The Other Half (Simulizi)

The Other Half (Simulizi)

Mi naomba iyo tovuti jamani uku nimekuta link ni manyotamanyota sioni
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya The Other Half, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya The Other Half, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond

Shukrani sanaa mkuu ubarikiwe kwa hili maana tulikuwa tunaisubiri kwa hamu sanaa aisee
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya The Other Half, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
Jioni inatoweaka sasa kigiza kinaingia
Weka mambo basi Habibu B. Anga
 
Habari chiefs, kwa Wapenzi wa Simulizi hii ya The Other Half, kuanzia leo jioni nitaweka muendelezo kama Episode 10 hivi.

Mnisamehe kwa ukimya, ratiba yangu imekuwa ngumu mno mno mno. Nikianza kuweka muendeleo leo jioni itakuwa imeanza rasmi kuendelea na mpaka tutafika mwisho.

Kumradhi kwa usumbufu uliojitokeza na asanteni kwa kusubiri.


Asante!


Habibu B. Anga alias "The bold"
To Infinity and Beyond
asante kwa kutukumbuka mkuu habibu, ukimaliza toa kitabu mkuu tukuunge mkono.
 
Mweee mweer mweee


Habibu b anga


Lait ungetambua ulipp ishia hii story ungetupia fastaa sasa sijui mwana umepatwa na nn aisee??


Dr Cindy ep37 shusha shusha Hapa mkuui
 
THE OTHER HALF



SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE




Previously…

Mzee Caleb anamaliza kufukua mabaki ya mifupa ya mkewe Suzanne na mwanaye Clinton kutoka kwenye kaburi lililopo nyuma ya nyumba yake. Mifupa mingine yote anaiweka kwenye mifuko miwili ya plastiki huku mafuvu ya vichwa akiyasaga na kuweka unga wake kwenye chupa mbili.

Akiwa anajiandaa kujitoa damu ili ampe kiumbe wa ajabu waliyepewa kwenye msitu wa Ox, vijana makomando waliomkimbia masaa kadhaa nyuma wanarejea na kumpa taarifa kuwa maafisa wa National Guard wametanda kwenye mpaka wa Maryland na jimbo la Washington na hawaruhusu mtu yeyote kuvuka.

Hawawezi kwenda kusini, kaskazini wala mashariki kwa kuwa huko wanapakana na miji ya Baltimore na Annapolis ambayo tayari imekwisha twaliwa. Chaguo pekee walilo nalo ni kubakia hapo watwaliwe pamoja na mji wao wa Maryland au waende Baltimore na Annapolis ambayo tayari imeshafanywa kuwa Anabelle.!




Episode 37

"Kurudi nyuma ndio kwenda mbele.!"

"Una maana gani mzee?"

"I say backwards is the only way forward!" Mzee Caleb aliongea huku anainuka kutoka pale sakafuni alipokuwa ameketi kutokana na kupigwa bumbuwazi kwa taarifa aliyopewa.

"Nimekusiki ndio maana nimekuuliza una maana gani?" Moja ya vijana wa Ethan aliuliza tena.

"Tunahitaji kurudi msituni tena.!!" Mzee Caleb aliongea huku anachukua tena mpira mwembamba na kisu na kuanza kushuka ngazi kwenda chini kwenye 'basement' ya nyumba.

Vijana wote saba wa Ethan nao waliinuka na kuanza kumfuata kule chini ambako alikuwa anaelekea.

"Kufanya nini ndani ya msitu?" Komando mwingine akauliza kwa kuhamaki.

"Kama kuna lolote la kutuokoa nadhani Masalia, mzee wangu na wenzake ndio pekee wanaweza kujua tufanye kitu gani! Na kama hakuna cha kufanya basi ni bora tutwaliwe tukiwa pamoja nao lakini….."

Mzee Caleb aliongea alafu akasita kumalizia sentesi yake.

"Lakini nini?" Kijana mwingine akauliza kwa woga.

"Lakini sina hakika kama tutawapata ndani ya msitu… Masalia wanahama hama muda wote kulingana na malengo yao… kwa hiyo tunachokwenda kufanya ni kubahatisha.!"

Hakuna ambaye aliuliza swali au kusema chochote kile. Ilionekana kwamba bahati haikuwa upande wao hata kidogo. Ilikuwa kama vile kila mti waliokuwa wanajaribu kuuparamia ulikuwa unateleza.

Walishuka na ngazi mpaka chini kwenye basement. Japokuwa ndani ya basement kulikuwa kuchafu, utando wa buibui kila mahala na makorokoro kibao lakini kutokana na utofauti wa yule kiumbe wa ajabu alikuwa ndiye kitu cha kwanza macho kukiona ukiingia tu ndani ya basement. Rangi nyekundu iliyotokea mwilini mwake ilikuwa imekooza zaidi na ilionekana kuendelea kukooza taratibu kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele. Bado alikuwa kama vile amelala usingizi ndani ya kile kitundu alichofungiwa.

"Unataka kufanya nini mzee?" Yule komando muongeaji sana akamuuliza Mzee Caleb huku anamtazama kwa macho ya udadisi.

"Tunahitaji kumpa damu huyu kiumbe kama tulivyoambiwa msituni.!" Mzee Caleb alijibu macho yake akimtazama yule kiumbe wa ajabu.

"Kwa hiyo unataka kutoa lita moja ya damu mwilini mwako?" Alimuuliza huku anatabasamu kifedhili kama 'anamuinjoi' hivi.

"Tunahitaji kumpa damu huyu kiumbe!" Mzee Caleb alirejea tena jibu lake huku akikwepesha macho na kumuangalia tena yule kiumbe pale tunduni.

"Frank! Nenda kwenye sanduku la huduma ya kwanza lete vifaa tunavyohitaji kutoa damu!" Komando muongeaji sana alimuagiza mwenzake.

Labda ilikuwa ni moja ya maadili yao ya kazi kwa sababu hii ilikuwa ni mara ya kwanza tangu kiongozi wao Ethan aondoke Caleb kuwasikia wanaitana kwa majina. Muda wote huu ambao walikuwa wote, mtu pekee ambaye Mzee Caleb alimfahamu jina alikuwa ni kiongozi wao Ethan ambaye hakuwepo hapa muda huu.
Yule kijana alikuwa kama vile amekisoma kile ambacho Mzee Caleb alikuwa anakiwaza kichwani.

"Jina langu ni Walker, huyu ni Justin, huyu Mickie, huyu Thabeet, huyu Rex, yule pale Saimon na aliyeondoka nadhani umesikia jina lake, Frank.!!" Yule komando muongeaji, Walker alijitambulisha na kuwatambulisha wenzake wote wengine sita waliosalia.

Yule komando, Frank aliyekwenda kuchukua vifaa vya kutolea damu alirejea mkononi akiwa na mipira kadhaa ya kutoa damu na vifaa vingine.

Hakuna komando ambaye aliongea neno lolote, lakini makomando watano kila mmoja alichukua seti ya vifaa na kukaa chini. Walker ambaye alionekana kama ndiye kiongozi wao baada ya Ethan kuondoka akaanza kuwachomeka mipira kwenye mishipa ya damu mmoja baada ya mwingine kwa ustadi kama ambavyo madaktari wafanyavyo.

Zilipita kama dakika ishirini na tano au thelathini za ukimya kila mtu akiwaza na kuwazua kichwani mwake kuwasubiria wenzao watano wanaotoa damu itimie kiwango kile ambacho walikuwa wanakihitaji.
Wote walikaa kimya kabisa wakionekana kila mmoja kuwa mbali kimawazo. Muda ulikuwa unayoyoma haswa. Walikuwa na labda Massa mawili tu kabla Maryland haijatwaliwa kuwa Anabelle. Tumaini la kuokoka kutokana katika uwezekano huu wa kutwaliwa pamoja na mji wa Maryland lilikuwa dogo mno. Japokuwa walikuwa wanajitahidi kufanya juhudi kadhaa kujiokoa lakini kwa namna Fulani kila mmoja wao alikuwa anajua ni nini kilikuwa mbele yao, kutwaliwa ndani ya Anabelle na kupotelea kusikojulikana.

"Nadhani imetosha.!" Walker alivunja ukimya na kuwazindua wenzake kutokana kwenye 'usingizi' wa mawazo wa takribani dakika theleathini. "Tupime hiyo damu tuone tuna kiwango gani!"

Makomando wote watano kila mmoja akajitoa mpira mkononi kwenye mshipa wa damu na kukandamiza kwa pamba mahala ambapo walichomeka sindano kuingia mshipani na kisha Walker kuchukua vipakiti vya plastiki vyenye damu kutoka kwa makomando wale watano na kuanza kuipima kwa kuweka kwenye chupa ambayo alikuwa nayo Mzee Caleb.

"Lita moja na…na… na kama robo hivi.!" Walker aliongea huku anamtazama Caleb kwa tabasamu la utani.

Chupa iliyoletwa na Caleb ilijaa yote mpaka juu shingoni na bado kipakiti kimoja cha damu kilibakia. Hii ilimaanisha kwamba walikuwa na lita moja na ushei, ambayo Walker alikisia kuwa ni Lita moja na robo.

"Sikumbuki kama Mzee wako kule msituni alieleza ni namna gani tunampatia hii damu… naamini sio kumnywesha mdomoni kama mtoto mchanga.!" Walker aliongea tena huku anatabasamu.

Mzee Caleb hakujibu chochote. Aliichukua chupa iliyojaa damu kutoka mkononi kwa Walker. Alipoishikilia mkononi alihisi kabisa joto ambalo lilikuwa linatoka kwenye damu. Alihisi kabisa uhai wa binadamu uliomo ndani ya hiyo chupa. Kwa kiasi fulani ilikuwa inaogofya kushikili chupa kubwa ya ujazo huo wa lita moja ikiwa imejaa damu ya binadamu ambayo bado ilikuwa ya moto kabisa kutoka kwenye mwili wa mtu. Chupa ilikuwa ndefu wastani wa kama urefu wa chupa ya soda lakini ilikuwa pana kiasi cha kurandana kabisa na upana wa bilauli ndogo.

Mzee Caleb alishikilia chupa mkononi akitafakari ni nini hasa afanye. Haikuwa busara kufungua kitundu na kuingia ndani ili kujaribu kumnywesha damu mdomoni mnyama huyu wa ajabu kwani hakuna ambaye alikuwa anajua mnyama huyu akipata damu ni nini ambacho kingetokea.

Mzee Caleb akachovya kidole kimoja kwenye damu. Mwili ulimsisika alipoingiza kidole chake kwenye dimbwi hilo la lita moja ya damu iliyo ya moto bado. Akachovya kidole na kutoa kisha akasogea karibu na kitundu cha yule mnyama na kukung'uta mara kadhaa ya damu juu ya mnyama huyu.

Matone kadhaa ya damu yalidondoka juu ya ngozi laini ya mnyama huyu ambayo sasa ilikuwa na rangi nyekundu iliyoiva haswa kiasi kwamba hata tone la damu lilipodondoka juu yake lilikuwa halionekani sawia ni wapi lilikuwa limedondokea.

Kuna kitu fulani hivi Caleb alikiona juu ya ngozi ya mnyama japo hakuwa na hakika sana. Akachovya tena kidole kwenye bilauli ya damu na kunyunyiza tena matone kadhaa ya damu juu ya mnyama huyu wa ajabu.
Naam, haikuwa anakosea wala kuona vibaya. Sehemu ambayo matone ya tamu ilikuwa inadondoka ilikuwa inabadilika na kuwa ya rangi nyeupe.

Mzee Caleb akasogea karibu zaidi na kitundu cha mnyama na kupenyeza ndani mkononi wake alioshikilia bilauli ya damu na kuimimina damu yote juu ya mnyama huyu.
 
Damu ilikuwa inamwagika juu ya mnyama huyu lakini ajabu ni kwamba alikuwa alowi. Yaani kama kwamba alikuwa anamimina maji kwenye sponji. Damu ilikuwa haimlowanishi kiumbe huyu badala yake ilionekana kufyonzwa ndani ya mwili wake.

Baada ya Caleb kumaliza kumimina damu yote, taratibu rangi ya ngozi ya mnyama huyu ilianza kubadilika na kuanza kurejea mwenye weupe.
Mzee Caleb na wenzake walikaa pembeni kushuhudia viroja hivi vilivyokuwa vinatokea mbele ya macho yao. Ndani ya kama dakika tano hivi rangi ile nyekundu iliyokolea ya ngozi ya huyu mnyama iligeuka na kuwa rangi nyeupe kabisa, nyeupe sana kufanana kabisa na weupe wa sufi au theluji. Hata mnyama mwenye japo hakuamka kabisa lakini alionekana kuhema.

"Nadhani tumefanikiwa au tumeongeze tena mpaka aamke l?" Walker aliongea.

"Hapana! Tuliambiwa lita moja ya damu itamfanya asife lakini pia hatoweza kuamka na kuleta madhara… tukiongeza hata damu kidogo nyingine tunaweza kujutia kufanya hivyo… nadhani mpaka hapa tumefanikisha!" Caleb akajibu.

"Kwa hiyo kifuatacho?" Walker akauliza tena.

"Tunaelekea msitu wa Ox!!" Caleb akajibu.

"Ooooh!! Mungu tu anajua kiasi gani nachukia ndani ya ule msitu natamani kungekuwa na wazo lingine!" Walker akaongea akiwa amekereka.

"Backwards is the only way forward! Mbebeni huyu mnyama twende, tuna chini ya Massa mawili kabla Maryland haijatwakiwa!" Caleb aliongea huku anaanza kuondoka kwenye basement kuzifuata ngazi zinazoelekea juu.


Lakini ghafla…..


"Oooh! Oooh! Oooh.. Aaah.!!"

Mzee Caleb alidondoka chini kwenye ngazi huku amejishika kifuani akiwa kama analalamika mauvimu.

"Mzee nini.!?" Walker na wenzake wawili walimbilia na kumuokota kutoka chini kwenye sakafu alikokuwa anagala gala na kumkalisha kitako.

"Imekuwaje mzee?" Walker akamuuliza tena huku amemtumbulia macho.

"Nipelekeni sebuleni! Njooni na huyo mnyama…" Mzee Caleb aliongea kwa taabu sana huku bado amejishika kifuani.

Walker na wenzake wawili wakambeba Caleb kuelekea juu sebuleni huku wenzao wanne waliosalia wakibeba kile kitundu chenye mnyama ndani yake.

"Vipi mzee? Mshituko wa moyo?" Walker aliuliza walipofika sebuleni.

"Hapana!" Caleb alijibu kwa shida sana.

"Ni nini kumbe?"


"Mnakumbuka niliwaeleza kuwa nilipokuwa mdogo mzee wangu aliwahi kunipeleka msituni ambako nilitolewa nusu ya nafsi yangu na kupewa mtu mwingine?" Mzee Caleb aliongea huku akiwa anahema juu juu.

"Ndio ndio! Umetueleza hapa kabla Ethan na Naomi hajaondoka kwamba mtu huyo ndiye ambaye alivamia Whitehouse na Makamu wa Rais David Logan kudhani ni wewe.!!" Walker alimjibu kwa haraka haraka.

"Naam! Niliwaeleza kwamba tunapaswa kumfuatilia yeye ili tuweze kuwapata The 46 na dalili ya kumpata yeye niliwaambia kuwa kuna hali huwa najisikia ndani yangu…"

"Ndio ndio mzee!"

"Ndio hali hii ninayojisikia sasa… yuko maeneo haya! Tulipanga tumtafute ila anaonekana ametutafuta yeye… kuna kitu kibaya anataka kukifanya… yuko karibu kabisa na hapa ndio maana najisikia namna hii ndani yangu!" Mzee Caleb aliongea akionekana kuwa kwenye maumivu makali akiendelea kuhema kwa shida sana.

Makomando hawakusubiri Caleb aseme neno lingine lolote lile, kila mmoja alikamata bunduki yake huku kidole kikiwa kwenye 'triger' tayari kwa kushambulia muda wowote ule. Kwa haraka na weledi waligawana kila mmoja akienda dirisha la upande fulani wa nyumba na kuchungulia nje kudadisi kama wanaweza kumona mtu huyo.

"Kwa hiyo tunafanyaje sasa mzee?" Walker ambaye alikuwa amebaki na Mzee Caleb pale alipo alimuuliza kwa kunong'ona.

"Backwards is the only way forward! Twendeni msitu wa Ox!" Mzee Caleb akajibu.

Walker akawapa wenzake maelekezo kwa ishara za vidole kuashiria kwamba wanatakiwa waondoke hapo haraka.

Safari hii Walker peke yake alimbeba Mzee Caleb kama vile amembeba mtoto mdogo mikononi, huku wenzake wanne wakibeba Kitundu chenye yule mnyama na wawili waliobakia wakitoa ulinzi kwa wenzao kwa kukaa pande zote mbili wakipepesa macho huku na huko kuhakikisha hawashambuliwi kwa kushitukizwa.


Walipanda kwenye magari kwa haraka huku, gari la kwanza wakipanda makomando wawili na nyuma kuweka tundu lenye yule mnyama. Gari la pili walipanda komando mmoja akiwa anaendesha kwenye usukani na siti za nyuma walikaa Walker na Mzee Caleb. Na gari la Tatu lilifuatia nyuma likiwa na makomando wawili.

Mzee Caleb bado alikuwa anaugulia maumivu kifuani. Walikuwa wamebakiwa na kama lisaa limoja na nusu kabla ya Maryland kutwaliwa.

Gari ziliendeshwa kwa spidi kubwa ajabu kama vile roketi lakini ajabu ni kwamba bado Mzee Caleb aliendelea kuugulia ile hali aliyokuwa anaisikia kifuani kumaanisha kwamba mtu huyo mwenye nafsi yake bado alikuwa anawafuatilia.

"Inawezekanaje hii? Huyo mtu ana kasi ya namna gani kukimbizana na gari mwenye spidi kubwa hivi?" Walker alihamaki.

"Si binadamu wa kawaida… au umewahi kusikia binadamu mwenye nafsi nusu?" Mzee Caleb aliongea.

"Anataka nini kwetu?" Walker akauliza.

"Mambo mawili… kwanza naamini amejua tunaelekea Ox na anataka kutuzuia… na pili anahitaji nafsi yangu nusu iliyobaki ili awe nayo kamili… kuna vitu anatakiwa kufanya na hawezi mpaka nafsi yote kamili iwemo ndani yake!"

"Vitu gani?"

Mzee Caleb hakujibu kitu bali alikuwa ameduwaa ametoa macho anatazama nje barabarani.

Pembezoni mwa barabara kulikuwa na msongamano mkubwa sana wa miti, na ndani yake alionekana mtu au kwa usahihi zaidi tuseme kivuli cha mtu. Mtu huyu hakuonekana hata kiganja cha mkono au ukucha. Alikuwa amevalia vazi zito jeusi tii kama kaniki ambalo lilimfunika kuanzia kichwani mpaka vidole vya mguu. Mahala pekee ambalo alikuwa anaonekana ilikuwa ni usoni ambako alikuwa anaonekana kwa mbali sana kutokana na vazi hilo kufunika kichwa. Alikuwa na uso wa ajabu wenye ngozi yenye mabaka kama chatu na macho mekundu ambayo yalikuwa yanawaka kama taa.

Mtu huyu alikuwa anakimbia kwa kasi isiyo ya kawaida. Japokuwa Makomando walikuwa wanaziendesha gari kwa spidi ya juu kabisa ya kiwendawazimu lakini mtu huyu alikuwa anakimbia kwa kasi hiyo hiyo bila kuachwa nyuma huku manguo yake meusi aliyojitanda mwili mzima yakipepea kutokana na upepo.

"Ni yeye?" Mzee Caleb alijibu huku bado amekodoa macho nje.

"Nani?" Walker akauliza.

"Ni yeye! Niliyewaeleza kuwa ana nusu ya nafsi yangu… ni yeye huyu!"

"Umesema kuna jambo wanataka kufanya haliwezekani mpaka mtu huyu awe na nafsi yako kamili! Ni kitu gani?" Walker akauliza kwa shauku.

"The 46 wanajiandaa kufanya kafara ya pili.!!" Mzee Caleb alijibu kwa sauti ya kutetema kwa woga huku bado akiangalia nje kwa binadamu yule mwenye nusu ya nafsi yake.



Itaendelea…



THE BOLD
 
THE OTHER HALF



SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE





Previously….


Rais was Marekani Bi. Laura Keith amehuisha Marshall Law nchi nzima baada ya dunia kukumbwa na giza la kabla muda wa mchna na giza kutoonyesha dalili yoyote ya kukoma. Chini ya sheria hii hakuna raia yeye ambaye anaruhusiwa kutoka nje au kuonekana mtaani. Maafisa wa vikosi vya kijeshi vya National Guard wamemwaga mtaani kote.

Hii inakuwa ni bahati mbaya kubwa kwa Bilionea Rodney Van Der Berg ambaye alikuwa nyumbani kwa familia ya Bw. Donald McLaren na mkewe Latisha ili kuomba mtoto wao Natalie awasaidie kumtafuta David Logan ambaye alikuwa ametekwa na watu wasiojulikana.

Lakini kuna gari la jeshi limefika nje ya nyumba ya Familia ya Donald McLaren na maafisa wawili wa National Guard walikuwa wameshuka huku wameshikilia mitutu ya bunduki na kwenda kugonga mlangoni.




EPISODE 38


Scarsdale, New York - Marekani


Mlango wa nyumba ya familia ya Bw. Donald McLaren ulifunguliwa na maafisa wa jeshi kuingia ndani.

"Habari.!" Afisa mmoja alisalimia.

Donald, mkewe Latisha, mtoto wao Natalie, Ron pamoja na walinzi wake, wote walikuwa kama vile hawajaisikia salamu walibakia wamewatumbulia macho tu.

"Gari iko tayari?" Ron aliwauliza wale wanajeshi.

"Iko tayari Mkuu?" Mwanajeshi mmoja akajibu.


"Nisubirini nje nakuja!" Ron aliwajibu kwa kifupi tu.

Wanajeshi wale wawili walitoka nje. Donald na mkewe walibakia wameduwaa wakishangaa ni nini kilikuwa kinaendelea.

"Nahitaji kwenda na Natalie sasa hivi bila kuchelewa!" Ron aligeuka nyuma kuwaangalia Donald na mkewe na kuwaeleza.

"Kwanza naomba utueleze ni nini kinaendelea hapa? Kwa nini hawa wanajeshi wakuletee gari?" Latisha aliongea akiwa na mshangao.

"Donald, Latisha! Sidhani kama ni jambo la kushangaza kwa mtu wa kaliba yangu kuweza kupata 'favour' za namna hii… labda tu niseme kwa ufupi kila kitu kina bei yake duniani… mmeridhika? Naweza kwenda na Natalie sasa?" Ron aliongea huku anatabasamu wa majivuno.

"Siwezi kukukabidhi binti yangu bila mimi mwenyewe kuwepo! Kama unahitaji kwenda na Natalie basi lazima na mimi niwepo" Latisha kaweka msimamo.

"Na siwezi kuacha binti yangu na mke wangu waondoke bila uwepo wangu! Lazima na mimi niwepo!" Donald nae akalipuka ghafla na kuweka msimamo kama wa mkewe.

"Hey, hey, hey! Samahani natamani tungeenda wote hata na ukoo wenu mzima… tatizo ni kwamba nadhani mnajua kuna Marshall Law na hakuna gari ya kiraia inayoruhusiwa barabarani… tumefanikiwa kupata gari moja tu ya kutusafirisha, kwa hiyo kama ni kwenda basi mchague ni nani ambaye ataenda kati yako na mkeo hatuwezi kutosha wote ndani ya gari!"

Hakukuwa na ubishi kwamba kama ni kwenda basi Latisha ndiye ambaye alitakiwa kwenda kwa kuwa yeye ndiye alikuwa mama mzazi na Donald alikiwa baba mlezi tu kwa Natalie.

Baada ya kukumbatiana na kufarijiana, Latisha na mwanaye Natalie wakiongozana na Ron pamoja na mlinzi wake mmoja waliondoka.

Ndani ya gari siti za mbele walikaa wale wanajeshi wawili ambao walikuja na ile gari na siti mbili za nyuma Ron, mlinzi wake, Latisha na Natalie walibanana kwa pamoja.

"Tunaelekea wapi bwana mkubwa?" Mwanajeshi ambaye alikuwa kwenye usukani aliuliza.

"Naval Observatory Circle… nyumbani kwa Makamu wa Rais!" Ron alijibu.

Natasha alitamani kumuuliza Ron kwa nini wanaenda nyumbani kwa mumewe wa zamanai wakati amewaeleza muda mchache uliopita kwamba ametekwa lakini hakuthubutu kuuliza swali lolote ambalo alihisi la siri kubwa mbele ya hawa wanajeshi wa National Guard.

Ilikuwa safari ndefu ya karibia masaa manne na nusu. Mpaka muda ambao walikuwa wanawasili ilikuwa tayari yapata karibia saa nne usiku lakini kutokana na giza lililokuwepo tangu mchana hakukuwa na tofauti yeyote ya muda ambayo ilihitaji kuitilia maanani.

Jengo la nyumba ya Makamu wa Rais lilikuwa limezungushiwa utepe wa njano wa polisi kutokana na tukio la mauaji ya maafisa wa Secret Services mahali hapo siku chache nyuma lakini ajabu ni kwamba kulikuwa na askari wawili tu wa kawaida ambao walikuwa wanalinda. Labda ni kwa sababu ya nchi kuwa kwenye wakati mgumu ndio maana vyombo vya ulinzi haviku havikuona umuhimu wowote wa kutumia rasilimali kubwa kulinda jengo tupu badala ya kulinda mitaani ambako kulikuwa na taharuki.

Wale wanajeshi wawili waliokwenda nao waliwasaidia kuwapitisha kwenye kizuizi cha polisi kwa kuongea na askari wale wawili ambao walikuwa wanalinda mahali hapa na moja kwa moja wakaingia ndani ya eneo hili la Makazi ya Naval Observatory Circle.

"Maagizo yetu yalikuwa kukupeleka mahala unakohitaji tu bwana mkubwa nadhani tumefanya hivyo na itakuwa sahihi tukirejea kwenye jukumu letu huko mitaani.!" Moja ya wale wanajeshi akaongea.

"Nahsukuru sana na amfikishieni Meja Lewis shukrani zangu!" Ron akashukuru na kupena mikono na wale wanajeshi.

Wanajeshi wakakwea kweye gari yao na kuondoka wakiwaacha hapa nje ya jumba la Makamu wa Rais.

"Unawaacha waondoke tukimaliza tunachofanya hapa tunatejea vipi nyumbani?" Latisha akamuiliza Ron.

"Usijali kuhusu hilo...!" Ron alijibu kwa kujiamini huku wakitembea kuufuata mlango wa nyumba.

Kutokana na nyumba kuwa tupu na tukio ambalo lilikuwa limetokea, hakuna mlango wowote ambao ulikuwa umefungwa.

Waliingia ndani kwenye sebule kubwa ya nakshi za fanicha za thamani lakini za enzi za "kikoloni". Japokuwa vitu hapa sebuleni hasa fanicha kuwa za enzi zilizopita lakini uthamani wake wa hali ya juu ulifanya sebule iwe nzuri na ya kuvutia kabisa.

Walitumia kama dakika kumi nzima kushangaa shangaa na kudadisi pale sebuleni. Wote wanne, yaani Ron, mlinzi wake, Latisha na Natalie kila mmoja alitumia muda wake kutazama sebule na kudadisi kadiri ambavyo alikuwa anaweza. Kila moja mara alishika picha Fulani akaiacha, mara ashangae Picha za viongozi wa zamani wa taifa, mara ashangao sanamu za kuchongwa na kufinyanga… ili mradi tu ilikuwa kudadisi japokuwa hata walichokuwa wanakidadisi hawakukijua. Japokuwa hapa ndani kulikuwa kunapendeza lakini bado sehemu kadhaa bado zilikuwa zimetapakaa damu kutokana na tukio la mauaji wa siku chache zilizopita.

"Ron! Tunafanya nini hapa?" Latisha aliuliza kwa kukereka baada ya kuchoka kushangaa na kudadisi bila kujua hata ni nini ambacho alipaswa kudadisi.

"Siwezi kusema ni nini hasa tunapaswa kuangalia lakini nina hakika kuwa kuna namna fulani ambayo David atakuwa ameacha usia kwa mtoto wake Natalie.! Tunachotakiwa kukifanya ni kuangalia kitu chochote kile ambacho kitawasha taa vichwani mwetu na kutufungulia njia ya kuijua siri ambayo David alikuwa anaifahamu.!"

"Bado sielewi ni kwa nini una uhakika asilimia mia kuwa David atakuwa ameacha ujumbe kwa ajili ya Natalie... OK, vyovyote vile tuendelee na hiki unchokifikiri.!" Latisha aliongea kwa kukereka huku anageuka kuendelea kushangaa shangaa tena.

Hakuwa amekosea, Rodney Van Der Berg alikuwa hasemi ukweli wote. Alichokuwa anakisema kilikuwa ni nusu tu ya ukweli wote anaoujua kuhusu David na kwa nini ana uhakika kuwa kuna ujumbe kwa ajili Natalie. Lakini alikuwa na sababu kwa nini hakutaka kusema ukweli wote. Alikuwa na sababu ya kifedhuli kabisa.

"Natalie baba yako alikuwa mtu 'busy' sana… ni namna gani mlikuwa mnatumia muda wenu pamoja pindi akipata muda mchache wa kuwa nawe?" Ron alimuuliza Natalie ambaye alikuwa busy kushangaa kinyago fulani kwa kuchingwa hapo sebuleni.

"Anh! Mara nyingi tulikuwa tunacheza table tenisi… yeye ndiye aliyenifundisha na kunifanya nipende table tennis mpaka sasa!" Natalie alijibu bila kugeuka akiendelea kushangaa shangaa tu.

"Mlikuwa mnacheza wapi hiyo table tennis?" Ron aliuliza kwa shahuku kubwa safari hii.

"Chini kwenye basement.!" Natalie alijibu tena kawaida tu akiendelea kushangaa shangaa.

Lakini kuna taa iliwaka kichwani kwa Ron.

"Twendeni!" Ron aliongea kwa haraka na kuanza kutembea kwa pupa.

"Wapi?" Natalie akauliza.

"Chini kwenye basement!" Ron aliongea bila kugeuka kwa sauti ya uroho huku tayari akiwa amepiga hatua kadhaa kuelekea kwenye mlango ambao kwa ndani chini ulikuwa na ngazi za kushuka chini kwenye basement.

Natalie, Latisha na mlinzi wa Ron walifuata nyuma nao kwa kasi wakishangaa shahuku hii ya ghafla ya Ron.




Itaendelea…



THE BOLD
 
Back
Top Bottom