Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,152
- 128,807
Wanabodi.
Kumbukumbu ni moja ya vitu ambavyo binadamu anaishi navyo milele hadi kufa navyo!. Ubongo ni kama computer hard disc, na uwezo wa kuhifadhi ni kama computer memory, kadri unavyohifadhi memory nyingi, ndivyo unavyoongeza space ya hard disc yako, wengine ni KB, wengine, MB, wengine ni GB na hata TB, jee wewe unaweza kujijua uko kundi gani?.
Naomba ujikumbushe the earliest thing kilichokutokea udogoni, mpaka leo unakikumbuka, ulipokuja kuhadithiwa ulikuwa na umri gani wakati huo unaweza kushangaa!.
Mimi wakati nikiwa mdogo kabisa, nikiwa naishi Arusha, mbio za mwenge zilipita nje kwetu!. By that time nilikuwa urefu wa buti ya jeshi, kwa sababu hapo barabarani nilipo simama, buti ilikuwa ndio usawa wa macho yangu!. Tukaja kuhama Arusha na kuhamia Tanga, nikiwa mkubwa naonyeshwa picha zangu tukiwa Arusha, naambia tulihama nikiwa 3 years, na wakati tunahama, mwenge ulikuwa haujapita, hivyo nilipoziona mbio za mwenge I was two years na mpaka leo nakumbuka!.
Nilianza Nursery shule ya St. Peters Kindergarten ya Tanga nikiwa 4 years. Mpaka leo, more than 30 years back, nakumbuka baadhi ya majina ya wanafunzi wa darasani kwangu na miongoni mwao ni Alex Shaba, David Naburi, Allen Semu, Irene Minja, Jane Mutayoba, Robert Kilala na Ana Kilala!. Jee wewe unaweza kuwakumbuka baadhi ya wanafunzi mliosoma nao vidudu?.
Nikiwa nursery ndio mara yangu ya kwanza kuvaa shati jeupe, suruali nyeusi, soksi nyeupe na viatu vyeusi!, kabla ya hapo ni raba na ndala tuu. Nilinunuliwa nguo hizi ili kucheza mchezo wa kuigiza mimi nikiwa ndio mfalme!.
Kitu cha ajabu, nimemaliza Chuo juzi juzi, kuna watu nakutana nao mtaani tunasalimiana vizuri, namuomba anikumbushe, ananiambia tulikuwa class moja Chuo!. Yaani wale wazamani ninawakumbuka, hawa wa sasa siwakumbuki!. Nilipojiuliza nikakuta hard dis itakuwa imejaa hivyo it can take no more!. Huyo Robert Kilala na Jene Kilala, baba yao alikuwa ana pikipiki, anawaleta wote wawili wamepakizwa mbele kwenye pikipiki, hivyo nikawa naishangalia sana pikipiki nikitamani na mimi kupandishwa!. Watoto wengine wakiletwa na magari, mimi kwetu hatukuwa na gari, napelekwa shule na dada akiitwa Marrita (Martha), sometimes nikifika shule, siingii kwanza darasani ili kuona pikipiki, kumbe siku ingine wanakuwa wamewahi zaidi na mimi nikiwakuta, I feel sorry, I've missed the fun!. Baadae nilipokuja kuwa mtu mzima I was mad about bikes!.
Jee wewe unakumbuka nini enzi za udogoni kabisa?!.
Remembering those good old days, makes you feel good!.
Feel Good!.
Pasco
Kumbukumbu ni moja ya vitu ambavyo binadamu anaishi navyo milele hadi kufa navyo!. Ubongo ni kama computer hard disc, na uwezo wa kuhifadhi ni kama computer memory, kadri unavyohifadhi memory nyingi, ndivyo unavyoongeza space ya hard disc yako, wengine ni KB, wengine, MB, wengine ni GB na hata TB, jee wewe unaweza kujijua uko kundi gani?.
Naomba ujikumbushe the earliest thing kilichokutokea udogoni, mpaka leo unakikumbuka, ulipokuja kuhadithiwa ulikuwa na umri gani wakati huo unaweza kushangaa!.
Mimi wakati nikiwa mdogo kabisa, nikiwa naishi Arusha, mbio za mwenge zilipita nje kwetu!. By that time nilikuwa urefu wa buti ya jeshi, kwa sababu hapo barabarani nilipo simama, buti ilikuwa ndio usawa wa macho yangu!. Tukaja kuhama Arusha na kuhamia Tanga, nikiwa mkubwa naonyeshwa picha zangu tukiwa Arusha, naambia tulihama nikiwa 3 years, na wakati tunahama, mwenge ulikuwa haujapita, hivyo nilipoziona mbio za mwenge I was two years na mpaka leo nakumbuka!.
Nilianza Nursery shule ya St. Peters Kindergarten ya Tanga nikiwa 4 years. Mpaka leo, more than 30 years back, nakumbuka baadhi ya majina ya wanafunzi wa darasani kwangu na miongoni mwao ni Alex Shaba, David Naburi, Allen Semu, Irene Minja, Jane Mutayoba, Robert Kilala na Ana Kilala!. Jee wewe unaweza kuwakumbuka baadhi ya wanafunzi mliosoma nao vidudu?.
Nikiwa nursery ndio mara yangu ya kwanza kuvaa shati jeupe, suruali nyeusi, soksi nyeupe na viatu vyeusi!, kabla ya hapo ni raba na ndala tuu. Nilinunuliwa nguo hizi ili kucheza mchezo wa kuigiza mimi nikiwa ndio mfalme!.
Kitu cha ajabu, nimemaliza Chuo juzi juzi, kuna watu nakutana nao mtaani tunasalimiana vizuri, namuomba anikumbushe, ananiambia tulikuwa class moja Chuo!. Yaani wale wazamani ninawakumbuka, hawa wa sasa siwakumbuki!. Nilipojiuliza nikakuta hard dis itakuwa imejaa hivyo it can take no more!. Huyo Robert Kilala na Jene Kilala, baba yao alikuwa ana pikipiki, anawaleta wote wawili wamepakizwa mbele kwenye pikipiki, hivyo nikawa naishangalia sana pikipiki nikitamani na mimi kupandishwa!. Watoto wengine wakiletwa na magari, mimi kwetu hatukuwa na gari, napelekwa shule na dada akiitwa Marrita (Martha), sometimes nikifika shule, siingii kwanza darasani ili kuona pikipiki, kumbe siku ingine wanakuwa wamewahi zaidi na mimi nikiwakuta, I feel sorry, I've missed the fun!. Baadae nilipokuja kuwa mtu mzima I was mad about bikes!.
Jee wewe unakumbuka nini enzi za udogoni kabisa?!.
Remembering those good old days, makes you feel good!.
Feel Good!.
Pasco