Kitu kikubwa cha kushangaza ni kwa nini Muro apewe special treatment ya kiasi hiki kwani swali kubwa ni jee hawezi akawa naye ni tapeli tu kwa kutumia mwanya wa yeye kuonekana mpiganaji mahiri wa rushwa?
Wangapi tunao ktk serikali wanaotaka kujitambulisha kuwa ni wapinga ufisadi kumbe ni hypocrites tu nao wamo? Ndugu zangu, haya yanawezekana sana tu.
Lakini tuangalie kwanza masuala ya msingi. Jee TBC ambako Muro aliko hivi sasa yaani chombo cha serikali ina dhamira ya dhati ya kuendesha kwa dhati vita dhidi ya rushwa rushwa ya wakubwa? Ni kama vile uniambie kuwa Daily News inaweza ikawa mstari wa mbele katika vita ya kupinga ufisadi hasa ufisadi wa wakubwa.
Muro alikuwa ITV na alihama kwenda TBC kwa ushawishi wa wakubwa akina manji, tanil Somaya na mafisadi papa wengine kwa misingi ya uhamisho wa wale wasanii wa Ze Comedi. Lengo ni kupunguza makali waliyokuwa nayo wakiwa ktk vyombo binafsi, hasa vya IPP ambavyo msimamo wao kuhusu ufisadi wa wakubwa unajulikana.
Ze komedi sasa hivi wamekwisha, wanaigiza rushwa za manesi na matrafiki -- siyo za wakati ule za akina Karamagi wanasaini mkataba wa Buzwagi ktk chumba cha hoteli moja ya London. Siku hizi hawawezi tena kuigiza vitu vya namna hiyo, wamekatwa makali na akina manji aliyewanunua na kuwapeleka TBC. Siku hizi wamebakia kuvaa sidiria na kuandama makarani etc.
Muro naye ni vivyo hivyo, alipelekwa TBC na hao hao mafisadi papa ili asiwe anawagusa, na badala yake awe anawaandama matrafiki na manesi tu.
Kwa hiyo ile dhana ya kusema Muro alikuwa anapambana na mafisadi papa ni dhihaka kubwa.
Na suala la kwa nini polisi, na siyo PCCB, wanalishughulikia suala hili linatokana na matashi ya mlalamikaji, Wage, na bila shaka alikuwa ana sababu zake za kutokwenda kulalamika kwa akina Hosea. Tunajua jinsi Hosea anavyoshughulikia rushwa hasa za wakubwa. Anawalinda sana ni taasisi ya hovyo kabisa kuhusu grand corruption.
Suala la pingu ndilo linaweza kumponza Muro kama hatalitolea maelezo ya kuridhisha kwa nini alikutwa nazo. Kwa kumtaka atoe risit, polisi wamefanikiwa kum-tie kwamba ni zake a very important step. Muro angeweza kushikilia siyo zake aliwekezewa tu na polisi.
Kuna wachangiaji humu ndani, na baadhi ya magazeti wanaona kuwa kwa vile ameonyesha risiti, basi hana kosa! Nashangaa hata MMKJJ katumbukia ktk ushabiki wa wazi wazi wa kumtetea Muro pamoja na kwamba kesi haijaenda mahakamani kwenye maamuzi ya sheria.
Kiuchunguzi wa polisi, Muro anatakiwa atoe maelezo ya pingu hizo, za kazi gani kwake anatembea nazo ktk gari. Kujilinda? Bastola sawa kwa ajili ya kujilinda. Lakini pingu? Hivi peke yake Muro anaeweza kumtia pingu mtu kiurahisi? Polisi wamefundishwa namna ya kumtia mtu pingu.
Halafu yeye ni mwanahabari tu, na maadili ya taaluma hiyo yanasisitiza mwandishi kuwa wazi katika kutafuta habari, asijifiche (asiji-conceal) identity yake na wala asitumie silaha ya aina yoyote. Hata hiyo bastola yake, asiitumie kukamua habari, ni ya kujilinda tu anapotishiwa maisha.
Jamani tujaribu kuwa objective. Na kama Muro ni shushushu kama wengine wanavyohisi, basi serikali inayo uwezo wa kusimamisha upelelezi na kuifutilia mbali kesi ili kumlinda. Hawa mashushushu nao hawaaminiki, nasikia walihusika pia ktk ufisadi wa EPA.