The Other Half (Simulizi)

images (41).jpg


THE OTHER HALF


SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE



EPISODE 45


Mlango wa oval office ukagongwa mara moja na kisha kufunguliwa.
Renaldo alisimama haraka haraka baada ya mlango kufunguliwa.

"Kila kitu kiko sawa chief?" Alikuwa ni moja wa maafisa wa Secret Services.

"Kila kitu kiko sawa kabisa!" Renaldo alijibu huku anazuga kwa kufunua makatasi anbayo aliyaokota chini na kuyashika mkononi.

"Nimesikia kama kuna purukushani hivi humu kwa dakika kadhaa.." yule afisa aliongea tena huku macho yake yakiwa kwenye vitabu pale chini ambavyo Renaldo alikuwa amevipangua.

"Kila kitu kiko sawa… yametokea matukio mengi leo kwa hiyo nahakikisha kama ofisi iko salama kabla ya Madam President kuanza kuitumia." Renaldo aliongea tena bila kumuangalia yule ofisa. Bado alikuwa anazuga kupekua makaratasi ambayo alikuwa ameyashika mkononi kwa kujiamini.

"Ok! Naomba kama naweza kujumuika nawe nikusaidie?" Yule afisa akaongea.

"Hapana! Nitamudu tu mwenyewe usijali.!"

Yule afisa akaganda anamtazama Renaldo kwa karibia nusu dakika nzima. Renaldo kutokana na uzoefu wake alifahamu kabisa kwamba hii haikiwa dalili nzuri. Kuna jambo ambalo lilikiwa linaendelea kichwani mwa yule afisa.

"Samahani… una jambo lingine?" Renaldo akamuuliza.


"Hapana chief… uwe na usiki mwema!"

Yule afisa akaaga na kuondoka. Renaldo alihisi kabisa kulikuwa na kitu cha ziada juu ya ujio wa huyu afisa wa Secret Services. Hakuja tu hivi hivi.

Akasimama katikati ya ofisi na kuanza kuwaza na kuwazua. Ni kitu gani hasa ambacho kilikuwa kimetokea hapa ofisini siku ambayo Makamu wa rais David Logan alipopotea? Ni nani ambaye alificha ule ujumbe wa karatasi na ile chupa yenye Hydrogen Peroxide?
Na je hii Hydrogen Peroxide ilitumika kufanya nini humu ofisini?

Hakutaka kupoteza muda zaidi. Akaondoka kutoka hapa Oval Office na moja kwa moja kuanza kuelekea kwehye chumba ambacho waliwafungia Naomi, Rupert na Ethan.

"Kuna shida!" Lilikuwa ndilo neno la kwanzaRenaldo kulitamka mara tu baadaya kuingia kwenye kile chumba cha stoo walichofungiwa akina Naomi.

"Nini?" Naomi aliuliza kwa shauku huku wakisogea karibu na pale ambapo Renaldo alikuwa amesimama.

"Kuna yeyote hapa kati yenu ambaye anaweza kunieleza nini maana ya hii karatasi?"

Renaldo aliongea huku anaitoa ile karatasi aliyoipata Oval Office kutoka mfukoni mwa suruali.

#1. 5847, San Filipe, Suite 2600
Huston, Texas 77057


#2. 8 ft X 5 ft


#3. Nov 7, 20…………

Ujumbe ulikuwa unasomeka kwenye kipande cha karatasi ambacho alikishikilia mkononi.

"Ni nini?" Rupert akauliza.

"Nilikuwa natarajia kuwa mnaweza kunipa jawabu?"

"Tunawezaje kukupa jawabu bila kufahamu ujumbe umetoka wapi au unahusu nini?" Rupert akajibu kwa hasira kidogo.

Mpaka sasa Renaldo alikuwa moyoni anahisi kabisa kuna jambo ambalo halikuwa sawa pale Whitehouse. Lakini kutokana na uzoefu wake wa masuala ya usalama haikuwa rahisi kwake kutoa tu taarifa fulani reja reja huku akihisi kabisa kuna uwezekano wa taarifa hiyo kuwa ni nyeti.

"Ok! Samahani kwa kuwauliza.." Akaongea na kuanza kugeuka kutoka nje ya stoo.

"Renaldo…Renaldo…!!" Naomi akamkimbilia na kumzuia asiondoke.
"Hivi ni mara ngapi unataka nikwambie hili suala… licha ya kwamba mmetufungia humu ndani lakini kumbuka kuwa mimi ni National Security Advisor na yule pale ni Mkurugenzi wa CIA na yule pale Ethan ni moja ya komando bora zaidi kwenye hii ardhi ya Marekani… kwahiyo hebu acha huu upuuzi wa kutuweka gizani namna hii? Tueleze hiyo karatasi inahusu nini?" Naomi alifoka.


"Kwanza kabisa pia unapaswa kukumbuka kuwa nimewaweka chini ya ulinzi hapa kwa amri ya Rais wa nchi ambaye ndiye amiri jeshi mkuu… pili ni kwa nia njema kabisa nimekuja kuwaonyesha hii karatasi na inaonekana kabisa hamfahamu inahusu nini? Kwa hiyo sioni sababu ya kusema kingine chochote.." Renaldo aliongea kwa kujiamini na kutaka kugeuka tena ili aondoke.

"Nafahamu kitu!" Naomi aliongea kuchokoza mjadala.

"Kitu gani?" Renaldo aligeuka na kuonekana kuhairisha nia yake ya kuondoka pale stoo.

"Huo mwandiko… ni mwandiko wa David Logan.!"

Renaldo akaiinua ile karatasi usawa wa uso wake ili kuitazama vyema.

"Damn it! Kwa nini sikung'amua hili?" Renaldo akang'ata midomo yake kwa kujilaumu kwa namna gani ameshindwa kuona suala jepesi kama hilo kwa mtu wa kaliba na wadhifa wake.

"Si hilo tu… kuna lingine nafahamu kuhusu hiyo karatasi.!" Naomi aliiongea tena safari hii kwa madaha huku anaelekea upande mmoja wa kile chumba na kwenda kukaa kwenye kiti. Alikuwa anajua kabisa amefanikiwa 'kumbananisha' Renaldo kwenye kona.

"Kitu gani kingine?" Renaldo aliuliza kwa shauku kubwa.

"No! Nishakwambia vya kutosha na mimi… tueleze kwanza hii karatasi inahusu nini kabla sijakwambia chochote kingine?" Naomi aliongea kwa msisitizo.

"Hauwezi kunipa masharti ya kunipa taarifa kuhusu usalama wa Taifa… kumbuka unaongea na afisa wa Secret Services na maslahi yangu ni kumlinda na Rais, makamu wa Rais na maslahi yao kwahiyo nakuamuru unipe hiyo taarifa sasa hivi!" Renaldo alijitahidi kuongea kwa kujitutumua japo alikuwa anajua fika kwamba alikuwa amebananishwa kwenye kona.

"Kumbuka pia unaongea na National Security Advisor na ni maslahi yangu ya kwanza kuhakikisha kuwa nchi yangu iko salama... kwa hiyo kama unataka taarifa niliyo nayo kwanza nieleze hiyo karatasi inahusu nini?" Naomi naye alijitutumua mpaka akainuka kutoka kwenye kiti na kusimama.

Wakabaki wanaangalia wamekaziana macho kwa dakia nzima. Kama vile paka wanaotaka kuraruana.

"Renaldo! Sote tuko timu moja hapa, sisi na wewe… najua inafahamu kwamba kuna kitu hakiko sawa na kuna kitu Madam President Laura Keith anakificha. Wote tunataka kuhakikisha taifa hili liko salama. Kwa hiyo badala ya kutunishiana misuli hapa tunaweza kuzungumza pamoja na kuisaidia nchi.!" Rupert akaongea kwa sauti ya busara huku amemshika bega Renaldo.

Renaldo akaonekana kupoa kidogo.

"Ok! Wacha niwaeleze…"

Akawaeleza namna ambavyo alikata shauri kwenda kutazama Oval Office kwa umakini kama ambavyo Naomi alikuwa amesisitiza. Akawaeleza ni namna gani ambavyo aligundua kwamba mistari miwili ya mwisho ya vitabu kwenye 'shelves' vilikuwa vimepangwa tofauti na ilivyo kawaida. Akawaeleza namna ambavyo alianza kupekua vitabu kwenye shelves hizo na hatimaye kukuta chupa ya Hydrogen Peroxide na kipande hicho cha karatasi.

"Inaonekana Logan alikua anaandika haraka haraka… alikuwa na hofu ya jambo fulani hivi... swali ni jambo gani ambalo alikuwa anahofia na kwa nini alikuwa anandika maelezo haya?" Rupert akachokoza mjadala.

"Naomi umesema kwamba kuna kitu kingine unafahamu kuhusu haya maelezo kwenye hii karatasi… kitu gani?" Renaldo akakumbushia kitu ambacho Naomi aliongea awali.

"Ndio! Hiyo anuani, 5847, San Filipe, Suite 2600
Huston, Texas 77057 … ni anuani ya nyumba ya baba yake Madam President Laura Keith jimboni Texas!!" Naomi akajibu.

Ukapita ukimya wa kama dakika nzima. Kila mmoja akiwa anajaribu kuwaza na kuwazua kichwani. Kuna uhusiano gani? Kwa nini Logana kama yeye ndiye kweli aliandika hii karatasi… hiyo anuania aliiandika kwa sababu gani?


"Nadhani tunapaswa kwenda kwenye hiyo anuani huko Huston, Texas kuangalia kuna nini?" Rupert akapendekeza.

"Muende wapi? Mko chini ya ulinzi kwa amri ya Rais wa nchi. Hata kama nikiwaruhusu mimi mtoke mnadhani maafisa wengine watakubali mtoke nje ya Whitehouse? Na msisahau kuwa Rais ametangaza Marshal Law… tunafikaje Texas ilhali jeshi limeamuriwa lisiruhusu mtu yeyote kuonekana mtaani?" Renaldo aliongea mfululizo.

Naomi akazungusha macho kudharau kile ambacho Renaldo alikuwa anakiongea. "Renaldo wewe ndio boss hawa maafisa wote hapa Whitehouse... ukiamua unaweza kututoa humu ndani... kuhusu huko nje hakuna mwanajeshi ambaye anaweza kutuzuia tusiende tunakotaka… tukiwaonyesha vitambulisho tu hakuna mahala ambako tutazuiwa."

"Nadhani hayutakiwi kwenda Texas!" Ethan ambaye alikuwa amekaa kimya muda wote hatimaye akaongea.

Wote wakageuka kumuangalia.

"Una maana gani?" Naomi akamuuliza.

Wote walikuwa na shauku ya kusikia maoni ya Ethan. Kwa wote ambao walikuwa hapa, hakukuwa na mtu ambaye alikuwa na uzoefu wa 'field' na mikiki mikiki kukaribia hata nusu ya komando jasusi Ethan.

"Umesema kuwa nyuma ya vitabu pia ulikuta Hydrogen Peroxide, si ndio?" Ethan akamuuliza Renaldo.

"Ndio. Sahihi kabisa.." Renaldo akajibu.

"Wote hapa tunafahamu kazi kuu ya kwanza ya Hydrogen Peroxide ni nini katika matukio ya kihalifu na ujasusi… watu wanaitumia kusafisha damu iliyomwagika eneo la tukio na kwenye mwili au nguo!!" Ethan akaeleza.

"Ndio tunafahamu!" Akina Naomi wakaitikia kwa pamoja.

"Renaldo umetueleza kwamba hakuna mtu anayejua ni saa ngapi au namna gani Makamu wa Rais David Logan alitoka ndani ya Whitehouse... mlichokuja kusikia tu ni maiti za maafisa wa Secret Services nyumbaji kwake Naval Observatory Circle huku yeye mwenyewe akiwa hajikani alipo.?"

"Ndio ni sahihi kabisa.!"

"Vipi kama nikikikueleza kwamba maafisa wale wa Secret Services waliuwawa ndani ya Oval Office na hii Hydrogen Peroxide ilitumika kusafisha damu isionekane? Na kwa kuwa huwezi kuacha maiti ndani ya Oval Office kwa sababu ituzua kizaa zaa kikubwa, baada ya hapo maiti zao pamoja na Logan zikasafirishwa mpaka nyumbani kwa Makamu wa Rais David Logan kule Naval Observatory Circle?" Ethan alieleza kwa kujiamini.

Wote nao taa zikaanza kuwaka vichwani mwao. Lakini bado kulikuwa na maswali mengi na sintofahamu.

"Haiwezekani mtu aingie ndani ya Whitehouse... afanye mauaji ya walinzi wa Makamu wa Rais na kisha asafirishe maiti bila sisi kufahamu!" Renaldo akaongea kwa mashaka.

"Ni kweli haiwezekani… lakini inawezekana kama waliotekeleza hayo walikuwa tayari ndani ya Whitehouse!" Ethan akaongea kwa fumbo.

"Unataka kusema kuna maafisa wa Secret Services wamehusika kwenye hili?" Renaldo aliongea huku akianza kupandwa na hasira.

"Inaonekana iko hivyo!" Ethan akajibu kwa kifupi.

"Haiwezekani!!" Renaldo aliongea kwa jazba.

"Inawezekana kabisa Renaldo…" Naomi akaingilia kati, "na hiyo ndio namna pekee yenye mashiko na mantiki kueleza ni nini kilitokea… swali la msingi la kujiuliza ni kwa nini walipeleka maiti kule Naval Observatory Circle nyumbani kwa Makamu wa Rais David Logan?"

"Nadhani kuna kitu walikuwa wanakita…" Rupert naye akachangia. "Nina kila sababu ya kuamini kuwa Logan hawakumuua pale Oval Office. Nahisi kipindi hao wahusika wanapambana na walinzi wake ndio yeye aliandika hioi kikaratasi… naamini baada ya hapo wakamchukua akiwa hai na kuna kitu walikuwa wanataka Logan awaonyeshe na kitu hicho kipo Naval Observatory Circle.!"

"Kabisa! Inaingia akilini.." Ethan akakubaliana na wazo la boss wake Rupert. "Swali ni je Logan aliwaonyesha hicho kitu? Na ni kitu gani? Na kuna njia moja tu ya kufahamu jawabu kama walikiona au hawakukiona na ni nini hicho kitu…"

"Njia gani?" Renaldo aliuliza kwa shauku.


"Inabidi utusaidie kufika Naval Observatory Circle sasa hivi!!" Ethan aliongea huku amemkazia macho Renaldo.



Itaendelea…


The Bold
To Infinity and Beyond
 
images (56).jpeg




THE OTHER HALF



SEASON 1 - THE LEGENDOF ANABELLE




EPISODE 46

Ron, Latisha na Nicole walikuwa wameitolea macho screen ya laptop kusikiliza na kuangalia kile ambacho kilikuwa kinaendelea. Kwa namna fulani ilikuwa inahuzunisha na kuogopesha kuwa katika hali ambayo walikuwa nayo muda huu.
Wao kuketi na kitazama video ambayo Logan alikuwa ameirekodi siku ambazo hazijulikani zilizopita ilikuwa ni kana kwamba walikuwa wanatazama ujumbe wa mwisho wa mtu kabla ya kujiua au kana kwamba ilikuwa ni kutazama ujumbe wa mwisho wa mtu ambaye alikuwa amejitoa muhanga.

Wote walikuwa kimya kabisa lakini woga, uchungu na wasiwasi ambao walikuwa nao ulikuwa unaweza kuhisiwa hata ukiingia tu kwenye chumba.
Latisha na mwanaye Nicole walikuwa wanaangalia kwa uso ambao ulikuwa unaakisi kabisa kile ambacho kilikuwa mioyoni mwao, wasiwasi na woga wa kumpoteza mtu ambaye walikuwa wanampenda kwa mioyo yao yote mpaka kwenye mifupa yao. Ron yeye alikuwa anaangalia kwa shauku kubwa na umakini.

Kama kuna swali ambalo wote walikuwa hawajajiuliza ni kwa nini Ron alikuwa bega kwa bega na wao kutaka kutatua hatari hii ambayo ilikuwa imeikumba ulimwengu. Mpaka muda huu ni Ron pekee ndiye ambaye alikuwa anajua ni kitu gani gasa ambacho alikuwa amekilenga moyoni mwake.

"….naamini uko mpweke mwanangu muda huu. Na kama unasikiliza ujumbe huu maana yake kwamba nimeshafairiki muda mwingi na pengine ujumbe huu ndio kitu pekee cha kukufariji. Hakuna haja ya kujiuliza ni kitu gani hasa kimetokea ulimwenguni. Na hakuna haja ya kutafuta jawabu. Haja yangu kubwa ni kutaka uwe salama mwanangu.."

Ujumbe wa video ulikuwa unaongea pale kwenye laptop.

"…Nicole! Unakumbuka mara yetu ya mwisho kusafiri tulienda wapi? Basi nahitaji ufike mahala hapo. Pamoja na ujumbe huu ambao unautazama, nadhani unaweza kuona files nyingine kadhaa. Tofauti na ujumbe huu files zilizosalia zote utahitaji neno la siri ili kuzifungua. Kwa hiyo nahitaji ufike mahala ambako tulienda mara ya mwisho mimi na wewe kisha utapata maelezo yaliyosalia. Nahitaji uwe salama mwanangu. Fika hapo haraka uwezavyo.!"

Ujumbe ukaishia hapo.

Haraka haraka Ron akajaribu kufungua files nyingine ambazo zilikuwa zimesalia lakini hakukuwa na mafanikio yoyote. Kila file ambayo alijaribu kuifungua ilikuwa inahitaji neno la siri ili iweze kufunguliwa.

"Daaammmnnn it!" Ron akainuka kwa hasira kutoka pale ambako alikuwa ameketi.

"Nadhani amefanya hivyo kwa sababu za kiusalama." Latisha akaongea huku naye anasimama.

"Sababu gani za kiusalama?" Ron akaulizankwa hasira.

"Namaanisha hii sababu ya kuweka maneno ya siri na kutaka kuyapata kutoka mahala kwengine amefanya hivyo kwa sababu za kiusalama. Vuta picha ingekuwaje kama ni mtu mwingine angepata fursa ya kugundua chumba hiki cha siri na kuona hizi recordings kabla yetu? Nadhani alichukua tahadhali mapema ili kulinda hicho ambacho kipo kwenye jumbe hizi.!" Latisha aliongea kwa msisitizo.
 
"Tahadhali gani? Kutuhangaisha kila sehemu kama vichaa?" Ron akaendelea kufoka tena kwa hasira.

"Tahadhali ya kuhakikisha kama isingelikuwa sisi… namaanisha Nicole na mimi! Kama isingelikuwa Nicole na mimk basi mtu mwingine asiweze kujua kilichomo ndani ya hizi files kwa sababu asingeweza kujua ni wapi ambapo tulisafiri mara ya mwisho kwa pamoja!" Latisha akaendelea kujieleza.

"Na ni wapi ambako mlisafiri kwa pamoja?"

"Ilikuwa miezi kama mitatu kabla hatujatalikiana… tulisafiri pamoja kwenda Bahamas. Nadhani ndiko huko ambako anamaanisha."

"Whaaaat?? Bahamas… tunafikaje Bahamas?" Ron akang'aka kwa hasira zaidi.

"Sijui lakini ndiko ambako tulienda kwa mara ya mwisho kama familia." Latisha alijibu huku amejiinamia kutokana na kujua fika kutowezekana kwa huko ambako wanatakiwa kwenda.

"Tunafikaje Bahamas na hii Marshall Law iliyotangazwa na Rais? Umeona ni namna gani imetuwia vigumu kufika hapa kutoka New York. Kama kusafiri tu ndani ya nchi imekuwa mtihani hivi, tunawezaje kutoka nje ya nchi?"

Swali la Ron lilibakia tu 'linaning'inia hewani'. Hakuna ambaye alikuwa na jawabu au hata pendekezo la nini wafanye mpaka kufika huko Bahamas. National Guard ilikuwa imemwagwa mchi nzima. Wanajeshi walikuwa na ruhusa ya kumpiga risasi yeyote yule ambaye angeonekana mtaani. Iliwachukua kiwango kikubwa cha ushawishi alionao Ron pamoja na rasilimali fedha zake kwa wao kuweza kufika hapa Washington kutokea jijini New York wanakoishi. Kwa hiyo taarifa hii kwamba inawapasa wafike Bahamas ilikuwa ni taarifa ya kukatisha tamaa kabisa.

"Safari ya mwisho haikuwa Bahmas.!!" Nicole ambaye alikuwa kimya muda wote hatimaye akaongea.

"Naam.!" Ron akageuka kwa shauku kumtazama.

"Safari ya mwisho hatukwenda Bahamas!" Nicole akaongea tena.

"Una maana gani Nicole. Safari ya mwisho sote tulisafiri pamoja mpaka Bahamas… mimi, wewe na baba yako. Ilikuwa miezi mitatu kabla hatujatengana.!" Latisha akaongea kwa mshangao, akishangaa kwa nini binti yake anasema kile ambacho alikuwa anakisema ilhali alikuwa na uhakika kabisa kuwa safari yao ya mwisho kama familia walisafiri kwenda Bahamas.

"Mama… hiyo ilikuwa ni safari yetu ya mwisho kama familia lakini haikuwa safari yetu ya mwisho mimi na baba… kuna sehemu tulienda mimi na yeye!" Nicole aliongea huku amewakazia macho.

Wote walijawa na shauku. Lakini Ron ndiye ambaye alikuwa na shauku zaidi. Uso wa Latisha ulikuwa na woga kuzidi shauku ambaye alikuwa nayo moyoni. Alikuwa hafahamu safari hiyo ya mwisho ya mwanaye Nicole na baba yake.

"Mlienda wapi Nicole?" Latisha aliuliza kwa mshangao na woga.


"BAAAAAAAAAAANG.!"

Zilikuwa ni kelele za ghafla za mlango wa kuingilia chini kwenye basement walipo ulikuwa umefunguliwa kwa kishindo cha kuvunjwa.

Ghafla zilisikika hatua za haraka haraka za watu ambao walikuwa wanateremka ngazi za basement kwa kasi kubwa.
Kwa haraka sana Ron, Nicole na Latisha walitoka kutoka kwenye kile kijichumba cha siri na kusimama katikati ya basement kuona ni nani ambao walikuwa wamewavamia.

"Msisogee hata hatua moja.!!!" Amri ilitoka huku wakionyeshwa mitutu ya bunduki.

Walikuwa ni Naomi, Rupert, Ethan pamoja na Renaldo ndio ambao walikuwa wameingia hapa kwa kishindo hivyo.
Baada ya wote kutazamana sawia hatimaye wakatambuana. Hakuna ambaye alikuwa hamtambua Latisha mke wa zamani wa Makamu wa Rais David Logan na mwanaye Nicole. Pia hakuna ambaye alikuwa hamtambui mfanya biashara maarufu Rodney Van Derberg.

"Mnafanya nini hapa?" Naomi ambaye ndiye pekee hakuwa na bunduki aliuliza kwa mshangao.

"Tuwaulize nyinyi mnafanya nini hapa?" Ron naye aliuliza swali kwa mshangao.



Itaendelea…


The Bold
To Infinity and Beyond
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom