Ok ila Pia Yesu hakusema kuwa Wote ni Manabii wa Uongo... ila alitupa Sharti kuwa Tutawatambua kwa Matendo yao..
sajumo
Maana kama Tutaendelea kusema kuwa Yesu alisema watakuja manabii wa Uongo na sisi Kila Tumuonapo Mtumishi anahubiri na kufanya miujiza Tukasema waongo basi Duniani hakutakuwa na Ukombozi wowote ule alioleta Kristo maana kuna Mambo ambayo Binadamu hatuwezi kuponya Au kuyatatua ila Yesu Kristo Pekee. Sasa kama wote ni Wa uongo basi hakuna Ukombozi au Ishara ya Kuwa Bado Yesu Yu hai nasi.
Kwahiyo inabidi tusikurupuke tu na Kusema kuwa ni Nabii wa Uongo ila tuchunguze kuwa kama Yatoka kwa Mungu wa ukweli ambaye ni Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo kwa Kuangalia Matendo yao na Kuuliza baadhi ya Waumini wa karibu na kusikiliza Testimonies mbalimbali na kuzichunguza kama ni za kweli au ni maigizo tu..
MFANO
Nabii wa Uongo siku zote hadumu. Utamjua tu kama ni Mpenda Sadaka, Mwongo, Anaabudu Sanamu (pesa, usherati, mchawi ). Anatumia Nguvu za Giza kutuliza Mapepo si kuyatoa n.k
Hawa wahubiri wapo hapa Tanzania na tunawafahamu..
ubarikiwe sana kwa ufafanuzi mzuri
Last edited by a moderator: