Kuna tetesi kuwa zile 115 charges dhidi yenu zinaelekea kufika mahala pabaya kwenu na huenda niyo sababu Pep kakimbia ligi mwaka mmoja mapema kabla ya mkataba wake kuisha.
Mnaweza kukatwa points 60 msimu ujao, kuzuiwa kushiriki transfers kwa miaka miwili, labda na faini kali juu.
Hii inamaana mtakuwa mnapambana kubaki ligi kuu maana kuwa kuanza na -60 maana yake ni hata mkishinda mechi zenu zote mnaweza kupata points 54 tu. Mkifungwa na kutoa sare kadhaa mnaweza kumaliza na chini ya points 40, kitu ambacho kitawaweka hatarini kushuka daraja.