Tecno Phantom A VS Samsung Galaxy S4 - Utofauti na Usawa!

Tecno Phantom A VS Samsung Galaxy S4 - Utofauti na Usawa!

nami natumia p3 karibu miezi 4 sasa nilitaka mwezi huu ninunue phantom a+ lakini ant tecno wameipondea mno sasa sijui nitanunua simu gani kwa laki 4 niliyo nayo(tayari nilikuwa nimeongea na mtu anichukule dar wiki ijayo.mimi nipo tarime)

Usiwasikilize ANTI TECNO wewe nunua kitu kitakachoifurahisha nafsi yako kulingana na pesa yako. Au kama vipi jichange hadi ifikie LAKI TISA ndo ukanunue samsung
 
kusema camera ya Tecno ziko sawa na IPhone 5 kisa zote ni 8mp huu ni utani na dharau kwa iPhone wanaoumiza vichwa kila siku watoke vipi, wakati Tecno ni copy anda past
 
Kwangu mm hela kama sio issue bora ununue Samsung S4 au samsung S4 mini Duos maana bei yake imeshuka kulinganisha na S4 nyingine so long as zote ni Samsung S4 bado niko in the track

Lkn Pia kuna swala la DATA na Battery

Samsung S4 kampita Phantom pia
sidhani kama Phantom hapa kafika HSDPA 42.2 Mbit/s(Download), HSUPA 5.76 Mbit/s(Upload)

Battery
Galaxy S4 kafika 2600 mAh, Li-ion
Phantom A+ kafika 2100 mAh, Li-ion

Mkuu sasa hivi hiyo simu inacheza na ngapi maana naikusanyia nguvu.!
 
Mkuu sasa hivi hiyo simu inacheza na ngapi maana naikusanyia nguvu.!

Mlimani city samsung fealers january mwanzoni nilikuta wanauza 750,000/-

Nilipoenda posta nikakuta 650,000/- na ni kwa madealer wa samsung walio authorised hivo hamna ufeki wala nn
 
.
Naamini una sim card zaidi ya mbili za mitandao tofauti....
.
.

Nna sim card mbili na nnatumia Galaxy duos

1609595_486196931501848_1794991582_n.jpg
 
Nna sim card mbili na nnatumia Galaxy duos

1609595_486196931501848_1794991582_n.jpg

.
Kaka unaona ulicho kiandika hapa
.
mie nitanunua
12(1).jpg



kuliko kununua hii

t4.jpg



mtu na akili zake atakuja aseme hii ni nzuri kwa sababu ina weka laini nne, inapiga muziki na blah blah kibao

kisha ataniambia naangalia majina,
.
Kwa hiyo kama una laini mbili iweje uchague
.
12(1).jpg

.
Hebu mda mwingine tuachane na spirit na CHUKI zilizO tujaa mioyoni juu ya hizi TECNO
.
kweli mtu na akili timamu uchague simu kama hiyo Joe Nyandigira......
.
Kama ni ni spirit sawa mana hata mimi huwa na hate sana pirated softwares kama vile photoshop
.
Na kinanikwamishaga kitu kimoja baadhi ya software zime lack blending option
.
Ila kama ndugu yangu utachagua hako ka nokia ka torch na kuiweka laini yako nyingine pembeni basi wewe ni
Jf senior anti-tecno member
.
 
Last edited by a moderator:
.
Kaka unaona ulicho kiandika hapa
.

.
Kwa hiyo kama una laini mbili iweje uchague
.
12(1).jpg

.
Hebu mda mwingine tuachane na spirit na CHUKI zilizO tujaa mioyoni juu ya hizi TECNO
.
kweli mtu na akili timamu uchague simu kama hiyo Joe Nyandigira......
.
Kama ni ni spirit sawa mana hata mimi huwa na hate sana pirated softwares kama vile photoshop
.
Na kinanikwamishaga kitu kimoja baadhi ya software zime lack blending option
.
Ila kama ndugu yangu utachagua hako ka nokia ka torch na kuiweka laini yako nyingine pembeni basi wewe ni
Jf senior anti-tecno member
.
obvious nilikuwa sijakuelewa swali lako,

ni heri niwe na nokia za tochi mbili kuliko kuwa na tecno ambalo ukiliwasha lazima ujifiche maana uo mkelele wake sasa, mimi sio anti tecno kama ambavyo unanilable wewe na wenzako, mimi tecno hawajani impress, siku nikiwakubali nitawasifia, mbona uwa tunabishana na chief-mkwawa sana tu kuhusu nokia lumia kwa sababu mimi sizifagilii kabisaaa na yeye ni mnazi wa nokia, anakuja na hoja nakuja na hoja tunabishana,
 
Last edited by a moderator:
Guys hivi kweli kabisa mtu mzima unasema kuwa kampuni ya TECNO haina headquaters. Seriosly???
Hii kampuni ilianzishwa mwaka 2006 Hong Kong. Na wana mpango wa kufungua viwanda vikubwa vya simu nchini Nigeria na Ethiopia bcoz Africa ndo soko lao walilo-target. Unavyowaambia watu kuwa kampuni haina makao makuu una maanisha nini? Kwahiyo hizi product zao wanatengenezea uchochoroni. Akili za kuambiwa changanya na zako walisema wazee wetu.
 
Guys hivi kweli kabisa mtu mzima unasema kuwa kampuni ya TECNO haina headquaters. Seriosly???
Hii kampuni ilianzishwa mwaka 2006 Hong Kong. Na wana mpango wa kufungua viwanda vikubwa vya simu nchini Nigeria na Ethiopia bcoz Africa ndo soko lao walilo-target. Unavyowaambia watu kuwa kampuni haina makao makuu una maanisha nini? Kwahiyo hizi product zao wanatengenezea uchochoroni. Akili za kuambiwa changanya na zako walisema wazee wetu.

Mkuu hawa wachina We waache tu mm nimeviona vifaa vya wachina vingi lkn huenda ni ukweli hamna cha headquartes wala nn
Kuna devices za Wachina zinaitwa SANEI TABLETS ni wale wale yaani hawaeleweki hawa wachina

Ukitaka kutu-impress uje na Link kuverify maneno yako vingginevyo kuongea hewani hawatakuelewa
 
obvious nilikuwa sijakuelewa swali lako,

ni heri niwe na nokia za tochi mbili kuliko kuwa na tecno ambalo ukiliwasha lazima ujifiche maana uo mkelele wake sasa, mimi sio anti tecno kama ambavyo unanilable wewe na wenzako, mimi tecno hawajani impress, siku nikiwakubali nitawasifia, mbona uwa tunabishana na chief-mkwawa sana tu kuhusu nokia lumia kwa sababu mimi sizifagilii kabisaaa na yeye ni mnazi wa nokia, anakuja na hoja nakuja na hoja tunabishana,


Hapo kwenye B and I umeniacha HOI
Kuna Lecturer siku moja seminar moja chuo kimoja aliumbuliwa na Kitecno hicho kwa mikelele yake

Yaani mm Tecno nilikuwa naifagilia sana lkn nilikuwa sijafunguka macho nina Tecno P3 yangu imenitesa mpaka nikafunga mkataba nayo na nimewapa wanangu wachezee maana haina tofauti na vile visimu vya watoto wa kuchezea
 
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na maswali mengi, ubishani na maneno kwamba Tecno Phantom A na Samsung Galaxy S4 zinafanana na zina uwezo sawa.

Kutokana na hilo, nimeona ni vyema nikazifananisha simu hizi kwa mwonekano na uwezo pia ili kama unataka kununua, ufanye maamuzi sahihi!

Simu zenyewe ndo hizo hapo chini kama unavyoziona kwenye picha!
View attachment 135107

Kwanza nitaanza kuzifananisha bei.
Tecno Phantom A: Tshs. 358,442.75
Samsung Galaxy S4: Tshs. 935,933.87

Hizi ni bei za makadirio. Bei zinaweza kuwa tofauti kulingana na mahali ulipo na duka pia. Ila kwa wastani, Samsung Galaxy S4 ina bei mara 3 zaidi ya Tecno Phantom A.

Tecno Phantom A ni nene Zaidi kuliko Samsung Galaxy S4. Pia ni nzito na ndefu Zaidi kuliko Samsung Galaxy S4.

Simu zote mbili zina screen za nchi 5. Resolution zake zipo kama hivi:
Tecno Phantom A: 1220 X 720
Samsung Galaxy S4: 1920 X 1080

Tofauti inapokuja kati ya hizi simu mbili ni Teknolojia iliyotumika katika kutengeneza screen zake. Samsung Galaxy S4 ina Super Amoled Screen wakati Techno Phantom A inatumia TFT Technology. Hii inamaanisha kwamba Display ya Samsung ipo sharp Zaidi. Ila kama haupo sensitive sana, ni ngumu kuona utofauti katika mwonekano wa vioo vya simu hizi.

Sasa ngoja tuongelee Camera za simu hizi zote mbili:

Samsung Galaxy S4:

  • Camera ya nyuma in 13 MegaPixel na inaweza ku-record video katika full High Definition. Ya mbele ina 2 MegaPixel.
  • Software ya Camera imeongezewa features nyingi pia.

Tecno Phantom A:

  • Camera ya nyuma ina 8 MegaPixel na ya mbele ina 1.2 MegaPixel. Camera hii ya nyuma inauwezo sawa na Camera zinazopatikana kwenye simu maarufu kama vile IPhone 4s, 5s na 5c. Sio mbaya kwa matumizi ya kawaida ingawa quality inakuwa chini kidogo ukifananisha na picha iliyopigwa kwa Samsung Galaxy S4.
  • Software ya Camera ni ya kawaida ambayo originally inakuja kwenye Android bila features zozote zilizoongezwa.

Sasa ni vyema tukatazama Operating Systems kwenye simu zote mbili. Simu zote hizi ni za Android 4.2. Ila Samsunga Galaxy S4 inakuja na Android 4.2.2 na Tecno Phantom A inakuja na Android 4.2.1.

Android inayopatikana kwenye Samsung Galaxy inakuja na Features & Customizations nyingi ambazo zimeongezwa ambazo hizo zinaipa look na feel ya Samsung.

Kwa upande wa pili, Android ya kwenye Tecno Phantom A, inakaribia kuwa sawa na Android Halisi inayotolewa na Google. Hawajafanya customizations ili angalau ilete mwonekano wa Ki-tecno Zaidi. Labda kwenye matoleo yajayo itafanyiwa marekebisho ingawa hata sasa bado inaonekana kuwa sexy!

Technical Specifications:
Tecno Phantom A:
Tecno Phantom ina Dual – Core Processor ambapo kila Core ina 1.2 GHz. RAM yake ni 1GB. Uwezo huu kwa simu ni wa kawaida na ni mzuri pia kwa shughuli za kila siku. Pia inafaa kwa kuchezea ma-game mazito kwa wale gamers.

Samsung Galaxy S4:
Kwa upande wa Samsung Galaxy S4, uwezo wake huku ni amazing. Ina processor yenye 8 cores. Cores 4 za kwanza kila mmoja ina uwezo wa 1.6 GHz na Cores 4 zinazobaki kila mmoja ina 1.2 GHz. RAM yake ni 2GB.

Specifications hizi ni Zaidi ya mahitaji ya simu. Sijui kama kuna Application yeyote ya simu duniani inayohitaji simu ya uwezo mkubwa kiasi hiki. Mimi naweza kusema ni wastage na labda ndo inayochangia simu hii kuwa na bei kubwa.

Kuwa na simu hii ni sawa na kubeba Computer kubwa na kutembea nayo barabarani!
Note: Kwa wageni kwenye teknolojia.

Tunaposema Processor ina Dual Core Processor, tunamaanisha kwamba ndani ya processor moja, kuna vi-processor vidogo viwili. Hii ina maana kwamba kupata speed kuu ya simu yako, unazidisha hiyo 1.2 kwa Tecno mara 2.

Kwa maana hiyo hiyo, Samsung Galaxy S4 ina vi-processor 8 ndani yake.

Hitimisho:
Nikitakiwa leo kununua simu, basi nitanunua Tecno Phantom A. Hii ni kwa sababu inafanya vitu vyote ambavyo Samsung Galaxy S4 inafanya. Pia inapatikana kwa bei ndogo na inaruhusu kuweka line 2 kwa wakati mmoja.

Kwa mtazamo wangu, kumiliki Samsung Galaxy S4 ni sawa na kuchezea hela. Labda kwa wale ndugu zangu akina Ngosha na Wahaya ambao kuwa na kitu cha gharama kunamaanisha High Status, hawa inawafaa hii Samsung Galaxy S4!
Nawasilisha.

Camera is more than just megapixels, just saying... Same case with displays, many factors come into play!! 😀
 
Tecno P3 yangu imenitesa mpaka nikafunga mkataba nayo na nimewapa wanangu wachezee maana haina tofauti na vile visimu vya watoto wa kuchezea
.
Ni nn hiki njunwa
.
Kweli p3 idharauliwe kiasi hicho kiongozi....
Sina imani kama ulikuwa hujui kabisa aina za simu mpaka uka chagua hiyo?
.
Mm sio mpenzi wa tecno ila nime boreka
.
 
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na maswali mengi, ubishani na maneno kwamba Tecno Phantom A na Samsung Galaxy S4 zinafanana na zina uwezo sawa.

Kutokana na hilo, nimeona ni vyema nikazifananisha simu hizi kwa mwonekano na uwezo pia ili kama unataka kununua, ufanye maamuzi sahihi!

Simu zenyewe ndo hizo hapo chini kama unavyoziona kwenye picha!
View attachment 135107

Kwanza nitaanza kuzifananisha bei.
Tecno Phantom A: Tshs. 358,442.75
Samsung Galaxy S4: Tshs. 935,933.87

Hizi ni bei za makadirio. Bei zinaweza kuwa tofauti kulingana na mahali ulipo na duka pia. Ila kwa wastani, Samsung Galaxy S4 ina bei mara 3 zaidi ya Tecno Phantom A.

Tecno Phantom A ni nene Zaidi kuliko Samsung Galaxy S4. Pia ni nzito na ndefu Zaidi kuliko Samsung Galaxy S4.

Simu zote mbili zina screen za nchi 5. Resolution zake zipo kama hivi:
Tecno Phantom A: 1220 X 720
Samsung Galaxy S4: 1920 X 1080

Tofauti inapokuja kati ya hizi simu mbili ni Teknolojia iliyotumika katika kutengeneza screen zake. Samsung Galaxy S4 ina Super Amoled Screen wakati Techno Phantom A inatumia TFT Technology. Hii inamaanisha kwamba Display ya Samsung ipo sharp Zaidi. Ila kama haupo sensitive sana, ni ngumu kuona utofauti katika mwonekano wa vioo vya simu hizi.

Sasa ngoja tuongelee Camera za simu hizi zote mbili:

Samsung Galaxy S4:

  • Camera ya nyuma in 13 MegaPixel na inaweza ku-record video katika full High Definition. Ya mbele ina 2 MegaPixel.
  • Software ya Camera imeongezewa features nyingi pia.

Tecno Phantom A:

  • Camera ya nyuma ina 8 MegaPixel na ya mbele ina 1.2 MegaPixel. Camera hii ya nyuma inauwezo sawa na Camera zinazopatikana kwenye simu maarufu kama vile IPhone 4s, 5s na 5c. Sio mbaya kwa matumizi ya kawaida ingawa quality inakuwa chini kidogo ukifananisha na picha iliyopigwa kwa Samsung Galaxy S4.
  • Software ya Camera ni ya kawaida ambayo originally inakuja kwenye Android bila features zozote zilizoongezwa.

Sasa ni vyema tukatazama Operating Systems kwenye simu zote mbili. Simu zote hizi ni za Android 4.2. Ila Samsunga Galaxy S4 inakuja na Android 4.2.2 na Tecno Phantom A inakuja na Android 4.2.1.

Android inayopatikana kwenye Samsung Galaxy inakuja na Features & Customizations nyingi ambazo zimeongezwa ambazo hizo zinaipa look na feel ya Samsung.

Kwa upande wa pili, Android ya kwenye Tecno Phantom A, inakaribia kuwa sawa na Android Halisi inayotolewa na Google. Hawajafanya customizations ili angalau ilete mwonekano wa Ki-tecno Zaidi. Labda kwenye matoleo yajayo itafanyiwa marekebisho ingawa hata sasa bado inaonekana kuwa sexy!

Technical Specifications:
Tecno Phantom A:
Tecno Phantom ina Dual – Core Processor ambapo kila Core ina 1.2 GHz. RAM yake ni 1GB. Uwezo huu kwa simu ni wa kawaida na ni mzuri pia kwa shughuli za kila siku. Pia inafaa kwa kuchezea ma-game mazito kwa wale gamers.

Samsung Galaxy S4:
Kwa upande wa Samsung Galaxy S4, uwezo wake huku ni amazing. Ina processor yenye 8 cores. Cores 4 za kwanza kila mmoja ina uwezo wa 1.6 GHz na Cores 4 zinazobaki kila mmoja ina 1.2 GHz. RAM yake ni 2GB.

Specifications hizi ni Zaidi ya mahitaji ya simu. Sijui kama kuna Application yeyote ya simu duniani inayohitaji simu ya uwezo mkubwa kiasi hiki. Mimi naweza kusema ni wastage na labda ndo inayochangia simu hii kuwa na bei kubwa.

Kuwa na simu hii ni sawa na kubeba Computer kubwa na kutembea nayo barabarani!
Note: Kwa wageni kwenye teknolojia.

Tunaposema Processor ina Dual Core Processor, tunamaanisha kwamba ndani ya processor moja, kuna vi-processor vidogo viwili. Hii ina maana kwamba kupata speed kuu ya simu yako, unazidisha hiyo 1.2 kwa Tecno mara 2.

Kwa maana hiyo hiyo, Samsung Galaxy S4 ina vi-processor 8 ndani yake.

Hitimisho:
Nikitakiwa leo kununua simu, basi nitanunua Tecno Phantom A. Hii ni kwa sababu inafanya vitu vyote ambavyo Samsung Galaxy S4 inafanya. Pia inapatikana kwa bei ndogo na inaruhusu kuweka line 2 kwa wakati mmoja.

Kwa mtazamo wangu, kumiliki Samsung Galaxy S4 ni sawa na kuchezea hela. Labda kwa wale ndugu zangu akina Ngosha na Wahaya ambao kuwa na kitu cha gharama kunamaanisha High Status, hawa inawafaa hii Samsung Galaxy S4!
Nawasilisha.

Uko sahihi mkuu. Ninayo Samsung S4 na pia nimenunua TECNO PHANTOM A+ Last week na sioni tofauti. kwanza techno inatunza charge kuliko S4 na ninaenjoy kama kawa.
 
hivi unaakili nzr wewe kucompare tecno na S4?
jiangalie akilili yako vzr, kuliko kupotosha wasojua.


jiulize ni kwanin bei imzunguke mara 3,
mwerevu yeyote hapo tu lazma astuke
 
hivi unaakili nzr wewe kucompare tecno na S4?
jiangalie akilili yako vzr, kuliko kupotosha wasojua.


jiulize ni kwanin bei imzunguke mara 3,
mwerevu yeyote hapo tu lazma astuke


Mbona unakurupuka mzee.....mwenzio katoa utofauti na usawa wa hizi simu kwa hoja...hujaelewa nini hapo
 
hivi unaakili nzr wewe kucompare tecno na S4?
jiangalie akilili yako vzr, kuliko kupotosha wasojua.


jiulize ni kwanin bei imzunguke mara 3,
mwerevu yeyote hapo tu lazma astuke

Mi akili yangu ina matatizo. Simple like that!

Ila na wewe jiangalie akili yako vizuri. Inawezekana ina matatizo kuliko yangu.
 
Back
Top Bottom