Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Mahmoud Thabit Kombo, amekanusha madai ya matumizi ya nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji wanaopinga zoezi la Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29.
Akizungumza na kituo cha televisheni cha Al-Jazeera siku ya Ijumaa, Waziri Kombo amesema hadi sasa hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa vikosi vya usalama vimetumia nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji hao.
Aidha, alibainisha kuwa serikali haina takwimu rasmi kuhusu idadi ya waliopoteza maisha.