TBC Kufunga matangazo yake wakati wowote kutoka sasa

Zacharia hupokelewi star tv, ulitoka kwa mbwembwe ukidhani umepata kumbe umepatikana, karibu kijiweni
 
Nazidi kuamini kile nilichokuwa naamini ya kuwa chombo, mtu na kitu chochote kinachotumika na ccm kwa ajili ya kuilinda na kutetea mabaya ya ccm hakidumu na huwa kinapotea mapema sana kwenye uso wa dunia
 
Taarifa ya habari saa mbili,

Nkamia akimwombea mwajiri wake wa zamani fedha toka serikali amesema TBC itafunga matangazo yake wakati wowote kuanzia sasa, akithibitsha hali hiyo amesema hawana kamera, vifaa vya kuchanganya matangazo hawana na kwamba 1.2 bilioni waliyopewa ni kwa umeme na millioni 500 ni ndogo walizopewa za uendeshaji

My Take:
Ni heri TBC ifungwe kwani haitusaidii kitu wanaendekeza libeneke la kuminya demokrasia

Hata hizo walipewa ilitakiwa CCM ndio wazitoe maana wao ndio wanaonufaika nayo kwa 99%!
wananchi kwa mtazamo wangu wananufaika kwa 1% kwenye kupunguza mawazo kwenye vipindi vya Bango na chereko chereko!
 
kwani TV zingine zinazojiendesha kibiashara zinawezaje?

Si wawaombe ushauri wengine.

Kuna vitu vingine huwa sielewi kabisa.

kweli kabisa, ila mimi nadhani ni visasi. Lakini at what cost?
Uzalendo kidogo tu hata kwa kazi inayokutunzia familia huwezi?
Kampuni zinaanza mradi wa tv kw mtaji mdogo zaidi ya huu walio nao tbc, na wanaendela na kuwa giants. Hii ni hila ya kijinga sana.
 
its like nightmare,TBC wana gharama kubwa za matangazo kuliko TV zingine iweje wao washindwe wakati wengine wana make money.Au matangazo ya serikali ni free na ya CCM.
 
Safi sana haina tija kwa watanzania,wamekaa kiupendeleo sana na ngoja peopl's power tuchukue madaraka 2015 tutasafisha kabisa pale,hatuhitaji watu ambao wananizamu za woga katika taasisi yoyote ya serikari.nawasihi waalimu wezangu wakae imara katika kumwaga suma kwa watoto.
Peopl's.............,
cdm vema,
vijana nguvu ya mabadiliko.
"kamata mwizi men"
 
Mbona pesa ya kuhonga kijingajinga Arumeru wanayo!?
Mbona Pesa ya kuwalipa mamia ya UWT Arumeru wanayo!?
NK
 
its like nightmare,TBC wana gharama kubwa za matangazo kuliko TV zingine iweje wao washindwe wakati wengine wana make money.Au matangazo ya serikali ni free na ya CCM.

Nimekuja gundua kuna watu wana masihara sana na kodi zetu.., hiki kituo kinaendeshwa kwa ruzuku, on top of that wanapata pesa za matangazo.., na mkataba wa startimes,,

Ndo matatizo ya kuingiza siasa kwny kuchagua watendaji.., waliona tido ni mwiba kwa ccm wakaweka kada wao pale.., ndo matokeo yake haya..,

itv ina almost two decades sasa, inajiendeshaje?? Hapo tbc ni lazma kuna embezzlement ya hali ya juu..,

Yani kweli hata c2c wanawashinda kweli na wakati mikoani huko hawaijui!!

Soln..., piga chini management yote, wawekwe watendaji creative with intergrity, na waache kituo kisiendeshwe kisiasa..., God damn! Aaaggh! Kuna mambo yanakera!
 
Duh, hii itakuwa noma sana. Pale kuna watu wengi wanategemea kuendesha maisha yao na familia. Kuna kila sababu ya kuangaliwa kwa umakini
 
Nakumbuka private tv stations walisha-raise issue ya TBC kurusha matangazo ya biashara huku wakiwa wanapewa ruzuku na kuomba either wapewe ruzuku tu au wasipewe ruzuku na kushindana na vyombo binafci kwa matangazo.. Serikali ikakataa.. Laana imewakuta..
Mkuu, hilo waliloomba TV binafsi ndilo ambalo lilipaswa kufanyika na ndilo linalofanyika kwa kawaida kwenye vyombo vya habari vya umma - kwa kuwa wanapatiwa ruzuku na serikali vinapaswa kujitoa kwenye ushindani, hasa ukitilia maanani kuwa hivyo vyombo binafsi baadaye vinatozwa kodi.

Kinachozidi katika TBC ni ubovu wa utendaji, ubadhirifu na kinachokosekana ni ukosefu wa ubunifu. TBC kama wangekuwa wabunifu wangeweza hata kujiendesha wenyewe kwa kuandaa na kuuza vipindi, filamu, documentries, kushirikiana na watu/vyombo binafsi katika utengenezaji wa filamu, uuzaji wa series na machapisho yao wenyewe kutoka maktaba zao....lakini wamekaaa hapo kama beki tatu.
 
Ndoto za kichaa na mwendawazimu we Television ya taifa inawezaje kufungwa wakati ndicho chombo kikuu cha kiserikali
 
Ndoto za mchana tena za mwendawazimu, we tokea lini kituo cha taifa cha habari kikafungwa. Nchi yoyote inategemea media za serikali kama source ya kufikisha ujumbe wa kiserikali na kuzima propaganda mbali mbali. Mapinduzi yote ya kijeshi yatokeapo miongoni mwa mambo ya awali ni kuchukua vituo vya matangazo vya kijeshi kwa hiyo ni ndoto kusema kituo kama hiki chenye umuhimu wa aina yake KIFE.
Kweli JF kuna wafalme juha wengi wenye ndoto za abunuwasi
 
Tuwahurumie akina Gabriel Zakaria, Kingalame na akina Marin H Marin jamani watakwenda wapi?
 
Ndoto za kichaa na mwendawazimu we Television ya taifa inawezaje kufungwa wakati ndicho chombo kikuu cha kiserikali

Serikali kama imeshindwa kuki-run unategemea kitu gani. Hv kama vitu nyeti kama umeme serikali imeshindwa kulipa how about TV
 
imechelewa kufa tena kifo cha mende
Irudishwe kuwa mali ya Umma itafufuka
waige ya KBC na BBC haiko mikononi mwa wizara bali umma
 
Ndoto za mchana tena za mwendawazimu, we tokea lini kituo cha taifa cha habari kikafungwa. Nchi yoyote inategemea media za serikali kama source ya kufikisha ujumbe wa kiserikali na kuzima propaganda mbali mbali. Mapinduzi yote ya kijeshi yatokeapo miongoni mwa mambo ya awali ni kuchukua vituo vya matangazo vya kijeshi kwa hiyo ni ndoto kusema kituo kama hiki chenye umuhimu wa aina yake KIFE.
Kweli JF kuna wafalme juha wengi wenye ndoto za abunuwasi

Ungefanya research kidogo ungegundua Serikali ilianzisha tv Station wakati wa utawala Ben.. Na Sumaye ndo aliekuwa mfuatiliaji.. Kwa hiyo kuanzia utawala wa mwinyi na kurudi nyuma hatukuwa na National tv yeyote.. Kwa hiyo kama iliwezekana wakati huo itawezekana hata sasa.. Kwa mliozoea kubebwa ndo itawawasha sana.. Kuwaita watu majuha sishangai.. Ndo nature yenu..
 
CCM Broadcasting Corporation a.k.a TBC. Nape si muwamegee katika hizo 1.2 bilioni za ruzuku.
 
Back
Top Bottom