Bei za vifurushi vya intaneti kuendelea kuwa juu ni ishara ya kubinywa kwa uhuru wa kutoa na kupata taarifa

Enigmatic_

Member
May 12, 2023
16
13
Sio mbali sana. Ni miaka mitatu kurudi nyuma bei za vifurushi vya intaneti ilikuwa ya kawaida sana. Kwa 1000 mtu angeweza kupata kifurushi cha GB1 kwa wiki. Leo hii, GB1 ni 3000.

Hebu fikiria kwa sasa, ni watu wangapi wameathirika na mabadiliko hayo? Mimi kipindi hicho, kulingana na bei kuwa rafiki, nilipata wasaa mzuri wa kusoma online courses mbalimbali. Lakini kwa sasa imekuwa vigumu. Siwezi kumudu gharama!

Kuna watu wanatengeneza pesa kupitia mtandao. Bloggers na youtubers wanategemea site visitors/viewers ili walipwe. Sasa gharama za vifurushi zinapokuwa juu maana yake automatically watazamaji wanapungua.

Serikali, kwa upande wake ni kama imeziba masikio. Danadana haziishi. Mwaka jana Rais aliagiza bei ziangaliwe lakini sijui hili jambo liliishia wapi.

Hili jambo, kwa upande wangu, naona ni kama njia ya kuzuia uhuru wa kutoa na kupata taarifa, Kitu ambacho ni kinyume na katiba yetu!
 
Kama mafuta, sukari, unga n.k vimepanda bei wapo kimya itakuwa hizo data ili muwasome vizuri na uovu wao.?
 
Mkumbuke pia kuna gharama za kuendesha mitandao. Gharama za vitu zinapopanda na pia gharama za kuendesha mitandao zinapanda.

Unapoona simu yako imeshika network na unapata internet kwa raha... ujue kuna gharama operators wanaingia ili upate hiyo huduma.

Kwa hiyo serikali haiwezi kuingilia tuu na kulazimisha bei zishushwe... wanachoweza kufanya ni kuratibu labda zisiwe za Anasa na kuumiza bila sababu.
 
Sio mbali sana. Ni miaka mitatu kurudi nyuma bei za vifurushi vya intaneti ilikuwa ya kawaida sana. Kwa 1000 mtu angeweza kupata kifurushi cha GB1 kwa wiki. Leo hii, GB1 ni 3000.

Hebu fikiria kwa sasa, ni watu wangapi wameathirika na mabadiliko hayo? Mimi kipindi hicho, kulingana na bei kuwa rafiki, nilipata wasaa mzuri wa kusoma online courses mbalimbali. Lakini kwa sasa imekuwa vigumu. Siwezi kumudu gharama!

Kuna watu wanatengeneza pesa kupitia mtandao. Bloggers na youtubers wanategemea site visitors/viewers ili walipwe. Sasa gharama za vifurushi zinapokuwa juu maana yake automatically watazamaji wanapungua.

Serikali, kwa upande wake ni kama imeziba masikio. Danadana haziishi. Mwaka jana Rais aliagiza bei ziangaliwe lakini sijui hili jambo liliishia wapi.

Hili jambo, kwa upande wangu, naona ni kama njia ya kuzuia uhuru wa kutoa na kupata taarifa, Kitu ambacho ni kinyume na katiba yetu!
Waziri wa sekta ya mawasiliano kazi kuchambana na Wananchi kule X.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Mkumbuke pia kuna gharama za kuendesha mitandao. Gharama za vitu zinapopanda na pia gharama za kuendesha mitandao zinapanda.

Unapoona simu yako imeshika network na unapata internet kwa raha... ujue kuna gharama operators wanaingia ili upate hiyo huduma.

Kwa hiyo serikali haiwezi kuingilia tuu na kulazimisha bei zishushwe... wanachoweza kufanya ni kuratibu labda zisiwe za Anasa na kuumiza bila sababu.
Ni ukweli usiopingika kwamba gharama za maisha zimepanda, na hivyo kuongeza gharama kwenye operesheni. Hapa tatizo ni hiyo gharama kutokuwa rafiki. Hebu fikiria kutoka 1000/1GB mpaka 3000/1GB ?
 
Back
Top Bottom