THE OTHER HALF
SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE
Previously….
Rais was Marekani Bi. Laura Keith amehuisha Marshall Law nchi nzima baada ya dunia kukumbwa na giza la kabla muda wa mchna na giza kutoonyesha dalili yoyote ya kukoma. Chini ya sheria hii hakuna raia yeye ambaye anaruhusiwa kutoka nje au kuonekana mtaani. Maafisa wa vikosi vya kijeshi vya National Guard wamemwaga mtaani kote.
Hii inakuwa ni bahati mbaya kubwa kwa Bilionea Rodney Van Der Berg ambaye alikuwa nyumbani kwa familia ya Bw. Donald McLaren na mkewe Latisha ili kuomba mtoto wao Natalie awasaidie kumtafuta David Logan ambaye alikuwa ametekwa na watu wasiojulikana.
Lakini kuna gari la jeshi limefika nje ya nyumba ya Familia ya Donald McLaren na maafisa wawili wa National Guard walikuwa wameshuka huku wameshikilia mitutu ya bunduki na kwenda kugonga mlangoni.
EPISODE 38
Scarsdale, New York - Marekani
Mlango wa nyumba ya familia ya Bw. Donald McLaren ulifunguliwa na maafisa wa jeshi kuingia ndani.
"Habari.!" Afisa mmoja alisalimia.
Donald, mkewe Latisha, mtoto wao Natalie, Ron pamoja na walinzi wake, wote walikuwa kama vile hawajaisikia salamu walibakia wamewatumbulia macho tu.
"Gari iko tayari?" Ron aliwauliza wale wanajeshi.
"Iko tayari Mkuu?" Mwanajeshi mmoja akajibu.
"Nisubirini nje nakuja!" Ron aliwajibu kwa kifupi tu.
Wanajeshi wale wawili walitoka nje. Donald na mkewe walibakia wameduwaa wakishangaa ni nini kilikuwa kinaendelea.
"Nahitaji kwenda na Natalie sasa hivi bila kuchelewa!" Ron aligeuka nyuma kuwaangalia Donald na mkewe na kuwaeleza.
"Kwanza naomba utueleze ni nini kinaendelea hapa? Kwa nini hawa wanajeshi wakuletee gari?" Latisha aliongea akiwa na mshangao.
"Donald, Latisha! Sidhani kama ni jambo la kushangaza kwa mtu wa kaliba yangu kuweza kupata 'favour' za namna hii… labda tu niseme kwa ufupi kila kitu kina bei yake duniani… mmeridhika? Naweza kwenda na Natalie sasa?" Ron aliongea huku anatabasamu wa majivuno.
"Siwezi kukukabidhi binti yangu bila mimi mwenyewe kuwepo! Kama unahitaji kwenda na Natalie basi lazima na mimi niwepo" Latisha kaweka msimamo.
"Na siwezi kuacha binti yangu na mke wangu waondoke bila uwepo wangu! Lazima na mimi niwepo!" Donald nae akalipuka ghafla na kuweka msimamo kama wa mkewe.
"Hey, hey, hey! Samahani natamani tungeenda wote hata na ukoo wenu mzima… tatizo ni kwamba nadhani mnajua kuna Marshall Law na hakuna gari ya kiraia inayoruhusiwa barabarani… tumefanikiwa kupata gari moja tu ya kutusafirisha, kwa hiyo kama ni kwenda basi mchague ni nani ambaye ataenda kati yako na mkeo hatuwezi kutosha wote ndani ya gari!"
Hakukuwa na ubishi kwamba kama ni kwenda basi Latisha ndiye ambaye alitakiwa kwenda kwa kuwa yeye ndiye alikuwa mama mzazi na Donald alikiwa baba mlezi tu kwa Natalie.
Baada ya kukumbatiana na kufarijiana, Latisha na mwanaye Natalie wakiongozana na Ron pamoja na mlinzi wake mmoja waliondoka.
Ndani ya gari siti za mbele walikaa wale wanajeshi wawili ambao walikuja na ile gari na siti mbili za nyuma Ron, mlinzi wake, Latisha na Natalie walibanana kwa pamoja.
"Tunaelekea wapi bwana mkubwa?" Mwanajeshi ambaye alikuwa kwenye usukani aliuliza.
"Naval Observatory Circle… nyumbani kwa Makamu wa Rais!" Ron alijibu.
Natasha alitamani kumuuliza Ron kwa nini wanaenda nyumbani kwa mumewe wa zamanai wakati amewaeleza muda mchache uliopita kwamba ametekwa lakini hakuthubutu kuuliza swali lolote ambalo alihisi la siri kubwa mbele ya hawa wanajeshi wa National Guard.
Ilikuwa safari ndefu ya karibia masaa manne na nusu. Mpaka muda ambao walikuwa wanawasili ilikuwa tayari yapata karibia saa nne usiku lakini kutokana na giza lililokuwepo tangu mchana hakukuwa na tofauti yeyote ya muda ambayo ilihitaji kuitilia maanani.
Jengo la nyumba ya Makamu wa Rais lilikuwa limezungushiwa utepe wa njano wa polisi kutokana na tukio la mauaji ya maafisa wa Secret Services mahali hapo siku chache nyuma lakini ajabu ni kwamba kulikuwa na askari wawili tu wa kawaida ambao walikuwa wanalinda. Labda ni kwa sababu ya nchi kuwa kwenye wakati mgumu ndio maana vyombo vya ulinzi haviku havikuona umuhimu wowote wa kutumia rasilimali kubwa kulinda jengo tupu badala ya kulinda mitaani ambako kulikuwa na taharuki.
Wale wanajeshi wawili waliokwenda nao waliwasaidia kuwapitisha kwenye kizuizi cha polisi kwa kuongea na askari wale wawili ambao walikuwa wanalinda mahali hapa na moja kwa moja wakaingia ndani ya eneo hili la Makazi ya Naval Observatory Circle.
"Maagizo yetu yalikuwa kukupeleka mahala unakohitaji tu bwana mkubwa nadhani tumefanya hivyo na itakuwa sahihi tukirejea kwenye jukumu letu huko mitaani.!" Moja ya wale wanajeshi akaongea.
"Nahsukuru sana na amfikishieni Meja Lewis shukrani zangu!" Ron akashukuru na kupena mikono na wale wanajeshi.
Wanajeshi wakakwea kweye gari yao na kuondoka wakiwaacha hapa nje ya jumba la Makamu wa Rais.
"Unawaacha waondoke tukimaliza tunachofanya hapa tunatejea vipi nyumbani?" Latisha akamuiliza Ron.
"Usijali kuhusu hilo...!" Ron alijibu kwa kujiamini huku wakitembea kuufuata mlango wa nyumba.
Kutokana na nyumba kuwa tupu na tukio ambalo lilikuwa limetokea, hakuna mlango wowote ambao ulikuwa umefungwa.
Waliingia ndani kwenye sebule kubwa ya nakshi za fanicha za thamani lakini za enzi za "kikoloni". Japokuwa vitu hapa sebuleni hasa fanicha kuwa za enzi zilizopita lakini uthamani wake wa hali ya juu ulifanya sebule iwe nzuri na ya kuvutia kabisa.
Walitumia kama dakika kumi nzima kushangaa shangaa na kudadisi pale sebuleni. Wote wanne, yaani Ron, mlinzi wake, Latisha na Natalie kila mmoja alitumia muda wake kutazama sebule na kudadisi kadiri ambavyo alikuwa anaweza. Kila moja mara alishika picha Fulani akaiacha, mara ashangae Picha za viongozi wa zamani wa taifa, mara ashangao sanamu za kuchongwa na kufinyanga… ili mradi tu ilikuwa kudadisi japokuwa hata walichokuwa wanakidadisi hawakukijua. Japokuwa hapa ndani kulikuwa kunapendeza lakini bado sehemu kadhaa bado zilikuwa zimetapakaa damu kutokana na tukio la mauaji wa siku chache zilizopita.
"Ron! Tunafanya nini hapa?" Latisha aliuliza kwa kukereka baada ya kuchoka kushangaa na kudadisi bila kujua hata ni nini ambacho alipaswa kudadisi.
"Siwezi kusema ni nini hasa tunapaswa kuangalia lakini nina hakika kuwa kuna namna fulani ambayo David atakuwa ameacha usia kwa mtoto wake Natalie.! Tunachotakiwa kukifanya ni kuangalia kitu chochote kile ambacho kitawasha taa vichwani mwetu na kutufungulia njia ya kuijua siri ambayo David alikuwa anaifahamu.!"
"Bado sielewi ni kwa nini una uhakika asilimia mia kuwa David atakuwa ameacha ujumbe kwa ajili ya Natalie... OK, vyovyote vile tuendelee na hiki unchokifikiri.!" Latisha aliongea kwa kukereka huku anageuka kuendelea kushangaa shangaa tena.
Hakuwa amekosea, Rodney Van Der Berg alikuwa hasemi ukweli wote. Alichokuwa anakisema kilikuwa ni nusu tu ya ukweli wote anaoujua kuhusu David na kwa nini ana uhakika kuwa kuna ujumbe kwa ajili Natalie. Lakini alikuwa na sababu kwa nini hakutaka kusema ukweli wote. Alikuwa na sababu ya kifedhuli kabisa.
"Natalie baba yako alikuwa mtu 'busy' sana… ni namna gani mlikuwa mnatumia muda wenu pamoja pindi akipata muda mchache wa kuwa nawe?" Ron alimuuliza Natalie ambaye alikuwa busy kushangaa kinyago fulani kwa kuchingwa hapo sebuleni.
"Anh! Mara nyingi tulikuwa tunacheza table tenisi… yeye ndiye aliyenifundisha na kunifanya nipende table tennis mpaka sasa!" Natalie alijibu bila kugeuka akiendelea kushangaa shangaa tu.
"Mlikuwa mnacheza wapi hiyo table tennis?" Ron aliuliza kwa shahuku kubwa safari hii.
"Chini kwenye basement.!" Natalie alijibu tena kawaida tu akiendelea kushangaa shangaa.
Lakini kuna taa iliwaka kichwani kwa Ron.
"Twendeni!" Ron aliongea kwa haraka na kuanza kutembea kwa pupa.
"Wapi?" Natalie akauliza.
"Chini kwenye basement!" Ron aliongea bila kugeuka kwa sauti ya uroho huku tayari akiwa amepiga hatua kadhaa kuelekea kwenye mlango ambao kwa ndani chini ulikuwa na ngazi za kushuka chini kwenye basement.
Natalie, Latisha na mlinzi wa Ron walifuata nyuma nao kwa kasi wakishangaa shahuku hii ya ghafla ya Ron.
Itaendelea…
THE BOLD