Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,748
- Thread starter
- #561
THE OTHER HALF
SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE
EPISODE 40
"Giza…. Giza nene ndio kitu cha kwanza ninachokumbuka, kulikuwa na giza nene, kulikuwa na baridi kali... Nilijawa woga! Kadiri ambavyo niliitamani kesho ndivyo ambavyo kesho ilizidi kuwa mbali kuzidi Jana… Jana ilikuwa inaonekana karibu zaidi na yenye kuwezekana kushinda kesho… imekuwa muda mrefu sana kiasi kwamba siwezi kuona tafouti ya uhalisia na maluweluwe… kitu pekee kilicho halisi kwangu ni giza nene na baridi Kali.!"
"Unakumbuka jina lako?" Akamuuliza tena.
Hakujibu moja kwa moja badala yake alijiinamia chini kwa dakika kadhaa. Haikuwa dhahiri kama alikuwa hajaelewa swali au labda alikuwa anafikiri au kujaribu kukumbuka.
Lakini kukumbuka nini? Jina lake?
"Jina langu?" Akainua kichwa chake na kuuliza swali badala ya kutoa jibu.
"Ndio jina lako… unalifahamu?" Akamuuliza tena.
"Nimekuwa mpweke kwa muda mrefu mno kiasi kwamba sikumbuki hata jina langu..." Akajibu akiwa amejiinamia tena kwa huzuni na uchungu.
Ilikuwa inaumiza moyo kumuona namna hii katika hali hii. Akiwa amechanganyikiwa kiasi hiki, kana kwamba uhalisia haukuwa na maana tena kwake.
Cindy akachuchumaa ili awe kwenye usawa mmoja wa uso kati yao.
"Unakumbuka nini?" Cindy alimuuliza kwa sauti ya taratibu ya uchungu.
Akajiinamia chini tena kukwepesha macho yake na Cindy. Sijui ilikuwa ni woga, aibu au alikuwa anatafakari tena. Lakini alijiinamia chini kwa uchungu na huzuni kubwa.
"Nakumbuka maumivu… maumivu yaliyodumu kwa muda mrefu zaidi kuliko nilivyovuta pumzi… mpaka muda huu nashangazwa hata imekuwaje bado niko hai, lakini naamini maumivu yale ndiyo yaliyofanya niupe uhai wangu thamani… kuna muda nilitamani kuukatisha uhai wangu alimradi tu maumivu yakome… kuna muda nilihisi kabisa siwezi kwenda mbele… kwa hiyo binti yangu hakuna ninachokikumbuka zaidi ya maumivu, maumivu makali na kiza kinene, baridi kali na woga.!"
Kumbukumbu hii ya maumivu japo haikumfanya akumbuke chochote cha maana lakini zilimrejeshea kumbukumbu ya maumivu aliyopitia, kumbukumbu ambayo alijitahidi kuiweka nyuma ya ubongo wake na kamwe asiitafakari.
Cindy akainua mikono yake taratibu na kumshika usoni. Uchungu ambao Cindy alikuwa anausikia moyoni mwake ulisababisha mpaka chozi limdondoke.
Akamshika kwa hisia kali uso wake na kumuangalia kwa mkazo ndani ya macho yake akiwa anabubujikwa na machozi.
"Wewe ni imara kuliko unavyodhani, kama usingali kuwa imara basi tusingekukuta hapa leo hii… Japo haukumbuki chochote lakini naomba uniamini hiki ninachokieleza… Jina lako unaitwa David Logan na wewe ni makamu wangu wa Rais nyumbani, Makamu wa Rais wa taifa la Marekani.!" Cindy akaongea kwa uchungu akitokwa machozi mapaka anatetemeka.
David Logan, Makamu wa Rais wa Marekani alikuwa chini sakafuni ameketi akiwa uchi kabisa amekondeana kiasi kwamba mpaka uso wake ulikuwa umebadilika. Alikuwa amedhohofu haswa. Mwili wake ulikuwa umejawa na makovu ya majeraha kila mahala kutokana na mateso ya muda mrefu ambayo alikuwa amepitia.
Alimkazia macho Cindy kwa mshangao kama vile alikuwa haamini au haelewi ni nini hasa alikuwa anamueleza.
"David Logan.? David Logan.? Hilo ndilo jina langu? Uhn David Logan.!!" Aliongea kwa kurudia rudia huku machozi yakimtoka taratibu na kutiririka mashavuni.
"Ndio… jina lako unaitwa David Logan na wewe ni Makamu wa Rais wa taifa Marekani… sijui umefika vipi hapa au nini kimetokea lakini nahitaji ujitahidi kukumbuka kwa nini umeletwa hapa? Kwa nini ulikuwa unateswa?"
"Kwa nini unataka kujua?" David Logan aliuliza kwa kushangaa kidogo.
"Ulimwengu mzima uko katika tishio la kuangamia na jibu lako wewe linaweza kuwa hatua ya kuepukana na tishio hilo!"
"Uhn nani? Mimi?" Logan aliongea kwa kujidharau kwa kujiona hakuwa anastahili kuwa na umuhimu wowote ule wa kuwa tegemeo la kuokoa ulimwengu kutoka kwenye kuangamia.
"Tishio gani? Jibu gani unataka?" Akauliza akiwa bado kama haamini kile ambacho alikuwa anaelezwa.
"Muheshimiwa sitaki kukuchanganya zaidi ya hivi ulivyo sasa… naomba ujaribu kukumbuka chochote kile, umefikaje hapa? Waliokuleta walikuuliza nini? Jitahidi kukumbuka Muheshimiwa!" Cindy alimuuliza kwa msisitizo.
Ubaya zaidi pia walikuwa hawajui kuwa David Logan alitekwa na watu wasiojulikana kutoka nyumbani kwake Naval Observatory Circle kwani lilipotokea tukio hili wao walikuwa tayari wako ndani ya Anabelle 27 (Dar es Salaam).
"Kwa nini wamemuacha hapa? Wao wenyewe wako wapi? Huu sio mtego?" Salim akauliza.
"Inawezekana! Sijui…" Cindy alijibu kwa kitete.
"Wana sababu gani kumuacha hapa? Kwa nini wasiende naye? Kama walihisi hawamuhitaji kwa nini wasimuue? Kwa nini wamuache hapa? Wenyewe wameenda wapi? Nina hisia mbaya Cindy..!!" Salim aliongea kwa wasiwasi huku anatamaza huku na huko pale chumbani kana kwamba muda wowote wenye Kasri lao wanaweza kutokea muda wowote ule.
"Ngoja tujaribu tena kupata majibu!"
Cindy aliongea huku wanaondoka kutoka pembeni ya chumba walipokuwa wanateta na kurejea pale alipo Logan na Magdalena.
"Kuna mafanikio yoyote?" Cindy alimuuliza Magdalena huku akamshika bega kuashiria kuwa asogee pembeni ili yeye aendelee.
"Hakuna kitu! Jaribu bahati yako…" Magdalena aliongea huku anasogea pembeni.
Cindy akachuchumaa tena ili awe usawa mmoja wa macho na Logan kisha akaanza tena maongezi.
"Muheshimiwa natamani sana ukumbuke kitu chochote kile… hata kama ni kidogo kiasi gani?" Cindy aliongea kwa msisitizo huku akimuangalia kwa huruma.
"Giza…. Giza nene ndio kitu cha kwanza ninachokumbuka, kulikuwa na giza nene, kulikuwa na baridi kali... Nilijawa woga! Kadiri ambavyo niliitamani kesho ndivyo ambavyo kesho ilizidi kuwa mbali kuzidi Jana… Jana ilikuwa inaonekana karibu zaidi na yenye kuwekzekana kishinda kesho… imekuwa muda mrefu sana kiasi kwamba siwezi kuona tafouti ya uhalisia na maluweluwe… kitu pekee kilicho halisi kwangu ni giza nene na baridi Kali.!"
Logan alijibu kwa kutamaka maneno yale yale ambayo aliyatamka awali. Neno kwa neno, sentensi kwa sentesi.
Wote walishituka kana kwamba wamesikia sauti ya jini au mzimu. Hawakuamini macho yao kile ambacho waliking'amua ghafla.
"He has been hypnotized…" (Amepumbazwa) Salim na Cindy waliongea kwa pamoja mshituko mkubwa.
"Nini?" Magdalena akauliza kwa mshangao.
"Wamempumbaza ufahamu wake na kumpandikizia maneno kwa kumkaririsha… hypnosis!" Salim aliongea kwa woga.
"Hapa ni sawa kama vile tunaongea na roboti tu!" Cindy akaongezea.
"Kama wamempampumbaza na kumpandikiza maneno ya kuongea hamdhani kwamba walijua kuwa tutakuja hapa? Hamdhani kuwa huu ni mtego? Na je ni kitu gani kingine wamempandikizia?" Magdalena aliongea kwa woga.
Wote watatu macho yao yakatua kwa David Logan. Ajabu ni kwamba David Logan ambaye muda mchache uliopita alikuwa analia na kujiinamia lakini safari hii aliwatazama kwa kuwakazia macho kwa hasira huku anasimama kutoka pale sakafuni ambako alikuwa ameketi.
"Nahisi nimeanza kuelewa nini kinaendelea!" Salim aliongea huku anawarudisha wenzake nyuma kwa tahadhari mbali na David Logan.
Itaendelea…
THE BOLD - 0718 096 811
To Infinity and Beyond
Pls: WhatsApp, Follow and Subscribe
SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE
EPISODE 40
"Giza…. Giza nene ndio kitu cha kwanza ninachokumbuka, kulikuwa na giza nene, kulikuwa na baridi kali... Nilijawa woga! Kadiri ambavyo niliitamani kesho ndivyo ambavyo kesho ilizidi kuwa mbali kuzidi Jana… Jana ilikuwa inaonekana karibu zaidi na yenye kuwezekana kushinda kesho… imekuwa muda mrefu sana kiasi kwamba siwezi kuona tafouti ya uhalisia na maluweluwe… kitu pekee kilicho halisi kwangu ni giza nene na baridi Kali.!"
"Unakumbuka jina lako?" Akamuuliza tena.
Hakujibu moja kwa moja badala yake alijiinamia chini kwa dakika kadhaa. Haikuwa dhahiri kama alikuwa hajaelewa swali au labda alikuwa anafikiri au kujaribu kukumbuka.
Lakini kukumbuka nini? Jina lake?
"Jina langu?" Akainua kichwa chake na kuuliza swali badala ya kutoa jibu.
"Ndio jina lako… unalifahamu?" Akamuuliza tena.
"Nimekuwa mpweke kwa muda mrefu mno kiasi kwamba sikumbuki hata jina langu..." Akajibu akiwa amejiinamia tena kwa huzuni na uchungu.
Ilikuwa inaumiza moyo kumuona namna hii katika hali hii. Akiwa amechanganyikiwa kiasi hiki, kana kwamba uhalisia haukuwa na maana tena kwake.
Cindy akachuchumaa ili awe kwenye usawa mmoja wa uso kati yao.
"Unakumbuka nini?" Cindy alimuuliza kwa sauti ya taratibu ya uchungu.
Akajiinamia chini tena kukwepesha macho yake na Cindy. Sijui ilikuwa ni woga, aibu au alikuwa anatafakari tena. Lakini alijiinamia chini kwa uchungu na huzuni kubwa.
"Nakumbuka maumivu… maumivu yaliyodumu kwa muda mrefu zaidi kuliko nilivyovuta pumzi… mpaka muda huu nashangazwa hata imekuwaje bado niko hai, lakini naamini maumivu yale ndiyo yaliyofanya niupe uhai wangu thamani… kuna muda nilitamani kuukatisha uhai wangu alimradi tu maumivu yakome… kuna muda nilihisi kabisa siwezi kwenda mbele… kwa hiyo binti yangu hakuna ninachokikumbuka zaidi ya maumivu, maumivu makali na kiza kinene, baridi kali na woga.!"
Kumbukumbu hii ya maumivu japo haikumfanya akumbuke chochote cha maana lakini zilimrejeshea kumbukumbu ya maumivu aliyopitia, kumbukumbu ambayo alijitahidi kuiweka nyuma ya ubongo wake na kamwe asiitafakari.
Cindy akainua mikono yake taratibu na kumshika usoni. Uchungu ambao Cindy alikuwa anausikia moyoni mwake ulisababisha mpaka chozi limdondoke.
Akamshika kwa hisia kali uso wake na kumuangalia kwa mkazo ndani ya macho yake akiwa anabubujikwa na machozi.
"Wewe ni imara kuliko unavyodhani, kama usingali kuwa imara basi tusingekukuta hapa leo hii… Japo haukumbuki chochote lakini naomba uniamini hiki ninachokieleza… Jina lako unaitwa David Logan na wewe ni makamu wangu wa Rais nyumbani, Makamu wa Rais wa taifa la Marekani.!" Cindy akaongea kwa uchungu akitokwa machozi mapaka anatetemeka.
David Logan, Makamu wa Rais wa Marekani alikuwa chini sakafuni ameketi akiwa uchi kabisa amekondeana kiasi kwamba mpaka uso wake ulikuwa umebadilika. Alikuwa amedhohofu haswa. Mwili wake ulikuwa umejawa na makovu ya majeraha kila mahala kutokana na mateso ya muda mrefu ambayo alikuwa amepitia.
Alimkazia macho Cindy kwa mshangao kama vile alikuwa haamini au haelewi ni nini hasa alikuwa anamueleza.
"David Logan.? David Logan.? Hilo ndilo jina langu? Uhn David Logan.!!" Aliongea kwa kurudia rudia huku machozi yakimtoka taratibu na kutiririka mashavuni.
"Ndio… jina lako unaitwa David Logan na wewe ni Makamu wa Rais wa taifa Marekani… sijui umefika vipi hapa au nini kimetokea lakini nahitaji ujitahidi kukumbuka kwa nini umeletwa hapa? Kwa nini ulikuwa unateswa?"
"Kwa nini unataka kujua?" David Logan aliuliza kwa kushangaa kidogo.
"Ulimwengu mzima uko katika tishio la kuangamia na jibu lako wewe linaweza kuwa hatua ya kuepukana na tishio hilo!"
"Uhn nani? Mimi?" Logan aliongea kwa kujidharau kwa kujiona hakuwa anastahili kuwa na umuhimu wowote ule wa kuwa tegemeo la kuokoa ulimwengu kutoka kwenye kuangamia.
"Tishio gani? Jibu gani unataka?" Akauliza akiwa bado kama haamini kile ambacho alikuwa anaelezwa.
"Muheshimiwa sitaki kukuchanganya zaidi ya hivi ulivyo sasa… naomba ujaribu kukumbuka chochote kile, umefikaje hapa? Waliokuleta walikuuliza nini? Jitahidi kukumbuka Muheshimiwa!" Cindy alimuuliza kwa msisitizo.
Ubaya zaidi pia walikuwa hawajui kuwa David Logan alitekwa na watu wasiojulikana kutoka nyumbani kwake Naval Observatory Circle kwani lilipotokea tukio hili wao walikuwa tayari wako ndani ya Anabelle 27 (Dar es Salaam).
"Kwa nini wamemuacha hapa? Wao wenyewe wako wapi? Huu sio mtego?" Salim akauliza.
"Inawezekana! Sijui…" Cindy alijibu kwa kitete.
"Wana sababu gani kumuacha hapa? Kwa nini wasiende naye? Kama walihisi hawamuhitaji kwa nini wasimuue? Kwa nini wamuache hapa? Wenyewe wameenda wapi? Nina hisia mbaya Cindy..!!" Salim aliongea kwa wasiwasi huku anatamaza huku na huko pale chumbani kana kwamba muda wowote wenye Kasri lao wanaweza kutokea muda wowote ule.
"Ngoja tujaribu tena kupata majibu!"
Cindy aliongea huku wanaondoka kutoka pembeni ya chumba walipokuwa wanateta na kurejea pale alipo Logan na Magdalena.
"Kuna mafanikio yoyote?" Cindy alimuuliza Magdalena huku akamshika bega kuashiria kuwa asogee pembeni ili yeye aendelee.
"Hakuna kitu! Jaribu bahati yako…" Magdalena aliongea huku anasogea pembeni.
Cindy akachuchumaa tena ili awe usawa mmoja wa macho na Logan kisha akaanza tena maongezi.
"Muheshimiwa natamani sana ukumbuke kitu chochote kile… hata kama ni kidogo kiasi gani?" Cindy aliongea kwa msisitizo huku akimuangalia kwa huruma.
"Giza…. Giza nene ndio kitu cha kwanza ninachokumbuka, kulikuwa na giza nene, kulikuwa na baridi kali... Nilijawa woga! Kadiri ambavyo niliitamani kesho ndivyo ambavyo kesho ilizidi kuwa mbali kuzidi Jana… Jana ilikuwa inaonekana karibu zaidi na yenye kuwekzekana kishinda kesho… imekuwa muda mrefu sana kiasi kwamba siwezi kuona tafouti ya uhalisia na maluweluwe… kitu pekee kilicho halisi kwangu ni giza nene na baridi Kali.!"
Logan alijibu kwa kutamaka maneno yale yale ambayo aliyatamka awali. Neno kwa neno, sentensi kwa sentesi.
Wote walishituka kana kwamba wamesikia sauti ya jini au mzimu. Hawakuamini macho yao kile ambacho waliking'amua ghafla.
"He has been hypnotized…" (Amepumbazwa) Salim na Cindy waliongea kwa pamoja mshituko mkubwa.
"Nini?" Magdalena akauliza kwa mshangao.
"Wamempumbaza ufahamu wake na kumpandikizia maneno kwa kumkaririsha… hypnosis!" Salim aliongea kwa woga.
"Hapa ni sawa kama vile tunaongea na roboti tu!" Cindy akaongezea.
"Kama wamempampumbaza na kumpandikiza maneno ya kuongea hamdhani kwamba walijua kuwa tutakuja hapa? Hamdhani kuwa huu ni mtego? Na je ni kitu gani kingine wamempandikizia?" Magdalena aliongea kwa woga.
Wote watatu macho yao yakatua kwa David Logan. Ajabu ni kwamba David Logan ambaye muda mchache uliopita alikuwa analia na kujiinamia lakini safari hii aliwatazama kwa kuwakazia macho kwa hasira huku anasimama kutoka pale sakafuni ambako alikuwa ameketi.
"Nahisi nimeanza kuelewa nini kinaendelea!" Salim aliongea huku anawarudisha wenzake nyuma kwa tahadhari mbali na David Logan.
Itaendelea…
THE BOLD - 0718 096 811
To Infinity and Beyond
Pls: WhatsApp, Follow and Subscribe