Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,502
- 51,098
Makampuni ya mawasiliano nchini yamezima data takriban wiki moja sasa. Wakati yakizima, hayakuwatangazia wateja juu ya uzimaji huo, na hivyo wateja wengi wakajikuta vifurushi walivyokuwa wameweka kwenda bure!
Lakini pia, kwa wale ambao hawakujua kuwa kuna kuzimwa kwa makusudi kwa mtandao waliendekea kununua vifurushi vingine wakidhani vifurushi vyao vya awali vimekwisha na hivyo kuingia hasara mara mbili, yaani kununua kifurushi usichokihitaji na pili kushindwa kukitumia kifurushi hicho.
Ninayataka Makampuni ya data Voda, TiGO, Airtel, Halotel na mengineyo yarudishe pesa zote za wateja za data walizozichukua huku wakijua hawawezi kutoa huduma ya internet kwa wateja.
Huu ni wizi, ni kunufaika kwa kupata pesa ambazo hukuzifanyia kazi. Ni uporaji wa fedha za wananchi.
Tunaitaka Serikali na TCRA ichukue jukumu la kuhakikisha wananchi wanakuwa compensated kwa Vifurushi vya data ambavyo hawakuvitumia mpaka muda ukaexpire.
Siyo wananchi wote walikuwa na VPN, wengine vifurushi vyao vilipotelea hewani, Tunataka kujua hizo pesa zimekwenda wapi na kwa nani.
Lakini pia, kwa wale ambao hawakujua kuwa kuna kuzimwa kwa makusudi kwa mtandao waliendekea kununua vifurushi vingine wakidhani vifurushi vyao vya awali vimekwisha na hivyo kuingia hasara mara mbili, yaani kununua kifurushi usichokihitaji na pili kushindwa kukitumia kifurushi hicho.
Ninayataka Makampuni ya data Voda, TiGO, Airtel, Halotel na mengineyo yarudishe pesa zote za wateja za data walizozichukua huku wakijua hawawezi kutoa huduma ya internet kwa wateja.
Huu ni wizi, ni kunufaika kwa kupata pesa ambazo hukuzifanyia kazi. Ni uporaji wa fedha za wananchi.
Tunaitaka Serikali na TCRA ichukue jukumu la kuhakikisha wananchi wanakuwa compensated kwa Vifurushi vya data ambavyo hawakuvitumia mpaka muda ukaexpire.
Siyo wananchi wote walikuwa na VPN, wengine vifurushi vyao vilipotelea hewani, Tunataka kujua hizo pesa zimekwenda wapi na kwa nani.