Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

TANESCO imekuwepo chini ya CCM na Serikali zake lakini hakuna kilichofanyika cha maana.LOWASSA ndio chaguo letu.
 
Mkuu na huyo mgombea wa ccm iliyo shindwa kutatua tatizo hilo naye ni miongoni mwa wanao takiwa kuonesha namna ya kuondoka tatizo la umeme?
 
Msiwe na mashaka na umeme wa uhakika. Kuna Mgombea mmoja tayari ameshatayarisha tena dili la MVUA toka Thailand!
 
Mgombea wa CCM bwana Magufuli hajawahi hata kutamka neno umeme toka kampeni zimeanza. Labda viwanda atakavyoanzisha tutatumia Power Bank. Pia ikumbukwe ccm wana allergy na umeme ndio maana hawauleti wa uhakika licha ya kutandaza nguzo karibu kila kijiji
 
Ni sababu ya ujinga wetu vinginvyo ilitakiwa kuyazomea mwanzo mwisho kili mkoa ili wajue watz tumechoka kudanganyika na hawa mafisiemu
 
Uchaguzi wa mwaka huu ni kati ya kutafuta fundi mpya wa kujenga nyumba mpya yenye misingi imara au kutafuta fundi wa kukarabati nyumba iliyochoka kuanzia kwenye msingi....uamuzi unao wewe.
 
TUMCHAGUE "macmilan lymo" tabu zote ziishe.
 
Mgombea wa CCM bwana Magufuli hajawahi hata kutamka neno umeme toka kampeni zimeanza. Labda viwanda atakavyoanzisha tutatumia Power Bank. Pia ikumbukwe ccm wana allergy na umeme ndio maana hawauleti wa uhakika licha ya kutandaza nguzo karibu kila kijiji

Hakitaja tu kashfa ya Richmond atakuwa ameshataja kadhia ya umeme!
 
TUMCHAGUE "macmilan lymo" tabu zote ziishe.

Jamaa anasema nchi hii ina rasilimali za kuendesha uchumi hata wa afrika nzima. na umasikini uliopo nchh hii ni laana kutoka kwa mungu ambayo inasababishwa na mwenge ambao ni ishara kuwa nchi hii inaongozwa kishetan
 
Jamaa anasema nchi hii ina rasilimali za kuendesha uchumi hata wa afrika nzima. na umasikini uliopo nchh hii ni laana kutoka kwa mungu ambayo inasababishwa na mwenge ambao ni ishara kuwa nchi hii inaongozwa kishetan

Ila anataka uraisi kwa kuwa Mungu ametoa maono miaka 100 iliyopita kuwa raisi wa tano atatoka kaskazini!
Hajafafanua mikakati yeyote ya utekelezaji wa mipango na juu ya utilisation ya hizo resources! Anachosema hakina mashiko maana kuwa na resources bila ya brain haina maana yeyote!
Mfano ndovu ana resources, pembe ambazo hazina matumizi kwake na wala hajui umuhimu wake! Tunataka brain ndio iendeshe resources, lkn kwa akili hizi za leo, just kwa kuwa chaguo la Mungu au uko handsome au uamuzi mgumu tu au kazi tu!
Tutakuwa kama ndovu tu, resources tulizonazo zitatuua na sio kutusaidia!
 
Kwa kweli hii hali ya tatizo la Umeme linakera sana na hakika litapunguza sana kura za CCM. Hebu fikiria sehemu kama Mbeya umeme unakuja saa 8 usiku, unakata saa 11.

Hapo kumbuka muuza vitumbua ameshindwa kusaga unga kwa sababu ya Umeme, Fundi seremala ameshindwa kukalaza mbao zake, muuza icecream hawezi tena kufanya biashara, Mwanafunzi hawezi tena kujisomea, fundi TV Radio na vitu vingine vinavyohitaji Umeme hafanyi tena kazi zake.

Kwa kweli Umeme ni kila kitu katika shughuli za kiuchumi, hivyo hasira za watu kukosa Umeme watazimalizia kwenye sanduku la kura tarehe 25/10/2015. Kuna sehemu nyingi matokeo ya mwaka huu yatashangaza wengi.

CCM hakikisheni hili tatizo linaisha kabla ya tarehe 25, la sivyo mtapoteza kura nyingi sana za Hasira.
 
Kweli kabisa. Kama kuna jambo litawagharimu sana CCM kwenye uchaguzi huu ni tatizo hili la umeme. Kazi kwao!
 
Zipungue tu maana hapana jinsi nyengine. Sikio la kufa halisikii dawa. Kifo cha nyani miti yote huteleza. Almost twenty years now tuna tatizo la umeme, badala ya kulisolve wao ndo wameligeuza mtaji wa kupiga hela. Richmond-dowans-escrow. Mimi nasema zipungue tu tumechoka.

Nakumbuka mwanzoni mwa utawala wa jk, alisema wamepewa msaada dola milioni 400 kutatua tatizo la umeme, miaka kumi sasa naona limemshinda.
 
Kwahiyo mnaona hili la umeme tuu.... mkinunuliwa generator ya kukodi kwa wiki mbili basi kura mtawapa,,, mshasahau bunge la katiba,,, escrow,,,, epa,,, matusi,,, folen...umaskiini wa tupa,,, kudharauliwa, ufisadi, afya mbovu,, elimu mbovu,,,, yani mpaka hurumaaa,, maji,,, tena wawakatie mpaka mwakani
 
Umeme umeleta shida kubwa sana kwa wananchi wanaotumia maji yanayozalishwa na umeme. Sehemu ninayoishi kabla ya uchaguzi wa CCM kule Dodoma tulikuwa tunapata maji ya uhakika lakini baada tuu ya uchaguzi ule kumalizika, tatizo la umeme lilianza na hili limesababisha hatujawai kuona maji ya uhakika zaidi ya michirizi mithili ya mkojo usiku wa manane.

Wito wangu kwa CCM, Mamlaka za maji zinazozalisha maji kwa kutumia umeme zitawasababishia kipigo sana 25/10/2015 kwenye sanduku la kura. Tanesco na Mamlaka za maji wakipanga ratiba zao vizuri mnaweza kuokoa baadhi ya kura lakini wananchi wamevunjika sana moyo kwa tatizo la uhaba wa maji uliosababishwa na kukosekana umeme.
 
mtu mwenye akili timamu hawezi kuvurugwa na umeme kwenye kupiga kura

Ni mwendawazimu tu anaweza kuipigia kura CCM ikiwa kazungukwa na matatizo lukuki. Maji hakuna, umeme hakuna, barabara mbovu, ajira hakuna. Angalia magazeti ya nipashe na mwananchi leo , jinsi wananchi wanavyokunywa maji ya ziwa pamoja na mifugo yao.
 
Back
Top Bottom