye sanduku la Pandora… na haikupswa kufunguliwa.. shida imeanzia hapo.!"
Mzee Caleb akajibu.
"Kwahiyo unamaanisha kwamba hiyo sehemu ambayo George Washington alificha hilo sanduku imegunduliwa na sanduku halipo?"
Akauliza Bi. Naomi Cole, mshauri wa Rais kuhusu usalama.
"Hakuna anayeweza kujua ni nini kimetokea na kama sanduku limepota au kuondolewa sehemu iliyohifadhiwa… ila ninachoamini ni kwamba ile chupa imetoka kwenye Pithos, lile sanduku la Pandora.. Na hii inamaanisha kwamba limefunguliwa... Namna pekee tunavyoweza kujinusuru na kinachoendelea duniani kote ni kutafuta mchoro uliopotea wa George Washington ili tuweze kufika sehemu Pithos ilipo na kuirejesha kwenye hali ya kawaida..!" Mzee Caleb akaongea kwa msisitizo mkubwa.
"Ile chupa iliyookotwa na wavuvi kutoka Maldives iko wapi?" Jemedari George Smith akauliza.
"Inafanyiwa utafirti Stanford University idara ya Akiolojia.!" Mkurugenzi wa CIA, James Ruppert akajibu.
"Hii chupa ilikuwa na nini ndani yake?" Mzee Caleb akauliza.
"Ndani ilikuwa na karatasi tu yenye maandishi ya kale mno ya kilatini… neno pekee ambalo tuliweza kulielewa kwenye hiyo karatasi ni 'Novus Ordo Sedorum' ikimaanisha 'The New Order Of Ages'!" Mkurugenzi wa CIA, James Ruppert akaeleza.
Mzee Caleb akashituka kweli kweli.
"Kwanini hamkuiweka hii taarifa kwenye vyombo vya habari, kuhusu hiyo karatasi ni hayo maneno?" Caleb akauliza kwa mshangao mkubwa.
"Ni ngumu kueleza umma kila kitu, taarifa nyingine muhimu ni lazima zibakie kuwa siri… vipi kwani mzee mbona umeshituka sana?" Ruppert akuliza.
"Nahitaji kuiona hiyo karatasi.!!" Mzee Caleb akaongea kwa hofu na kupaniki huku anainuka.
"Oooh samahani mzee! Tueleza nini unafikiria?" Makamu wa Rais akauliza.
"Mheshimiwa, nimesema nahitaji kuiona hiyo karatasi sasa hivi!!" Mzee Caleb akaongea kwa msisitizo huku ametoa macho.
Bila maelezo zaidi wote wakainuka na kuanza kutoka nje. Katibu Mkuu kiongozi mara moja akawajulisha watu wa Secret Service kuaandaa chopa ya Rais Marine One kwa ajili ya kuelekea Stanford University.
Dakika kama tano baadae wote walikuwa mbele ya Marine One.
"Mheshimiwa, sidhani kama kuna ulazima wa wewe kuongozana nasi… ni vyema ukiendelea na majukumu mengine hasa zoezi la kumtafuta Rais! Tuache sisi tuendelee na hili na kisha tukueletee mrejesho!" Ruppert akajaribu kumshawishi Makamu wa Rais abaki.
"Acha kupoteza muda.. Let's gooo!" Makamu wa Rais akajibu kana kwamba hajasikia kilichoongelewa na Mkurugenzi wa CIA na akaamuru wengine wote wapande kwenye chopa na kuondoka.
Wote wakapanda, Makamu wa Rais, Mzee Caleb, Katibu Kiongozi Kevin, Bi. Naomi Cole na Mkurugenzi wa CIA James Ruppert.
Muda si mrefu Marine One ilitua chuo Kikuu cha Stanford.
Baada ya kuwasili, moja kwa moja wakaongozwa na Secret Service mpaka kwenye Jengo la Idara ya Akiolojia.
Na walipofika hapa wakaongozwa moja kwa moja mpaka kwenye maabara inayotumia kuhifadhi vitu vya kale.
Makamu wa Rais na msafara wake walipoingia ndani ya maabara hii waliwakuta wenyeji wao, wataalamu wa Akiolojia wanawasubiri, lakini ajabu ni kwamba walikuwa na hofu kubwa kwenye nyuso zao.
Baada ya kusalimiana nao Makamu wa Rais akaanza kuongea.
"OK! Nadhani mnafahamu kwanini tuko hapa?? Tunahitaji kuona chupa ambayo iliokotwa na wavuvi nchini Maldives na hasa hasa tunahitaji kuona karatasi ambayo ilikutwa ndani yake.!" Makamu wa Rais, David Logan akaongea.
"Mr. Vice President nasikitika kukwambia kuwa chupa hiyo wala karatasi yake hatunayo?" Mtaalamu mmoja aliyevalia miwani kubwa ya macho akaongea kwa woga na heshima kubwa.
"Nini??? Imeenda wapi?" Makamu wa Rais akauliza kwa hasira.
"Chupa huwa inahifadhiwa kwenye jokofu hili hapa la chini ya sentigredi za selsiasi -18 ili ibakie kwenye hali yake ya asili… lakini leo tulivyoambiwa kuwa unakuja kwa ajili ya chupa hii.. Tulipoitoa chupa kwenye jokofu ili tuiandae upate kuiona, tukagundua kuwa chupa iliyomo ni feki.. Imebadilishwa.. Na tunaamini ni mmoja kati yetu kwenye idara ndio amefanya hilo!" Yule mtaalamu akajieleza.
"Ni nani? Na amefanya hivyo kwa dhamira ipi?"
"Tunaamini ni Dr. Cindy Wheaton amefanya hivi… yeye ndiye alikuwa in charge kwa chupa hii na kuongoza tafiti.!"
"Yuko wapi?" Makamu wa Rais akauliza kwa hasira.
"Ameenda Tanzania wiki ya Tatu hii sasa… ameenda kufanya tafiti kuna miji mitatu nchini humo imetwaliwa na kuwa Anabelle.!"
Alipoongea sentesi hii mzee Caleb alishituka na kuishiwa nguvu mpaka kukaa chini.
"No no no no.! Siamini kama anataka kufanya ninachokiwaza… no no.! Tafuteni mawasiliano naye haraka niseme naye!!" Mzee Caleb akaongea huku anakaa chini kwa hofu na kunyong'onyea.
"Ni nini mzee?" Ruppert akauliza.
ITAENDELEA JUMNANNE..