TeamLowassa hatuna chetu Ikulu!

TeamLowassa hatuna chetu Ikulu!

Mkuu,

Sio uzushi, na sijasema Mkapa Alikuwepo. Kuwa muelewa.

Haya mambo yalikuwa 'behind the scene' ila sasa yamedhihirishwa na hao wazee kuwa wapo upande upi.

Ushauri wao ni kwamba: Makongoro ataunganisha wana CCM ambao kwa mujibu wa maelezo yao, CCM kwa sasa imejaa nyufa.

HUWA NIKIONA POST ZAKO NAKEREKA KWANI ULIKUWA HUJUI HLO AU?CCM WOTE HAWAFAI HATA HUYO KONGORO NYERERE PIA NI WALAWALE SBB ATAINGZWA NA SYTEM ILEILE YAKINA MAFISADI KWA MASLAHI YAO.mda umefikga wa mabidiliko vote 4 ukawa kwa maslahi mapana ya nchi yetu ya neema na utajiri wa kila aina.
 
Sidhani kama nyerere angekuwa hai angekubali mtoto wake agombee uraisi sidhani.
 
1.UBUNGE ULITENGULIWA na mahakama kwa kosa la kuanza kampeni mapema
2.Cha pombe Mkapa/uhuru kenyatta na bush wamefanya lipi baya kwa nchi zao sababu ya POMBE
3.ameiheshimu sana nchii hii kwa kutokuwa mtoto fisadi.Je makongoro utamfananisha na FRED LOWASSA/RIDHIWAN au HUSSEIN MWINYI?????

taja nani anafaa zaidi ya makongoro ccm???



Hamna zaidi ya Lowassa
 
tatizo sio CCM kwa ujumla wake bali ni top uongozi
huko china chama kimoja kimetawala miaka kibao na kikawa kila RUSHWA NA UFISADI ILE MBAYA-rais mpya wa china JIN ameamua kupamba na RUSHWA na sasa watawala na maofisa wa Zamani wako magerezani na wengine wamenyongwa

HATA kama CDM/CUF wataingia madarakani ila KIONGOZI mkuu au rais ndiye dira na sio CHAMA KWA UJUMLA WAKE
africa kama china hatuna taasisi imara kwa hiyo tunaitaji viongozi imara.MAREKANI NA ULAYA WANA TAASISI IMARA kwa hiyo hata fisadi akiwa rais bado atakuwa na wakati mgumu wa kufisadi

Wananchi tulipotaka kumaliza haya matatizo kwa kutumia katiba tuliweka maoni yetu ili iwe mwongozo mzuri,lakini sikuona Makongoro wa nani aliyetutetea zaidi yakutukandamiza isipokuwa Warioba na Butiku.Hao wawili tu ndio niliowasikia kati ya wana Ccm wote,ndio mana nasema tena ili tuwe salama tunapaswa tuiondoe Ccm kwanza alafu tutengeneze Katiba mpya alafu kama hiyo Ccm itakuja kuludi ije huku tukiwa na msingi mpya
 
Bora wamuweke hata huyo kuliko Lowasa, atakikost chama....Jina la Nyerere ndo karata ya CCM kuwarubuni wa TZ ili kuchukua nchi tena...tunawapa UKAWA.
 
Hata akiwa rais hana ubavu wa kupambana na mafisadi ndani ya chama watampelekesha tu na sidhani ana karama kama za baba yake. Ila kwa waheshimiwa kumpitisha wana lao jambo wao watakuwa salama salmini lakini sisi walalahoi tutazidi kuangamia kwa kukosa maarifa.
 
Kamati Kuu (CC) ya CCM itakuwa imewatukana watanzania wote matusi ya nguoni kama jina la Lowassa litakuwemo katika yale yanayoenda NEC.

Ajenda ya kwanza ya CC iwe kuondoa jina la Lowassa ndipo mchakato unendelee.
 
Mkuu,

Sio uzushi, na sijasema Mkapa Alikuwepo. Kuwa muelewa.

Haya mambo yalikuwa 'behind the scene' ila sasa yamedhihirishwa na hao wazee kuwa wapo upande upi.

Ushauri wao ni kwamba: Makongoro ataunganisha wana CCM ambao kwa mujibu wa maelezo yao, CCM kwa sasa imejaa nyufa.

Hiyo ni kwa mujibu wao, je, na wewe kwa mtazamo wako binafsi unakubali kwamba CCM imejaa nyufa?
 
Niwaambie kitu .. Sizungumzi kwa unafiki. Nilipomuona Makongoro asubuhi hii kwenye Clouds TV. nimebubujikwa na machozi....nasema kwa dhati.

AISE UNA MATATIZO C BURE.KWELI TZ YETU IMEKUWA SHAMBA LA BIBI ATARITHI HADI MJUKUU....HAYA SASA MAKORONGO NYERERE BDYE HUSENI MWINYI THEN RITZ KIKWETE THEN MTOTO WA MAKONGORO THEN MJUKUU WA RIZ1 aise hatari sna tutabaki kwenye cycle ile ile na mawazo yale yale bila mabadiliko sbb yakufanya kz kimazoea bila kutegemea ufanisi
 
ki ukweli ccm waki mpitisha Makongoro UKAWA tutachapwa mapema sana...jina la Baba yake lita mbeba sana na jinsi watanzania wengi walivyo mazuzu mmhhh tuombe Mungu.

Mkuu kampeni strategy huwa zina change kutokana na mgombea .................. lets wait and see. Time will tell!! To me Makongoro anaweza kuwa rahisi sana kudeal naye kuliko mtu kama Magufuli au Membe!!
 
kwa hiyo unatuambia kuwa lowassa alikuwa anaiwakilisha ukawa huko ccm?mbona hueleweki?ukawa inapambana na ccm,na si makongoro au lowasa,labda umechanganya ukawa na gamba mwenzio laki si pesa huyo ndiye aliyekuwa akimtukuza huyo fisadi wenu.

afadhali wewe unaakili kidogo ya kuona mbaliii
 
Mkuu kampeni strategy huwa zina change kutokana na mgombea .................. lets wait and see. Time will tell!! To me Makongoro anaweza kuwa rahisi sana kudeal naye kuliko mtu kama Magufuli au Membe!!

Utadeal vipi na mtu ambae hajawahi kuwa serikalini.
 
Tanzania kama Tanzania, hakuna upinzani wa ukweli, hakuna cha hao UKAWA au nani sijui, maana ukiviangalia vizuri hivyo vyama vya upinzani vinaendeshwa kwa matukio, hawana sera za kueleweka utakuta tukio fulani likitokea, basi wamelishikilia, likiisha wanakaa kimya likitokea tukio lingine basi wanalishupalia hivyo hivyo reference mgomo wa madereva wa mabasi, katiba mpya, etc etc yani Tanzania hakuna upinzani bado, ni unafiki kwenda mbele na uchu wa madaraka
Ndugu vipi kama chama tawala haina uchu wa madaraka basi iachie ukawa!
 
Back
Top Bottom