Tenda ya Bomba la gesi ya Mtwara

Tenda ya Bomba la gesi ya Mtwara

Upo sahihi PASCO Exim Bank of China wanajua rushwa ya kimataifa wanajua bei ya watawala wa kiafrika, watawala wetuwamepiga dili hapa,kwenye ishu ya bandari gati namba 13 na 14 ngawira zilitembezwa Wizarani ,TPA,TISS, kwa wabunge na washauri wa RAIS. Mzee Nundu alitolewa sadaka kwa uaminifu na uadilifu wake.Leo hatujifunzi tunafurahia mkopo wa aina ile ile wenye masharti ya mzabuni, mhandisi, mhandisi mshauri, msimamizi mmoja, wapi na wapi mwalimu wewe, mwanafunzi wewe, na bado unajisahihishia.

Kama Nundu ni msafi hivyo mbona hafunguki ? Kila siku anasemwa tu lakini kakaa kimya tu. U patriotism wake upo wapi? Angekua mchapa kazi hivyo angejiuzulu kama Mrema wakati ule na kumwaga kila kitu hadharani. Angethubutu hayo Urais ungekuwa wake 2015 kwa chama chochote kile.
Vinginevyo naona ni walewale tu.
 
wakuu? ina maana fast jet ni ya Riziwan? ndo maana wanataka gesi iende kule wanakotaka wajenge bandari nyingine?
 
inasemwa hata aliyetujengea uwanja wa taifa keshapigwa risasi!
Ndio mkuu sikutaka kulisema hilo, Serikali ya Kichina ilipopata tetesi kwamba msimamizi mkuu wa mradi huo kala rushwa - jamaa hawakumlazia damu muhusika wakambeba mzobemzobe na kwenda kumtwanga risasi ya kisogoni!
 
Naomba kutumia model ya ile Tenda ya Bandari

1. Ilitangazwa lini-Hikutangazwa

2. Consultant alikuwa nani?-CCCC

3. Estimates zake zinasemaje? zilianza Dola milioni 360 cha juu cha nanii na nanii ikafika 460-560 hadi 660

4. Tenda ilitangazwa na idara zipi za serikali?-Haikutangazwa

5. Kampuni ngapi ziliomba hiyo tenda?-moja CCCC

6. Majina ha hizo kampuni zilizoomba yako wapi?-CCCC

7. Evaluation team ya hiyo tender ilihusisha akina nani? -Wataalamu walipekwa China na CCCC

8. Pre qualification stage zilipita kampuni ngapi?-1 CCCC

9. Zilizoshindwa zilitolea kwa vigezo vipi? Hazikuwepo

10 .Technical specs za huu mradi ni zipi?-ziliandaliwa na CCCC

11. Financial specs za huu mradi mbona siri kubwa?-Ziliandaliwa na CCCC

12. Je kampuni ngapi za wana Mtwara zilihusishwa hata kwenye sub contracting?

13. jE mtwara development agency WALIHUSISHWAJE KWENYE HUU MPANGO?

14. hIZI TUHUMA ZA WATU KULA PESA cHINA NI KWELI? - ni uwongo!.

Hili la bandari CCCC ndio waliofanya feasibility study kwa ghara yao wenyewe!
CCCC wakatafuta funder Exim Bank
CCCC wakawa ndio wajenzi
CCCC wakaomba goverment guarantee wakapata!.
CCCC ndio wangerun mpaka utakapolipwa!.

Waziri Nundu akasmell a fish, akasimamisha kila kitu, wakamruka waziri, wakamtumia naibu waziri, government guarantee ikatoka bila kuombwa na waziri husika!. Waziri Nundu akamwaga ugali, JK akawatema wote, Mwakiembe ndie akamalizia kusafisha bandari.

Sasa ni zamu ya TPDC.
Pasco.
Cheap is expensive? Calculate.
 
1. Ilitangazwa lini2. Consultant alikuwa nani?3. Estimates zake zinasemaje?4. Tenda ilitangazwa na idara zipi za serikali?5. Kampuni ngapi ziliomba hiyo tenda?6. Majina ha hizo kampuni zilizoomba yako wapi?7. Evaluation team ya hiyo tender ilihusisha akina nani?8. Pre qualification stage zilipita kampuni ngapi?9. Zilizoshindwa zilitolea kwa vigezo vipi?10. Technical specs za huu mradi ni zipi?11. Financial specs za huu mradi mbona siri kubwa?12. Je kampuni ngapi za wana Mtwara zilihusishwa hata kwenye sub contracting?13. Je, Mtwara Development Agency WALIHUSISHWAJE KWENYE HUU MPANGO?14. Hizi TUHUMA za watu kula pesa China ni kweli?
Watu wengine bana, hivi unajua terms za mkopo husika au umeamua kubwabwaja tu
 
Mkuu sisi ndio tulikwenda wenyewe kuomba msaada CHINA tukawalilia hali, wakakubali kutoa mkopo kwa riba nafuu na grace periond nzuri - vile vile wenyewe ndio watafanya kila kitu sisi tunakabidhiwa mradi uliyo kamilika - Serikali ya Uchina haiwezi kuleta watu wababaishaji kwenye miradi inayo husu Serikali kwa Serikali, wanajuwa vizuri Kampuni zipi huko Uchina za kutekeleza mradi kama huu wa kutandaza bomba na pump za kusukuma gesi.Mbona watu wanawasakama Wachina sana, mbona tumewahi kushuhudia miradi ya ujenzi wa barabara unofadhiliwa na Wajapani lakini Wajapani wanaleta makampuni yao kujenga barabara mfano: Kajima na Konoike bila ya kutangaza tenda, si hilo tu hapo zamani Wajapani waliwahi kutoa fedha za kununulia mchele kwa mashariti kwamba ununuliwe Ujapan kwenyewe hili ni jambo la kawaida tu - why pick on CHINESE!!Haya tuje kwa mradi wa kujenga Hydro Electric mto Rufiji/Stigler Gorge - Wabrazil watatoa pesa zao, Macontractors wao katika utekelezaji wa mradi huo, Brazil haiwezi kukubali kutoa fedha alafu sisi tujifanye kutafuta Ma-contractos kutoka nchi nyingine, mambo mengine hatuna jinsi mkuu.Mwisho labda niseme kwamba kuna mradi wa kutandaza mabomba ya gesi huko Pakstani kama sikosei, wahusika wa mradi huu ni Wachina nafikili urefu wake hauna tofauti na huu wa kwetu, gharama za ujenzi na kila kitu hazizidiani na mradi wa hapa kwetu na kumbuka Pakstani hiko karibu na Uchina kijografia kuliko sisi - kuna baadhi ya watu wanafikili Wachina wamejipanga kutuibia?
Mkuu ufafanuzi umenyooka , ila wapotoshaji hawakawii kujitokeza
 
The same applies to Bandari ya Bagamoyo, Can we get the answers to the very questions
 
1. Acha upotoshaji kwa hoja zako , kuhusu mkopo wa Exim Bank of China, tuliuchukua kwa kudanganywa kuwa kutakuwa na grace period katika ulipaji wake baada ya mradi kukamilika na hivyo katika kufanya appraisal ya financing ya mradi wa bomba la gesi watawala wakakakimbilia China kukopa, lakini kwa namna mradi ulivyo tungeweza kupata pesa za mkopo kutoka benki nyinginezo duniani tena kwa riba ndogo isipokuwa kwa kuwa wakubwa walijua exim bank of china ni kichochoro cha rushwa walikimbia kukopa pale, kumbuka hawa exim china kwenye kukopesha serikali hawafanyi kitu kinaitwa credit rating na hawafanyi tathmini ya kuona mradi wao wanajali kampuni za China zifanye kazi basi provided ninyi mnacommitment ya kulipa. Kwa taarifa yako hata wahisani wetu wa maendeleo wenye kuchangia bajeti hawajaridhika na haraka tuliotumia kufanya maamuzi ya kukopa China bila kuangalia hali halisi ya mradi.2. Gharama za ujenzi unazoongelea PAKISTAN zipo chini kulinganisha na za kwetu kwa maana kwanza umbali wa bomba lao ni mrefu kuliko wetu, pia eneo la ujenzi ni gumu kijiografia na mwisho kipenyo cha bomba lao ni kubwa kuliko letu. Hoja ya ulinganifu wa bomba hilo na letu ipo humu JF itafute . Acha kuupotosha umma kuhusu mradi huu ambao umefunikwa na wapiga dili na maprofesa kama muhongo wameingia kichwa kichwa bila kujua waliowateua ni watu wa aina gani.
Wazushi ni wengi sana humu jamvini
 
Mkuu nafikili unaelewa kinacho endelea kati ya mataifa ya Magharibi na Uchina - vita hii ndio inaendelea katika mradi huu, wanaweza kusema chochote cha kuwazulia Wachina as if na wenyewe hawahusiki na vices wanazo watuhumu Wachina!! Ingechukuwa muda gani kupata mkopo kutoka nchi za magharibi ambazo hali yao ya kifedha si nzuri, wangetoa mashariti gani; je kampuni ya magharibi inayohusika kusafirisha GESI kwa njia ya bomba kutoka Kilwa unataka kunieleza hiko clean sio kwamba ilikuwa inachezea TAIFA letu kwa kubadilisha badilisha tariff za GESI wakati mwingine kuifunga kabisa kwa visingizio vya kila aina, Je TANESCO ilikuwa inalipa kiasi gani cha fedha kwa mwezi kwa kampuni hii ya kinyonyaji ambayo ilikuwa imepania kuzima ushindani wa kibiashara katika usafirishaji wa gesi nchini, walikuwa wanataka wabaki wao tu! - hilo mbona amlisemi, mnawashambulia Wachina tu.We unafikili kwa nini Serikali iliwashtukia kampuni hii kutokana na umangameza wao, Serikali ilikata shauri la kaomba msaada kutoka kwa Wachina ili wasaidie kujenga a parallel bomba kumaliza ukiritimba huu ambao ulikuwa umekubuhu! Nini kijili walipo pata habari kwamba Wachina wanakuja kujenga Bomba mbadala, walilalamika sana si hilo tu walishirikisha World Bank ili wakwamishe Wachina kwa kutoa visingizio vya kubuni tu - hata wafadhili wanao changia bajeti ya TAIFA letu waka jump kwenye bandwagon la kuwasema vibaya Wachina - wote hao i.e World Bank, Wafadhili lao moja i.e kupiga vita Wachina.Mwanzo nilifikili malumbano haya labda yanasukumwa na mambo ya partisian lakini baada ya kulichunguza kwa umakini naona si kweli. Kwa nini tuone ajabu Wachina kufanya kila kitu, kwani ujenzi wa TAZARA walishirikisha mataifa gani? Hapa nimeuliza mbona Projects karibu zote zanazo husu Japan nchini mwetu, Wajapan ndio ufanya kila kitu na sijawahi kusikia malalamiko kuhusu hilo - why pick on Chinese!
Mkuu nakuomba usipoteze muda kuwaelimisha wapotoshaji , viwavi wengi hapa jf huwa hawapendi kuelewa ukweli.
 
Tutasikia mengi mpaka hili la Gesi liishe na wasipokuwa makini litaondoka na watu hili.....
 
JK arudishe hela za wachina bomba halijengwi ila umeme utasafirishwa kwenda DSM!
 
kwa nini waandishi wetu hawaulizi haya maswali kwa wahusika?

Waandishi gani? Kibonde? Au wale wa Habari Leo? Au yule Ag Managing Editor wa Daily News waliyempiga kibuti?
 
Wabongo kwa fitna siwawezi, mbona miradi mingi inafuata taratibu hizo mnazouliza na tunaishia kuibiwa?
 


Kama Nundu ni msafi hivyo mbona hafunguki ? Kila siku anasemwa tu lakini kakaa kimya tu. U patriotism wake upo wapi? Angekua mchapa kazi hivyo angejiuzulu kama Mrema wakati ule na kumwaga kila kitu hadharani. Angethubutu hayo Urais ungekuwa wake 2015 kwa chama chochote kile.
Vinginevyo naona ni walewale tu.

Mwenzie mwakyembe hata mwaka bado bandari isha hanza kutakata. Tatizo alicheka na Nyani akajikuta kala mabua.
 
Back
Top Bottom