Kingine jamani siziwezi kurupushani, mara sijui kwenda kariakoo kukurupua nini, naweza kusema naenda kariakoo nikifika natafuta sehemu nakunywa zangu juice narudi nyumbani, au sijui daladala jamani naweza jikuta sina hela lakini nachukua tax hata elfu 40 ili mradi tu niwe nimerelax, kwanza nikienda kwenye mziki au bar yani nahisi nachanganyikiwa na ile miziki, kwanza maeneo kama hayo labda niwe na mpenzi wangu tena awe ni mtu anayejielewa (napenda mtu ambae amenizidi sana xoz i feel more secured) ambae tunaweza kuongea mambo ya msingi sio yule anaamka na bia mkononi anaenda kwa stage kucheza, maana naweza kupata hasira nikupige hata kwenzi, kingine jamani nikimpenda mtu naweza hata kufa maana siwezi kucheat siwezi kufanya nini, yani napenda from head to toe, nazama mzima mzima, halafu sasa nakuwa nauwezo wa kugundua kama huyu mtu labda leo hayupo katika mazingira mazuri au anacheat na nikipiga simu tu nagundua au kuna maswali ambayo naweza kumuuliza anajiuma uma baadae anajikuta amesema tu ukweli, kingine ninakuwa na hasira za haraka lakini zinawahi kuisha, mfano hata ni mdogo wangu kaniudhi naweza hata nikampiga hapo hapo halafu nikisharudi kukaa mwenyewe nikirewind najikuta namuomba msamaha, kingine sipendi kabisa kukaa na hasira/ kitu chochote moyoni yani siwezi mpaka ni-solve siku nyingine mpaka nashindwa kwenda kazini najikuta naomba ruhusa kama naumwa maana siwezi kufanya chochote mpaka sura inabadilika, mpaka nitafute suluhu kwanza, halafu kuna watu wanakwambia eti ukiwa na stress uende unywe pombe, for sure i cant, mimi nikiwa na stress naweza kujifungia ndani hata siku mbili sitaki kelele yetote, naweza jikuta the whole week sijawasha tv na redio mpaka kifurushi cha dstv kilishaisha wala sikujua, in short thats how I am
