DOKEZO Tabata Bonyokwa hatujaona tone la maji wiki ya tano sasa, DAWASA mnatuona manyani?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,076
4,113
Ni mambo ya ajabu sana huku tulipofikishana. Septemba 21 mwaka huu DAWASA iliuhakikishia umma wa Tabata kuwa kutakuwa na uhakika wa maji, lakini mpaka leo navyopandisha mnakasha huu kuna baadhi ya mitaa maji kwetu yamebaki kuwa ndoto.

Hata kama ni mgao, ndio wiki nne na zaidi? Hapana kwakweli tumevumilia tumechoka, tunaomba maji na sisi tufurahie kama wengine.

Mbunge wetu Bonnah Kamoli tuliyempitisha kwa kura za kutosha naona hana msaada kabisa kwetu japokuwa anaishi Bonyokwa.

Mvua zinazoendelea nchini nilitegemea zipunguze shida ya maji kwa asilimia kubwa, lakini inaonesha DAWASA bado hawajajipanga na wanafanya kazi kwa mazoea.

Sisi wakazi wa Bonyokwa, mtaa wa Shedaffa na mitaa jirani tunaomba mtufungulie maji nasi tufurahie maisha, kama ninyi mnavyofurahia kututumia bill kubwa kwa huduma ambayo mnatunyima kwa asilimia 80.

Pia soma > DAWASA, Segerea kuna mgao wa maji kimyakimya? Wiki ya pili mitaani hakuna maji!

Asanteni kwa kunisikiliza.

UPDATES:
- Dar: DAWASA imeanza kutekeleza kazi ya kufunga kifaa cha kusukuma maji kwenda Bonyokwa
 
Wanazingua sanaa hao jamaa ,kuunganisha maji pia imekuwa kizungumkuti wanalalamika hawana mita sijui tatizo ni nini na hizo mita sijui zinapatikana mbinguni au wapi
 
Inasikitsha sana.. poleni, kuna maeneo mengine Dar nimesikia nayo maji hakuna.
 
Na huyo mbunge wenu atapita tena

Mtamchagua anajuwa,hana wasi wasi

Ova
 
Ni mambo ya ajabu sana huku tulipofikishana. Septemba 21 mwaka huu DAWASA iliuhakikishia umma wa Tabata kuwa kutakuwa na uhakika wa maji, lakini mpaka leo navyopandisha mnakasha huu kuna baadhi ya mitaa maji kwetu yamebaki kuwa ndoto.

Hata kama ni mgao, ndio wiki nne na zaidi? Hapana kwakweli tumevumilia tumechoka, tunaomba maji na sisi tufurahie kama wengine.

Mbunge wetu Bonnah Kamoli tuliyempitisha kwa kura za kutosha naona hana msaada kabisa kwetu japokuwa anaishi Bonyokwa.

Mvua zinazoendelea nchini nilitegemea zipunguze shida ya maji kwa asilimia kubwa, lakini inaonesha DAWASA bado hawajajipanga na wanafanya kazi kwa mazoea.

Sisi wakazi wa Bonyokwa, mtaa wa Shedaffa na mitaa jirani tunaomba mtufungulie maji nasi tufurahie maisha, kama ninyi mnavyofurahia kututumia bill kubwa kwa huduma ambayo mnatunyima kwa asilimia 80.

Pia soma > DAWASA, Segerea kuna mgao wa maji kimyakimya? Wiki ya pili mitaani hakuna maji!

Asanteni kwa kunisikiliza.
Hawa Dawasa hovyo sana, wamewafungia hata mvua huko.
 
Hawa Dawasa hovyo sana, wamewafungia hata mvua huko.
Bibie bora ubakie tu huko Calgary na Edmonton Alberta canada. Uwe unarudi nyumbani tu likizo mkuranga ulipochimba kisima.

Kulikuwa na haja gani ya SGR?

These people really sucks.
 
Sisi watu weusi tuna walakini. Huwezi ukatumia matrillion ya pesa kujenga reli ya kisasa SGR wakati wananchi wako hawana maji safi na salama.

Yani tufe wote tu.
 
Back
Top Bottom