Tatizo la maji Mjini Arusha sasa limekuwa sugu

Tatu

JF-Expert Member
Oct 6, 2006
1,100
313
Tatizo la maji mjini Arusha sasa limekuwa sugu. Inakuwaje maji yanakatwa kwa zaidi ya siku tatu bila accountability yoyote? Shida hasa ni nini?

Kumekuwa na mvua za kutosha Arusha na mikoa yote kwa ujumla kwa hiyo suala la upungufu wa maji isiwe kisingizio.

Kwa kweli hii hali haikubaliki hata kidogo. Ingekuwa ni siku moja ingeeleweka japo nayo sio sahihi.

Tunahitaji majibu sahihi kutoka kwa wahusika ikiambatana na usitishaji wa hii karaha.
 
Kumekuwa na maboresho makubwa sana ya miundombinu ya maji ikiwa ni pamoja na kujengwa matanki.

Lakini cha kushangaza huduma za maji zimekuwa ni changamoto, muda mwingine kisingizio huwa ni umeme.

Lakini umeme haujawahi kukatika 24hrs. Ama mkurugenzi wa jiji anashindwa kazi yake kwa kuhakikisha mamlaka za maji zinafanya kwa ufanisi.
 
Yaani hayana hata aibu,na mita yqnakuja kusoma kila mwezi,huku yakijua wazi kabisa kuwa maji hakuna.
 
Tatizo la maji mjini Arusha sasa limekuwa sugu. Inakuwaje maji yanakatwa kwa zaidi ya siku tatu bila accountability yoyote? Shida hasa ni nini?

Kumekuwa na mvua za kutosha Arusha na mikoa yote kwa ujumla kwa hiyo suala la upungufu wa maji isiwe kisingizio.

Kwa kweli hii hali haikubaliki hata kidogo. Ingekuwa ni siku moja ingeeleweka japo nayo sio sahihi.

Tunahitaji majibu sahihi kutoka kwa wahusika ikiambatana na usitishaji wa hii karaha.
Siyo maji tu umeme, barabara ndiyo usiseme n.k
 
Mariam Ditopile akiwa ni viti maalum Kingolwira alileta maji ya wahisani na yametufaa miaka na miaka.sasa Moruwasa wanatukatia maji wakisema watu tumeongezeka.Mvua ikinyesha wanasema kuna matope kwenye matank,jua likiwaka wanasema ukame inabidi tufungulie kwa mgao,sasa miezi hii mitatu mvua inanyesha wapo kimya na bill zinasoma 00.
Tubinafishe kwa mchina hii mamlaka hukubwakijua mishahara yao ni kazi ya kuuza maji kwa ufanisi kuliko kukaa na taasisi ambayo wanajiamini wakikosa mapato watalipwa tu.
 
raza la madTatizo la maji mjini Arusha sasa limekuwa sugu. Inakuwaje maji yanakatwa kwa zaidi ya siku tatu bila accountability yoyote? Shida hasa ni nini?

Kumekuwa na mvua za kutosha Arusha na mikoa yote kwa ujumla kwa hiyo suala la upungufu wa maji isiwe kisingizio.

Kwa kweli hii hali haikubaliki hata kidogo. Ingekuwa ni siku moja ingeeleweka japo nayo sio sahihi.

Tunahitaji majibu sahihi kutoka kwa wahusika ikiambatana na usitishaji wa hii karaha.
Tangu CCM wajitangaze kushinda isivyo halali, na tanguy Baraza la Maadiwani liwe chama kimoja , tuendelee kuona ugumu kama tupo Hargeisa , somalia.
 
Back
Top Bottom