The Other Half (Simulizi)

The Other Half (Simulizi)

4c7c5accd875f0e8ac5a7d9d13e2c6de.jpg


THE OTHER HALF



SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE




EPISODE 39


"…labda baada ya yote haya tutaishi kuiona siku nyingine, tutaishi kuona tena jua likichomoza. Labda iko siku tutaishi tena kushuhudia ulimwengu ukiamka kutoka jaani.

Kuna mahala tupo. Kila nafsi. Ulimwengu mzima. Kuna mahala tupo na tumekuwa kama gonjwa. Gonjwa ambalo tumedhamiria kulihamisha mpaka sayari nyingine. Labda jina zuri si ugonjwa, bali ni ulevi.

Ulevi ndio laana kubwa zaidi iliyo juu ya dunia. Ulevi wa uharibifu. Kiu ya kuharibu kwa minajili ya kujipambanua kuboresha. Ni ulevi tu.

Ndio maana kila mahala ambako tulipewa msitu, tumerejesha jangwa. Kila mahala ambako kulikuwa na chemi chemi tumepafanya kame, na kila mahala ambako tulipewa utajiri tumepafukarisha kwa kutupwa.

Dunia si sehemu ya kwanza kuwa na uhai. Yawezekana uhai ulikuwepo enzi za kale sayari ya Mirihi au labda Sayari Mshtarii. Pengine hata Zohali palikuwa na uhai. Lakini baada ya miaka elfu elfu uhai ulikoma japo zenyewe sayari bado zingalipo hata sasa. Hazikukubali zenyewe kufutika ili kuendekeza ulevi wa viumbe hai vilivyomo.

Baada ya miaka elfu elfu mingine, Dunia inapita katika mkondo huo. Ardhi inakataa na kupambana kupinga ulevi uliotamalaki hapa kwetu. Ulevi wa uharibifu. Labda mwaka huu au labda mwakani. Lakini ni dhahiri kwamba Dunia nzima ikiisha kufanywa Anabelle uhai utakoma. Na Dunia itabaki pweke kama Sayari Utaridi ama Zuhura.

Kifo ndicho kinakipa thamani Uhai. Kutokuwa nacho ndiko kunatoa thamani ya kuwa nacho.
Kabla ya kupatwa ni lazima kupotea.

Labda baada ya miaka mia au labda miaka elfu. Labda iko siku tutaishi tena. Labda iko siku uhai utarejea tena.

Kama ilivyotokea Sayari ya Utaridi, Zuhura, Mirihi na Zohali miaka elfu elfu iliyopita ndicho hicho kinapaswa kutokea duniani. Ni lazima ulimwengu wote utwaliwe na kugeuzwa Annabelle…"



MARYLAND, MAREKANI

Mzee Caleb alikuwa ameshikilia kifua na anahema kwa nguvu haswa. Hata wale vijana makomando ambao walikuwa naye walikuwa wameanza kupata wasiwasi kama Mzee Caleb atakuwa nao akiwa hai kwa muda mchache ujao.

"Mzee bado unajisikia vibaya? Simuoni yule mtu?" Walker aliongea huku anamshikilia sawia Mzee Caleb pale alipo kwenye gari.

Yule binadamu wa ajabu, kiumbe ambaye Mzee Caleb aliwaeleza kwamba ana nusu ya nafsi yake alikuwa haonekani tena katika upeo wa macho yao. Walikuwa wamefika pahala ambako ndiko kulikuwa kubatumia kama njia ya kuingilia msituni. Kwa muda wote tangu watoke nyumbani kwa Mzee Caleb mtu huyo alikuwa anakimbia kwa kasi sawa sawa na magari walivyokuwa wakiyaendesha. Lakini ajabu kwamba walipofika hapa kwenye eneo la kuingia msituni hawakumuona tena.

Lakini Mzee Caleb bado alikuwa anasikia maumivu kifuani kwake kuashiria kwamba bado mtu huyo alikuwa karibu yao.

"Ni…mtego!" Mzee Caleb aliongea kwa taabu sana.

"Mtego gani?" Walker akamuuliza.

"Hataki tumuone kwa makusudi lakini bado yuko hapa hapa ndio maana najisikia hivi… nadhani anatala tuingie ndani ya msitu ili atumalize huko huko!"

"Kwa hiyo tunafanyaje?" Walker aliuliza kwa mshangao na woga.

"Kama nilivyosema, 'backwards is the only way forward!' Lazima tuingie tena ndani ya msitu!" Mzee Caleb akamjibu.

Hakukuwa na muda wa mjadala au mabishano tena. Walikuwa wamebakiwa sasa na kama saa moja pekee kabla ya mji wa Maryland kutwaliwa. Kwa hiyo kama kuingia ndani ya msitu ndilo lilikuwa tumaini pekee la kubakia hai basi hakukuwa na muda wa kujadili.
[03/02, 16:00] Nifah: Baada ya wote kwenye magari matatu kupeana ishara fulani wakashuka kwa pamoja. Kama ambavyo walitoka kule nyumbani kwa Mzee Caleb ndivyo ambavyo pia waliingia ndani ya msitu.

Makomando wanne walibeba tundu lenye yule mnyama wa ajabu. Walker alimbeba Mzee Caleb mikononi kama vile amebeba kitoto kichanga. Na makomando wawili waliobakia mmoja alitangulia mbele na mwingine nyuma kuhakikisha kuwa wako salama. Lakini pia hawakusahau ile mifupa ya familia ya Mzee Caleb. Mfuko mmoja wa plastiki uliojaa mifupa na chupa mbili zilizojaa unga wa mafuvu ya kichwa.

Taratibu na kwa umakini mkubwa wakaanza kuingia ndani ya msitu wa Ox. Walifuata njia ile ile ambayo walikuja nayo mara ya kwanza wakiwa na Naomi na Ethan.

Kila ambavyo walikuwa wanatembea baada ya kila dakika kadhaa, pembezoni mwao mwa njia waliyokuwa wanapita, mbali kidogo kwenye miti iliyoshonana walikuwa wakiona kama kivuli cha mtu kinapita kwa kasi na kisha kupotea. Yule kiumbe wa ajabu, binadamu mwenye nusu ya nafsi ya Mzee Caleb.

Kila ambavyo kivuli hicho kilipokuwa kikipita kwa kasi na wao kuongeza umakini wao maradufu wakidhani kwamba labda huo ndio ulikuwa wakati ambao kiumbe huyo atawavamia lakini ajabu ni kwamba hakufanya hivyo. Alipita kwa kasi kama kivuli kwenye miti miti na kisha kupotea. Baada ya dakika kadhaa anapita tena na kupotea. Vivyo hivyo.

"Wa…lker..!" Mzee Caleb alinong'ona kwa taabu akiwa amebebwa mikononi mwa Walker kama katoto kadogo.

Walker hakujibu chochote, aliinamisha tu sikio lake na kumsikiliza. Muda huu walikuwa wameacha kutembea taratibu. Walikuwa wanatembea kwa kasi karibia na kukimbia. Ulikuwa umebaki muda mchache sana, kama dakika arobaini tu kabla ya mji wa Maryland kutwaliwa.

"Unajua huyo kiumbe anachokifanya?" Mzee Caleb alijikaza na kuuliza kwa kutamka sentensi sawia.

Walker akatibgisha kichwa kuashiria kuwa hakujua ni nini kiumbe huyo anakifanya.

"Anataka kututumia tumuongoze mpaka tunapoenda kisha ndio atimize azma yake!"

Japokuwa Walker alishituka ndani ya nafsi lakini alijitahidi asionyeshe mshituko wake wazi wazi. Aliendelea kutembea haraka huku amembeba Mzee Caleb mikononi.

"Naomba chupa yenye unga wa mifupa ya fuvu la kichwa na damu iliyobakia"

Bila kuongea chochote kile Walker alimgeukia mwenzake aliye nyuma yao akiwapa ulinzi na kumuamuru kumpa chupa yenye unga wa mifupa na kifuko cha plastiki kilichosalia damu ambayo waliitoa walipokuwa nyumbani kwa Mzee Caleb.
Walker akachukua vyote viwili, chupa ya unga na kifuko cha damu na kumkabidhi Mzee Caleb.

Safari iliendelea. Muda huu walijongea kama wanakimbia kabisa, nusu saa tu ilikuwa mbele yao kabla ya Maryland kutwaliwa na kuwa Anabelle.

Baada ya kukimbia kwa takribani dakika tano nyingine hatimaye walitokea pale walipokuwa wanaenda. Mahala ambako kulikuwa na kaburi la babu yake Caleb.

Siku tatu zilizopita walipofika mahala hapa kwa lengo la kutafuta Book Of Codes walikuwa kaburi limefukuliwa na mifupa ya zaidi ya binadamu mmoja imetapakaa lakini kitabu hakipo na waling'amua kuwa kikundi cha waoiganaji wa 'Sacta Cedes' walikuwa wamewawahi na kuchukua kitabu. Lakini leo hii walipofika ajabu ni kwamba walikuta lile kaburi limefukiwa na hakukuwa na mfupa wowote ule uliozagaa juu ya ardhi.

Wakiwa wanashangaa hiki walichokikuta hapa, ghafla walihisi kuna kitu kimesimama mbele yao kwenye vichaka, pembeni ya kaburi kwenye miti iliyosongana. Kivuli cha mtu.
Alikuwa ni kiumbe yule mwenye nusu ya nafsi ya Mzee Caleb ambaye alikuwa anawafuatilia tangu watoke nyumbani kwake. Kama ambavyo mzee Caleb alikuwa amehisi, kiumbe huyu kabla hajawadhuru alikuwa anataka ajue akina Caleb walikuwa wanaelekea wapi na labda kwa nini. Na hatimaye alijua… mahala hapa! Kaburini kwa babu yake Caleb. Na alijua fika kwa nini walikuwa wekimbilia hapa.

Binadamu yule wa ajabu taratibu akaanza kitoka kwenye miti na vichaka, kule ambako kulikuwa kunamfanya aonekane kama kivuli gizani. Alitoka nankupiga hatua za taratibu kuelekea pale Kaburini ambako Mzee Caleb na wenzake walikuwa wamesimama.

Walker na makomando wenzake wakainua bunduki zao.

"Msipige risasi.!" Mzee Caleb aliongea kwa taratibu.

Yule kiumbe akazidi kusogea karibu zaidi. Nguo zake nyeusi tii kama kaniki zilizomfunika kuanzia unyayo wa mguu hadi kichwani zilimfanya hata uso wake uonekane kwa shiida sana. Lakini kadiri ambavyo alikuwa anawasogelea ndivyo ambavyo Mzee Caleb, Walker na wenzake walizidi kumuona uso wake wa dhahiri.

Alipiga hatua za taratibu mpaka kufika pale Kaburini na kusimama umbali wa kama tano tu kutoka pale ambapo Caleb na wenzake walikuwa wamesimama. Alipofikia umbali huu ndipo ambapo waliweza kumuona sawia usoni.

Alikuwa na sura sawa sawa kabisa na sura ya Mzee Caleb. Walikuwa wanafanana kabisa kama mapacha. Pia naye alikuwa na sura ya kizee kama Caleb lakini mwili wake ukionekana mkakamavu na wenye nguvu kushinda hata wale makomando ambao alikuwa nao Mzee Caleb. Lakini licha ya kufanana huku, ngozi ya kiumbe huyu usoni alikuwa na mabaka kama mabaka ya chatu au kenge. Pia macho yake yalikuwa ya rangi ya kahawaia iliyofifia sana na mboni nyekundu ambazo rangi yale ilikolea kufanya kuwa kama mwali wa moto. Mwili mzima ulikuwa umefunikwa na manguo hayo myeusi. Ni uso pekee ndio ambao alikuwa anaonekana.

"Hello Caleb.! Nimeisubiria siku ya leo kwa muda wa zaidi ya miaka arobaini.!" Aliongea binadamu huyu wa ajabu kwa sauti nzito ya kukwaruza sana. Aliongea huku anatabasamu kifedhuli na meno yake marefu yaliyochongoka haswa kuchungulia nje.


Itaendelea…



Habibu B. Anga 'The Bold' - 0718 096 811
To Infinity and Beyond

Pls: WhatsApp, Follow and Subscribe
 
Back
Top Bottom