Adhabu ni kubwa mno na kwa watu wasio na makosa.
1. mkosaji (kama amekosa) alikuwa gwajima.
2. adhabu wamepewa malaki ya waumini nchi nzima, hawatatakiwa kusali kwa sababu ya kosa la mtu mmoja.
3. kwa nini waumin wahukumiwe kwa mamkosa ya gwajima?
4. serikali ya rais muislam inafanya hivyo, hawaoni kama wataeleweka vibaya? tangu lini msikiti hata mmoja tu ulishawahi kufungwa hapa nchini, kwanini mfungie tu kanisa kubwa kama hilo,kwanini mnagawa watanzania?
imagine, maelfu ya watanzania wanaosali kanisa la ufufuo na uzima lililopo Tanzania, na nje ya nchi, wamefutiwa usajili kwa hio makanisa yao hayapo, kwa sababu tu mtu mmoja amekemea utekaji na uuaji wa raia. wale waumin wana kosa gani sasa? wale maaskofu mikoani nao waliyahubiri hayo? kinachoonekana ni kwamba, aliyetoa wazo hili sio mtu wa mlengo wa makanisa ya gwajima na inawezekana sio mkristo, ni mtu mwenye chuki na dini, ndio maana ameattack kanisa loote wakati kulikuwa na uwezekano kuadhibu gwajina na wengine wakaendelea kuabudu. Mungu ataamua!