Najiuliza maswali mengi sana kuhusu hali ya upatikanaji wa nishati ya umeme nchini, HALI NI MBAYA watanzania jueni Hali ni MBAYA, ukiona CCM wanakubali tukae gizani na wakati huu wa HATARI wa kampeni ambapo kila kitu wanajitahidi kiwe VIZURI ili kutuhadaa tutoe kura, FAHAMU HALI NI MBAYA SANA.
MSEMO MMOJA WA KISWAHILI UNASEMA "ukiona Paka kakubali kulala chali, Anza kumwomba Mungu".
Ni dhahiri shahiri kuwa kama tutakosea CCM ikarudi madarani October 25 Basi nchi nzima itazima totolooo, GIZA. maana hapa ndio wanaomba kura NCHI ipo GIZANI na hawana jinsi.. Wakiyapata tena hayo Madaraka? Jibu unalo.
UTETEZI wa Tanesco eti wanaingiza umeme wa gesi Taratibu ni kituko, aisee kweli wanatuona malofa, duh!
Swali ni hili, Kabla ya UMEME kutoka MTWARA miezi minne iliopita nini kilikuwa kinawasha umeme nchi nzima?
Kwani icho kilikuwa kinawezesha nchi nzima kuwa na umeme kabla ya gesi kuanza kutoka mtwara ni kimeenda wapi? Nchi hii inakufa na Tanesco kwa mujibu wa Mbowe imefilisika
Changa la MACHO hili.
NI WAKATI WAKUITEKETEZA CCM.
**** ======== *******
Wanatundanganya, Tanzania Ya "Magufuli" ITAKUWA ya VIWANDA, viwanda? labda wawashe kwa Power Bank.