Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,419
- 5,020
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, leo Agosti 10, 2026, amewasilisha Ripoti ya Utendaji ya Robo ya Nne ya Mwaka wa Fedha 2025/26 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikionesha mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya uhalifu wa mitandaoni.
Katika ripoti hiyo iliyochakata kipindi cha kuanzia Aprili hadi Juni 2026, takwimu zinaonesha kuwa matukio ya ulaghai yaliyoripotiwa yamepungua kwa asilimia 25.29 ikilinganishwa na robo iliyopita.
Waziri Kairuki amebainisha kuwa kupungua kwa matukio hayo kumetokana na upekuzi na ukaguzi wa kina uliofanywa na TCRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mbeya, na MaraPamoja na mafanikio hayo, Waziri amewasihi wananchi kuendelea kuwa waangalifu na kutotoa namba zao za siri (PIN), OTP, au kubofya kiungo (link) kisichojulikana.
Aidha, amesema TCRA inaendelea na uhakiki wa usajili wa laini za simu (SIM card verification) ili kuhakikisha usalama wa watumiaji wote katika mazingira ya kidijitali yanayokua kwa kasi nchini Tanzania