The Other Half (Simulizi)

The Other Half (Simulizi)

jina la hiyo blog wadau najua kuweka link jau.. tupeni jina tu hayo mengine ya dotcom tutajiongeza wenyewe
 
Tovuti inaitwa digitaldrimz Africa.com

Ukiingia nenda kwenye option ya short story utazikuta.
shukrani saanaa mkuu nimeipata.. pale stori inaishia ep36,jamaa labda alitoa utaratibu mwingine wa jinsi yakumalizia stori labda?
 
aisee hili ni bonge moja la fasihi nilowahi kukutana nalo aisee!! kila kitu humu kwenye stori kimepigiwa mahesabu makali yani calculator,compass,kamusi na lile jedwali la kemikali na makorokocho yote yakitaallam yametumika kuandaa hili season. Mkuu THE BOLD wewe una balaaaa
 
shukrani saanaa mkuu nimeipata.. pale stori inaishia ep36,jamaa labda alitoa utaratibu mwingine wa jinsi yakumalizia stori labda?
Usijali mkuu, endelea sehemu ya 37 kwenye huu Uzi hadi sehemu alipoishia nimesahau sehemu ya ngapi, ila tafuta umu utaziona zimefuatana.
 
THE OTHER HALF


SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE



EPISODE 43



Mara kadhaa ulimwengu umewahi kufikia katika mstari wa mwisho kabisa ambao kama ungevuka mstari huu basi ndio ungekuwa mwisho wa ustaarabu ambao binadamu amepambana maelfu ya miaka kuujenga. Katika vitabu vya kale tunaelezwa kuwa ulimwengu uliwahi kufika kwenye mstari huu kipindi cha Nuhu. Lakini pia ulimwengu ulifika tena kwenye mstari huu kwenye karne ya 7 AD na pia karne ya 16 AD.
Lakini katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni tumekuwa tukiufikia mstari huu kwa mara nyingi ndani ya muda mchache. Ndani ya miaka mia moja pekee iliyopita tumefikia mstari huu mara mbili. Mara ya kwanza ilikuwa 1914 - 1945 na mara ya pili ilikuwa mwaka 1939 - 1945.
Kabla ya hapa zilikuwa zinapita karne kadhaa au hata maelfu kadhaa ya miaka kabla ya kuufikia mstari huu tena. Lakini ni ajabu kwamba kwa kipindo cha miaka mia moja pekee tumefikia mstari huu mara mbili. Pangine hii ilikuwa ni dalili. Dalili ya kile ambacho kitafuata. Dalili ya kitakachotokea mwaka 2038. Dalili ya ulimwengu mzima siku moja kugeika kuwa Anabelle.



Rabat, Morocco

Wote watatu walikuwa wamesimama kwa tahadhali wakiwa wamemkodolea macho Logan pale ambako alikuwa amesimama. Kutokana na alivyo uchi wa mnyama na hasira ambazo alikuwa nazo usoni, Logan alikuwa anaonekana kama vile mnyama.

Cindy, Salim na Magdalena walikuwa wanapiga hatua za taratibu sana kurudi nyuma mlangoni, Logan naye alikuwa anapiga hatua za taratibu kuwafuata. Walikuwa wamekaziana macho kama wanataka kurukiana.

"Jina lako ni Logan. Wewe ni Makamu wa Rais wa taifa la Marekani na sisi sio adui zako.!" Cindy aliongea kwa tahadhali huku yeye na wenzake wakiendelea kurudi nyuma.

Logan hakuongea chochote kile, hasira usoni mwake zilizidi kuwa dhahiri zaidi. Alikuwa amepandwa na hasira kiasi kwamba mpaka mwili ulikuwa unatetemeka.

Salim kutokana na uzoefu wake wa masuala ya intelijensia na mambo ya ulinzi alijua ni nini ambacho kilikuwa kinafuata. Wakati wenzake wakirudi nyuma yeye akabakia kama hatua mbili hivi mbele yao. Akawa kama ngao ya wenzake.

"Salim? Unafanya nini?" Magdalena aliongea kwa mshituko baada ya kuona Salim akiwa amebaki mbele na harudi tena nyuma pamoja nao.

"Eidha tumdhuru au atudhuru… siko tayari kufa kirahisi hivi.." Salim aliongea huku akiwa amemkazia macho Logan ambaye walokuwa wamesogeleana kubakia kama hatua tano tu kati yao.

"Hapana Salim! Tafadhali…."

"Magdalena! kaa kimya!!" Salim aliongea kwa ukali kumnyamazisha Magdalena asiendelee kuongea.

Zilikuwa zimebakia kama hatua tatu tu sasa kutoka mahala ambako alisimama Salim na alipo Logan.

Logan alikuwa kama amepandwa na 'mzuka'. Alikuwa anatetemeka mpaka meno yanagongana. Alikuwa na hasira haswa. Alitumbua macho kumtazama Salim. Salim naye alimkazia macho bila kutingishika hata kidogo.
Ghafla Logan akaruka kama mnyama kumvamia Salim. Salim alionekana dhahiri kwamba alikuwa anatarajia Logan angefanya hivyo, alimkinga kwa mikono yake miwili ili asimvae mwilini na kisha akamsukuma kwa nguvu na Logan kuanguka kwa kishindo sakafuni. Akiwa sakafuni anapaparika ili ajiinue na kugeuka, Salim alimrukia mgongoni na kuanza kumshindilia ngumi mfululizo.

Ilikuwa ni kana kwamba kuangalia mchezo wa watu wanaopanda ng'ombe dume mgongoni na kuanza kuruka ruka nao.
Salim alikuwa juu ya mgongo wa Logan akimshindilia ngumi. Logan alikuwa anaruka ruka na kupaparika ili kujinusuru.

"Noooo Salim! Nooo..!" Magdalena na Cindy walikuwa wanapiga kelele kwa pamoja kumsihi Salim asiendelee na shambulizi hilo ili wote wawili asije mmoja wao kudhulika.


"Ole wako ufanye ujinga mwingine!"
Cindy akatoa mkwara.

"Nini kinaendelea?" Salim akauliza.

"Ameanza kukumbuka… anakumbuka jina la mwanaye Natalie… ndilo ananong'ona hapo muda woye huu!" Cindy akamfafanulia.

Cindy akachuchumaa chini kumkaribia Logan pale sakafuni alipokuwa amejikunyata. Kisha akanyoosha mkono na kumgusa taratibu mgongoni.
Logan alifyatuka kama vile alikuwa ameguswa na nyoka. Akasogea pembeni kabisa ukutani.

Kwa mara ya kwanza tangu adondoke pale sakafuni aliinua uso na kuwatazama. Uso wake sasa hivi ulikuwa umejawa na woga na si hasira tena. Alikuwa anawatazama kwa macho ya woga kiasi kwamba ilikuwa inaumiza moyo. Ilikuwa inapasua moyo kumuona mtu muhimu na mwenye nguvu kubwa duniani kama Logan katika hali hii, akiwa uchi wa mnyama, damu zinamvuja huku amejawa na woga na wasiwasi usoni.

"Hey! Its ok… hatuko hapa kukudhuru, sisi ni marafiki kabisa kwako… tafadhali usiogope.! Cindy aliongea kwa sauti ya upole na taratibu sana ili kumtoa hofu Logan.

Logan bado alikuwa anawaangalia kwa mshangao na hofu kana kwamba ndio kwanza amewaona.

"Mheshimiwa tafadhali kama unaweza kukumbuka chochote namna gani ulifika hapa, nani alikuleta na ni maswali gani ambayo walikuuliza… chochote unachoweza kukumbuka muheshimiwa kitakuwa na msaada mkubwa sana.!" Cindy aliongea kwa upole na kubembeleza.

Logan aliwatumbulia macho tu. Lakini safari hii alikuwa anawaangalia kwa 'upeo wa kupitiliza'. Yaani alikuwa anawatazama lakini kama vile akili yake ilikuwa mbali inatafakari. Kama vile anaangalia kitu kilichombali sana kuzidi akina Cindy walio mbele yake.

"Natalie..!" Logan alitamka tena jina la mwanaye. Safari hii alilitamka sawia bila kunong'ona. Alilitamka huku machozi yakiwa yanamlenga lenga.

"Natalie amefanyaje muheshimiwa?" Cindy akauliza.

"Namuhitaji Natalie.!" Logan aliongea kwa upole huku anamtazama Cindy.

"Muheshimiwa nina wasiwasi hilo halitowezekana kwa sasa." Cindy alijibu.

"Kwa nini?"

"Natalie yuko nyumbani Marekani… hapa tulipo ni Rabat, Morocco!" Cindy alimfafanulia.

"Rabat!" Logan alihamaki.

"Ndio muheshimiwa… tuko Rabat."

"No no nooo!! Haiwezekani.." Logan alitaharuki huku anaanza kujikongoja na kuinuka.

"Haiwezekani nini muheshimiwa?" Cindy aliuliza kwa mshangao kidogo.

"Haiwezekani kuwa Rabat!! No no nooo haiwezekani…" Logan aliongea kwa kuchanganyikiwa huku anashika kichwa na kuanza kutembea tembea pale chumbani.

Salim alikuwa amekuja na nguo fulani hivi kama shuka jeusi, akampatia Logan ili aweze kujisitiri.

"Muheshimiwa kwa nini unasema haiwezekani kuwa Rabat?" Cindy aliuliza tena kwa udadisi.

"Walisema kuwa makao makuu yako jangwa la Nevada." Logan aliongea huku amejiinamia chini kama amechanganyikiwa na habari hizi za kwamba wapo Rabat, Morocco.

"Makao makuu ya nini? Nani hao waliosema?" Cindy aliuliza kwa mshangao mkubwa.

Wote mle ndani ghafla walikumbwa na mshtuko baada ya kumsikia Logan akisema kwamba, "Walisema kuwa makao makuu yako jangwa la Nevada!"

Wakati wao wakimshangaa, naye Logan aliinua uso na kuwashangaa. Dhahiri kwamba alikuwa anawashangaa kwa kushindwa kuelewa kile ambacho alikisema. Alikuwa anawaangalia kwa uso fulani hivi wa mashaka. Inaonekana kwamba alisema kile alichokisema kwa kuamini kwamba akina Cindy wataelewa. Kitendo cha akina Cindy kutoelewa kulimfanya awaangalie kwa mashaka na mshangao.

"Who are you guys?" Logan aliwauliza huku anawaangalia kwa mashaka.

"We are the good guys… please stay calm!" Cindy alijitajidi kumtoa hofu.

"I asked who are you!" Logan aliuliza kwa sauti ya ukali kidogo na kumaanisha.

"Ok ok muheshimiwa.! Mimi naitwa Cindy, raia wa Marekani na ni mwana akiolojia… huyu hapa anaitwa Salim ni afisa usalama kutoa TISS nchini Tanzania… na huyu hapa anaitwa Magdalena ni mwana baiolojia kutoka chuko kikuu cha Kenyatta nchini Kenya… tumepitia mambo mengi sana ila kwa kifupi tuliingia kwenye Anabelle 27 ambao ulikuwa ni mji wa Dar es Salaam nchini Tanzania kufanya utafiti… baadae tukafanikiwa kutoka na kujikuta tuko pwani ya hapa Rabat Morocco na baadae baada ya kufuatilia nyayo pale kwenye mchanga wa pwani


Lakini Salim alikuwa kana kwamba na yeye amepandwa na shetani. Aliendelea kumtandika Logan ngumi mfululizo kama vile alikuwa asikii vilio vya akija Cindy wakimsihi.

Ghafla damu zikaanza kutapakaa pale sakafuni. Logan alikuwa ameanza kuvuja damu usoni kutokana na kipigo kikali ambacho kilikuwa kinaendelea pia damu ilikuwa inatoka na mwilini ambako alikiwa na majeraha makubwa ambayo alikuwa nayo tangu wamemkuta hapo kutokana na kuteswa na watu ambao walikuwa wamemteka. kutokana na kipigo kikali ambacho kilikuwa kinaendelea. Damu zilikuwa zinamwagika haswa. Logan licha ya akili zake kuchezewa na kuwa na hasira kama mnyama lakini alionekana kushindwa kumudu umahiri wa mwana usalama Salim. Au labda aliwahiwa au kuzidiwa ujanja.

"Salim utamuua!! Hapanaaaaa Salim… Saliiiimmm…"

Cindy ana Magdaelena waliendelea kupiga kelele kumsihi Salim asiendelee kushusha kipigo.
Magdalena ilimbidi ajitose na kumrukia Salim mgongoni. Maana yake sasa mgongoni kwa Logan kulikuwa na Salim pamoja na Magdalena. Kutokana na uzito wote watatu wakadondoka chini Sakafuni. Magdalena alimng'ang'ania Salim kama vile wapigana mieleka wanavyokabana kabali. Alimshikilia kwa nguvu zake zote huku akimnasua kutoka kwa Logan.

"Stop it Salim… please stop!" Magdalena aliongea kwa uchungu karibia na kulia.

Hatimaye alifanikiwa kuwaachanisha. Salim alikuwa anahema kama mbwa. Logan alilala chini kwa maumivu akiwa amejikunyata kama katoto kadogo.

"Nimekwambia sisi sio adui zako… tuko hapa kwa ajili ya kusaidia… kwa hiyo tuambie nini kimetokea hapa la sivyo…" Salim alikuwa anaongea kwa hasira huku anahema kama mbwa.

"Toka nje Salim… toka nje.." Cindy alifoka.

Ilibidi Magdalena amkokote Salim mpaka nje ili kumuweka mbali na Logan.

"Tafadhali Salim… kuwa mtulivu, unachokifanya akisaidii chochote zaidi ya kuongeza mkanganyiko!" Magdalena alimsihi Salim baada ya wote kutoka nje ya chumba kile walichomuacha Cindy na Logan.

"Alikuwa anataka kutuvamia na kuturarua… unataka kusema hakuona usoni mwake? Nisingemvamia kwanza tungekuwa chakula chake leo..!"

Salim aliongea kwa pupa huku bado anahema kama mbwa. Dhahiri kabisa akili yake bado ililiwa haijatulia.

"Tafadhali kaa hapa na usubiri!" Magdalena alimuamuru kama vile alikiwa anaongea na mtoto mdogo.

Magdalena alimuacha Salim hapo nje ya chumba na kurudi tena ndani.

"Nahisi akili yake imeanza kukaa sawa kiasi." Cindy akaongea mara tu baada ya Magdalena kurudi ndani.

"Nani? Salim? Bado anahema tu kama mbwa utadhani ameingiwa na shetani rohoni.!" Magdalena akajibu.

"Hapana Magdalena… namuongelea Logan! Naona akili zinaanza kumrejea taratibu. Kipigo kimesaidia ah" Cindy akafafanua huku akimalizia na sentesi ya utani na kumkonyeza Magdalena.

"Kwa nini unasema akili zimeanza kurudi?" Magdalena aliuliza kwa shauku kubwa.

"Msikilize..!"


"Na…na…nat… na… nat!"

Loga alikuwa amejikunyata sakafuni kama mtoto huku ananong'ona kitu fulani.

"Sielewi anachokisema!" Magdalena akaongea kwa kukata tamaa.

"Msikilize kwa umakini."

Magdalena ilimbidi mpaka apige magoti chini ili kuinamisha kichwa karibu na Logan na kutega sikio asikie kile ambacho Logan alikuwa anakizungumza.

"Na…na…nat…natalie… natalie!" Logan alinong'ona.

"Natalie??" Magdalena aliinuka na kumuuliza Cindy kwa mshangao.

"Yes Natalie! Ni jina la mtoto wake, mwanaye wa pekee." Cindy akajibu huku usoni akiwa na tabasamu la matumanini.

"Ameanza kukumbuka?" Magdaleba akauliza kwa shauku.

"Yes.! Naamini ameanza kukumbuka sasa… kama amekumbuka jina la mwanaye nahisi kumbukumbu zimeanza kurejea kichwani. "Muite Salim!"

"Wa nini? Aisije akafanya uninga mwingine."

"Hapana muite… anapaswa kujua hili."

Magdalena akatoka nje kwa haraka na kama baada ya dakika moja akarejea akiwa ameongozana na Salim wakitemvea kwa haraka na shauku.

"Inaonekana ngumi zangu zimesaidia kumtikisa ubongo!" Salim akaongea kwa utani mara tu baada ya kuingia ndani.

"Unasema mliingia ndani ya Anabelle?? Hakuna ambaye amewahi kuingia ndani ya Anabelle na kutoka." Logan aliwauliza kiudadisi.

"Ni kisa kirefu muheshimiwa.!" Cindy hakutaka kuanza kusimulia maswahibu ambayo walikuwa wamepitia mpaka kufika hapo.

"Una uhakika tuko Morocco?" Logan alimuuliza Cindy.

"Nina hakika kwa asilimia mia moja muheshimiwa kwamba hapa ni Rabat, Morocco."

Logan akajiinamia tena kama anatafakari hivi.

"Kwa nini walisema makao makuu yako jangwani Nevada?" Logan aliongea peke yake huku bado akiwa amejiinamia.

"Nani Muheshimiwa aliyesema makao makuu yako jangwani Nevada? Makao makuu ya nini?" Cindy akauliza tena kwa udadisi zaidi.

"Twendeni niwaonyeshe kitu.."

Logan aliongea na kuanza kutoka nje ya chumba huku Cindy na wenzake wakimfuatia nyuma kwa shauku kubwa.



NAVAL OBSERVATORY CIRCLE - YALIPO MAKAZI WA MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI

Wote watatu walikuwa wameingia ndani ya kichumba kile kidogo. Ron, Latisha na Natalie.

Kijichumba hiki kidogo kilikiwa nadhifu mno kilichopakwa rangi ya kijivu chumba kizima. Vitu pekee ndani ya chumba hiki vilikuwa kabati dogo la kioo lilipo upande wa kulia ukiingia ndani ya hiki kijichumba, kabati ambalo ndani yake kulikuwa na kitu kimoja tu, kompyuta mpakato.
Pia kulikuwa na kiti cha kukaa cha kiofisi kilichopo upande mwingine wa chumba na mbele yake kulikuwa na kamera iliyo kwenye kwenye stendi yake ya kurekodia.

Japokuwa ndani ya kichumba kile kulikuwa na vitu kadhaa lakini wote macho yao yalitua kwenye ile kompyuta mpakato ambayo ilikuwa ndani ya kikabati kile kodogo cha kioo.

"What happened to you Logan… what where you doing here?" Latisha aliongea kwa masikitiko kuonyesha maumivu ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Ilikuwa inamuuma moyo kuona kwamba mtu aliyempenda sana, mtu mchangamfu, mwenye kupenda urafiki na watu, mwenye kupenda kwenda 'out' kila siku ati kumbe alikuwa na kijichumba cha siri cha namna hii. Kijichumba ambacho kamera iliyopo hapa inaonyesha alikuwa akijirekodi jumbe za siri ili kweka kumbukumbu.
Latisha aliumia moyo akijiuliza ni nini kilitokea au nini ambacho mume wake huyo wa zamani alikijua na kumbadili Logan kuwa mtu wa namna hii.

"Nadhani tutazame humu.!"

Wote waligutushwa kutoka kwenye mawazo na sauti ya Natalie ambaye tayari alikuwa ameshikilia laptop mkononi kutoka kwenye kile kijikabati.

"Wow! Hutaki kupoteza muda… hebu tuone." Ron aliongea na kuchukua laptop kutoka mkononi mwa Natalie na kuiweka juu ya kiti.
Akaifunua kwa haraka na kisha kuiwasha. Uzuri haikuwa na neno la siri, kuonyesga dhahiri kwamba Logan alitaka mtu atakayeipata kuona kilichomo ndani yake.

Baada ya Laptop kuwaka, juu yake kwenye uwanja wa 'desktop' kulikuwa na mafaili kadhaa… kama kumi hivi au zaidi. Yote yalikuwa na tarehe tofauti. Ron akabofya faili la kwanza ambalo lilikuwa juu kabisa kushoto mwanzoni. Ndani ya file kulikuwa na 'Video'. Ron akaibofya video na ikaanza kucheza.

Kwenye screen alitokea Logan… alikuwa anaangalia mbele moja kwa moja. Inaonekana kipindi alipokuwa anajirekodi kichwani mwake hakuwa anaiwaza kamera iliyo mbele yake bali alikuwa anamuwaza huyo ambaye ataenda kuitazama video hii. Alikuwa anamuwaza mwanaye wa pekee, Natalie.
Aliangalia mbele kwa muda mrefu sana bila kusema chochote. Machozi kama yalianza kumlenga lenga hivi. Natalie ambaye alikuwa akiangalia na kina Ron na Mama yake, tayari machozi yalikuwa yana tiririka shavuni.

Ilikuwa dhahiri kwamba Logan alikuwa anataka kuongea lakini alikuwa anshindwa kupata nguvu ya kusema kile ambacho alikuwa anataka kukisema. Akajiinamia kidogo hivi na kupeleza mkono wake machoni kuzuia yale machozi yaliyokuwa yanataka kudondoka. Kisha akainua uso na kutazama mbele tena na kisha kuanza kuongea.

"Mwanangu… kama unatazama ujumbe huu naamini uko mpweke hapo ulipo. Uko mpweke nafsini mwako. Labda kitu pekee kilichobakia cha kukufariji ni ujumbe huu. Sijui kama kuna yeyote aliyesalimika duniani. Sijui kama tumeshinda au tumeshindwa. Sijui. Kwa mambo niliyoyaona na yale ambayo naamini yatatokea nashindwa hata kupata maana halisi ya ushindi au ladha yake. Vyovyote vile lakini naamini huu ni mwisho wa ustaarabu wa dunia uliyokuwa unaijua. Sitaki kukuacha na maswali baba yako alikiwa ni mtu wa namna gani, na sitaki ubaki na maswali ni namna gani dunia imefikia hapa… kwa hiyo wacha nikueleze sisi tulikuwa ni akina nani… na wacha nikueleze wewe ni nani.! Na la msingi zaidi, wacha nikueleze ni namna gani nimepambana."



Itaendelea…


The Bold - 0718 096 811
To Infinity and Beyond

WhatsApp, Subscribe and Follow
IMG-20180514-WA0050.jpg
 
Yajayo yanatisha. Shukrani sana mkuu Habib Anga. Msalimie sana Shunie mwambie namshuru sana kwa mkufu wa malkia wa Goshen. Kitu kilinipa raha sana kwa kipindi hicho. Mpaka story ikawa imeisha mm nikawa naona kama bado hivi.
 
Yajayo yanatisha. Shukrani sana mkuu Habib Anga. Msalimie sana Shunie mwambie namshuru sana kwa mkufu wa malkia wa Goshen. Kitu kilinipa raha sana kwa kipindi hicho. Mpaka story ikawa imeisha mm nikawa naona kama bado hivi.
Khaaaaa mwenyewe si nipo hapa The Bold ananijulia wapi mm mpaka umpe salaam zangu mkuu jamani
 
Back
Top Bottom