Tecno ndio mpango mzima
Te te te
Tecno ndio mpango mzima
CheearsssssI think you are wrong. Kuna watu wengi tu sio wa iphone peke yake wanategemea reviews za sites kama hizo ili ziwasaidie kufanya maamuzi sahihi. Mimi pamoja na kupenda kwangu Lumia (tena ni mnazi) sikununua mpaka nilipopitia baadhi ya hizi sites za tech kuelewa vizuri pros na cons za device niliyonunua. People will still buy iphones sababu wanazipenda na ni nzuri lakini ukweli ni kuwa kwa taarifa hizi mauzo ya iPhone 6+ yatapungua sana tu. Pengine kwa sababu hili tatizo haliligusi iphone 6 zenyewe zitaendelea kutoka kwa kiwango kikubwa. Mi si mpenzi sana wa iphone lakini kwa tatizo hili iphone 6+ siwezi kumshauri mtu anunue, ntamshauri ahamie kwenye 6 tu, 4.7" siyo size mbaya sana.
Kama inaanza kupinda hata ikiwekwa mfuko wa mbele, siyo habari nzuri. Kwa wanazi wa apple ambao wanasema hili si tatizo basi ndo wale wanaitwa 'mahaba niue'. Mimi na unazi wangu wa windows phone OS, nakiri bado kuna kazi ya kufanya upande wa software, na wala siwezi kuanza kubisha vitu ambavyo ni wazi.
tukiongelea wateja wa apple mkuu hata usipowapa specifications watanunua tu, yaani hata apple wakae kimya waanze kufanya presale kabla hawajawaonesha watu simu itavyokuwa amini nakwambia simu itagombewa kama njugu za kuchoma! hao ndiyo wapenzi wa apple walivyo. Kuhusu simu kupinda ikiwa imewekwa mfuko wa mbele na wewe unaamini mkuu?!!..hizo exageration tu, sema ikipewa pressure kidogo inapinda, siyo imekaa tu ipinde! Mimi ni mnazi wa kitambo sana wa Apple Inc. na hakuna simu za nyuma ambazo mimi sijawahi kununua, lakini kwenye 6s nilisema toka haijatoka kwamba sijaipenda hiyo design imekaa ovyo na sitanunua, upande wa design simu iliyoshinda kwa maoni yangu ni Note Edge, softwareni iOS 8, wala huwa sibishani kishabiki mkuu huwa napenda kuongea facts tu kwa sababu mwisho wa siku hizi simu hatupewi bure tunanunua cash, siwezi kusema mimi kufa na kuzikana ni Nokia hata iweje nisifie tu!
tukiongelea wateja wa apple mkuu hata usipowapa specifications watanunua tu, yaani hata apple wakae kimya waanze kufanya presale kabla hawajawaonesha watu simu itavyokuwa amini nakwambia simu itagombewa kama njugu za kuchoma! hao ndiyo wapenzi wa apple walivyo. Kuhusu simu kupinda ikiwa imewekwa mfuko wa mbele na wewe unaamini mkuu?!!..hizo exageration tu, sema ikipewa pressure kidogo inapinda, siyo imekaa tu ipinde! Mimi ni mnazi wa kitambo sana wa Apple Inc. na hakuna simu za nyuma ambazo mimi sijawahi kununua, lakini kwenye 6s nilisema toka haijatoka kwamba sijaipenda hiyo design imekaa ovyo na sitanunua, upande wa design simu iliyoshinda kwa maoni yangu ni Note Edge, softwareni iOS 8, wala huwa sibishani kishabiki mkuu huwa napenda kuongea facts tu kwa sababu mwisho wa siku hizi simu hatupewi bure tunanunua cash, siwezi kusema mimi kufa na kuzikana ni Nokia hata iweje nisifie tu!
Jibu lako ni neno moja tu: Semsationalism, wewe hujiulizi kwa nini mtu ukalie simu kubwa namna hii? Hebu ni nani kati yetu anakalia Samsung Galaxy Note au SOxy Xperia Z Ultra?
Wapenzi wa Apple asilimia kubwa ni 'Mahaba Niue', Ndugu zangu wawili wa kuzaliwa nao ni mfano mzuri, nawajua vizuri. Siyo kitu kibaya sana kwa sababu hata bidhaa yenyewe siyo mbaya. ila ushabiki maandazi wa kupinga hata ukweli ndio tatizo langu. Na wapo wanokubali mapungufu yaliyo kwenye apple, sina tatizo nao. after all no one or nothing is perfect.
Kuhusu kubend sikumaanisha uiweke tu mfuko wa mbele halafu ipinde kirahisi kama karatasi, pressure kidogo za hapa na pale lazima ziwepo. ila nawapinga wanaofikiria au kubisha kuwa mpaka uiweke mfuko wa nyuma na uikalie.
Hata NoKIA walikua hivohvo,lakin wakapoteza wateja taratibu,kimsing wateja hawakimbii ghafla tu,hata blackberry walikimbia taratibu..
Watakaochukizwa na iphone ya sasa hawatapata attention kwa inayotoka mwakan..ndivyohivo
Mkuu. Millah Nafuatilia post zako nying sana,n mtu unaejua sana kuhusu simu na ni mtu unaejua sana kuhusu haya mambo..
LAKINI TATZO LAKO KUBWA NI KWAMBA UNACHANGIA KISHABIKI,.
Sidhani kama utakua akili timamu kusema hilo sio tatzo,yani ukiweka mfukon(hata wa mbele kwenye suruali) ukikaa tu inajkunja,we unasema sii tatzo.!!!
Kwenye hili jukwaa hua hatulet ushabiki,tunaongeaga ukweli hata ukikuuma,ndo maana utamkuta chief-mkwawa. Kwenye thread hii anaisifia android kwa kitu fulan kwenye thread nyngne anaiponda kwa sababu flani..
hivo jirekebishe mkuu,sidhan kama wewe unaipenda iphone zaid ya. CYBERTEQ lakin kwenye ukweli kakubali
ni kweli zina matatizo, lakini mauzo ya iPhone hayategemei gsm arena, wateja wa iPhone ni wachache sana wanaotembelea gsm arena kwa sababu gsm arena huwa wanapata info za iPhone late sana. navyowafahamu wateja wa iphone hili tatizo bado halitawazuiya kununua iPhone, provided kwakmba wako covered na warranty!
hiv ngoja niulize kwa matumiz ya kawaida we una haja gan ya kubend namna ile simu?
pili wangap wanaweka simu mifuko ya nyuma tanzania hii hata kitoch tu ukiweka kitapasuka
nafikir tuanze na weekenes za internal ambazo znarelate moja kwa moja na simu(softwares)
Na hata hvyo kila biashara ina competitors usitegemee makampuni mengne ya simu yasitoe negative feedback on others product,kwahyo hata samsung wangetoa ya kwao bado watu wangekuja na kucoment negatively same way like what they do right now
la msing kama unapenda samsung lg whatever penda kwa mapenz yako hakuna mtu atakaekwambia utumie iphone or siemens if they still exist!
Kwani Note 4 ina nini jipya zaidi ya fremu ya aluminium badala ya plastiki? What sort of proof do you want?
Nikipata muda nitakuletea several comparison and between the two. Naamini comparison hiyo itatoa jibu lako
unayo uniuzie!Nokia 3310 ndio mpango mzima
kumbe mwenzangu ulikuwa unaipigia hesabu kimyakimya?!!
Wateja wa iPhone 6 na 6Plus wamepata specs za simu hiyo wiki moja kabla ya simu kutoka kwenye Keynote rasmi. Na info hizo ziko wazi kenywe mtandao wa Apple. Na hata GSMArena hawawezi kutoa specs zitakazosaidia kujua kupinda au kutokupinda kwa iPhone!