TBC1 Inaipendelea CHADEMA na Kuihujumu CCM?

Kwa vile Mbowe aliongea sense ndo maana coverage yake ilipewa uzito! siku moja moja si mbaya kha...
 
Ninachojua Tbc ni ccm damudamu kama wameipendelea cdm leo yawezekana kuna tatizo. Maybe wamecheleweshewa salary wakamind si nasikia siku hz every 23rd salary out.
 
Hii ya leo kuhusu TBC haina ukweli hili li TV ni lakwenu waccm wala msilalamike, kama haikuonyeshwa habari ya Helikopta yenu ccm na uwingi wa watu katika mapokezi ujue hali ilikuwa mbaya sasa hawako tayari kuiaibisha ccm kwa kuonyesha idadi ndogo ya washabiki waliokuwepo.

Kwa taarifa tu ni kwamba nimeiacha kuangalia TV la ccm wiki imepita sasa, kwa hiyo uyasemayo wewe si ya kweli!!!!!!!!!!!.
 
Ninachojua Tbc ni ccm damudamu kama wameipendelea cdm leo yawezekana kuna tatizo. Maybe wamecheleweshewa salary wakamind si nasikia siku hz every 23rd salary out.

idadi ya waganga njaa waliokuwa wanaisubiri chopa laccm lilikuwa chini sana mpaka wakaona aibu kuionyesha hiyo picha kwenye tarifa ya habari na bado. CCM wamebanwa kaskazini,kusini mashariki na hapo magharibi tukiwabana anzeni kuondoka wenyewe ikulu.
 
Jana saa mbili usiku nilikuwa nikiangalia taarifa ya habari ya TBC1 na habari kuu jana ilikuwa ni kutua kwa mahelkopita huko Igunga kwa ajili ya kutumika katika mikutano ya kampeni. TBC1 walionyesha helkopita ya CCM ikitua na Makamba akapokelewa na Mwigulu na watu wengine. Kisha ikaonyeshwa kwa UFUPI SANA Mwigulu akihutubia na kisha makamba akasikika akisema maneno mawili matatu tu basi. Pia TBC1 haikuonyesha UMATI wa watu ambao hao viongozi wa CCM walikuwa wakihutubia!! Kwa kifupi coverage kwa CCM ilikuwa kidogo sana.

Kisha nikashuhudia coverage ya CHADEMA. Walianza kuonyesha helkopita ikiwa angani na maneno CHADEMA yakionekana, kisha wakaionyesha helkopita ikiwa eneo fulani ambalo naamini ni kituo cha mafuta ikiwa inakunywa mafuta. Baada ya hapo helkopita ya CHADEMA ikaonyeshwa ikitua huko Nkinga na Mwenyekiti wao akashuka na kuhutubia. Kinyume na walivyo cover hotuba ya CCM, hapa Mbowe alipewa muda mreeefu akihutubia kuhusu mambo ya siasa na dini na wakati huohuo TBC1 ikionyesha umati wa watu ambao Mbowe alikuwa akihutubia. Baada ya hotuba TBC1 walionyesha helkpita ya CHADEMA ikituka kuondoka eneo la mkutano.

Kwangu mimi naona TBC1 hawakuitendea haki CCM kwa kuipa coverage kidogo sana hasa juu ya helkopita ambayo imegeuka kuwa ni kete ya kisiasa huko Igunga. Pia TBC1 hawakumuonyesha mpambanaji Magufuli wakati akiunguruma huko Igunga.

Kimbunga you know what?

TBC1 walionyesha uhalisia wa mambo yalivyokuwa jana kule Igunga. Camera zao zilimwonyesha Nnape cjui na Januari wakiteremka kwenye Chopa lakini hawakuonyesha umati wa watu waliohudhuria pale MAANA HAUKUWEPO!! Wewe ulitegemea waelekeza camera kwenye miti na uwanja mtupu?Waliona aibu maana hakukuwa na watu.

Lakini Mbowe alipotua na Chopa ule UMATI ULIKUWA NI WA KUFA MTU. Nilifurahia sana taarifa ya TBC1 jana jioni maana walionyesha HALI HALISI BILA KUCHAKACHUA. Tunataka coverage ya namna hii mpaka siku ya kupiga na kuhesabu kura.
Big up TBC1!
 
siyo kwamba wamefanya hivyo kwa bahati mbaya bali wana malengo yao lengo kuu nikuwapa nafasi ccm siku ya mwisho ya kampeni ilikuongeza mhemko..pili alicho kuwa anakiongea mbowe ni swala la kitaifa ambalo kila mtanzania angependa kulisikia kutoka kwa kiongozi wa juu hasa xhama tawala akiliongelea kwa hisia kali tofauti na wanavyofanya magamba wanalifanya mtaji wa kujiatia kura bila kujari madhara yatokanayo na kampeni zao hizo chafu..

Mkuu umeona mbali, nakuunga mkono.
 
Moderator alijisahau. Nadhani jana alipewa barua ya onyo.
 
Kimbunga you know what?

TBC1 walionyesha uhalisia wa mambo yalivyokuwa jana kule Igunga. Camera zao zilimwonyesha Nnape cjui na Januari wakiteremka kwenye Chopa lakini hawakuonyesha umati wa watu waliohudhuria pale MAANA HAUKUWEPO!! Wewe ulitegemea waelekeza camera kwenye miti na uwanja mtupu?Waliona aibu maana hakukuwa na watu.

Lakini Mbowe alipotua na Chopa ule UMATI ULIKUWA NI WA KUFA MTU. Nilifurahia sana taarifa ya TBC1 jana jioni maana walionyesha HALI HALISI BILA KUCHAKACHUA. Tunataka coverage ya namna hii mpaka siku ya kupiga na kuhesabu kura.
Big up TBC1!

mkuu makoye, baadhi yetu (yawezekana na wewe uko kwenye kundi hili) si waumini sana wa flamboyance and show-offs. ni waumini wa modesty and efficiency.

perhaps crazy (but frank) questions from me...... ni nini impact ya the likes of tbc1 kule igunga kwa context uliyoiweka hapo juu kwenye nyekundu? hizi tv clips zinaweza ku-influence vipi na kwa kiasi gani mustakabali wa mosi, turn out kwenye polling stations na pili, matokeo yenyewe?

mimi ninadhani impact yake zaidi ni kutoa matumaini (ambayo yanaweza kuwa sahihi au kinyume chake) kwa viongozi na followers wa vyama husika walioko igunga na kwingineko kuliko uhalisia wa kitakachotokea kwenye polling day.
 
Back
Top Bottom