Tenda ya Bomba la gesi ya Mtwara

Tenda ya Bomba la gesi ya Mtwara

mkuu asante kwa kuleta hii hoja. Kuna bandiko hapa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu juu ya mpango wa 2010 wa ujenzi wa hili bomba. Umeeleza vizuri sana na gharama halisi lakini katika vitu ambavyo wahenge walitufundisha ni kuwa "ukitaka kusema uongo basi kuwa na kumbukumbu". Serikali hii hii imesahau iliyoyasema na kufanya wizi wa mchana. Wengi wanasema na hili litapita lakini wasisahau kuwa suala la Richmond lilikuwa rahisi hata zaidi ya hili na halikupita japo DOWANS wananyemelea $$$$$$ zao pale hazina!
 
Naomba kutumia model ya ile Tenda ya Bandari

1. Ilitangazwa lini-Hikutangazwa

2. Consultant alikuwa nani?-CCCC

3. Estimates zake zinasemaje? zilianza Dola milioni 360 cha juu cha nanii na nanii ikafika 460-560 hadi 660

4. Tenda ilitangazwa na idara zipi za serikali?-Haikutangazwa

5. Kampuni ngapi ziliomba hiyo tenda?-moja CCCC

6. Majina ha hizo kampuni zilizoomba yako wapi?-CCCC

7. Evaluation team ya hiyo tender ilihusisha akina nani? -Wataalamu walipekwa China na CCCC

8. Pre qualification stage zilipita kampuni ngapi?-1 CCCC

9. Zilizoshindwa zilitolea kwa vigezo vipi? Hazikuwepo

10 .Technical specs za huu mradi ni zipi?-ziliandaliwa na CCCC

11. Financial specs za huu mradi mbona siri kubwa?-Ziliandaliwa na CCCC

12. Je kampuni ngapi za wana Mtwara zilihusishwa hata kwenye sub contracting?

13. jE mtwara development agency WALIHUSISHWAJE KWENYE HUU MPANGO?

14. hIZI TUHUMA ZA WATU KULA PESA cHINA NI KWELI? - ni uwongo!.

Hili la bandari CCCC ndio waliofanya feasibility study kwa ghara yao wenyewe!
CCCC wakatafuta funder Exim Bank
CCCC wakawa ndio wajenzi
CCCC wakaomba goverment guarantee wakapata!.
CCCC ndio wangerun mpaka utakapolipwa!.

Waziri Nundu akasmell a fish, akasimamisha kila kitu, wakamruka waziri, wakamtumia naibu waziri, government guarantee ikatoka bila kuombwa na waziri husika!. Waziri Nundu akamwaga ugali, JK akawatema wote, Mwakiembe ndie akamalizia kusafisha bandari.

Sasa ni zamu ya TPDC.
Pasco.

Thanks Bro,kumbe wakati mwingine unawaza vizuri,heshima inaanza kurudi taratibu
 
Wazushi ni wengi sana humu jamvini

Heshima yako mkuu, sisi tumekwisha timiza wajibu wetu kama wazalendo, uzuri Watanzania wengi ni wepesi ku-grasp mambo wakielimishwa vizuri, watakaa chini wa-digest tahadhali zote tulizo hanika humu. At the end of the DAY watapata picha kamili ni kitu gani kinajili behind the scene. God bless U mkuu.
 
Splendid indeed MKuu, hapo umenena - kama kuna Waswahili wanataka kufanya ujanja hapa na pale basi wachukuliwe hatua, lakini tusilahumu Wachina wholesale, bei za mabomba yenye diameter tofauti inajulikana, gharama za kutandaza bomba kwa kilometer moja inajulikana na hii inategemea mabomba yatapitishwa kwenye geographical formation ya aina gani, bei za pump na pump house za kusukumia gezi zinajulikana, gharama za usafirishaji wa mabomba kwa njia ya majini kutoka Uchina kuja hapa kwetu zinajulikana, logistic ya kusafirisha mabomba mpaka kwenye site zinajulikana, mtu ukiwa na information hii ni rahisi kuwakamata wajanja sasa tatizo liko wapi. Eti wachina wanaonga ili wapate miradi, watu wa magaharibi ni wa ajabu sana - Serikali ya Tanzania ndio ilikwenda kuomba mkopo kutoka kwa Wachina, sio mkopo tu walipewa na jukumu la kutekeleza project nzima mpaka mwisho, what's wrong with that if I may ask? Juzi Juzi hapa nilimsikia Waziri Mkuu wa Uchina Tigen-Ping akiseama wazi wazi kwamba kiongozi yeyote akikamatwa anakula rushwa anatwangwa risasi, na Wachina hawana utani katika hilo.

Mkuu I can't disagree with you kwenye dunia ya leo ni vigumu kuibiwa bila kujijua ni Chief Mangungo tu na wenzake wa enzi hizo ndo waliibiwa hivyo otherwise kila wizi unaofanyika humu nchini lazima ufanywe kwa ridhaa ya viongozi wetu wasiokua na uzalendo hapo wanaotuibia sio wachina bali ni viongozi wetu na ndio maana ukiongelea swala la huu mradi wanakua wakali kama simba kwa mradi wa Pakistan kwa mfano utaona tofauti kubwa sana ya bei kule bei ni wastani wa 1.2M usd per mile na bomba lao ni la kipenyo kikubwa na linapitia kwenye maeneo magumu kijiografria wakati sisi huku linapita mchangani tu na ni almost 3M usd per mile huu ni wizi wa wazi kabisa na unaweza kuta wachina walitoa genuine estimates lakini wakubwa hapa wakaweka cha juu kama kwenye mradi wa upanuzi wa bandari
 
Mkuu sisi ndio tulikwenda wenyewe kuomba msaada CHINA tukawalilia hali, wakakubali kutoa mkopo kwa riba nafuu na grace periond nzuri - vile vile wenyewe ndio watafanya kila kitu sisi tunakabidhiwa mradi uliyo kamilika - Serikali ya Uchina haiwezi kuleta watu wababaishaji kwenye miradi inayo husu Serikali kwa Serikali, wanajuwa vizuri Kampuni zipi huko Uchina za kutekeleza mradi kama huu wa kutandaza bomba na pump za kusukuma gesi.


Mbona watu wanawasakama Wachina sana, mbona tumewahi kushuhudia miradi ya ujenzi wa barabara unofadhiliwa na Wajapani lakini Wajapani wanaleta makampuni yao kujenga barabara mfano: Kajima na Konoike bila ya kutangaza tenda, si hilo tu hapo zamani Wajapani waliwahi kutoa fedha za kununulia mchele kwa mashariti kwamba ununuliwe Ujapan kwenyewe hili ni jambo la kawaida tu - why pick on CHINESE!!


Haya tuje kwa mradi wa kujenga Hydro Electric mto Rufiji/Stigler Gorge - Wabrazil watatoa pesa zao, Macontractors wao katika utekelezaji wa mradi huo, Brazil haiwezi kukubali kutoa fedha alafu sisi tujifanye kutafuta Ma-contractos kutoka nchi nyingine, mambo mengine hatuna jinsi mkuu.


Mwisho labda niseme kwamba kuna mradi wa kutandaza mabomba ya gesi huko Pakstani kama sikosei, wahusika wa mradi huu ni Wachina nafikili urefu wake hauna tofauti na huu wa kwetu, gharama za ujenzi na kila kitu hazizidiani na mradi wa hapa kwetu na kumbuka Pakstani hiko karibu na Uchina kijografia kuliko sisi - kuna baadhi ya watu wanafikili Wachina wamejipanga kutuibia?


Nyinyi ndiyo mmevunja utaratibu ambao ungetoa hayo majibu. Kwa hiyo unathibitisha mradi huu ni wa mfukoni ndiyo maana ni siri, ndiyo maana kuna maswali yasiyo na majibu. Nchi hii chini ya utawala wa CCM ni hovyo kabisa.
 
Mkuu sisi ndio tulikwenda wenyewe kuomba msaada CHINA tukawalilia hali, wakakubali kutoa mkopo kwa riba nafuu na grace periond nzuri - vile vile wenyewe ndio watafanya kila kitu sisi tunakabidhiwa mradi uliyo kamilika - Serikali ya Uchina haiwezi kuleta watu wababaishaji kwenye miradi inayo husu Serikali kwa Serikali, wanajuwa vizuri Kampuni zipi huko Uchina za kutekeleza mradi kama huu wa kutandaza bomba na pump za kusukuma gesi.


Mbona watu wanawasakama Wachina sana, mbona tumewahi kushuhudia miradi ya ujenzi wa barabara unofadhiliwa na Wajapani lakini Wajapani wanaleta makampuni yao kujenga barabara mfano: Kajima na Konoike bila ya kutangaza tenda, si hilo tu hapo zamani Wajapani waliwahi kutoa fedha za kununulia mchele kwa mashariti kwamba ununuliwe Ujapan kwenyewe hili ni jambo la kawaida tu - why pick on CHINESE!!


Haya tuje kwa mradi wa kujenga Hydro Electric mto Rufiji/Stigler Gorge - Wabrazil watatoa pesa zao, Macontractors wao katika utekelezaji wa mradi huo, Brazil haiwezi kukubali kutoa fedha alafu sisi tujifanye kutafuta Ma-contractos kutoka nchi nyingine, mambo mengine hatuna jinsi mkuu.


Mwisho labda niseme kwamba kuna mradi wa kutandaza mabomba ya gesi huko Pakstani kama sikosei, wahusika wa mradi huu ni Wachina nafikili urefu wake hauna tofauti na huu wa kwetu, gharama za ujenzi na kila kitu hazizidiani na mradi wa hapa kwetu na kumbuka Pakstani hiko karibu na Uchina kijografia kuliko sisi - kuna baadhi ya watu wanafikili Wachina wamejipanga kutuibia?

miKATABA YA PAKISTANI haiwezi kuwa sawa na yetu inayo fichwa kana kwmba imeandikwa kwenye nyeti za mkuu fulani,na Pakistani itakuwa bomba linakotoka wanachi pale wana mrahaba wao wa kuwanufaisha na si POROJO kama za kina MUHOGO,laa yawezekana nao wamefanya ujinga pia lakini hayo ni yao na ujinga ni wao kama wamefanya hivyo sisi lazima tuangalie maslahi ya wahusika.
 
Naomba kutumia model ya ile Tenda ya Bandari
Sasa ni zamu ya TPDC.

Pasco.

Ahsante kwa majibu ya Ukweli

Nina imani Pasco utanijibu swali langu moja tu.

Baada ya hayo yote kujibiwa kama ulivyojibu Je TAKUKURU hawana uwezo wa kuhoji ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi kama kama huu ulivyofanywa?
 
Heshima yako mkuu, sisi tumekwisha timiza wajibu wetu kama wazalendo, uzuri Watanzania wengi ni wepesi ku-grasp mambo wakielimishwa vizuri, watakaa chini wa-digest tahadhali zote tulizo hanika humu. At the end of the DAY watapata picha kamili ni kitu gani kinajili behind the scene. God bless U mkuu.

Amen Mkuu
 
mkuu sasa naona unafika mbali, yaani unaanza kuingilia 10% za watu eeee. haya mzee endelea...
 
Mkuu I can't disagree with you kwenye dunia ya leo ni vigumu kuibiwa bila kujijua ni Chief Mangungo tu na wenzake wa enzi hizo ndo waliibiwa hivyo otherwise kila wizi unaofanyika humu nchini lazima ufanywe kwa ridhaa ya viongozi wetu wasiokua na uzalendo hapo wanaotuibia sio wachina bali ni viongozi wetu na ndio maana ukiongelea swala la huu mradi wanakua wakali kama simba kwa mradi wa Pakistan kwa mfano utaona tofauti kubwa sana ya bei kule bei ni wastani wa 1.2M usd per mile na bomba lao ni la kipenyo kikubwa na linapitia kwenye maeneo magumu kijiografria wakati sisi huku linapita mchangani tu na ni almost 3M usd per mile huu ni wizi wa wazi kabisa na unaweza kuta wachina walitoa genuine estimates lakini wakubwa hapa wakaweka cha juu kama kwenye mradi wa upanuzi wa bandari


Mkuu najua waswahili ndio walio bobea katika nyanja za ku-doctor figures na kuongeza vitu chungu mzima vya uongo na kweli katika miradi ya kitaifa. Wachina wakishugulikia mradi huu wa GESI basi kwetu hiyo itakuwa a golden chance ya kuwakamata with their pants down culprits wote walio kubuhu katika mchezo huu wa ufisadi na wizi wa mchana; kama kutakuwepo ushahidi wa kweli wa ufujaji wa fedha zilizo tolewa na Serikali ya Kichina kusaidia ujenzi wa mabomba ya gesi - nakwambia nchi haitakalika.


Kwa nini nasema hivyo:
(a) Wachina hawana utani na wala RUSHWA kama wakipata taarifa ya kuaminika kuhusu wizi watachukua hatua mara moja bila ya kujali cheo/ushikaji na undugu, watapokea kwa mikono miwili taarifa yoyote bila ya kujali mtoa taarifa anatoka Serikalini au ni raia wa kawaida kutoka Taifa lolote lenye miradi inayo gharimiwa na Wachina.


(b) Wachina wanagharimia mradi wote kwa pesa yao waliotoa kama mkopo, hivyo hawawezi kuvumilia watu wajanja kutafuna hela zao bila ya kujali kama wezi ni Waswahili wa hapa hapa au Wachina wenzao.


(c) Kama ubadhilifu wa funds za mradi wa Kichina ukiwa proven - basi wahusika wa pande zote watatiwa mbaroni, upande wa China watapigwa risasi kwa upande wa Tanzania Serikali yetu italazimishwa kuwachukulia hatua kali na kutangaza majina ya wahisika adhalani, Wachina hawawezi ku-treat kwa SIRI swala la ufisadi/wizi wa funds zao.


Sasa nini cha kufanya: Tuwaache Wachina watujengee mradi huu muhimu Kitaifa mpaka mwisho, wakisha maliza na kwa bahati nzuri wametupa a long grace period kabla ya kuhanza kurudisha mkopo wao, basi muda huo utatupatia nafasi ya kuwahoji Wachina waeleze kwa nini gharama za mradi unaofanana na hule wa Paskistani lakini kwetu unaonekana gharama zimekuwa kubwa wakati kipenyo cha bomba ni kidogo ukilinganisha na bomba zilizo pelekwa Pakistan, gharama za kutandaza bomba per kilometer kwetu zinaonekana zimezidi wakati geological formation ya Pakistani na Pwani ya Tanzania kuna tofauti kubwa kwa hiyo kwa akili za kawaida gharama za utandikaji wa mabomba unatakiwa huwe chini zaidi hapa kwetu and not the other way around. Serikali ya Kichina ikipewa maswali kama haya basi watalazimika kufatalia what WENT WRONG na ku-apprehend wahusika wakuu kirahisi na bila huruma.
 
Nadhani mkataba ulisainiwa chumbani somewhere huko China kwenye lijihoteli.
Sasa sijui wanaume wazima wasaini mikataba kwa usiri vyumbani huko ugenini!
Makalio yao yalisalimika kweli????[wamefanyiwa mchezo mbaya hao hawakusalimika wameliwa utamu
 
Ahsante kwa majibu ya Ukweli

Nina imani Pasco utanijibu swali langu moja tu.

Baada ya hayo yote kujibiwa kama ulivyojibu Je TAKUKURU hawana uwezo wa kuhoji ukiukwaji mkubwa wa taratibu za manunuzi kama kama huu ulivyofanywa?
.
Kwani kwenye Richmond, TAKUKURU walisema nini?, vivyo hivyo kwa Gulf Stream, BAE radar na sasa bombo la gesi!.
Kama umebahatia kuwajua the real people behind Richmond, they are the same, "big fish", hicho
Kitakukuru ni nini, ni kama ukucha tuu kwenye kidole!.
Pasco.
 
Nadhani hapa lawama msiwape wachina,mbona hatuoni wachina wakileta ujinga Zimbambwe? tujilaumu wenyewe,sisi watanzania kwa kupenda njia za mikato ktk kufanya mambo yetu.
na kuhusu pesa za mikopo hususani hii mikopo kutoka nchi mbalimbali,wao huja na masharti yao na kwa mfano moja ya sharti waliloliweka kuhusu mradi wetu wa gesi ilikuwa ni kuuza gesi nje ya Tanzania,serikali ililikataa hili,kwa hiyo si kila masharti wanayotuwekea tunayakubari hapana,yapo yanayokubalika na yapo yasiyokubalika,kwa mfano kuhusu wakandarasi ni kawaida kuwatumia wakandarasi wa nchi husika maana hii itasaidia mradi kufanywa kwa kiwango na ubora unaotakiwa na tukumbuke kuwa Tanzania bado hatuna wakandarasi wenye uwezo wa kufanya miradi mikubwa kama hiyo,mfano mnzuri ni hizi shule za kata,wamatumika wakandarasi wa ndani kufanya kazi hiyo,nandeni mashuleni na mtajionea nyufa kwa madarasa yaliyojengwa ndani ya miezi 6 iliyopita.
hata kama serikali ingeongozwa na chama chochote kile pinzani,isnge kubali miradi iliyokopewa pesa nyingi zitakazolipwa na kodi ya wananchi kuharibiwa kwa kupewa mkandarasi aliyeshindwa kujenga shule zetu za kata.ila nacho kielewa mimi kuna kazi wakandarasi wetu wa ndani hupewa kupitia miradi mikubwa kama hii ya gesi na barabara.
 
Tenda ya Bomba la gesi ya Mtwara
1. Ilitangazwa lini
2. Consultant alikuwa nani?
3. Estimates zake zinasemaje?
4. Tenda ilitangazwa na idara zipi za
serikali?
5. Kampuni ngapi ziliomba hiyo
tenda?
6. Majina ya hizo kampuni
zilizoomba yako wapi?
7. Evaluation team ya hiyo tender
ilihusisha akina nani?
8. Pre qualification stage zilipita
kampuni ngapi?
9. Zilizoshindwa zilitolewa kwa
vigezo vipi?
10. Technical specs za huu mradi ni
zipi?
11. Financial specs za huu mradi
mbona siri kubwa?
12. Je kampuni ngapi za wana
Mtwara zilihusishwa hata kwenye
sub contracting?
13. Je, Mtwara Development Agency
WALIHUSISHWAJE KWENYE HUU
MPANGO?
14. Hizi TUHUMA za watu kula pesa
China ni kweli?
 
Very essential questions, on a serious note, unafaa kuwa mbunge!!!
 
maswali mazuri ila sasa yapo sehemu ambayo sidhani kama kuna atakae kuwa anamajibu ya kuridhisha........
 
Kwa ufupi kama mnakumbuka ilikuwa tugawane na mwekezaji 50% to 50% cha ajabu baada ya mtoto wa mfalme kukamatwa condition zimebadilika ni Wadanganyika tutapata 20% na mchina anapata 80% na ndivyo Jk alivyosainishana kumwokoa Prince
 
Back
Top Bottom