Emmanuel TV nimekuwa naiangalia kwa muda mrefu sasa, nadhani kabla watu wengi wa humu jamvini hawajaanza kuitazama. Je unakumbuka siku moja hiyo TV ilitoa kioja eti mwanamke aliyepimwa hospital kuwa ana uvimbe kwenye tumbo la uzazi na alipokuja kwa maombi basi ule uvimbe ukaanza kumtoka kupitia sehemu zake za siri na TV ikawa inaonyesha live. Naona anaona alifanya kioja siku hiyo ndio maana siku hizi anasema huo uvimbe unayeyuka kwa jina la Yesu. Mbona wakati ule haikuwa hivyo? Amejifunza kuwa watu walimshangaa. Kuna maswali machache kuhusiana na huduma ya TBJ ambayo hakuna mfuasi wake anawezakutoa jibu . Maana yake ni kwamba hata hao wafuasi wake wana mashaka. Inaelekea wafuasi wengi wa TBJ hawajasoma Bible kwanza na wanakuja moja kwa moja kukutana naye ndio maana wanashindwa kuhoji anayoyafanya. Ufahamu kuwa hata kama kweli kuna mijuiza inayofanyika kwenye sinagogi lake SIO LAZIMA ITOKE KWA MUNGU, HATA SHETANI ANAFANYA MIUJIZA VILEVILE. Petro na Yohana wlipofika mlangoni mwa hekalu wakakuta kiwete anaomba pesa walimponyesha, lakini huyu jamaa watu wanakuja kwenye sinagogi lake wakiwa viwete anawapa mchele na pesa. Haya wafuasi wa TBJ kwa nini asiwatibu kama wale mitume wa Yesu? Wale viwete anaodai kuwaponyesha wanaonyeshwa kwenye TV kuanzia wanapoanza kuingia mlangoni mpaka wanapokaa na hata muda unaoitwa wa uponyaji, kama sio fix ni nini? Biblia inasema imani huja kwa kusikia Neno la Mungu sio kusikia shuhuda. Sasa huyu mtaalam TBJ muda mrefu ni shuhuda na unabii neno linasomwa chini ya 5% ya muda wa TV. Na hata anapofafanua neno la Mungu, kwa mtu aliyeisoma hiyo Bible kisawasawa anabaki na maswali mengi ya kujiuliza kuhusu uelewa wa huyo anayejiita nabii. Yesu alipoponyesha watu aliwaambia wasimweleze mtu, mbona TBJ muda wote ni testimony? Toeni majibu. Anointing water ya zamani na ya sasa zina tofauti gani, ni katika maombi au ni katika materials? Sisi Wakristo tumeonywa kuwa ukimwona mtu anaangamia ukamwacha bila kumpa tahadhari basi ujue damu yake itakuwa juu yako. Wale wafuasi wa TB Joshua nawapa tahadhari kuwa mnayemfuata hana uhusiano na utumishi wa Mungu aliyeainishwa katika Bible, labda mungu mwingine ambaye Amri ya kwanza ya Mungu wa Bible inakataza kabisa kumwabudu.
Wewe ni mkristo...I second you.
Siku Ukijitambua Utamjua Tb Joshua Ni Mtumishi Wa Mungu, Kama Hujawahi Kumsikiliza Na Kusoma Bible Utapga Porojo Najua Kwakua Unaongozwa Na Mapepo, Tangu Lini Jambazi Akamsapoti Mtumish Wa Mungu
Emmanuel TV nimekuwa naiangalia kwa muda mrefu sasa, nadhani kabla watu wengi wa humu jamvini hawajaanza kuitazama. Je unakumbuka siku moja hiyo TV ilitoa kioja eti mwanamke aliyepimwa hospital kuwa ana uvimbe kwenye tumbo la uzazi na alipokuja kwa maombi basi ule uvimbe ukaanza kumtoka kupitia sehemu zake za siri na TV ikawa inaonyesha live. Naona anaona alifanya kioja siku hiyo ndio maana siku hizi anasema huo uvimbe unayeyuka kwa jina la Yesu. Mbona wakati ule haikuwa hivyo? Amejifunza kuwa watu walimshangaa. Kuna maswali machache kuhusiana na huduma ya TBJ ambayo hakuna mfuasi wake anawezakutoa jibu . Maana yake ni kwamba hata hao wafuasi wake wana mashaka. Inaelekea wafuasi wengi wa TBJ hawajasoma Bible kwanza na wanakuja moja kwa moja kukutana naye ndio maana wanashindwa kuhoji anayoyafanya. Ufahamu kuwa hata kama kweli kuna mijuiza inayofanyika kwenye sinagogi lake SIO LAZIMA ITOKE KWA MUNGU, HATA SHETANI ANAFANYA MIUJIZA VILEVILE. Petro na Yohana wlipofika mlangoni mwa hekalu wakakuta kiwete anaomba pesa walimponyesha, lakini huyu jamaa watu wanakuja kwenye sinagogi lake wakiwa viwete anawapa mchele na pesa. Haya wafuasi wa TBJ kwa nini asiwatibu kama wale mitume wa Yesu? Wale viwete anaodai kuwaponyesha wanaonyeshwa kwenye TV kuanzia wanapoanza kuingia mlangoni mpaka wanapokaa na hata muda unaoitwa wa uponyaji, kama sio fix ni nini? Biblia inasema imani huja kwa kusikia Neno la Mungu sio kusikia shuhuda. Sasa huyu mtaalam TBJ muda mrefu ni shuhuda na unabii neno linasomwa chini ya 5% ya muda wa TV. Na hata anapofafanua neno la Mungu, kwa mtu aliyeisoma hiyo Bible kisawasawa anabaki na maswali mengi ya kujiuliza kuhusu uelewa wa huyo anayejiita nabii. Yesu alipoponyesha watu aliwaambia wasimweleze mtu, mbona TBJ muda wote ni testimony? Toeni majibu. Anointing water ya zamani na ya sasa zina tofauti gani, ni katika maombi au ni katika materials? Sisi Wakristo tumeonywa kuwa ukimwona mtu anaangamia ukamwacha bila kumpa tahadhari basi ujue damu yake itakuwa juu yako. Wale wafuasi wa TB Joshua nawapa tahadhari kuwa mnayemfuata hana uhusiano na utumishi wa Mungu aliyeainishwa katika Bible, labda mungu mwingine ambaye Amri ya kwanza ya Mungu wa Bible inakataza kabisa kumwabudu.
Sasa Yupi ni wa Kweli. . AU hawapo Duniani?
yesu alishasema kutakuja kuwapo na manabii wa uwongo( T B JOshua) nao wataonesha ishara za maajabu
cshanga kuona mkristo akiangukia kwa mpuuz ka tb josh coz najua aidha ni mvivu kusoma bible au hafuat mafundisho ya bble