Tecno User Vs Samsung and iphone user

Tecno User Vs Samsung and iphone user

Mimi ninetumia sana Sumsung tatizo chaji, unakuwa unatembea na power bank utazani kama Hajar anavyotoka na mkoba, Tecno ya kwanza kutumia ilikuwa Camon 6+ nashukuru ilikuwa inakaa na chaji siku nzima na natumia mtandao hadi porini inashika kuliko hata waliokuwa na Iphone, kwasasa natumia Camon 8 iko vizuri. Ila nataka nirudi kwenye Samsung au nichukue IPhone ingawa kwa kazi nazofanya kudongosha simu kitu cha kawaida hapo nawaza hasara pia.
Tecno wana vitu vichache tu vya kurekebisha ila zitakuja kuwa simu kali sana kwa baadae
 
Wateja wa tecno ndo wanaongoza kwa route pale aggrey na likoma, yan asubuh katoka kununua tecno K7, hajafka hata nyumbn akiingia kwenye mtandao wameshatoa tecno K7 plus. Hawa jamaa wanawazungusha sana wateja wao na ndio maana weng n full stress, simu ukiiweka mfukoni ukitoa umeshawapigia ma X wako wote, unamwandikia mtu wa heshma msg unaandika poa kule inafka papuchu, hapo sijagusia vifurush ulivyojiunga bla kujua na mikopo
 
Hahaaaaa. Hapo nitashindwa kutoa ushahidi sababu mie huwa naamini matumizi ndio yanafanya simu ikae na chaji au kutokaa na chaji.

Huwezi sema Tecno inakaa na chaji wakati kutwa nzima upo job na ikitokea umeperuzi simu basi ni muda wa breakfast au lunch.

Kila simu inakaa na chaji kikubwa ni aina ya matumizi tu.
Nakusaidia, zipo nyingi tuu
Mfano ni hii niliyonayo, siyo tecno ila betri yake ni mhA 3000, tangu ichajiwe jana asubuh ina 39% sasahivi, na ikumbukwe ni weekend so nimeitumia saanaa...
 
Watu wa samsung na i phone wakija hapa lazima wapinge tu mkuu?
Ni kweli mkuu, ila naamini wanapnga kwa sababu zilizo wazi.
Nimewah kuwa na mawazo yakusema matumizi ya tecno na sumsung/iphone ni yale yale, na nikaongeza kwakusema mengine ni ufahari na ulimbukeni wa majina ya kampuni, ila trust me niliiona tofauti nilipotumia brand zote, ni tofauti kubwa sana
 
Ni kweli mkuu, ila naamini wanapnga kwa sababu zilizo wazi.
Nimewah kuwa na mawazo yakusema matumizi ya tecno na sumsung/iphone ni yale yale, na nikaongeza kwakusema mengine ni ufahari na ulimbukeni wa majina ya kampuni, ila trust me niliiona tofauti nilipotumia brand zote, ni tofauti kubwa sana
Kabisa mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom