TCRA: Mawakala wa mitaani ruksa kusajili line za simu

MPUNGA MMOJA

JF-Expert Member
May 30, 2015
304
401
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeondoa zuio la kampuni za simu nchini kuwatumia mawakala kusajili laini za simu mitaani.

Akizungumza Jumatano Aprili 14, 2021 mkurugenzi wa mamlaka hiyo, Dk Jabir Bakari amesema mamlaka hiyo imeondoa zuio hilo na sasa kampuni za simu zitaendelea kuwatumia mawakala kufanya usajili.

Zuio hilo lilitolewa Februari 16, 2021 na utekelezaji wake ulitakiwa kuanza Mei mosi, 2021 ambapo usajili wa laini ulitakiwa kufanyika kwenye maduka ya kampuni husika.

“Kampuni za simu zinaweza kuendelea kuwatumia mawakala bila kuathiri usajili sahihi wa laini kwa mfumo wa kibayometria.”

“Hili litafanyika wakati tunaendelea kufanya tathmini upya ya namna bora inayoweza kutumiwa na watoa huduma kuwasimamia mawakala,” amesema akiwataka mawakala kutumia weledi katika utendaji wao wa kazi.

Chanzo: Mwananchi
 
Hawa TCRA waanze kwanza kutekeleza agizo lao la kushusha bei za vifurushi siyo kuleta maagizo mepesimepesi wakati yale ya msingi wanashindwa kuyasimamia!
 
Kwani nani aliwakataza. Mbona tulikuwa tunasajili tu . Kila rangi tutaona!

Ndio nimeshangaa maana mawakala mitaani wapo kibao wanasajili lines Kama kuna mwendawazimu alizuia inabidi atolewe haraka,haoni kwamba kuna watu wamejiajiri na wanaingiza kipato?
 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeondoa zuio la kampuni za simu nchini kuwatumia mawakala kusajili laini za simu mitaani.

Akizungumza Jumatano Aprili 14, 2021 mkurugenzi wa mamlaka hiyo, Dk Jabir Bakari amesema mamlaka hiyo imeondoa zuio hilo na sasa kampuni za simu zitaendelea kuwatumia mawakala kufanya usajili.

Zuio hilo lilitolewa Februari 16, 2021 na utekelezaji wake ulitakiwa kuanza Mei mosi, 2021 ambapo usajili wa laini ulitakiwa kufanyika kwenye maduka ya kampuni husika.

“Kampuni za simu zinaweza kuendelea kuwatumia mawakala bila kuathiri usajili sahihi wa laini kwa mfumo wa kibayometria.”

“Hili litafanyika wakati tunaendelea kufanya tathmini upya ya namna bora inayoweza kutumiwa na watoa huduma kuwasimamia mawakala,” amesema akiwataka mawakala kutumia weledi katika utendaji wao wa kazi.

Chanzo: Mwananchi
 
Back
Top Bottom