Tb Joshua alivyonipa utajiri

Tb Joshua alivyonipa utajiri

Ukiangalia kwa undani hawa wanajiita walokole samahani sana wale nitakaowagusa ila ni ukweli, wengi wao ni walongo,walozi na wazandiki wakubwa lakini ukiwaona wanalia iiiiii utajua kweli ni watu wa maana na kwamba kweli wanamjua Mungu!!!ila ni watu walongo na wanapotosha sana, naamni siku ya mwisho lokoles wengi wataungua...
 
teh teh...ayo maji jinsi yanavyo uzwa km karanga uko nigeria nahisi wote wangekua km ww CHACHA..samahani eti restaurant yako watu wameja mpaka chooni wapo radhi wale na divi uku wengine wakikata GOGO
 
Heading yako iko vizuri kuwa TB Joshua amekupa utajiri. Umekosea hapo mwishoni ulipomtaja Yesu kwani hakuna uhusiano wa anointing water na Neema ya Bure iliyotolewa na Yesu Kristo wala haiuzwi kwa bei yeyote. Hiyo anointing water ni ibada ya sanamu na ushirikina ambayo chanzo chake ni shetani. Shetani anasema ukinisusujudia na kunitumikia nitakupa milki yote ya dunia. Yesu anasema tafuteni kwanza ufalme wa mbinguni na haki yake na hayo yote mtazidishiwa...hapo usimmsingizie Yesu.

"..nanyi hamfahamu ya kuwa nyumba ikigawanyika yenyewe ndani yake, haiwezi kusimama..? Marko 3:25.."

Haya ndiyo maneno Yesu aliyowaambia mataifa waliodhani ya kuwa alikuwa akitoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo (Beelzebuli).
 
Walewale

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
tuna waasibu humu alafu anatupa hesabu ambazo sio

Nimejaribu kutumia profesheno yangu nimesindwa. Hiyo mil 240 ni faida kwa miezi 4,tuchukulie hiyo faida ni 30% ya mauzo yake yote kwa miezi 4 tunapata jumla ya mauzo(turnover) yake yote ni 800m kwa kila mwezi 200m,kila siku 6.7 mil. Huo mgahawa unaouza 6.7 mil kwa siku unapatikana nchi hii,basi ni noma INNOCENT CHACHA. Tafta njia nyingine ya kudanganya. Twambie uko wap huo mgahawa na unaitwaje.
 
Last edited by a moderator:
TB Joshua ni mchawi tu kama wengine huko Nigeria.

Bora sisi wapagani
 
Kwa mwanadamu haiwezekani lakini kwa MUNGU yote yanawezekana. ili muujiza Uitwe muujiza lazma kuwe na kitu extraordinary yaaani kipitacho ufahamu na reasoning ya mwanadamu na ndicho kilichotokea kwa Huyu jamaa. Ndo maana watu mnabakia kushangaa shangaa tu
 
Mi celewi kbsa nmechanganyikiwa ukwel ni upi sasa yesu pia alifanya miujuza kama kufanya ile mikate na samaki kuliwa na wengi..kutuliza bahari na wanafunzi wake walipovua walipata samaki wengi lakini pia biblia inaonya juu ya manabii Waongo mm
 
kama utakumbuka, miezi miwili iliyopita nilikuja na post juu ya kutoa shukrani kwa yesu kwa kumtumia mtumishi wa mungu tb joshua kuniponya tatizo langu la uvimbe sehemu za siri ambalo lilikuwa likinifanya kushindwa kusimamisha uume wangu kwa miaka zaidi ya 4. Uponyaji wa tatizo langu ulifanyika kupitia maji maarufu ya anointing water yanayoandaliwa na kutolewa na tb joshua ministries.

Leo nataka nikushirikishe juu ya jinsi maji hayo yalivyonipa fusso 2, coaster 3, nyumba 2, na restaurant 3.

Nilianza biashara yangu miezi 4 iliyopita. Kalikuwa ni kamgahawa kadogo tu lakini kwasababu niliamini kwenye nguvu iliyomo ndani ya yesu, sikuwa na hofu yoyote kuwa mafanikio yanakuja.

Kabla ya hapo, nilisikia shuhuda za watu mbaimbali ambao walitajirika baada yakutumia anointing water kwa imani. Nikaamua kuyatumia haya maji kwenye biashara yangu kwa imani kubwa. Nilichokifanya ni kupuliza haya maji kwenye milango na makabati ya chakula huku nikiamrisha wateja wafurike kwenye biashara yangu kwa jina la yesu.

Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2. Watu wanajaa kwenye restaurant hadi nikaamua kuweka viti na meza eneo la jikoni na bafuni. Wateja wako radhi hata kula huku wamesimama au wamechuchumaa. Inapofika muda wakufunga huwa inabidi niwafukuze wateja vinginevyo tunaweza kukesha.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

Asante yesu. Asante tb joshua

better is not good enough best is yet to come

sty tuned mpendwa.....nikupe ushuhuda nilitoa hapa ...nilitoka kwenye kampuni moja kwa mpango wa redenders nikapata kampuni moja kule arusha lakini ikiwa arusha ..nikawa kila ijumaa napanda gari la magazeti kuja na kurudi jumapili...nikapata ajali moja na hilo gari nilipona nikamshukuru mungu ...ijumaa yake ilikuwa mwisho wa mwezi nikaandika resignation letter nikaomba wasinilipe mshahara ...nikarudi dar kuona familia yangu

nilikaa wiki nikimuuliza mungu kama ni mpango wako basi nipate kazi dar......baada ya wiki mbili jumamosi dady ...tb joshua akiwa anahubiri akasema kwenye tv viewers all over the word naona kuna watu wana shida kwenye ndoa zao pesa..na kazi...akaanza wale wenye shida na kazi ...remove your past pic put your new pic in the office...akasema tuanze kuchora niko ofisini ,,niko na secretary na wengineo nikiwaongoza...baada ya kuchora akasema tuombe tukaomba

LEO UKIFIKA NYUMBANI KWANGU KUNA PIC KAMA SANAMU NIMECHORA MTU YUKO OFISINI NA SECR PEMBENI NIMEBANDIKA UKUTANI NI MI NA FAMILIA YANGU WANAJUA UMUHIMU WA ILE PIC

aikuwa kiini machompendwa baada ya wiki mbilinikaitwa kwenye kampuni moja nzuri tu ...kwenye interview baada ya hapo nikiwa kwenye interview nikakumbuka msemo wa dady una kemea na kuamuru adui zako wote washindwe kwa jina la yesu....


Tukiwa saba ilipofika saa saba mchana tukaitwa wanasubiri hr wa kampuni husika kutoka kenya

anatua saa tisa kumbe kuna watu walikimbia job wanaingia sananee...ilipofika saa nane tukabaki 4

ilipofika saa kumi tukaambiwa tuelekee serena hotel...waliposema vile wawili wakatoa all the best jamani sisi tunawahi kazini aikuwa mapenzi ya mungu

serena tukabaki wawili...tulipofika pale...kwenye itnerview tu kutaja jina langu kila mtu anashtuka

akaanza kusema kweli wewe unatufaa mwenzangu alipoitwa..tukasubiri hukumu

baada ya dk 25 wakatuita wakasema nimechaguliwa kuwa mana..... Na mungu ambariki mana of GOD TB JOSHUA

rember better is not good enough best is yet to come
 
Kwa mwanadamu haiwezekani lakini kwa MUNGU yote yanawezekana. ili muujiza Uitwe muujiza lazma kuwe na kitu extraordinary yaaani kipitacho ufahamu na reasoning ya mwanadamu na ndicho kilichotokea kwa Huyu jamaa. Ndo maana watu mnabakia kushangaa shangaa tu

Mungu akubariki mkuu!
 
Kama utakumbuka, miezi miwili iliyopita nilikuja na post juu ya kutoa shukrani kwa Yesu kwa kumtumia mtumishi wa Mungu TB Joshua kuniponya tatizo langu la uvimbe sehemu za siri ambalo lilikuwa likinifanya kushindwa kusimamisha uume wangu kwa miaka zaidi ya 4. Uponyaji wa tatizo langu ulifanyika kupitia maji maarufu ya ANOINTING WATER yanayoandaliwa na kutolewa na TB JOSHUA MINISTRIES.

Leo nataka nikushirikishe juu ya jinsi maji hayo yalivyonipa FUSSO 2, COASTER 3, NYUMBA 2, na RESTAURANT 3.

Nilianza biashara yangu miezi 4 iliyopita. Kalikuwa ni kamgahawa kadogo tu lakini kwasababu niliamini kwenye nguvu iliyomo ndani ya Yesu, sikuwa na hofu yoyote kuwa mafanikio yanakuja.

Kabla ya hapo, nilisikia shuhuda za watu mbaimbali ambao walitajirika baada yakutumia ANOINTING WATER kwa imani. Nikaamua kuyatumia haya maji kwenye biashara yangu kwa imani kubwa. Nilichokifanya ni kupuliza haya maji kwenye milango na makabati ya chakula huku nikiamrisha wateja wafurike kwenye biashara yangu kwa jina la Yesu.

Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2. Watu wanajaa kwenye restaurant hadi nikaamua kuweka viti na meza eneo la jikoni na bafuni. Wateja wako radhi hata kula huku wamesimama au wamechuchumaa. Inapofika muda wakufunga huwa inabidi niwafukuze wateja vinginevyo tunaweza kukesha.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

ASANTE YESU. ASANTE TB JOSHUA

Acha kudanganya umma.huu ni uongo uliopitiliza kabisa
 
Kama utakumbuka, miezi miwili iliyopita nilikuja na post juu ya kutoa shukrani kwa Yesu kwa kumtumia mtumishi wa Mungu TB Joshua kuniponya tatizo langu la uvimbe sehemu za siri ambalo lilikuwa likinifanya kushindwa kusimamisha uume wangu kwa miaka zaidi ya 4. Uponyaji wa tatizo langu ulifanyika kupitia maji maarufu ya ANOINTING WATER yanayoandaliwa na kutolewa na TB JOSHUA MINISTRIES.

Leo nataka nikushirikishe juu ya jinsi maji hayo yalivyonipa FUSSO 2, COASTER 3, NYUMBA 2, na RESTAURANT 3.

Nilianza biashara yangu miezi 4 iliyopita. Kalikuwa ni kamgahawa kadogo tu lakini kwasababu niliamini kwenye nguvu iliyomo ndani ya Yesu, sikuwa na hofu yoyote kuwa mafanikio yanakuja.

Kabla ya hapo, nilisikia shuhuda za watu mbaimbali ambao walitajirika baada yakutumia ANOINTING WATER kwa imani. Nikaamua kuyatumia haya maji kwenye biashara yangu kwa imani kubwa. Nilichokifanya ni kupuliza haya maji kwenye milango na makabati ya chakula huku nikiamrisha wateja wafurike kwenye biashara yangu kwa jina la Yesu.

Huwezi kuamini, mauzo yalibadilika kutoka shs laki 2 kwa siku hadi milioni 2. Watu wanajaa kwenye restaurant hadi nikaamua kuweka viti na meza eneo la jikoni na bafuni. Wateja wako radhi hata kula huku wamesimama au wamechuchumaa. Inapofika muda wakufunga huwa inabidi niwafukuze wateja vinginevyo tunaweza kukesha.

Ndani ya miezi 3, nimejenga nyumba 2, nimenunua coaster 3, fusso 2 na niko mbioni kufungua restaurant nyingine 2.

ASANTE YESU. ASANTE TB JOSHUA

Inawezekana umepata uponyaji na hizo baraka, lakini hayo mafanikio unayosema hata mtoto wa darasa la kwanza huwezi kumdanganya. Lete hapa mapato na matumizi na jinsi ulivyoweza kununua hayo magari na kujenga hizo nyumba kwa miezi mitatu. Labda nyumba ya udongo. weka picha za nyumba.
 
Tatizo ni umaskini wa akili na roho. Unadhani wote ni maskini wa akili kama wewe? Tuambie na kodi unalipa shilingi ngapi?
 
Mungu atusaidie, mi huwa najiuliza ivi kuna haja ya kuusaka utajiri kiasi hiki.Mbona katika bibilia watumishi wengi wa Mungu walikufa maskini tu.Watumishi wa Mungu wa enzi izi washajua watu wanataka uponyaji na utajiri.Basi kila anaefungua kanisa anaelekeza nguvu zake uko.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom