Wakuu dunia ya leo hakuna kitu inaitwa bure tena, huku nchi za dunia ya tatu ndio tunaona mambo haya maajabu na hii inatokana na kulemazwa na mfumo wa kizamani wa bure bure
Labda tuangalie mfumo wa urushaji matangazo kwenye mfumo huu wa dijitali ili tuelewane
Zamani mtu yeyeto anaweza kuanzisha tv station yake labda akaiita miningits tv akawa anafanya vipindi vyake na kwa mfumo wa analojia maana yake alikuwa anaweka dish lake na kurusha na wenye tv zao za analogi wanadaka na kuendelea na maisha
mfumo wa dijitali umekuja kivingine maana sasa meningits tv atahitaji mtambo mkubwa wa kurusha matangazo kwa digitali kitu ambacho ni kigumu kwake
kinachofuatia ni watatokea watu wenye uwezo wa kurusha matangazo kwa dijitali na watakuwa wanakusanya tv station kadhaa za nje na ndani na kuziweka kwenye ving'amuzi vyao kisha kivirusha kidijitali na hii hufanyika kwa makubaliano ya kibiashara zaidi, hapa inabidi meningits tv aende kwa hawa jamaa ajiunge nao wamrushie matangazo yake
Hadi sasa tuna Ting, Startimes, Zuku na Easytv kama sijakosea, hawa ndio wanarusha matangazo kidijitali kupita vingamuzi vya fta na setelaiti
sasa wenye tv stations wanayo haki ya kuchagua kufanya kazi na nani kati ya wenye ving'amuzi hawa kulingana na offer zao, lakini ikaibuka hoja inamaana mtu atalazimika kununua ving'amuzi vingapi kuona local channel mbalimbali?
hapo sasa TCRA ikaja na ubabe kwa manufaa ya mwananchi kwa kuwalazimisha wenye tv stations 5 walizoita za kitaifa kuingia mikataba na wenye ving'amuzi wote.
Wakatoa agizo kwamba lazima ITV, EAT, STARTV, TBC na CHANNEL10 ziingie mikataba na wenye ving'amuzi wote na pia ikatoa amri wenye ving'amuzi warushe chaneli hizo tano bure hata kama muda wa package ya kawaida ukiisha basi chaneli hizi ziendelee kuonekana
Hadi hivi sasa kampuni zote zinarusha chaneli hizo tano lakini bado hawajaafikiana vizuri kibiashara kwasababu ya ulazima waliopewa na TCRA
Sasa hizi tv station zingine kama DTV, clouds nk wanalazimika kutafuta kampuni moja ya kufanya nayo kazi au kama wakiweza basi wataingia mkataba hata na kampuni zaidi ya moja, kwataarifa nilizo nazo Clouds tv wameshindwana na Startimes na wamekwenda Zuku
Kama hutaki usumbufu wa kulipia kwa mwezi walau kwa muda huu wakati bado tupo ugenini kwa dijitali basi unaweza kufunga dish la free chanel na utaweza kuona baadhi ya stations zinazorusha matangazo kwa setelaiti....na hii ni kwa muda tu maana biashara ikichanganya watazitoa na utalazimika kuziangalia kupitia ving'amuzi