The Other Half (Simulizi)

The Other Half (Simulizi)

THE OTHER HALF



SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE



EPISODE 40

"Giza…. Giza nene ndio kitu cha kwanza ninachokumbuka, kulikuwa na giza nene, kulikuwa na baridi kali... Nilijawa woga! Kadiri ambavyo niliitamani kesho ndivyo ambavyo kesho ilizidi kuwa mbali kuzidi Jana… Jana ilikuwa inaonekana karibu zaidi na yenye kuwezekana kushinda kesho… imekuwa muda mrefu sana kiasi kwamba siwezi kuona tafouti ya uhalisia na maluweluwe… kitu pekee kilicho halisi kwangu ni giza nene na baridi Kali.!"

"Unakumbuka jina lako?" Akamuuliza tena.

Hakujibu moja kwa moja badala yake alijiinamia chini kwa dakika kadhaa. Haikuwa dhahiri kama alikuwa hajaelewa swali au labda alikuwa anafikiri au kujaribu kukumbuka.
Lakini kukumbuka nini? Jina lake?

"Jina langu?" Akainua kichwa chake na kuuliza swali badala ya kutoa jibu.

"Ndio jina lako… unalifahamu?" Akamuuliza tena.

"Nimekuwa mpweke kwa muda mrefu mno kiasi kwamba sikumbuki hata jina langu..." Akajibu akiwa amejiinamia tena kwa huzuni na uchungu.

Ilikuwa inaumiza moyo kumuona namna hii katika hali hii. Akiwa amechanganyikiwa kiasi hiki, kana kwamba uhalisia haukuwa na maana tena kwake.

Cindy akachuchumaa ili awe kwenye usawa mmoja wa uso kati yao.

"Unakumbuka nini?" Cindy alimuuliza kwa sauti ya taratibu ya uchungu.

Akajiinamia chini tena kukwepesha macho yake na Cindy. Sijui ilikuwa ni woga, aibu au alikuwa anatafakari tena. Lakini alijiinamia chini kwa uchungu na huzuni kubwa.

"Nakumbuka maumivu… maumivu yaliyodumu kwa muda mrefu zaidi kuliko nilivyovuta pumzi… mpaka muda huu nashangazwa hata imekuwaje bado niko hai, lakini naamini maumivu yale ndiyo yaliyofanya niupe uhai wangu thamani… kuna muda nilitamani kuukatisha uhai wangu alimradi tu maumivu yakome… kuna muda nilihisi kabisa siwezi kwenda mbele… kwa hiyo binti yangu hakuna ninachokikumbuka zaidi ya maumivu, maumivu makali na kiza kinene, baridi kali na woga.!"

Kumbukumbu hii ya maumivu japo haikumfanya akumbuke chochote cha maana lakini zilimrejeshea kumbukumbu ya maumivu aliyopitia, kumbukumbu ambayo alijitahidi kuiweka nyuma ya ubongo wake na kamwe asiitafakari.
Cindy akainua mikono yake taratibu na kumshika usoni. Uchungu ambao Cindy alikuwa anausikia moyoni mwake ulisababisha mpaka chozi limdondoke.
Akamshika kwa hisia kali uso wake na kumuangalia kwa mkazo ndani ya macho yake akiwa anabubujikwa na machozi.

"Wewe ni imara kuliko unavyodhani, kama usingali kuwa imara basi tusingekukuta hapa leo hii… Japo haukumbuki chochote lakini naomba uniamini hiki ninachokieleza… Jina lako unaitwa David Logan na wewe ni makamu wangu wa Rais nyumbani, Makamu wa Rais wa taifa la Marekani.!" Cindy akaongea kwa uchungu akitokwa machozi mapaka anatetemeka.

David Logan, Makamu wa Rais wa Marekani alikuwa chini sakafuni ameketi akiwa uchi kabisa amekondeana kiasi kwamba mpaka uso wake ulikuwa umebadilika. Alikuwa amedhohofu haswa. Mwili wake ulikuwa umejawa na makovu ya majeraha kila mahala kutokana na mateso ya muda mrefu ambayo alikuwa amepitia.

Alimkazia macho Cindy kwa mshangao kama vile alikuwa haamini au haelewi ni nini hasa alikuwa anamueleza.

"David Logan.? David Logan.? Hilo ndilo jina langu? Uhn David Logan.!!" Aliongea kwa kurudia rudia huku machozi yakimtoka taratibu na kutiririka mashavuni.

"Ndio… jina lako unaitwa David Logan na wewe ni Makamu wa Rais wa taifa Marekani… sijui umefika vipi hapa au nini kimetokea lakini nahitaji ujitahidi kukumbuka kwa nini umeletwa hapa? Kwa nini ulikuwa unateswa?"

"Kwa nini unataka kujua?" David Logan aliuliza kwa kushangaa kidogo.

"Ulimwengu mzima uko katika tishio la kuangamia na jibu lako wewe linaweza kuwa hatua ya kuepukana na tishio hilo!"

"Uhn nani? Mimi?" Logan aliongea kwa kujidharau kwa kujiona hakuwa anastahili kuwa na umuhimu wowote ule wa kuwa tegemeo la kuokoa ulimwengu kutoka kwenye kuangamia.
"Tishio gani? Jibu gani unataka?" Akauliza akiwa bado kama haamini kile ambacho alikuwa anaelezwa.

"Muheshimiwa sitaki kukuchanganya zaidi ya hivi ulivyo sasa… naomba ujaribu kukumbuka chochote kile, umefikaje hapa? Waliokuleta walikuuliza nini? Jitahidi kukumbuka Muheshimiwa!" Cindy alimuuliza kwa msisitizo.

Ubaya zaidi pia walikuwa hawajui kuwa David Logan alitekwa na watu wasiojulikana kutoka nyumbani kwake Naval Observatory Circle kwani lilipotokea tukio hili wao walikuwa tayari wako ndani ya Anabelle 27 (Dar es Salaam).


"Kwa nini wamemuacha hapa? Wao wenyewe wako wapi? Huu sio mtego?" Salim akauliza.

"Inawezekana! Sijui…" Cindy alijibu kwa kitete.

"Wana sababu gani kumuacha hapa? Kwa nini wasiende naye? Kama walihisi hawamuhitaji kwa nini wasimuue? Kwa nini wamuache hapa? Wenyewe wameenda wapi? Nina hisia mbaya Cindy..!!" Salim aliongea kwa wasiwasi huku anatamaza huku na huko pale chumbani kana kwamba muda wowote wenye Kasri lao wanaweza kutokea muda wowote ule.

"Ngoja tujaribu tena kupata majibu!"

Cindy aliongea huku wanaondoka kutoka pembeni ya chumba walipokuwa wanateta na kurejea pale alipo Logan na Magdalena.

"Kuna mafanikio yoyote?" Cindy alimuuliza Magdalena huku akamshika bega kuashiria kuwa asogee pembeni ili yeye aendelee.

"Hakuna kitu! Jaribu bahati yako…" Magdalena aliongea huku anasogea pembeni.

Cindy akachuchumaa tena ili awe usawa mmoja wa macho na Logan kisha akaanza tena maongezi.

"Muheshimiwa natamani sana ukumbuke kitu chochote kile… hata kama ni kidogo kiasi gani?" Cindy aliongea kwa msisitizo huku akimuangalia kwa huruma.

"Giza…. Giza nene ndio kitu cha kwanza ninachokumbuka, kulikuwa na giza nene, kulikuwa na baridi kali... Nilijawa woga! Kadiri ambavyo niliitamani kesho ndivyo ambavyo kesho ilizidi kuwa mbali kuzidi Jana… Jana ilikuwa inaonekana karibu zaidi na yenye kuwekzekana kishinda kesho… imekuwa muda mrefu sana kiasi kwamba siwezi kuona tafouti ya uhalisia na maluweluwe… kitu pekee kilicho halisi kwangu ni giza nene na baridi Kali.!"

Logan alijibu kwa kutamaka maneno yale yale ambayo aliyatamka awali. Neno kwa neno, sentensi kwa sentesi.

Wote walishituka kana kwamba wamesikia sauti ya jini au mzimu. Hawakuamini macho yao kile ambacho waliking'amua ghafla.

"He has been hypnotized…" (Amepumbazwa) Salim na Cindy waliongea kwa pamoja mshituko mkubwa.

"Nini?" Magdalena akauliza kwa mshangao.

"Wamempumbaza ufahamu wake na kumpandikizia maneno kwa kumkaririsha… hypnosis!" Salim aliongea kwa woga.

"Hapa ni sawa kama vile tunaongea na roboti tu!" Cindy akaongezea.

"Kama wamempampumbaza na kumpandikiza maneno ya kuongea hamdhani kwamba walijua kuwa tutakuja hapa? Hamdhani kuwa huu ni mtego? Na je ni kitu gani kingine wamempandikizia?" Magdalena aliongea kwa woga.

Wote watatu macho yao yakatua kwa David Logan. Ajabu ni kwamba David Logan ambaye muda mchache uliopita alikuwa analia na kujiinamia lakini safari hii aliwatazama kwa kuwakazia macho kwa hasira huku anasimama kutoka pale sakafuni ambako alikuwa ameketi.


"Nahisi nimeanza kuelewa nini kinaendelea!" Salim aliongea huku anawarudisha wenzake nyuma kwa tahadhari mbali na David Logan.




Itaendelea…


THE BOLD - 0718 096 811
To Infinity and Beyond

Pls: WhatsApp, Follow and Subscribe
 
EPISODE 14 IKO HEWANI TAYARI.... TAFADHALI TEMBELEA TOVUTI ILI KUISOMA...

kuisoma kwa urahisi, nenda juu kabisa pale kwenye "Trending" utaiona au shuka chini kabisa kwenye Categories kisha chagua "SHORT STORIES"...


d3b0741a2402304b8564c5aa672b4034.jpg
Tovuti inaitwaje mkuu au weka link
 
THE OTHER HALF


SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE



EPISODE 41


"…je tunafahamu wapi tunapaswa kuwa? Wapi ni nyumbani kwetu katika universe? Na kama kweli tunafahamu kwanini siku zote hatufanyi chochote? Lazima kuna jambo la zaidi katika maisha… jambo la zaidi ya kula na kulala, zaidi ya kuoa na kuolewa, zaidi ya fedha, zaidi ya nyumba, zaidi ya anasa zote tunazotamani!! Lazima kuna jambo la zaidi.. mwanadamu anaishi umri chini ya miaka 100. Hii ni sawa na punje ya mchanga ukilinganisha na zaidi ya miaka bilioni 4 ambayo dunia yetu imekuwepo. Kwa lugha nyingine maisha ya binadamu juu ya uso wa dunia ni kama punje ya mchanga iliyodondoshwa katikati ya bahari. Negligible.!!
Swali ni namna gani tunaweza kufanya maisha yetu haya mafupi duniani na kuwa kama 'iceberg' baharini badala ya punje ya mchanga? Tunawezaje kukumbukwa hata baada ya miaka elfu toka sasa uhai wetu unapokoma?
Lazima kuna la zaidi katika maisha… there must be more to this life, a place to belong and a purpose for us all.!!"



Ndani ya msitu wa Ox - Maryland, Marekani

Yule binadamu wa ajabu alikuwa anapiga hatua za taratibu sana huku akiwasogolea waliposimama Mzee Caleb na wenzake.
Alikuwa na muonekano sawa kabisa na Mzee Caleb. Walifanana sura, kimo na hata umri wao ulionekana kufanana. Yule binadamu wa ajabu naye pia alikuwa na hali ya uzee kama Caleb, tofauti tu ni kwamba mwili wake ulikuwa kakamavu zaidi. Alikuwa imara zaidi na mkakamavu kushinda hata wale makomando wa CIA akina Walker ambao walikuwa pamoja na Caleb.

Walker na wenzake bado walikuwa wameshikilia bunduki zao kuelekea alipo yule binadamu wa ajabu lakini macho yao yalikuwa yakipepesa kutoka kwa Mzee Caleb kwenda kwa yule binadamu na kisha kurudi tena kwa Caleb. Walikuwa wameduwaa kutoka na mfanano huu wa Mzee Caleb na yule binadamu.

Japokuwa binadamu huyu alikuwa amefanana na Caleb kwa sura na kimo, lakini haikuwa rahisi kumtazama kwa dakika nzima mfululizo pasipo kutazama pembeni kutokana na namna alivyokuwa anaogofya.
Alikuwa amejitanda nguo nyeusi kama shuka mwili mzima na kuacha kichwa pekee pamoja na vidole vya mikono. Ngozi yake nyeupe ya uzungu ilikuwa imebadilika na kuwa rangi fulani nyeusi iliyochanganya na ukijani kwa mbali. Pia ngozi ya kiumbe huyu usoni alikuwa na mabaka kama mabaka ya chatu au kenge. Pia macho yake yalikuwa ya rangi ya kahawaia iliyofifia sana na mboni nyekundu ambazo rangi yale ilikolea kufanya kuwa kama mwali wa moto. Mwili mzima ulikuwa umefunikwa na manguo hayo myeusi. Ni uso pekee ndio ambao alikuwa anaonekana
Alikuwa na nywele nyeusi kabisa tii za urefu wa wastani ambazo zilikiwa zimelala kichwani mwake kama vile vimeloa maji au zimelambwa na mbwa.

Kucha zake za vidole zilikuwa ndefu kiasi kwamba labda yumkini hakuwa kuzikata tangu ameliona jua.

Namna ambavyo alikuwa anawatazama kwa kujiamini na kusogea tarataibu, alikuwa anaogopesha kiasi cha kutosha kabisa kumfanya mtu atokwe haja bila kujijua.

"..nimeisubiri siki ya leo kwa kipindi kirefu sana Caleb.!" Yule binadamu aliongea huku anatembea taratibu shuka lake lile kama kaniki likiburuza chini kwenye majani makavu.

"…msipige risasi!!" Mzee Caleb aliwasisitiza tena huku akiwa amemkazia macho yule binadamu.

Mzee Caleb akachukua mfuko ambao ulikuwa na zile chupa zenye unga wa mifupa ya mafuvu ambayo alifukua nyuma ya nyumba yake kisha akaanza kuumwaga kuzunguka pale ambapo walikuwa wamesimama yeye na wenzake.

Yule binadamu hakuonekana na haraka. Alikuwa anajiamini kabisa na alichokuwa anakifanya. Akabakia anamuangalia Mzee Caleb kwa dharau namna anavyomwaga ule unga kutengeneza duara kuwazunguka.


"…unafanya nini Caleb?" Walker akamuuliza Caleb kwa kunong'ona.

"Hawezi kuingia ndani ya hili duara la huu unga wa mifupa ya mafuvu ninao umwaga!" Caleb akamjibu.

"Mbona anatabasamu na wala hana wasiwasi wa kukuzuia ulipokuwa unamwaga huo unga?" Walker akauliza tena kwa udadisi zaidi.

"Anahisi tunajisumbua tu kwa kuwa muda wowote kutoka sasa Maryland itatwaliwa… sijui tumebakiwa na muda gani kabla Maryland kugeuka Anabelle?"

"Tuna chini ya dakika kumi!" Komando mwingine akajibu kwa sauti ya chini ya kunong'ona.

Yule binadamu aliendelea kutembea taratibu mpaka kufika kwenye kingo za duara la unga wa mifupa ya fuvu ambalo lilochorwa na Caleb. Alipofika hapo kwa mara ya kwanza kabisa akatabasamu.
Alikuwa na meno marefu ambayo yalikuwa kwenye ncha kama yamesagika na kutengeneza ukungu fulani wa rangi nyeusi ya damu.

"Unahisi hiki unachokifanya kitawasaidia kwa muda gani Caleb? Muda mchache ujao Maryland inakiwa chini ya himaya yetu… Maryland inageuka Anabelle!! Unahisi hiki unachokifanya kinawasaidia nini?" Yule binadamu aliongea huku anatoa tabasamu la kifedhuli.

"Yuko sahihi?" Walker aliuliza kwa woga.

"Nadhani japo sina uhakika. Lakini nahisi Maryland ikigeuka kuwa Anabelle huu unga wa mifupa hauna nguvu yoyote tena kumzuia asiingie ndani ya hilo duara tulilolizungushia kujikinga..!"

"Kwa nini huu unga una uwezo wa kumzuia asivuke?" Walker akauliza tena.

"Walker mwanangu hatuko darasani hapa… huu sio muda sahihi wa kuniuliza haya maswali… tusubiri baada ya hizo dakika kumi tuone kitakachotokea.!"

"Paaaaaaaaaaaaaaggghhhh.!!"

Radi kali zilikuwa zinapiga mfululizo huku giza likianza kutanda taratibu na hali ya baridi kuanza kuwa kubwa zaidi. Dalili tosha kwamba muda wowote ule Maryland inageuka kuwa Anabelle.

Yule binadamu bado alikuwa amewakazia macho huku anatabasamu kifedhuli akiwa amesimama kwenye kingo za lile duara. Alionekana dhahiri kabisa nafsi yake ilikuwa inabirudika na namna macho ya akina Caleb, Walker na wenzao yalivyojawa na hofu pamoja na woga kutokana na namna ambavyo walijua ni dhahama gani inayowasubiri mbele yao dakika kadhaa zijazo.

"Mpango wako ni nini kutuleta huku msituni?" Walker aliuliza kwa sauti ya woga.

"Masalia… baba yangu na wale wenzake ambao tulionana nao juzi ndio pekee ambao wanajua namna ya kuingia na kutoka ndani ya Anabelle. Kama wakirejea hapa tena na kutukuta labda wanaweza kutusaidia.!" Mzee Caleb alimjibu Walker pasipo kumtazama. Macho yake alikuwa ameyakaza muda wote kuelekea kwa yule binadamu.

"Umesema wakirejea?? Wakirejea lini? Labda tumebakiwa na dakika tatu au labda tano… wanarejea muda gani?" Walker aliuliza kwa hasira zilozochanganyika woga mkubwa zaidi.

"Sijui ni muda gani watarejea?" Mzee Caleb alijibu tena pasipo kumtazama.

"Tufanye nini?" Walker alizidi kuchanganyikiwa.

"Labda tusali sala zetu za mwisho!!" Safari hii Mzee Caleb alimjibu Walker na kugeuka kumtazama usoni.

Walitazamana kwa sekunde kadhaa huku Walker akionyesha macho ya wasiwasi wa kifo huku Mzee Caleb akionyesha macho ya kumaanisha kile ambacho alikuwa amekisema.

"Kuna mwenye kiberiti?" Mzee Caleb akavunja ukimya ambao ulikuwa umetawala ghafla mara baada ya kuwaambia wasali sala za mwisho.

Mmoja wa makomando akaingiza mkono mfukoni na kumpa kiberiti cha sigara.

"Unataka kufanya nini?" Kama kawaida Walker aliuliza tena badala ya kusubiri kuona nini Mzee Caleb anakitaka kufanya.

Mzee Caleb hakujibu chochote safari hii. Aliinama chini na kuwasha kiberiti na kisha kukielekeza pale chini kwenye mduara ambao alikuwa amemwaga unga wa mifupa ya fuvu kuwazunguka.

Ule unga ulianza kuwaka taratibu na baadae ukashika kasi wote ukiwa unaungua na kutengeneza moto wa duara kuwazunguka Mzee Caleb na wenzake kama namna ambavyo alikuwa ameumwaga.
Unga uliwaka huku unatoa harufu fulani kali kama nyama iliyooza ambayo ilikuwa inaungua kwa moto.

"Unafanya nini Caleb?" Walker aliuliza tena kwa mara nyingine.

Mzee Caleb alikaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kumjibu.

"Hiyo harufu inayotoka kwenye hiyo mifupa nataka baba yangu aisikie kwa haraka popote alipo. Kama ambavyo mbwa hawezi kusahau harufu ya bwana wake mtunzaji ndivyo ambavyo naamini baba yangu japo si binadamu yule wa kawaida lakini hawezi kusahau harufu hii… mifupa ya mjukuu wake na mkwe wake…" Mzee Caleb alijibu bila kumuangalia Walker. Alikuwa amerejea kumkazia macho yule binadamu wa ajabu.

"Kwa nini haukifanya hivi muda wote?" Walker akarejea na swali lingine.

"Sina hakika kama baba na wenzake Masalia watasikia harufu hii muda gani na kuja ndani ya wakati… kama ningeliwasha moto huu unga mapema na wasingetokea basi huyu kiumbe mbele yetu angekuwa ameshatugeuza asusa muda mwingi sana… maana naamini huu moto hauwezi kuwaka zaidi ya dakika tano… nimewasha sasa hivi kwa kuwa hatuna chaguo lingine… sekunde yeyote kutoka sasa Maryland inageuzwa Anabelle na hakuna cha kumzuia huyu kiumbe mbele yetu… kwa hiyo hakuna haja ya kuendelea kusubiri bila kutupa kete yetu ya mwisho!" Mzee Caleb alieleza kwa sauti thabiti kabisa.

Yule bibadamu mbele yao kwenye kingo za duara hakusogea hata hatua moja wala kutikisika baada ya moto ule kuwashwa. Aliendelea kutabasamu zaidi huku amekaza macho kwa Mzee Caleb akionekana kuwa na hakika kabisa kuwa Mzee Caleb na wenzake hakuna namna ambayo wangeweza kuokoka leo hii kutoka kwenye mikono yake.

"Paaaaaaaaaaaaaggggghhhhh"

Radi zililia kwa kishindo zaidi na kwa mfululizo zaidi huku kiza kikigubika anga na baridi likibadilika ghafla na kuwa kama vile wako kwenye ziwa la maji ya barafu tupu.
Ni dhahiri kwamba Maryland ilikuwa inageuka sasa kuwa Anabelle. Labda ilikuwa imebakia chini ya dakika moja pekee au labda sekende kadhaa tu kabla ya Maryland kuwa rasmi Anabelle mpya.

Mzee Caleb na wenzake wakaanza kusikia mabadiliko kwenye miili yao. Kama vile walikuwa wanapatwa na kizunguzungu kilichokuwa kinawafanya wasione vyema, kama vile pumzi haiji sawa sawa.

"PAAAAAAAAAAAGGGHH.!!"

Radi kubwa zaidi ya kishindo ilipiga. Kizunguzungu kikaongezeka. Uwezo wa kuona mbele ukapungua. Pumzi ikaanza kuwa nzito na miili ikaanza kuishiwa nguvu na kulegea.

"Its over Caleb!! Nimeisubiri hii siku kwa muda mrefu sana… its over!!" Yule binadamu akaongea kifedhuli huku anapiga hatua kujiandaa kuvuka lile duara walilopo akina Caleb ambalo lilikuwa linamzuia asiweke kuwafikia muda wote huu.

Lakini kabla hajaingia ndani ya duara, kabla Maryland haijawa Anabelle rasmi. Zikiwa zimebakia kama sekunde kumi tu au labda tano. Wote wakaanza kusikia sauti masikioni mwao. Kama sauti ya watu wananong'ona, kama sauti ya watu kupekua kwenye vichaka. Sauti kama ile ile ambayo Mzee Caleb na wenzake waliisikia hapa siki tatu zilizopita walipokuja kutafuta Book Of Codes. Sauti ya kuashiria kuwasili kwa Masalia. Baba yake Mzee Caleb na wanachama wenzake.

Yule binadamubwa ajabu alionekana kushituka na kuanza kugeuka huku na huko ili ajue kama ni kweli Masalia wamewasili au la. Kwa mara ya kwanza sura yake ya kutisha ilionyesha woga. Woga wa kuhofia Masalia, baba yake Mzee Caleb na wenzake.

Mzee Caleb, Walker na wenzao pia walisikia sauti hii masikioni mwao ya ujio wa masalia… lakini miili ilikuwa imishiwa nguvu kabisa wasiweze hata kutabasamu au kutazama kushuhudia kama ni kweli walikuwa Masalia wamewasili. Muda pia ulikuwa umeisha, Maryland ilikuwa inageuka rasmi kuwa Anabelle mpya.

"PAAAAAAAGGGGHH.!!" Kishindo kikuu cha radi kama tetemeko la ardhi kilisikika mara moja na ya mwisho. Mji wa Maryland ulikiwa umegeuka rasmi na kuwa Anabelle.
[04/01, 20:22] Official Robot: Mzee Caleb, Walker na wenzao hawakuhisi pumzi tena na wala hawakuweza kuona mbele, ilikuwa ni kiza kitupu machoni mwao… miili iliishiwa nguvu na wote kwa pamoja wakadondoka ardhini.
Lakini wakiwa wanadondoka japokuwa walikuwa na ufahamu nusu tu, Mzee Caleb alihisi kama kuna mikono ya mtu japo ilikuwa ya baridi mno… alihisi kuna mikono ya mtu imemgusa na kumdaka.!!
Mwili wake wote ukasisimka kwa hofu kutokana na kutokujua kama amedakwa na Masalia au yule binadamu mbele yao ndio alikuwa amemtia mikononi??



Itaendelea….


The Bold
 
nzuri inapendeza nafikiri utakuja kuwa mwandishi nguli na kufahamika zaidi,ila itabidi uhamie lugha ya kimataifa!
watu fulani watakuona tu ukiendelea na mwendo huu.
nafikiri kitu fulani kizuri kukujia!.
 
Hahaha kumbe hii kitu ya Pandora box kuna mpaka movie zake, nmeikubali ni Kali sana
 
hii simulizi ndo huwa inanifanya niingie kila mda jf yan kama movie ila huwa sipend kukatishana huku utamu kipande kimoja unaweza kaa hata mwez hamna duuh
 
flat%2C1000x1000%2C075%2Cf.jpeg




THE OTHER HALF


SEASON 1 - THE LEGENDNOF ANABELLE




Sio mara moja au mara mbili, bali mara mia kadhaa nimewahi kuuliza na kujiuliza, "..kesho inataka nini kutoka kwangu? Nafanyaje pale sauti pekee ninayoisikia kichwani mwangu ni neno “subiri”? Hata nikiamua kusubiri siwezi kuepuka kesho isifike, ni lazima kutakucha na itanipasa kupambana na mashetani yanayonisubiri huko kesho!


Kesho itakapofika, nikijitoa muhanga nafsi yangu kuokoa kitu pekee chenye thamani kwenye maisha yangu, mtu ninayetamani aishi kuliko nafsi yangu! Je, usiku akienda kulala atakumbuka kafara yangu? Je, ulimwengu utakumbuka ushujaa wangu?
Ni siku ngapi atalala akikimbuka kafara yangu kabla ya kusahau?

Nashindwa kuiondoa sauti ninayoisikia kichwani mwangu, kadiri ninavyojitahidi kutoisikiliza ndivyo sauti inavyokuwa kubwa zaidi kichwani mwangu, sauti ya neno moja tu “subiri”!

Ni mahali gani ambapo natakiwa kuchora mstari wa kusubiri, na muda gani natakiwa kusonga mbele?
Nahisi kama nimejifungia kwenye dunia ya peke yangu… nahofia hata kuinua mguu kukanyaga hatua moja mbele, kwa kuhofia naweza kuharakisha kesho ikafika haraka, na naogopa pale itakapofika kwa kuwa kichwani mwangu bado sijapata jawabu… kesho inataka nini kutoka kwangu?.”




EPISODE 42


Ron alikuwa anatembea haraka haraka kuufuata mlango uliokuwa unaelekea chini kwenye basement ya nyumba hiyo baada ya Natalie kusema kwamba yeye na baba yake Logan walikuwa wakipendelea sana kucheza tabke tennis kila muda ambako baba yake hakuwa kazini. Latisha na mwanaye walikuwa wanafuata nyuma wakitembea haraka haraka karibia na kukimbia.

Ron alifika mpaka kwenye mlango na kuufungua. Ukifungua mlango tu unakutana na ngazi zinazoshuka chini kwenye basement yenyewe. Kabla hajaanza kushuka chini kwanza kabisa Ron alipapasa ukutani mkono wake wa kushoto na kuwasha taa ya kule chini kwenye basement na kisha ndipo alianza kushuka ngazi hizi huku nyuma yake akifuatiwa na Latisha na mtoto wake Natalie.

Ukiingia humu ndani ya basement mkono wa kushoto kulikuwa na maboksi ya vitu mbali mbali vimepangwa. Pembeni ya maboksi haya kulikuwa na baisikeli ya mtoto wa kama miaka 10 au 12 hivi. Hii ilikuwa ni baisikeli ya Natalie kipindi wanaishi wote na baba yake kabla ya ndoa ya Latisha na David Logan kusambaratika.

Macho ya Natalie na mama yake Latisha yalipotua kwenye hii baisikeli waliiangalia kwa muda mrefu sana na kwa huzuni sana kutokana na kumbukumbu ya huzuni iliyokuwa inawajia kichwani kutokana na kuiona baisikeli hii. Japokuwa ndoa ya Latisha na Logan ilikuwa imevunjika na sasa Latisha yuko kwenye ndoa nyingine na mumewe Donald McLaren lakini hakukuwa na ubishi kwamba Logan ndiye alikuwa mpenzi wa maisha wa Latisha. Kuona baisikeli hii kulirejesha tena kumbukumbu zote za furaha kipindi familia yao iko imara. Alikumbuka namna ambavyo katika siku za kwanza za kununuliwa kwa baisikeli hiyo walivyokuwa wakimshikilia Natalie baisikeli apande na kisha kumshikia tena akiwa anajifunza kuiendesha.

Kumbukumbu hizi haizikuwa zimemteka tu Latisha pekee bali pia hata Natalie. Japokuwa moyoni mwake alikuwa amejawa na kinyongo dhidi ya baba yake lakini ukubwa wa upendo ambao alikuwanao juu ya baba yake ulikuwa ni mkubwa mno. Baada ya kuitazama baisikeli hii ndipo ambapo alijua ni kwa kiasi gani alikuwa amemkosa baba yake.
Wote wawili Natalie na mama yake Latisha kwa mbali machozi yalikuwa yakiwalenga lenga baada ya kumbukumbu hizi kuwajia upya kichwani na ukweli uliopo kwamba mtu huyu wanayempenda haswa alikuwa ametekwa na watu wasiojulikana na kuna uwezekano wasimuone tena.

Katikati ya basement kulikuwa na meza ya mchezo wa “table tennis”.
Macho ya Natalie yaliganda kwenye meza hii kwa muda mrefu zaidi. Machozi ambayo mwanzoni yalikuwa yakimlenga lenga sasa hivi yalianza kutirika taratibu shavuni mwake. Meza hii ina kumbukumbu nyingi za furaha kati yake na baba yake. David Logan kutokana na majukumu yake ya kiserikali pamoja na matamanio yake ya kutaka kuwa kiongozi mkuu wa nchi siku moja ilimfanye awe 'busy' kweli kweli.


Upande huu wa kushoto kulikuwa na kabati tupu la vitabu. Kabati lilikuwa na vumbi kiasi kutokana na kutowekewa kitu chochote kwa muda mrefu.
Ron alisogelea kabati na kuanza kuingalia kwa makini zaidi. Alihisi kwamba kulikuwa na kitu cha ziada kuhusu hii kabati japo hakuweza kung'amua mara moja ni kitu gani.

"Kwa hiyo nini kinaendelea baada ya hapa??" Latisha aliuliza huku bado akiwa amemkumbatia Natalie. Wote wawili walikuwa wameacha kulia muda huu.

"Sijui kwa kweli… hisia zangu zilikiwa zinaniambia kuwa kama kuna siri Logan alikuwa anataka kuificha kwa ajili ya Natalie basi lazima siri hiyo itakuwa humu kwenye basement. Sijui tunafanyaje baada ya hapa…" Ron aliongea huku anageuka huku na huko pale kwenye basement.

Hakukuwa na kitu chochote kingine hapa kwenye basement zaidi ya yale maboksi mkono wa kulia, table tennis katikati na hili kabati mkono wa kushoto.

"Hakuna stori yoyote au kitu fulani kuhusu hili kabati.!!" Ron aliwauliza Latisha na Natalie akitarajia labda kuna historia fulani nyuma ya kabati hili kama ilivyo kwa ile ya table tennis katikati ya chumba.

"Hapana…" Latisha akajibu.

"Hapana… ndio kwanza naliona leo hilo kabati" Natalie akaongezea.

"Aaaaarrrrggghhh.!" Ron akajikuta anakereka mwenyewe kwa kuhisi kama amegonga mwamba na hisia zake hazikuwa sahihi.

Akaisogelea tena hii kabati. Akaiangalia tena kwa makini. Akaangalia pale chini sakafuni ilikosimama. Akaona kitu.
Hii kabati ilikuwa kama imesogezwa hivi. Yaani, kutokana na hii basement kutotumika mara kwa mara ilipelekea chini kuwe na vumbi. Na siku zote kitu kikiwa kwenye sakafu yenye vumbi kwa muda mrefu na baadae kusogezwa hata ukirejesha tena kama ambavyo kilikuwa awali bado kuna alama fulani inabaki pale chini sakafuni kwenye vumbi kuonyesha hiki kitu kilisogezwa hapa na kisha kurejeshwa tena. Hicho ndicho ambacho Ron alikiona.

Akalisogelea karibu zaidi kabati hili na kisha kulisogeza kutoka pale lilipo. Nyuma ya kabati kulikuwa na mlango mdogo uliofichwa na pembeni ya kitasa chake kulikuwa na 'keypad' ambayo ilikuwa inawaka rangi nyekundu.

Ron aligeuka kuwatazama Latisha na Natalie huku akitoa tabasamu kubwa kama vile mtoto mdogo amekuta boksi la lolipop chumbani kwake.

"Got you Logan… nilijua tu siri zako zitakuwa hapa kwenye basement.!!" Ron aliongea kwa mbwembwe huku akijaribu kufungua mlango kwa kitasa. Haukufunguka. Ilionekana dhahiri kwamba ilikuwa inahitajika kuingiza neno la siri kwenye keypad pale pembeni kabla ili kufungua mlango.

"C'mooon Logan, mbona unafanya maisha yetu yawe magumu hivi??" Ron alikereka tena baada ya kuona hicho kizingiti kingine kizito zaidi cha neno la siri.

Latisha na Natalie pia wakasogea mpaka pale mlangoni.

"Una hisia kali sana Ron… lakini unajuaje kama humu ndio kuna hizo siri tunazohitaji?" Latisha akauliza baada ya kufika pale mlangoni.

"Latisha sababu pekee ya mtu kuwa na chumba cha siri kwenye basement ni kwa kuwa ana siri nzito ambazo anahitaji kuziweka salama… kwa hiyo labda mnisaidie tu kukisia neno la siri!" Ron akajibu

"Sina hata 'idea'.!" Latisha akajibu haraka huku anatikisa kichwa.

Wakaanza kukisia kwa kujaribu kila kitu ambacho walihisi inaweza kuwa neno la siri sahihi. Wakajaribu mwaka wa kuzaliwa wa Logan lakini ikakataa halikuwa neno la siri sahihi. Wajaribu tarehe ya kuzaliwa ya Natalie, wakajaribu tarehe ya kuzaliwa na Latisha. Vyote vikakataa. Wakajaribu tarehe ya harusi kati ya Logan na Latisha, ikakataa. Wakajaribu tarehe waliyotalikiana, nayo ikakataa.

"Dah hapa tumegonga mwamba.!" Natalie alivuta pumzi ndefu na kuishusha.

"Lazima kuna kitu mtakuwa mnakijua na ndio litakuwa neno la siri jitahidini kukumbuka… c'mon guys!" Ron aliongea kwa pupa akijitahidi kuwatia hari wasikate tamaa.

"Hizo tulizojaribu ndio zilikuwa namba pekee ambazo nahisi labda angetumia kama neno la siri kama alikiwa anahitaji Natalie asipate shida kukumbuka.!" Latisha aliongea kwa kukata tamaa.

Lakini Latisha aliposema sentesi ya "kama alikuwa anahitaji Natalie asipate shida kukumbuka" kuna taa ikawaka kichwani kwa Ron.


Lakini kila ambako alikiwa anapata muda wa kupumzika alikuwa anatumia muda huo mwingi kucheza table tennis na mwanaye Natalie. Walikuwa wakicheza na wakichoka wanakaa chini hapo kwenye basement na 'kupeana stori'. Logan akimsimulia mwanaye visa vyake vya ujana na utoto na huku Natalie naye akimpa 'umbea' wa shuleni kwao na marafiki zake. Meza hii ilikuwa ni alama kubwa ya urafiki kati ya Natalie na baba yake Logan.

Natalie aliiangalia kwa muda mrefu huku machozi yakimtoka hasa hasa akikumbuka ukweli kwamba baba yake hayupo tena na kuna uwezekano wasipate tena nafasi ya kucheza mchezo huo pamoja.

"Seven nil, twelve five" Natalie aliongea kwa kwikwi ya kilio huku machozi yakimtoka.

"Naam.!!" Ron alijibu kwa mshituko na kugeuka kumuangalia Natalie.

"Seven nil, twelve five.!" Natalie aliongea tena kwa kwikwi ya kilio huku akijiziba uso kwa viganja vya mikono na kuangua kilio kikubwa zaidi.

Latisha akasogea taratibu na kumkumbtia Natalie huku naye machozi yakimtoka lakini pasipo kutoa kilio cha sauti.

"Sssssshh nyamaza mama sssshhh.!!" Natalie alimkumbatia mwanaye na kumbembeleza.

"Sijakuelewa Natale, 'Seven nil twelve five' ina maana gani?" Ron aliuliza kwa macho ya udadisi huku akiwasogelea pale waliposimama Natalie na Latisha.

"Hayo ndio yalikuwa matokeo yetu ya mwisho mimi na baba… 'seven nil, twelve five'!!" Natalie aliongea huku kwikwi ya kilio ikiwa imepungua kidogo safari hii.

Ron na Latisha wote walibaki kimya bila kusema chochote wakimuangalia Natalie kuashiria kwamba walikuwa wanataka kusikia zaidi.

Natalie akaendelea…

"Siku hiyo nilikuwa nimetoka shuleni na msongo mkubwa sana wa mawazo… nilikuwa nimegombana na rafiki yangu kipenzi kabisa. Nilivyorudi nyumbani nikajifungia chumbani sikutaka kuongea na mtu yeyote yule wala kuonana na mtu au kula chakula. Jioni baba alirudi nakumbuka alikuwa anajiandaa alikuwa na safari ya kwenda Washington siku hiyo. Alipofika nyumbani akaelezwa kwamba nilikuwa nimejifungia chumbani siku nzima sitaki kula wala kuonana na mtu. Kwa hiyo akaja mpaka nje ya chumba changu na kuanza kunigongea. Aligonga kama dakika tano nzima sikujibu wala kufungua mlango. Akavua tai yake na kukaa chini nje ya mlango wangu akaniambia kuwa hatoenda safari yake mpaka aone nimetabasamu, kwa hiyo atakesha hapo hapo nje ya mlango. Hata baada ya kusema haya sikufungua mlango au kumjibu. Akaanza kinihadithia 'stori' za utoto wake na jinsi ambavyo na yeye utotoni aliwahi kugombana na rafiki yake kipenzi utotoni. Akaanza kunihadithia visa walivyokuwa wanafanyiana ili kulipiziana kisasi. Kuna muda alihadithia visa ambavyo nilishindwa kujizuia nikaanza kucheka. Huyo ndio alikuwa baba yangu, alikuwa anajua hisia zangu na namna gani anaweza kunirejeshea tabasamu. Nikafungua mlango na baba akaingi na kunikumbatia na kunieleza kuwa haijalishi nitagombana na marafiki wangapi lakini yeye atakuwa na mimi siku zote. Akanichukua na tukashuka chini kwenye basement na kuanza kucheza table tennis. Tulicheza michezo miwili. Mchezo wa kwanza nilimfunga 'Seven nil' na mchezo wa pili nikamfunga 'twelve five'. Nadhani aliniacha nishinde makusudi, lakini majonzi yangu yote yaliondoka na akasafiri kwenda washington na kuniacha nikiwa na tabasamu. Tulikuwa kila mara tukiongea kwenye simu namtania "seven nil, twelve five' na alijiapiza kuwa akirudi lazima michezo yote miwili anifunge saba bila. Lakini hatukuwahi kucheza tena, kwani akiwa huko washington ndio ikaibuka skendali ya kujihusisha kimapenzi na sekretali wake na wiki kadhaa baadae wakatalikiana na mama. Kwa hiyo mpaka leo hii siwezi kuondoa kichwani matokeo ya mchezo wetu wa mwisho, 'seven nil, twelve five'.!"

Natalie akamaliza kueleza na kuanza tena kulia huku akilala kifuani kwa mama yake. Latisha alimkumbatia tena kwa uchungu machozi yakimtoka bila kutoa sauti ya kilio.
Wote wawili katika muda huu ndipo ambapo walijewa na hisia zilizowakumbusha ni kwa kiasi gani wanampenda Logan licha ya mambo yote mabaya ambayo alikuwa ameyafanya na kusababisha familia yao kusambaratika. Ni katika wakati kama huu ndipo ambapo unafahamu ni kwa kiaisi gani unampenda mtu pindi tu ukimpoteza.

Wakati Natalie na Latisha wamekumbatiana na kubembelezana, Ron aligeuka na kuendelea kudadisi kila kona ya hiyo basement.


"Natalie mwanzoni ulipoona table tennis ulikuwa unasema nini? 'nil twelve…' nini tena?" Ron aliuliza kwa udadisi.

"Matokeo yetu ya mwisho ya table tenis, 'Seven nil, twelve five'.!" Natalie akajibu akitoa macho naye kama taa imewaka kichwani.

Ron akageuka mlangoni haraka haraka na kuingiza tarakimu hizo kwenye keypad, 7-0-1-2-5.

Aliponingiza tu ile keypad ikabadilika rangi kutoka nyekundu na kuwa kijani.

"Yeeeessss.!!" Ron alishangilia.

Haraka haraka akshika kitasa na kufungua mlango. Mlango ulifunguka na mbele yao kulikuwa na kijichumba kidogo.

Kijichumba hiki kidogo kilikiwa nadhifu mno kilichopakwa rangi ya kijivu chumba kizima. Vitu pekee ndani ya chumba hiki vilikuwa kabati dogo la kioo lilipo upande wa kulia ukiingia ndani ya hiki kijichumba, kabati ambalo ndani yake kulikuwa na kitu kimoja tu, kompyuta mpakato.
Pia kulikuwa na kiti cha kukaa cha kiofisi kilichopo upande mwingine wa chumba na mbele yake kulikuwa na kamera iliyo kwenye kwenye stendi yake ya kurekodia.

Hatimaye siri ambayo walikuwa wanaitafuta kwa udi na uvumba ilikuwa mbele yao ndani ya chumba hiki. Siri ambayo ilisababisha Logan kutekwa na watu wasiojulikana. Siri ambayo waliamini inaweza kuuokoa ulimwengu kutoka kwenye kugeuzwa kuwa Anabelle. Siri ambayo kikundi cha siri cha The 46 wanailinda kwa maisha yao yote. Siri hiyo waliamini hatimaye wameifikia ndani ya chumba hiki.



Itaendelea…


Muhimu: Ushauri ambao mmekuwa mkinipa kwa muda mrefu hatimaye nimeufanyia kazi. Ndani ya wiki mbili zijazo nitatoa kitabu changu cha kwanza kabisa cha simulizi ya Vipepeo Weusi. Kama ambavyo mmekuwa mkiniunga mkono kwenye nyuzi hizi kwa miaka mitatu sasa naomba pia sapoti yenu katika hatua hii mpya ambayo naichukua. Kwa pamoja tupambane kurejesha utamaduni wa watu kujisomea na tuinue kizazi kipya chenye maarifa.

Naomba baraka zenu ili project hii iwe na mafanikio na hatimaye nitoe vitabu vingi zaidi na zaidi.

Asanteni sana.


Habibu B. Anga "The Bold"
To Infinity and Beyond
 
Back
Top Bottom