Tupo mkuuMpo?
Mnaionaje team yenu ya msimu huuTupo mkuu
Mkuu,Mnaionaje team yenu ya msimu huu
Unasema???? Ongeza sautiMmejikausha kama hakuna kinachoendelea
View attachment 3655654
Wachambuzi wa Bongo bana dah.....kinachowakost man city ni sajili mbovo, Huwezi kutoka kwenye KDB, Bernando, Mahrez, Gundogan halafu ukaishia kwa Anderson, forden, Doku, semenyo Dah inasikitisha sana
Pep sio mchezajiNyie watu kaondoka Pep ubingwa hampati tena hadi 2050
Wachambuzi wa Bongo bana dah.....
Mzee umeanza kuchambua matokeo kabla mpira haujachezwa. Jana unasema Anderson, Semenyo na wengine ni sajili mbovu, wakati Man City leo ndiyo wanaanza ligi. Hata hawajapewa muda wa kuonyesha uwezo wao. Uchambuzi wa mpira sio kutaja majina ya KDB, Bernardo, Mahrez na Gündogan halafu moja kwa moja ukahukumu vizazi vipya. Subiri wacheze kwanza ndio tupime usajili.
Hapo ndipo sikubaliani na wewe. Ukisema anguko la City lilianza misimu mitatu iliyopita,hao jamaa wengi wao hawajaja leo, anguko la City limeanza misimu miatatu iliopita, na sababu kuu ni replacement za wachezaji waliopo mwanzo zinashindwa kuwa na standard kama za watangulizi wao.
Hapo ndipo sikubaliani na wewe. Ukisema anguko la City lilianza misimu mitatu iliyopita,
2022/23
City ilishinda UEFA Champions League kwa mara ya kwanza, Premier League na FA Cup — TREBLE.
2023/24.
City ilishinda Premier League kwa mara ya 4 mfululizo na points 91. Gündogan na Mahrez walikuwa tayari wameondoka, lakini City bado wakachukua title.
David Silva alipoondoka tuliambiwa pia City itashuka kwa sababu hakuna atakayefikia standard yake. Lakini De Bruyne akaendelea kuwa engine ya creativity ya City. Na De Bruyne hakuhitaji kuwa David Silva mwingine ili City iendelee kushinda.
Vivyo hivyo Fernandinho alipoondoka, Rodri ndiye aliyekuja kuchukua nafasi yake. Lakini Rodri hakuhitaji kuwa Fernandinho mwingine, alikuja na style yake mwenyewe, akawa mmoja wa viungo bora duniani na akashinda Ballon d’Or. Na Rodri ndiye aliyefunga goli la ushindi kwenye Champions League final ya 2023, akasaidia City kukamilisha Treble.